Thursday 8 February 2018

Kesi ya Sugu yahairishwa kwa muda

Ubishani wa kisheria umeibuka katika kesi inayowakabili Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema),  Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa  Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya hoja ya wakili wa washtakiwa, Peter Kibatala kutaka kuanza na shahidi wa kwanza ambaye ni Mkuu Upelelezi Mkoa wa  Mbeya, kupingwa na Jamhuri.

Mabishano kati ya pande hizo mbili yametokea leo Februari 8, 2018 na kusababisha Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite kuahirisha kesi kwa muda na kuwaita mawakili wa pande zote na kwenda nao ofisini kwake ili wakajadiliane.

Awali, Kibatala aliieleza Mahakama hiyo kwamba wapo tayari kuendelea na utoaji ushahidi na ataanza na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO).

“Mmh! Naona kama kuna ukakasi,  eti hakimu upande wa Serikali?” amehoji hakimu Mteite.

Wakili wa Jamhuri,  Joseph Pande alisimama na kupinga kwa shahidi huyo kuwa wa kwanza huku akisisitiza  kwamba katika utetezi huo, watuhumiwa ndiyo wanaopaswa kuanza.

"Kimsingi anayetakiwa kuanza ni mtuhumiwa kujitetea na kama atakuwa na  mashahidi ndipo wataitwa hao mashahidi wake. Sasa hii itakuwa ni jambo la ajabu kutokea kama ataanza shahidi tofauti na mhusika mkuu (mshtakiwa),” amesema Pande.

Kibatala alisimama na kumpinga Pande akidai hakuna kifungu cha sheria kinachozuia kufanya hivyo na wala hakuna athari yoyote.

“Hapa tutakuwa tunapoteza muda bure. Hakuna katazo  lolote kisheria,” amesema Kibatala.

Kutokana na mabishano hayo Mteute amewaita mawakili hao kwa ajili ya kujadiliana, hivyo kuahirisha kesi hiyo kwa muda.

Sugu na Masonga wanakabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambayo wanadaiwa kuitoa Desemba 30, 2017


Wanaume Arusha wagoma kwenda kliniki na wake zao

Kampeni  ya kuwataka wanaume waongozane na wenza wao wajawazito kiliniki kwa ajili ya kupata ushauri wa kitaalamu  kuhusu afya ya uzazi sambamba na uzazi wa mpango, inaelekea kukwama katika jiji la Arusha na hivyo kutishia kinamama kukosa matibabu.

Katika kampeni hiyo  ambayo mama anayeshindwa kufika na mumewe kiliniki hunyimwa  cheti ili  kuweka mkazo suala hilo.

Kutokana na hali hiyo, suala hilo limesababisha wajawazito  jijini Arusha  kubuni mbinu mpya ya kukodi vijana kuwasindikiza hospitali.

Naibu Meya wa Jiji la Arusha ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya  madiwani wa kupambana  na Ukimwi, Viola Likindikoki alitoa taarifa hiyo juzi wakati akiwasilisha taarifa yake ya robo tatu ya mwaka uliomalizika Januari mwaka huu.

Amesema mgomo wa wanaume wengi katika jiji la Arusha, unawapa  wakati mgumu  wanawake wanaotakiwa kuambatana na waume zao kliniki kutokana na kuwakatalia hivyo kuwalazimu kukodi vijana ili mradi tu waonekane na waume zao ili wapatiwe huduma.

Amewataka viongozi wote wa ngazi ya kata na vijiji kuungana kusisitiza umuhimu wa watu wote kuhudhuria kliniki au kupima maambukizo  kwa lengo la kutambua hali halisi na kupata msaada wa haraka.

“Unajua wafadhili waliokuwa wanafadhili hizi kampeni za kutokomeza Ukimwi wengi wamejitoa, hivyo sisi viongozi tunaowawakilisha wananchi tusibweteke bali iwe chachu ya sisi kupambania maisha ya wananchi wetu.”

Akizungumza na waandishi wa habari, Diwani wa Ngarenaro, Issaya Doita amesema wanaume wengi wanakimbia kuongozana na wanawake hao kutokana na wengi siyo waume zao au wanabanwa na shughuli nyingi za kikazi

“Huu mji ni wa utalii, una pilikapilika nyingi za kusaka uchumi wa nyumbani hivyo wanaume wengi wanakwambia wana kazi nyingi hawawezi kwenda kukaa kliniki halafu jioni walale njaa, lakini sababu nyingine wanayotuambia baadhi yao si wake zao bali ni ‘mchepuko’ hivyo wanaogopa taarifa zao kuwekwa,” amesema Doita.

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia amesema  watahakikisha wanawake kliniki wanakuwa na waume zao la sivyo watafuatilia taarifa zao na watakaobainika kukodi vijana wataumbuliwa.


Jaji Mkuu aionya serikali

Jaji Mkuu nchini Kenya David Maraga, ameilaumu serikali ya nchi hiyo kwa kufanya maamuzi kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi hiyo katika kukabiliana na upinzani.

Jaji Maraga ametoa kauli hiyo ikiwa imepita masaa kadhaa tokea kufukuzwa kwa mwanasheria maarufu ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshuhudia kuapishwa Raila Odinga katika viunga vya 'Uhuru Park' kufukuzwa nchini humo na kupelekwa Canada huku akiwa chini ya uangalizi wa serikali.

Katika maelezo yake Jaji Maraga, amesema malalamiko yaliyopelekwa Mahakamani yalikuwa wazi na majukumu ya kufanyia maamuzi yalikuwa ya Mahakama kutokana na kwamba ndio chombo pekee cha kutetea haki kwa kila mmoja pamoja na serikali yenyewe.

Jaji huyo ametoa tamko hilo la kuionya serikali kwa kushindwa kutii sheria kutokana na kitendo cha serikali ya Kenya kuonekana kudharau maamuzi ya mahakama


Mbosso aanza kuchekelea mafanikio WCB

Usiku wa kuamkia January 29 mwaka huu label ya WCB walimtambulisha msanii mpya ambaye ni Mbosso aliyekuwa Yamoto Band.

Licha ya Mbosso kutambulishwa usiku huu pia siku hii hiyo ndipo wimbo wake wa kwanza ‘Watakubali’ ulitoka official baada ya hapo awali kushirikishwa na WCB katika ngoma yao ya pamoja ‘Zilipendwa’.

Ikiwa ni zaidi ya wiki moja tangu wimbo huo utoke, leo February 8 umeweza kufikisha views milioni moja katika mtandao wa YouTube kitu ambacho Mbosso anasema hakuwahi kukifikiria.

“Sikuwahi kufikiria hata siku moja kama na Mimi kuna siku nitatoa wimbo wangu na ukapokelewa kwa mikono miwili kiasi hichi, ni Baraka tu za Mwenyezi Mungu na support kubwa mnayonipa wadau na mashabiki wa mziki,” amesema .

Diamond, Mobeto wamaliza fofauti zoa

Msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond amesema mazungumzo katika kesi yake Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa watoto kati yake na mwanamitindo Hamisa Mobeto,  imekwenda vizuri.

“Niseme tu mambo yameenda vizuri na kama mnavyojua mambo ya mahakamani ikitokea ninahitajika nitakuja,” amesema.

Diamond alifika mahakamani hapo leo Februari 8, 2018  kusikiliza kesi inayomkabili ya matunzo ya mtoto Prince Abdul iliyofunguliwa na Mobeto.

Amesema yeye na Mobeto hawana shida yoyote, ila kuna watu waliokuwa wakizungumza maneno na kumchochea Mobeto.

"Tunahitaji kuweka mambo sawa. Tunahitaji kuwa katika mstari kwa sababu vitu vidogo vinaharibu upande wa mama na upande wa baba kwa hiyo tulikuwa tunaweka mambo sawa ili kesho na keshokutwa yasilete sintofahamu baina yetu,” amesema na Diamonda na kuongeza:

“Ikitokea kuna mtafaruku baina ya mtoto, kila mtu anakuwa na mawazo yake, kwa hiyo ni lazima kumjenga mtoto na kuhakikisha kuwa mtoto anajengwa na kulelewa  katika malezi bora.”

Alipoulizwa ni kiasi gani cha fedha anachoweza kumudu kutoa kwa ajili ya matunzo ya mtoto huyo, amesema kiasi cha fedha kinazungumzwa zaidi lakini mtoto anahitaji matunzo mengi.

"Kiasi cha pesa tunachoandika sehemu kama hizi tunazungumza tu. Mtoto ana mahitaji mengi wakati mwingine mtoto wako unaweza kumpa hata Sh100 milioni. Huwezi kusema siwezi kumpa kwa sababu niliandikisha nitampa Sh100,000. Tumeweka mazingira mazuri ya kiasi kitakachomfanya akue katika malezi bora,” amesema.

