Friday 24 November 2017

Yanga yasema Uwanja wa Kaunda lazima ukamilike



Yanga haitanii bwana! Hakika ndilo neno sahihi la kulitumia baada ya wanachama wa klabu hio kuungana na uongozi wao kujaza vifusi kwenye Uwanja wao wa Mazoezi wa Kaunda ikiwa ni matengenezo ya hatua ya kwanza.

Mchakato huo wa kujaza vifusi kwenye sehemu ya kuchezea ya uwanja huo unaotuamisha maji wakati wa mvua nyingi, unafanikishwa kwa asilimia kubwa na nguvu za wanachama wa klabu hio walioamua kujitolea.

Hio ni awamu ya kwanza kabla ya mchakato huo kuhamia kwenye awamu ya pili na tatu ili kukamilisha mchakato mzima unaoaminika kuwa utapunguza gharama kwa klabu hio, Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwassa amethibitisha juu ya hilo.

“Tumeanza mchakato wa kupajaza, kwa ushirikiano wa wanachama, tunaamini malengo yetu yatatimia, malengo yetu ni kupajaza hapa ili kupunguza gharama, tunafanya kazi na wanachama, hatujaweka mikakati ya kumpa mkandarasi yeyote kwa sasa,” amethibitisha Mkwassa.

No comments:

Post a Comment