Friday 24 November 2017

VIDEO: Majengo ya Lugumi yakosa Wateja, Docta Shika atajwa



Dar es Salaam. Jumba la kifahari la mfanyabiashara, Said Lugumi limekosa mteja wa kulinunua.

Katika mnada uliomalizika Leo mchana Novemba 24 Mbweni JKT, ulioendeshwa na Kampuni ya Udalali ya Yono, wanunuzi waliojitokeza wameshindwa kufikia bei elekezi
TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.... USIKOSE KUSUBSCRIBE

Mkurugenzi wa Kampuni ya Yono, Scholastika Kevela amesema wateja waliojitokeza wamefikia Sh510 milioni ambayo iko chini ya mategemeo.

"Tunahamia nyumba ya Upanga, kama atapatikana mteja leo tunaweza kurudi na tukamuuzia na masharti ni yaleyale kwamba lazima mteja akifika bei alipe hapa hapa asilimia 25 na asilimia 75 ndani ya siku 14," amesema Kevela

Nyumba hii imeshindwa kununuliwa kwa mara ya tatu baada Septemba 7 kujitokeza kama leo na Novemba 9 ambao unadaiwa ulivurugwa na 'Bilionea' Dk Louis Shika.

Tofauti na ulivyokuwa Novemba 9, leo kila aliyefika katika mnada huo alitakiwa kujiandikisha ikiwamo waandishi wa habari huku ulinzi ukiwa umeimarishwa  zaidi .

No comments:

Post a Comment