Msanii huyo amesema kupitia kesi hiyo amejifunza vitu vingi na kwamba,  mazungumzo yao ndani ya mahakama hiyo ni siri yao: “mambo yamekwisha.”

Amesema atahakikisha mtoto huyo anakuwa katika mazingira mazuri, kumsomesha kadri ya uwezo wake utakavyoruhusu kwa maelezo kuwa maisha ni kupanda na kushuka.

“Kuna wakati unakuwa hauna unasema leo mie sina basi mambo yanakuwa Bundasiliga leo mnakula mihogo maisha ndivyo yalivyo,” amesema.

Wabunge ANC wakutana kumjadili Zuma

Afrika Kusini.  Kamati ya Bunge ya Chama cha ANC (caucus) inakutana mchana huu katika kikao cha siri ambacho hata hivyo ajenda zake hazikuwekwa wazi kwa waandishi wa habari.

Kamati hiyo inakutana huku kukiwa na shinikizo linalomtaka Rais Jacob Zuma kuachia madaraka.

Duru za habari zinasema kiongozi mkuu wa ANC, Cyril Ramaphosa ndiye atayehutubia kikao cha kamati hiyo inayokutana mjini Cape Town.

Maofisa wa chama hicho hawakuwa tayari kueleza ajenda muhimu za mkutano huo wa dharura mbali ya kusisitiza kuwa ni mkutano wa ndani.

Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge hao huenda wakajadili suala la kuondoka madarakani kwa Rais Zuma na kipindi cha mpito kuelekea katika uchaguzi mkuu mwakani.

Awali, Ramaphosa amesema amekuwa akifanya  mazungumzo ya moja kwa moja na Rais Zuma kuhusiana na kipindi cha mabadiliko na masuala yanayohusu wadhifa wa rais wa nchi hiyo.

Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009 na ambaye anakabiliwa na madai ya ufisadi amekuwa na nafasi finyu ya ushawishi tangu Ramaphosa arithi nafasi ya kiongozi mkuu wa ANC.

Katika taarifa, Ramaphosa amesema yeye na Zuma wanatarajia kukamilisha mazungumzo na waifahamishe nchi kuhusiana na mazungumzo katika siku zijazo.

 Amesema mazungumzo hayo ni nafasi ya kutafuta suluhisho bila kuleta mgawanyiko nchini humo.

Wabunge ANC wakutana kumjadili Zuma

Afrika Kusini.  Kamati ya Bunge ya Chama cha ANC (caucus) inakutana mchana huu katika kikao cha siri ambacho hata hivyo ajenda zake hazikuwekwa wazi kwa waandishi wa habari.

Kamati hiyo inakutana huku kukiwa na shinikizo linalomtaka Rais Jacob Zuma kuachia madaraka.

Duru za habari zinasema kiongozi mkuu wa ANC, Cyril Ramaphosa ndiye atayehutubia kikao cha kamati hiyo inayokutana mjini Cape Town.

Maofisa wa chama hicho hawakuwa tayari kueleza ajenda muhimu za mkutano huo wa dharura mbali ya kusisitiza kuwa ni mkutano wa ndani.

Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge hao huenda wakajadili suala la kuondoka madarakani kwa Rais Zuma na kipindi cha mpito kuelekea katika uchaguzi mkuu mwakani.

Awali, Ramaphosa amesema amekuwa akifanya  mazungumzo ya moja kwa moja na Rais Zuma kuhusiana na kipindi cha mabadiliko na masuala yanayohusu wadhifa wa rais wa nchi hiyo.

Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009 na ambaye anakabiliwa na madai ya ufisadi amekuwa na nafasi finyu ya ushawishi tangu Ramaphosa arithi nafasi ya kiongozi mkuu wa ANC.

Katika taarifa, Ramaphosa amesema yeye na Zuma wanatarajia kukamilisha mazungumzo na waifahamishe nchi kuhusiana na mazungumzo katika siku zijazo.

 Amesema mazungumzo hayo ni nafasi ya kutafuta suluhisho bila kuleta mgawanyiko nchini humo.

Tigo wapunguza gharama

Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo imepunguza gharama za kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kitaifa na kimataifa kwa asilimia 27.5.

Takwimu zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonyesha kuwapo kwa punguzo hilo katika robo ya nne ya mwaka iliyoishia Desemba 2017 ikilinganishwa na robo ya tatu ya mwaka ulioishia Septemba.

Ripoti ya robo ya tatu ilionyesha kuwa Tigo ndiyo mtandao wenye gharama kubwa Tanzania katika kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi kitaifa na kimataifa jambo ambalo limekuwa tofauti na robo ya nne ya mwaka.

Katika robo ya tatu ya mwaka wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh360 kwa dakika (kabla ya VAT) katika kupiga simu ndani ya mtandao ambayo imeshuka hadi kufikia Sh261 katika robo ya nne ya mwaka, ikiwa ni pungufu ya Sh99 sawa na asilimia 27.5.

Hata hivyo, kushuka kwa gharama za kupiga simu ndani ya mtandao katika robo ya nne, takwimu zinaonyesha kuwa  tozo za Tigo bado zipo juu ya wastani wa gharama za kupiga simu ambazo ni Sh249 kwa dakika.

Katika kupiga simu nje ya mtandao wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh480 kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imeshuka hadi kufikia Sh348 ambayo ni sawa na pungufu ya asilimia 27.5.

Licha ya kuwapo kwa punguzo hilo, tozo hiyo bado ipo juu ya wastani wa gharama za kupiga simu nje ya mtandao ambazo ni Sh329 kwa dakika.

Katika kupiga simu Afrika  mashariki wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh1,022 kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imepungua hadi kufikia Sh739 katika robo ya nne ya mwaka ikiwa ni pungufu ya Sh283 sawa na asilimia 27.7.

"Kupungua kwa gharama hizo kumeifanya Kampuni ya Tigo kuwa miongoni mwa kampuni zinazotoza tozo iliyo chini ya kiwango cha wastani ya kupiga simu Afrika ya Mashariki ambayo ni Sh745 kwa dakika,"amesema.

Katika kupiga simu kimataifa, Tigo ilikuwa ikitoza Sh1,737 katika kupiga simu kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imepungua hadi kufikia Sh1,258, ikiwa ni pungufu ya Sh479 sawa na asilimia 27.6.

Kupungua kwa gharama hizo kunaifanya Tigo kuwa chini ya wastani wa tozo za kupiga simu kimataifa ambayo ni Sh1,273.

Kutuma ujumbe mfupi
Katika kutuma ujumbe ndani ya mtandao, Kampuni ya Tigo imepunguza gharama hadi kufikia Sh51 katika robo ya nne ya mwaka kutoka Sh70 iliyokuwapo katika robo ya tatu ya mwaka, hiyo ni sawa na pungufu ya Sh19 sawa na asilimia 27.14.

Tozo hizo za kutuma ujumbe mfupi ziko sawa na wastani uliowekwa  wa Sh51 kwa kila ujumbe.

Katika kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kimataifa gharama imepungua hadi kufikia Sh156 katika robo ya nne ya mwaka kutoka Sh 215 ya robo ya tatu ya mwaka ikiwa ni pungufu ya Sh59 sawa na asilimia 27.4.

Gharama hizo ziko juu ya wastani wa tozo za kutuma ujumbe nje ya nchi ambayo ni Sh95.

Serikali yakiri uwepo wa mgogoro kati ya wananchi na JWTZ

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi amekiri kuwepo kwa mgogoro wa wananchi na Jeshi la Kujenga Taifa (JWTZ) eneo la Kisakasaka.

Akizungumza leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Jimbo la Dimani Juma Ally Juma aliehoji Kuna mgogoro wa  kati ya Jeshi la polisi na wananchi wa Kisakasaka hali iliyoleta  wasiwasi kwa wananchi,  Je? ni lini serikali itapatia ufumbuzi wa mgogoro huo?

“Ni kweli kwamba mgogoro huu ni wa muda mrefu nataka nimfahamishe Mh. Juma kwamba mimi binafsi nimefika eneo hilo nilifanya mazungumzo na uongozi wa kikosi pamoja na uongozi wa eneo pamoja na wananchi wa pale kulizungumza na kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi inachokwamisha kutatua sasa hivi ni suala la fedha za kupima kwasababu jeshi lilisharidhia kufanya mabadiliko ya mipaka yake ili wananchi wanaoonekana ndani ya kambi waweze kutolewa lakini   .Hata hivyo nitazungumza na Mh. Mbunge ili kumueleza zaidi ni hatua gani zinazostahili kuchukuliwa kwa mujibu wa ziara niliyoifanya pale na fedha zikipatikana,” amesema Waziri Mwinyi.

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

Orezi collaborates with Tekno on his first single of 2018 titled ‘Whine for Daddy.’ The song comes after his 2017 hit songs, ‘Hallelujah’ and ‘Cooking Pot’.

Orezi describes ‘Whine for Daddy’ as a “Sugar Daddy jam” aimed at making people dance. According to him, “I was just trying to make a record that people can dance to, just whine and Daddy will take care of you.”




Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download




Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download




Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download

New VIDEO: Chindo Man ft Rayvanny – Mama Lao

New VIDEO: Chindo Man ft Rayvanny – Mama Lao

New VIDEO: Chindo Man ft Rayvanny – Mama Lao


DOWNLOAD VIDEO

Wednesday 7 February 2018

Hizi ndizo Njia tatu za kupunguza foleni Dar

Wakati Serikali ikiendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali kukabiliana na changamoto ya foleni jijini Dar es Salaam, Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (Jica) limekuja na mwarobaini wa tatizo hilo.

Timu ya wataalamu wa shirika hilo imefanya utafiti ulioonyesha njia mbalimbali zinazoweza kutumiwa kukabiliana na foleni kubwa, ikiwamo ujenzi wa reli.

Akizungumza wakati wa uwasilishaji wa mpangilio wa sekta ya usafirishaji katika Jiji la Dar es Salaam kwa mwaka 2018 hadi 2040, mwakilishi wa Jica nchini, Toshio Nagasa alisema kufikia mwaka 2040 wakazi wa jiji hilo watakuwa wameongezeka kutoka milioni sita hadi 12. Kutokana na ongezeko hilo Nagasa alisema ni muhimu kwa Serikali kuweka mazingira wezeshi ya usafiri ili kuwezesha sehemu zote za jiji kufikika kwa urahisi huku shughuli za uchumi zikiendelea.

“Kukabiliana na msongamano utakaojitokeza katika kipindi hicho ni muhimu Serikali ikafikiria kujenga miradi ya reli, ambayo inaweza kusafirisha watu wengi kwa pamoja, hii itasaidia kupunguza magari binafsi kuingia barabarani,” alisema.

Licha ya reli, mpango huo umeshauri kuwapo kwa barabara za juu katika makutano ya Morocco, Chang’ombe na Mwenge.

Kingine kilichoelekezwa katika mpango huo, ni uwapo wa miji midogo maeneo ya pembezoni ili kupunguza msongamano katikati ya jiji.

Kauli ya Serikali

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Spora Liana alisema wataalamu hao wameshauri miji hiyo midogo iwekewe huduma zote za msingi ili watu wengi wasiende mjini. Alisema utekelezaji wa mradi huo utagharimu Sh19.1 bilioni ukihusisha ujenzi wa miundombinu.

Wakati huohuo, mkurugenzi wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam mhandisi Patrick Mfugale alimweleza waziri wa Ujenzi na Usafirishaji wa Lesotho, Lehlohonolo Moramotse, kuwa mradi wa ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere (Tazara) wenye thamani ya Sh95 bilioni, unatarajia kukamilika Mei na kutumika rasmi mwishoni mwa Oktoba. Waziri huyo yupo nchini na wataalamu wa wizara yake kujifunza namna ambavyo wenzao wanasimamia ujenzi, ukarabati na utunzaji wa barabara.

Serikali yaahidi kuboresha mishahara

Serikali ya Tanzania imeahidi kuanza kuboresha maslahi ya watumishi ya walimu ikiwemo mishahara yao kipindi hiki kutokana na kumaliza zoezi la muda mfupi la uhakiki wa wafanyakazi hewa katika sehemu mbalimbali za ajira.

Hayo yamewekwa wazi na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI George Joseph kakunda leo (Jumatano) katika mkutano wa 10 kikao cha saba cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Karagwe Innocent Bashungwa alipotaka kujua ni lini serikali itawapandishia mishahara walimu.

"Utaratibu huu ambao ulikuwa umesimama kwa kipindi kifupi cha miaka kama miwili hivi kupisha uhakiki wa watumishi ambapo ni zoezi lililofanywa kwa umahiri na ueledi mkubwa, baada ya kuwa tumelikamilisha sasa tutaingia kwenye awamu ambayo ni ya kuboresha maslahi ya watumishi ikiwemo mishahara yao", amesema Kakunda.

Kwa upande mwingine, Mhe. kakunda amewatoa hofu walimu wote ambao hawakupandishwa madaraja yao kutokea mwaka 2016 hadi 2017 na kudai katika mwaka huu wa fedha wameshafanya matayarisho wa kupandisha madaraja hayo.

Askari Magereza 11 wasimamishwa

Jeshi la Magereza Tanzania limewasimamisha kazi askari wake kumi na moja waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za mauaji ya mwanakijiji, Aloyce Makalla (41) wiki iliyopita.

Taarifa kutoka ndani ya jeshi hilo zinasema askari hao walisimamishwa kazi na Kamishna Jenerali wa Magereza, Dk Juma Malewa juzi.

Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tanga, John Masunga alithibitisha kusimamishwa kwa askari hao lakini hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa undani zaidi akisisitiza kuwa msemaji wa jeshi hilo ni Kamishna Jenerali pekee.

Askari waliosimamishwa ambao walishafikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Korogwe mwishoni mwa wiki mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Kassim Mkwawa ni Jonas Makere, Shadrack Lugendo, Lazaro Stephen, Mussa Zuberi, Ramadhan Yusuf, Robert Alfred, Fhidirish Osmas, Alfonce Revocatus, Mbesha Naftari, Hamis Msola na Michael Elias.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa hatua ya kuwasimamisha kazi askari hao imechukuliwa ikiwa ni kupisha vyombo vya sheria kufanya kazi yake kwa uhuru zaidi na kwamba hatima yao itategemea uamuzi wa mahakama hiyo.

Askari hao wa Wilaya ya Korogwe walifikishwa katika mahakama hiyo wakikabiliwa na shtaka la kumuua, Makalla, ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Kerenge wilayani humo.

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwanasheria mwandamizi wa Serikali, Saraji Iboru kuwa Januari 22 saa 9.30 katika kitongoji cha Mapangoni Kijiji cha Kerenge, washtakiwa hao kwa pamoja walimuua mwanakijiji huyo.

Iboru ambaye alikuwa akisaidiana na mwendesha mashtaka kiongozi, Shosa Naiman alidai kwamba siku ya tukio, washtakiwa hao walikwenda nyumbani kwa Makalla wakimtuhumu kwamba Januari 15 alimjeruhi askari mwenzao aitwaye Sajenti Stephen.

Washtakiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo kisheria wa kusikiliza kesi za mauaji. Hakimu Mkwawa aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 15 itakapotajwa tena.

Hii ndio gharama aliyotumia Vanessa Mdee kuandaa albamu yake mpya ‘MoneyMonday’

Msanii wa muziki, Vanessa Mdee amedai ametumia gharama kubwa katika kuiandaa albamu yake mpya MoneyMonday.

Muimbaji huyo amesema kuwa albamu ya MoneyMonday mpaka kukamilika imemgharimu zaidi ya shilingi za Kitanzania Milioni 100.

“Nimetumia fedha nyingi lakini kwangu sioni tatizo lolote, niliangalia zaidi jinsi gani watu watatambua Vanessa kafika wapi katika kukua kimuziki, fedha hiyo nililipa idara zote kuanzia wasanii walioshiriki matangazo, video nk na bado naendelea kutoa kwa kuwa matangazo bado yanaendelea ,” Vanessa aliuambia mtandao wa Dar 24.

Ameongezea kuwa hajutii matumizi ya kiasi hicho kikubwa cha fedha kwa kuwa lengo lake hasa ni kutoa kazi itakayomwongezea heshima kwenye muziki wake sambamba na kuhakikisha inawifikia watu wa aina zote.

Hivi karibuni Vanesa ameachia albamu yake katika ukumbi wa Mlimani City.

Vanessa ni kati ya wasanii wachache ambao wanajaribu kurudisha utamaduni wa kutengeneza Albamu katika muziki wa Bongo fleva jambo ambalo kwa siku za nyuma limekuwa likififia na kupotea.

Naye Diamond Platinum anajipanga kuaachia albamu yake ya Mtoto wa Tandale ambapo juzi alitaja baadhi ya sababu zilizomfanya acheleweshe kutoka kwa albamu hiyo.

Waziri Nchemba aongoza oparesheni ya kuteketeza ekari sita za bangi

Waziri wa mambo ya ndani nchini, Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Mwigulu akishirikiana na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,(RPC)Charles Mkumbo pamoja na vikosi vya askari wa jeshi la polisi mkoani hapa walilazimika kuacha magari yao njiani na kutembea umbali wa kilomita 5 milimani kufika katikati ya msitu huo ambapo wamiliki wa mashamba hayo walitokomea kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo Mwigulu alisema kwamba serikali itaendelea na oparesheni pande zote za nchi na haitasita kuwakamata wahusika wote na kutaifisha magari yatakayotumika kusafirisha bangi.

Akizungumza na askari waliokuwa wakishiriki katika zoezi hilo Mwigulu mbali na kuwapongeza kwa kazi wanayofanya lakini aliwambia kwamba pamoja na kufanikiwa kuteketeza madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani lakini waongeze juhudi pia katika kupambana na madawa ya kulevya yanayotengenezwa viwandani.

“Niwapongeze sana songeni mbele na kazi ya kukamata madawa yote ya kulevya mmefanya kazi kubwa sana ya kukabiliana na madawa ya kulevya yanayolimwa mashambani ongezeni bidii kukamata na yale yanayozalishwa viwandani,” alisema Waziri Mwigulu.

Hata hivyo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha(RPC),Charles Mkumbo alisema kwamba jumla ya ekari sita za mashamba ya bangi zimeteketezwa na kusisitiza kwamba oparesheni hiyo ni endelevu katika mkoa wa Arusha na wilaya zake.

Aidha Kamanda Mkumbo alifichua mbinu mpya wanayotumia wamiliki wa mashamba hayo kwamba kwa sasa wameamua kulima mashamba hayo katikati ya misitu kwa lengo la kujificha ili kukwepa mkono wa sheria.

“Walidhani kulima bangi katikati ya misitu hatutawakamat sisi tuna mbinu nyingi na hatutakubali kuona vijana wetu wanaharibikiwa kwasababu ya bangi.”

Vanessa Mdee atoa ufafanuzi kuhusu ngoma zake na Diamond kuchezwa Nigeria



Msanii wa muziki Bongo, Vanessa Mdee ametolea ufafanuzi kauli yake iliyodai alipofika Nigeria alikuta ngoma za wasanii toka Bongo zinazochezwa ni zake na za Diamond.

Baada ya kauli hiyo Vanessa amekuwa akishambuliwa na mashabiki hasa wa team Kiba kuwa kauli yake ni yenye upendeleo kwa upande mmoja. Kupitia Instagram Vanessa ameamua kumjibu shabiki aliyehoji kuhusu hilo.

vanessamdee @ze_masta my love hiyo issue nilikuwa nazungumza kitu kikubwa zaidi lakini wenye akili zao wamegeuza imekuwa hivyo. Na Ukiangalia lengo la jibu langu ilikuwa kuwahamasisha waTanzania wathamini na waPromote zaidi mziki wa home maana wenzetu ndivyo wanavyofanya.

Sasa wapi hapo nimemdiss kaka? Kaka anajua mimi shabiki yake sasa tutafika kweli kila neno linageuzwa kuwa negative when in truth I was just shedding light on what I was seeing. Jamani.

Hapo Jux Vanessa aliiambia Clouds Fm alipoenda Nigeria kwa ajili ya kutangaza albamu yake ‘Money Mondays’ katika moja club alizopita alikuta ngoma zinazochezwa kutoka Bongo ni ya Patoranking na Diamond ‘Love You Die’ na ile aliyoshirikiana na Reekado ‘Move’.

Msigwa amfungukia Kigwangalla Bungeni

Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya CHADEMA, Mhe. Peter Msigwa amefunguka na kumchana Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala na kudai kuwa anafanya kazi kwa mizuka na mihemko na kuisumbua sekta ya Utalii na Maliasili nchini.

Msigwa amesema hayo wakatii alipokuwa akichangia bungeni taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji, mjini Dodoma na kudai kuwa Mawaziri vijana wamekuwa na mihemko.

"Niwashauri hawa Mawaziri vijana fursa 'opportunity is atrracted by talent, skills, perfomance and abillity. Show your talent and abillity people will love you' hawa Mawaziri wa zamani hawa kwa mfano Lukuvi, Tizeba tunawaona wakijibu hoja wanajibu hoja siyo za kimihemko kiasi kwamba unaridhika hata Waziri akikujibu unapenda lakini Mawaziri vijana wengi mnaonekana mnayofanya katika Serikali hii kiasi kwamba Serikali ijayo muonekane hamna tija" kwa sababu mna mihemko sana"

Mbali na hilo Msigwa alikwenda mbali zaidi na kumnyooshea mkono Waziri wa Maliasili na Utalii na kudai amekuwa na maamuzi ya ajabu jambo ambalo linapelekea kiongozi huyo kuivuruga Wizara hiyo.

"Utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana na akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutafuta umaarufu atauvuruga kwa muda mfupi sana, Utalii kwenye pata la taifa unaingiza asilimia 20 na forex ni kubwa inatokana na utalii kwa hiyo hicho si kitu kimoja mtu anaweza kuamka leo anasema nimeharibu na hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika, wawezekaji huko nje wanataka kuona kunatabirika wao kufanya biashara zao. Haiwezekani huyu Waziri anatoa amri mpaka mapolisi wanamkataa anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani, huyu huyu Waziri anatoa amri anapingana na Waziri wa Ardhi, huyu huyu Waziri mmoja anapingana na Waziri wa Uvuvi hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanakuwa na mizuka na kufanya kazi kwa mizuka wote kama tunalipenda taifa letu tufanye kazi kwa kupendana" alisisitiza Mchungaji Msigwa

. Nassari: katika Jimbo langu kumeanza kuibuka migogogro juu ya michango

Arusha. Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki (Chadema) Joshua Nassari, ameitaka Serikali kutoa tamko moja juu ya michango ya chakula shuleni kama ni halali ama la ili kuzuia migogoro ambayo imeanza kuibuka.

Akizungumza na Mwananchi leo Februari 7 Nassari amesema  katika jimbo lake kumeanza kuibuka migogoro juu ya michango ya chakula kwani kuna wazazi ambao walikuwa wamechangia mara baada ya shule kufunguliwa na sasa wanataka warejeshewe michango yao.

‘’Hili  suala limeleta utata mkubwa na mgongano baina ya walimu, Kamati za shule na wazazi, kwani  baadhi ya wazazi wameaminishwa kuwa Serikali imetoa fedha kugharamia mahitaji yote ya shule," amesema

Amesema  ni muhimu kuwepo na tamko moja ni michango gani, ambayo ni marufuku na ipi ambayo inakubalika na hivyo kuwekwa utaratibu mzuri wa kuikusanya.

Alisema anachofahamu ni kuwa Serikali, haijapiga marufuku michango ya chakula, bali kinachotakiwa ni wazazi kutoa kwa hiari yao baada ya kukubaliana katika vikao lakini jambo hili linapaswa kuelimishwa.

Waraka namba 3 wa mwaka 2016 juu ya suala la elimu bure, pia umeeleza jukumu la chakula cha wanafunzi kwa shule za kutwa na sare za shule ni la wazazi.

Diwani wa kata ya Imbaseni, Gabriel Mwanda alisema katika kata yake, kuna wazazi walichanga chakula shuleni, lakini kutokana na tamko la serikali la kuzuia michango wameanza kuidai.

"Hili ni tatizo, tumejaribu kuwaeleza wazazi juu ya umuhimu wa michango baadhi wameelewa na wengine bado hawajaelewa" amesema

Mwanda amesema ni ukweli ni kuwa fedha ambazo zinapelekwa shuleni, hazitoshi mahitaji yote lakini sintofahamu iliyopo sasa isipopatiwa ufumbuzi itaathiri sekta ya elimu.

"Suala la chakula kwa watoto  shuleni ni muhimu sana hivyo tumekuwa tukishauri wazazi kuchanga kwa hiari lakini watoto wasirejeshwe nyumbani kwa wazazi wao kwa kushindwa kuchangia chakula," amesema.

Katika shule nyingi wilaya ya Arumeru, kamati za shule zilikuwa zimepitisha mchango wa debe mbili za mahindi na kilo tano za maharage kwa ajili ya chakula na tayari shule zilipofunguliwa wazazi walichanga.

Hata hivyo, kutokana na kuibuka utitiri wa michango shuleni, hivi karibuni Rais John Magufuli alitangaza kupigwa marufuku walimu kupokea michango mashuleni na akawataka wazazi ambao wanataka kujitolea kupeleka michango yao kwa  wakurugenzi.

Wakulima wa Mahindi watoa kilio chao kwa Serikali

Wakulima wa mahindi mkoani Njombe wamedai kuwa bado hawajaanza kuona manufaa ya kufunguliwa kwa mipaka kutokana na wafanyabiashara kutochukua mahindi waliyonayo licha ya bei ya zao hilo ikiwa ni chini ya kawaida.

Wakulima hao wamesema kuwa kufunguliwa kwa mipaka hakuna faida kwao kwa kuwa mazao hayanunuliwi kutokana na wafanyabiashara wanaotoa mazao nje ya nchi tayari wana mahindi ya kutosha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mkoani Njombe wakulima hao wamesema kuwa zao hilo sasa halina soko la uhakika na bei yake imekuwa ni ya chini mpaka shilingi 4500 kwa debe moja la kilo 20 ambazo pamoja na kushuka hakuna mteja anaye fika kununua.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe nayo inalalamika kwa kutonunuliwa kwa mazao hayo ambayo ni moja ya chanzo chake cha mapato ambapo awali ilitegemewa wakala wa hifadhi ya chakula (NFRA), watanunua mazao hayo.

Kambale wa Singida United aiomba radhi klabu yake



Nyota wa kimataifa wa Singida United Kambale Salita gentil ameiomba msamaha klabu hiyo baada ya kumsimamisha kwa muda usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu uwanjani.

Taarifa ya klabu hiyo iliyotolewa leo na Mkurugenzi mtendaji Festo Richard Sanga imeeleza kuwa kiungo huyo aliyesajiliwa kwenye dirisha dogo ametambua kosa lake na kuomba kupunguziwa muda wa adhabu.

Sehemu ya taarifa hiyo pia imenukuu maneno ya Kambale ambaye amesema, ''Naomba sana mnisamehe, mimi ni mtoto wenu, mimi ni kijana wenu na mimi ni mfanyakazi wenu, naomba wachezaji wenzangu wanisamehe pamoja na uongozi wa klabu yangu, tukio hili halitajirudia tena''.

Kambale alimpiga mchezaji wa timu ya Green Worriors kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho kitendo kilichopelekea kuoneshwa kadi nyekundu. Singida United ilishinda mchezo huo na kusonga mbele.

Singida United leo jioni inashuka kwenye dimba la CCM Kirumba kukipiga na wenyeji Mbao FC kwenye mchezo wa ligi kuu. Singida United inashika nafasi ya nne ikiwa na alama 30.

Luis Enrique akubali kurithi mikoba ya Antonio Conte?

Habari kutoka Hispania zinaeleza kuwa meneja wa zamani wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique ameonekana kukubali kurithi mikoba ya kocha Antonio Conte ndani ya Chelsea.

Nafasi ya Conte ndani ya kikosi cha Blues imeonekana kuwa mashakani tangu wiki iliyopita baada ya kupata matokeo mabaya ya kufungwa 3 – 0 dhidi ya Bournemouth na yale ya 4-1 mbele ya Watford siku ya Jumatatu.

Kufuatia mwenendo wa kusuasua kwa kikosi cha Chelsea mmiliki wa timu hiyo Mromania Abramovich anampango wa kumpatia mkataba wa miaka miwili na nusu kocha Enrique mwenye umri wa miaka 47 ambao atakuwa the blues hadi mwaka 2020 hii ni kwa mujibu wa chombo cha Sports.

Chadema yasema mgombea Udiwani wa Chama hicho alipewa fedha ajitoe

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema mgombea udiwani wa chama hicho Kata ya Buhangaza Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, Athanas Makoti (28) alilazimishwa kupokea rushwa ya Sh8milioni na watu waliomteka na kumjeruhi ili ajitoe kwenye uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 7, 2018 makao makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Dk Mashinji ameliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kuchukua hatua.

Makoti alitekwa Februari 2, 2018 katika mazingira ya kutatanisha na kupatikana Februari 5, 2018 saa moja asubuhi akiwa ametelekezwa na watu wasiojulikana jirani na Hospitali ya Kagando iliyopo Wilaya ya Muleba. Mgombea huyo amelazwa katika hospitali hiyo mpaka sasa.

Dk Mashinji amesema Makoti alikuwa anatoka kwenye maandalizi ya uchaguzi, akaita bodaboda ili arejee nyumbani lakini likatokea gari nyuma yake na kumchukua kwa nguvu.

“Watekaji hao walimfunga kitambaa usoni akapoteza fahamu. Walimzungusha maeneo mbalimbali na alipozinduka hakujua aliko. Walimtaka akubali kupokea Sh8 milioni na ajitoe kwenye uchaguzi, hata hivyo alikataa ndipo wakaanza kumtesa,” amesema Dk Mashinji,

“Hizi ni njama za kisiasa kutaka kuvuruga uchaguzi katika kata ya Buhangaza,” amesema.

Amesema kwa mujibu wa maelezo ya mgombea huyo, alitekwa kwa madhumuni ya kisiasa.

“Tunalaani  kitendo cha mgombea wetu kutekwa, kuteswa na kulazimishwa kupokea fedha ili ajitoe kwenye uchaguzi,” amesema.

VIDEO: BAKWATA Watoa Tamko

Baraza la Waislamu Tanzania BAKWATA, kupitia kwa Msemaji wa Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Khamis Mataka leo wametoa  majina ya Taasisi 15 ambazo zimekubaliwa na kupewa idhini ya kupeleka Mahujaji ambao wataenda kuhiji na pia zimeratibiwa na kupewa hisa ya kufanya safari.

Sheikh Mataka amewataka waislamu wote nchini kuzingatia taratibu zote zilizowekwa na BAKWATA ili kuepuka usumbufu ama matapeli ambao wanajitokeza kwa kipindi cha kuelekea HIJJA.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHU KUSUBSCRIBE


VIDEO: Uchumi wa Tanzania umepanda na nakuongoza kuwa na Uongozi Bora

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas, amesema hali ya uchumi wa Tanzania imeimarika ikilinganishwa na awamu zilizopita ambapo imeshika nafasi ya 48 kwa nchi zenye uchumi jumuishi duniani, pia ni ya pili Afrika ikifuatiwa na Tunisia ambapo kusini mwa jangwa la Sahara ni ya kwanza.

Abbas alikuwa akizungumza leo jijini Dar es Salaam na  waandishi wa habari ambapo mambo mengine aliyozungumzia ni kuhusu kifo cha mkongwe wa siasa nchini marehemu Kingunge Ngombale-Mwiru aliyemuita kuwa ni msahafu wa siasa za Tanzania.
Pia Abbas alitumia fursa hiyo akisema kwamba atakuwa na utaratibu maalum wa  kuzungumza na waandishi wa habari kila mwisho wa mwezi ambao utatolewa karibuni.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.....................USISAHAU KUSUBSCRIBE...................

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

Audio | Timbulo – Promise | Mp3 Download

DOWNLOAD

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda

New VIDEO: Mesen Selekta Ft Rayako – Kinanda


DOWNLOAD VIDEO


Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

Audio | Chemical ft Beka Flavour – Asali | Mp3 Download

DOWNLOAD

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video

New Video | Maromboso ( Mbosso ) _ Riziki | Official Video


Sunday 4 February 2018

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote

DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote
Vigour - Pande Zote
DOWNLOAD: Vigour – Pande Zote


Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne kuundwa

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt Rehema Nchimbi amewataka viongozi wa vijiji na kata mkoani humo kuhakikisha wanatunga sheria ndogo ya kunyonyesha ndani ya miezi minne ili kuondokana na tatizo la ukosefu wa lishe kwa watoto.

Dkt Nchimbi ametoa agizo hilo Juzi Ijumaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vifaa vya kutambua hali ya lishe kwa watoto na akinamama wajawazito katika kijiji cha Saranda wilayani Manyoni.

“Kunyonyesha ni lazima, Wenyeviti wa vijiji na kata hakikisheni mmetunga sheria ndogo kwa ajili ya kudhibiti akinamama wote wasionyonyesha watoto wao kulingana na taratibu za afya,”amesema Dkt. Nchimbi.

Mhe Nchimbi amelazimika kutoa agizo hilo baada ya kusomewa taarifa inayoonesha kuwa ni asilimia 54 pekee ya watoto mkoani Singida ndio hubahatika kunyonyeshwa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita.

Akisisitizia suala hilo Dkt. Nchimbi amesema kuwa ulazima huo usibakie kuwa ni wa majukwaani tu bali utekelezwe kisheria na atakayepatikana aadhibiwe, hata hivyo, mhakikishe adhabu hiyo haisababishi mama kumkimbia mtoto.

Aubameyang aanza kuonyesha makali yake Arsenal

STAA mpya wa Arsenal Pierre-Emerick Aubameyang jana alianza mchezo wake wa kwanza kwenye timu hiyo na kufanikiwa kuifungia bao moja kwenye ushindi wa 5-1 dhidi ya Everton katika mchezo wa Ligi Kuu England.

Aubameyang amejiunga na Arsenal kwenye dirisha hili la usajili na huu ulikuwa mchezo wake wa kwanza kuitumikia timu hiyo ya London na kupata ushindi mnono hata hivyo Aaron Ramsey aligeuka nyota kwenye timu hiyo baada ya kufunga mabao matatu ‘hat trick’.

Arsenal ilianza mchezo huo kwa kasi ya hali ya juu na ndani ya dakika 20 za kwanza timu hiyo ilikuwa mbele kwa mabao 4-0.

Ramsey, alifanikiwa kuifungia Arsenal bao la kwanza katika dakika ya sita ya mchezo akimalizia pasi safi ya Henrikh Mkhitaryan, ambaye alipata pasi kutoka kwa Mesut Ozil.

Dakika ya 14, Laurent Koscielny, alifanya kazi kubwa baada ya kuifungia Arsenal bao la pili baada ya kumalizia pasi iliyopigwa na Shkrodan Mustafi.

Iliwachukua Arsenal dakika sita tu kujipatia bao la tatu ambalo liliwekwa tena kimiani na Ramsey na kuwafanya waendelee kutakata.

Dakika ya 36 ya mchezo, Mkhitaryan alifanya kazi kubwa na kutoa pasi yake ya pili ya bao baada ya kumtengea Aubameyang mpira safi ambaye hakufanya kosa na kuuchopu akaifungia timu yake bao la nne.

Hata hivyo, Theo Walcott ambaye anaitumikia Everton akiwa anacheza mchezo wake dhidi ya timu yake ya zamani alionyesha kiwango kizuri kipindi cha kwanza ambapo alitolewa uwanjani katika dakika ya 63 na kupigiwa makofi na wachezaji pamoja na mashabiki wa timu hiyo ya London kuonyesha heshima kwake.

Dakika mbili baada ya kutolewa Everton walifanikiwa kujipatia bao moja kupitia kwa Calvert Lewin na kufanya matokeo kuwa 4-1.

Kipa wa Arsenal, Petr Cech aliumia na kutolewa kwenye mchezo huo na nafasi yake kuchukuliwa na David Ospina katika dakika ya 69.

Dakika ya 74, Ramsey alikamilisha `hat trick’ yake baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Mkhitaryan ambaye naye alitoa pasi ya tatu ya bao kwenye mchezo huo.

Katika mchezo wa awali, Manchester United walipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Huddersfield, huku staa mpya wa timu hiyo, Alexis Sanchez akiifungia timu yake bao moja likiwa ni la kwanza kwake kuanzia ajiunge nayo akitokea Arsenal.

Bao lingine la United liliwekwa kimiani na Romelu Lukaku, huku Manchester City wao wakitoka sare ya bao 1-1 na Burnley.

TANO Z IJAZO ARSENAL

Tottenham -UGENINI- Feb 10

Ostersund -UGENINI- Feb 15

Ostersund -NYUMBANI- Feb 22

Man City -UGENINI- Feb 25

Man City -NYUMBANI- Mar 1

Arsenal: Cech (Ospina 69), Bellerin, Koscielny, Mustafi, Monreal (Kolasinac 45), Ramsey (Wilshere 74), Xhaka, Mkhitaryan, Ozil, Iwobi, Aubameyang.

Subs: Lacazette, Chambers, Maitland-Niles, Elneny.

Scorers: Ramsey 6, 19, 73, Koscielny 14, Aubameyang 37

Booked: Koscielny, Mustafi

Everton: Pickford, Keane (Davies 45), Williams, Mangala, Kenny, Schneiderlin, Gueye, Martina, Walcott (Calvert-Lewin 60), Niasse (Tosun 77), Bolasie.

Subs: Rooney, Tosun, Sigurdsson, Holgate, Robles.

Scorers: Calvert-Lewn 64

Referee: Neil Swarbrick

Tunda amfungukia Aunt Ezekiel

Tunda Sebastian ‘Tunda’.

MUUZA nyago maarufu Bongo na mwenye visa kila kukicha Tunda Sebastian ‘Tunda’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuirudisha heshima yake aliyokuwa akiitoa kwa staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel, kama ilivyokuwa huko nyuma.
Staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel akiwa na mpenzi wake Moze Iyobo.

“ Mimi nilikuwa najua ni mwenye busara lakini hakuna kitu hivyo siwezi kumuheshimu tena hata kidogo maana zamani nilikuwa namchukulia kama dada lakini nimemvua cheo hicho kabisa kwangu hakipo,” alisema

Tunda.

Mtemela: baadhi ya Viongozi wa Kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro

Askofu mstaafu wa Kanisa Anglikana, Donald Mtetemela amesema baadhi ya viongozi wa kanisa wanaweza kuwa chanzo cha migogoro kutokana na tamaa ya mali na madaraka.

Askofu Mtetemela amesema hayo leo Jumapili Februari 4,2018 wakati ya misa ya kuwekwa wakfu na kusimikwa Askofu mteule Jackson Sosthnes wa kanisa hilo Dayosisi ya Dar es Salaam.

Amesema migogoro makanisa ni kazi ya shetani anayevuruga huduma ya Mungu ili isifanikiwe, hivyo kuwa katika hali ya hatari muda wote.

Askofu Mtetemela amesema migogoro haiwahusu waumini wa kanisa hilo pekee bali makanisa yote.

“Migogoro ni njia ya shetani ili kudhoofisha huduma ya kanisa, kazi yake ni kuingiza watu wasiofaa ili waweze kuwa viongozi. Utakuta mtu amevaa ngozi ya kondoo kumbe mbwa mwitu na wengine wanaingiza maandiko ambayo si maneno yaliyoandikwa kwenye vitabu vya dini,” amesema.

Amesema migogoro huleta chuki na roho ya kulipiza kisasi.

Amemweleza Askofu Jackson kuwa kazi yake si nyepesi, hivyo anatakiwa awe imara.

Askofu Jackson anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Valentino Mokiwa aliyeondolewa madarakani na uongozi wa juu wa kanisa hilo takriban mwaka mmoja uliopita.

Hospitali ya Aga Khan yaandaa Kampeni kuhamasisha Wananchi kupima saratani ya Utumbo



Hospitali ya Aga Khan kwa kushirikia na Mpango wa Taifa wa Damu Salama imeandaa kampeni kuhamasisha wananchi kupima saratani ya utumbo ili kujihami na ugonjwa huo.

Upimaji wa saratani ya utumbo ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya saratani duniani ambayo huadhimishwa kila Februari 4.

Akizungumza leo Jumapili Februari 4,2018 daktari bingwa wa magonjwa ya saratani wa Hospitali ya Aga Khan, Dk Harrison Chuwa amesema hospitali hiyo imeamua kuhamasisha upimaji wa ugonjwa huo baada ya kuona kuna ongezeko la wagonjwa.

Amesema ili kujua kama una ugonjwa huo, kuna kipimo ambacho kinauzwa kwenye maduka ya dawa.

"Kipimo hiki unaweza kujipima mwenyewe ukiwa nyumbani, ukibainika kuwa na saratani ya utumbo ndipo unaweza kuwaona madaktari kwa uchunguzi zaidi," amesema.

Daktari bingwa wa magonjwa ya saratani wa hospitali hiyo, Dk Aleesha Adatia amesema ugonjwa huo unatibika iwapo mgonjwa atawahi kutibiwa.

"Wagonjwa wengi huwa wanafika hospitali wakiwa wamechelewa, tunashauri watu kujipima kwa kutumia kipimo hicho angalau mara moja kila mwaka," amesema.

Kuhusu dalili, Dk Adatia amesema ni kutoka damu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuchoka na kupungua uzito.

Ofisa kutoka Mpango wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Fatma Mjungu amesema wanashirikiana na hospitali hiyo kwa kuwa kuna mahitaji makubwa ya damu kwa wagonjwa wa saratani.

"Ndiyo maana tupo hapa wakati wenzetu wanahamasisha upimaji wa saratani ya tumbo sisi tunahamasisha watu wajitolee kuchangia damu," amesema.

Amesema asilimia 25 ya damu inayokusanywa na mpango huo inatumiwa na wagonjwa wa saratani.

Amesema asilimia 42 ya damu inayokusanywa na mpango huo inatumiwa na watoto, huku asilimia 21 ikitumiwa na akina mama.

"Hivyo, ongezeko la saratani ya utumbo inasababisha matumizi makubwa ya damu, tunaomba jamii ichangie damu," amesema.

Sugu atembelewa na Wabunge wa Chadema, CUF Mahabusu



Wabunge wamefika Gereza Kuu la Ruanda jijini Mbeya kumjulia hali mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Sugu'.

Waliomtembelea Sugu ni mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema na wa Tandahimba (CUF), Katani Katani.

Sugu na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wapo mahabusu wakikabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Lema na Katani wakiongozwa na mwenyeji wao Mbunge wa  Viti Maalumu, Sophia Mwakagenda pia wamefika nyumbani kwa Desderia Mbilinyi, mama mzazi wa Sugu eneo la Sae jijini Mbeya kwa ajili ya kumfariji na kumtia moyo kutokana na misukosuko anayopitia mtoto wake.

Wakizungumza na familia ya Sugu, wabunge hao wamesema yupo gerezani kwa kuwa anapigania haki za wananchi.

Lema amemtaka mama huyo kuwa na moyo wa uvumilivu.

Shamsa Ford afunguka kuhusu ndoa yake



MSANII mwenye uwezo mkubwa anapokuwa mbele ya kamera Shamsa Ford, amefunguka kuwa kama angeamua kufuata mambo ya mjini na kujivika ustaa mwingi kama wafanyavyo wengine ingewezekana mpaka leo hii ndoa yake isingekuwepo kabisa.

Akizungumza na gazeti hili Shamsa, alisema kuwa ameamua kujishusha kabisa kwasababu anaamini kwenye ndoa hakuna ufundi wala ustaa wowote zaidi ya kujiheshimu na kutambua kuwa unapopewa heshima ya kuwa mke na wewe lazima uibebe ipasavyo.

“Siwezi kufanya ujinga wa kuichezea ndoa yangu kabisa kwani ndoa ni kitu adimu mno hivyo unapoipata lazima uilinde na kama ustaa uuache mlangoni unapoingia nyumbani la sivyo itakuwa ni shida na ndoa haiwezi kudumu,” alisema Shamsa.

Rais Magufuli asema anaposikia matatizo yametokea huwa anajiuliza akimbilie wapi

Rais Dkt. John Magufuli amesema mara zote anaposikia matatizo yametokea eneo fulani fulani huwa anajiuliza akimbilie wapi ili aweze kupata msaada wa utatuzi wa jambo hilo bila ya kuleta athari yeyote katika taifa.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Februari 04, 2018) wakati alipohudhuria hafla ya kumweka wakfu na kumsimika Mchungaji Jackson Sosthenes kuwa Askofu wa tano wa Kanisa la Anglikana Dayosis ya Dar es Salaam.

"Sisi viongozi wa serikali mara nyingi huwa tunawategemea viongozi wa makanisa na misikiti katika kutuongoza, nafahamu serikali haina dini lakini naheshimu sana dini na kuthamini mawaidha pamoja na mafundisho yanatolewa na viongozi wa dini wawe waislamu, wakristo hata wahindu tunayaheshimu sana", alisema Rais Magufuli.

Pamoja na hayo, Rais Magufuli aliendelea kwa kusema "siku zote sisi viongozi ndani ya serikali huwa tunafurahi sana kuona makanisa na misikiti ikiwa imetulia, unaposikia mahali fulani fulani kuna migogoro sisi viongozi na hasa mimi huwa najiuliza ninapopata matatizo ntakimbilia wapi. Kwa sababu makanisa na misikiti ni sehemu ya uponyaji wa roho zetu. Uponyaji wa roho ni mahali ambako kuna manufaa zaidi kuliko kwenye uponyaji wa mwili".

Kwa upande mwingine, Dkt. Magufuli amedai endapo mahali kwenye uponyaji wa mwili ukisikia kumeanza matatizo basi unapaswa kutazambua jinsi taifa unaloliongoza roho zake zitakavyopotea.

TUNDA: SIWEZI KUMUHESHIMU ANTI N’GO

Tunda Sebastian ‘Tunda’.
MUUZA nyago maarufu Bongo na mwenye visa kila kukicha Tunda Sebastian ‘Tunda’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuirudisha heshima yake aliyokuwa akiitoa kwa staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel, kama ilivyokuwa huko nyuma.
Staa maarufu wa filamu Aunt Ezekiel akiwa na mpenzi wake Moze Iyobo.
“ Mimi nilikuwa najua ni mwenye busara lakini hakuna kitu hivyo siwezi kumuheshimu tena hata kidogo maana zamani nilikuwa namchukulia kama dada lakini nimemvua cheo hicho kabisa kwangu hakipo,” alisema
Tunda.


DODOMA TENA! KAIBUKA NABII MWINGINE MPYA KAMJIBU NABII TITO! (VIDEO)


SHAMSA FORD: NINGEKUWA MZEMBE NINGESHAHARIBU

Shamsa Ford
MSANII mwenye uwezo mkubwa anapokuwa mbele ya kamera Shamsa Ford, amefunguka kuwa kama angeamua kufuata mambo ya mjini na kujivika ustaa mwingi kama wafanyavyo wengine ingewezekana mpaka leo hii ndoa yake isingekuwepo kabisa.
 
Akizungumza na gazeti hili Shamsa, alisema kuwa ameamua kujishusha kabisa kwasababu anaamini kwenye ndoa hakuna ufundi wala ustaa wowote zaidi ya kujiheshimu na kutambua kuwa unapopewa heshima ya kuwa mke na wewe lazima uibebe ipasavyo.
 
“Siwezi kufanya ujinga wa kuichezea ndoa yangu kabisa kwani ndoa ni kitu adimu mno hivyo unapoipata lazima uilinde na kama ustaa uuache mlangoni unapoingia nyumbani la sivyo itakuwa ni shida na ndoa haiwezi kudumu,” alisema Shamsa.

DIAMOND: WEMA, MOBETO NA TUNDA NI FAMILIA YANGU

Wema Sepetu.
MKURUGENZI wa lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WCB’, Diamond, amefungukia ishu yake na mastaa watatu, Wema Sepetu, Hamisa Mobeto na Tunda Sabasita.
 
Amesisitiza kuwa urafiki wao umepitiliza kiasi cha kuwa sehemu ya familia yake. Akizungumza na Spoti Xtra, Diamond alisema kwamba wasanii hao hayuko nao kimapenzi tena.

Mkurugenzi wa lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WCB’, Diamond.
“Kikubwa watu wanatakiwa watambue kwamba Wema alikuwa mpenzi wangu enzi hizo lakini kwa sasa hatuna mapenzi zaidi ya kuwa marafiki waliyopitiliza, kwani tuko kama ndugu

           Hamisa Mobeto.
“Kwa maana hiyo utagundua wazi kuwa hata huko nyuma tulikuwa tukigombanishwa zaidi na mashabiki zetu jambo ambalo sasa haliwezi kujirudia kwa sababu tumeshakua watu wazima.




Tunda Sabasita
“Suala la Tunda linasemwa sana ila ukweli ni kwamba hata yeye ni rafiki yangu mkubwa na ndiyo maana anaonekana sana katika familia yangu, suala la Mobeto lipo wazi kabisa kuwa ni mzazi mwenzangu hivyo naye atabaki kama rafiki wa karibu tu kwa kila jambo letu linapotokea.

“Pamoja na kwamba juzi hakutokea katika utambulisho wa Maromboso kwani kadi ya mwaliko tulimpa sema hakuja kutokana na kupata dharura,” alisema Diam-ond.

WASTARA AMWAGA MACHOZI AIRPOT, AKIONDOKA INDIA KUTIBIWA (VIDEO)

Msanii wa filamu za Kibongo, baada ya kuchangiwa fedha kwa ajili ya kwenda kutibiwa mguu nchini India, hatimaye leo ameondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea nje ya nchi kwa matibabu.

MZEE KINGUNGE NGOMBALE-MWIRU KUZIKWA KESHO …RATIBA IPO HAPA

Mzee Kingunge Ngombale Mwiru enzi za uhai wake.
RATIBA  ya mazishi ya aliyekuwa mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, iliyotolewa na familia yake  leo inaonyesha atazikwa kesho Jumatatu katika shughuli itakayoanza saa 9:30 hadi 11:30 katika makaburi ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo iliyotolewa na mwenyekiti wa kamati maalum ya shughuli hiyo, Omary Kimbau, inaonyesha kwamba mwili wa marehemu utatolewa leo saa 10 jioni Hospitali ya Muhimbili na kupelekwa nyumbani kwake Victoria/Makumbusho ambako ibada na mila zitafanywa usiku mzima.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, shughuli zitakazofanywa kesho ni kama ifuatavyo:
 
Jumatatu tarehe 5/2/2018
– Saa 1:00 asubuhi mpaka saa 2:00 asubuhi waombolezaji kuwasili nyumbani kwa ajili ya kuanza taratibu za mazishi.
– Saa 2:00 asubuhi mpaka saa 3:30 asubuhi kupata kifungua kinywa
– Saa 4:00 asubuhi mpaka saa 5:00 misa nyumbani kwa marehemu
– Saa 6:00 mwili kuwasili Karimjee Hall  kuagwa
– Saa 6:00 mchana 9;00 kuaga mwili wa marehemu
– Saa 9:00 alasiri mpaka 9:30 kuelekea makaburini Kinondoni
– Saa 9:30 mpaka 11:30 maziko
– Saa 11:30 jioni 12:30 kuelekea nyumbani kwa chakula cha jioni
1:30 usiku mpaka. 2:45 chakula cha usiku waombolezaji wote
3:00 usiku- waombolezaji wote hitimisho la shughuli nzima
Kingunge Ngombale-Mwiru alifariki Ijumaa wiki hii katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa amelazwa akitibiwa majeraha baada ya kuumwa na mbwa wake.

Tunda "Diamond nipo nae karibu, nionane na Zari niongee naye nini?

Tunda "Diamond nipo nae karibu, nionane na Zari niongee naye nini?

Video Vixen maarufu Bongo Tunda ambaye amekuwa akihusishwa kutoka kimapenzi na Star Diamond Platnumz, amezungumza kwenye Exclusive Interview ambapo ameongelea ishu ya yeye kudaiwa kutoka kimapenzi na Diamond huku akielezea kama Zari the Boss Lady alishawahi kumtafuta kuhusu ishu hiyo..
SHOW MORE



Wabunge wamtaka Waziri Mpango kubadili sera za Taifa



picha ya mtandao

Hali ya uchumi nchini imewaibua wabunge wakitaka Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango kubadili sera za Taifa ili kuchochea ukuaji wake.

Wakichangia taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Bunge za Bajeti; Uwekezaji na Mitaji na ile ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwa mwaka 2017 juzi, wabunge hao walisema hali hiyo inajidhihirisha kutokana na takwimu zilizotolewa na taasisi kadhaa ikiwamo Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe alisema umefika wakati kwa Wizara ya Fedha na Mipango kukubali kubadili sera za kibajeti.

Alinukuu takwimu za BoT za mwaka 2011 hadi Desemba 2017 kuwa Pato la Taifa kwa mwaka 2011 lilikua kwa asilimia 7.8 lakini sasa inakisia litakua kwa asilimia 6.8.

Mbunge huyo alisema pia mzunguko wa fedha umeshuka kutoka asilimia 22 kwa mwaka 2011 hadi asilimia 1.8 mwaka huu na ukuaji wa usafirishaji nje wa mazao hasa ya kilimo kilichoajiri watu wengi, pia umeshuka.

Bashe alisema ongezeko la idadi ya watu ni asilimia zaidi ya mbili lakini ukuaji wa kilimo ni asilimia 0.04 , hivyo hakuna muunganiko.

Alisema takwimu hizo zinatoa jibu kuwa sera za Taifa hazitoi kichocheo cha ukuaji wa biashara na uchumi katika nchi.

“Hili jambo tunaweza kusema humu ndani ya Bunge lisiufurahishe upande wa Serikali lakini tuna jukumu la kuwaambia ukweli na ni muhimu Wizara ya Fedha na Mipango ikakubali kwamba sera za Wizara ya Fedha si rafiki katika kuchochea uchumi wetu kukua,” alisema Bashe na kuongeza kuwa taarifa iliyopelekwa kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Msajili wa Hazina inaonyesha mapato ya BoT yanayotokana na biashara yameshuka kwa asilimia 63.

Alimshauri Waziri wa Fedha atakapowasilisha bungeni mpango wake wa maendeleo kwa mwaka wa fedha 2018/19 awasilishe na muundo wa namna gani Tanzania inawekeza katika uzalishaji.

Akijibu suala hilo, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema baadhi ya hatua chache zinazochukuliwa kukuza uchumi ndizo zenye matukio ya moja kwa moja lakini nyingi zinachukua muda kuona matokeo.

Alisema Serikali inachofanya sasa ni kutumia fedha nyingi za bajeti kuongeza au kuchachua miundombinu na kulipa madai ambayo yamehakikiwa.

Alisema hatua nyingine wanazochukua ni kushusha kodi katika maeneo ambayo wanahamasisha kama Taifa.

Mbunge wa Momba (Chadema), David Silinde alisema katika taarifa ya wepesi wa kufanya biashara kwa viashiria vya nchi kumi na moja ambavyo vimetolewa, Tanzania imeporomoka kwa viashiria saba.

Alichambua kipengele cha upitishaji wa shehena bandarini akisema takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ni nchi ya 180 kati ya 190 ingawa bandari ndiyo mahali pekee kunakoiingizia nchi fedha nyingi.

Alisema hali ni mbaya na katika Bandari ya Dar es Salaam kwani kuna mlundikano wa makontena ambayo yamezuiwa kwa sababu ya mgongano.

“Watu wa TBS (Shirika la Viwango) wanasema hawawezi kuruhusu makontena yatoke mpaka wapate certification kutoka TRA (Mamlaka ya Mapato). TRA wanasema hawawezi kutoa mizigo hadi wapate certification kutoka TBS unaweza kuona contradiction (mgongano) ya watu wanaofanya kazi katika Serikali moja, wanavyoshindwa kufanya kazi kwa pamoja,” alisema.

Alisema kwa kuonyesha kuwa uchumi umeendelea kuyumba, Serikali imefunga baadhi ya benki kwa utetezi kuwa wigo wake ni mdogo.

“Ukiangalia zile benki 12, benki nane zinatakiwa kufungwa kwa sababu zina - run (zinajiendesha) chini ya faida. Nilipenda Serikali iangalie hili,” alisema.

Alisema mzunguko wa fedha umepungua kwa asilimia 45 na watu hawawezi kuagiza vitu lakini bado Serikali imekuwa ikisema kuwa fedha zipo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee alisema katika bajeti zilizopita, kambi ya upinzani ilisema kitendo cha kuondoa kodi ya majengo kwenye halmashauri kwenda TRA ni kuzifanya zisiendelee.

Alisema Waziri wa Fedha na Mipango anavunja sheria kwa makusudi katika suala la kodi ya majengo kwa sababu Serikali imeshindwa kukusanya kodi na kuirejesha katika halmashauri kama sheria inavyomtaka.

“Mnatudanganya kuwa mmefanikiwa nitakupa mfano mmoja wa halmashauri yetu (Kinondoni) 2016/17 walikusanya Sh10 bilioni wakiwa na Halmashauri ya Ubungo tukawa tunapanga kuongeza mkapata tamaa mkachukua… Sasa hivi miezi sita imepita hamjaleta hata senti tano,” alisema.

Hata hivyo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji alisema wanarejesha fedha walizozikusanya kutoka na kodi ya majengo kama sheria inavyotaka.

“Tukisema kule Geita wakusanye kodi ibaki kulekule na kule Mererani wakusanye inayotokana na Tanzanite ibaki kulekule hatutakuwa na Taifa.”

Alisema bajeti ya maendeleo ya Mkoa wa Dar es Salaam ilikuwa ni Sh14.2 bilioni na wamepeleka Sh11 bilioni ambayo ni asilimia 70 kwa miezi sita lakini kodi waliyokusanya ya majengo ni Sh10 bilioni.

“Nimuulize Kinondoni walikusanya Sh10 bilioni lakini ni mradi gani wamefanya kwa kodi ya majengo? Tusilidanganye Taifa hili na tukalikatakata, ”alisema.

Alisema Mdee analidanganya Bunge na kwamba mwaka 2014/15 Kinondoni ilikusanya Sh5 bilioni lakini Serikali ilipeleka zaidi ya Sh9 bilioni kwa ajili ya maendeleo.

Ufisadi katika vitambulisho

Katika mchango mwingine, Silinde alisema mradi wa hati za kusafiria umekuwa ukitekelezwa kwa gharama za dola 40 milioni za Marekani.

“Kuna taarifa nimezipata kuwa mradi huo ulikuwa na thamani ya dola 16 milioni sawa na pauni 11 milioni. Kuna taarifa kuna kampuni ambayo ilishapewa memorandum of understanding (makubaliano ya awali) ambayo haikusainiwa hadi dakika ya mwisho lakini mwisho wa siku ilipewa kampuni ya HID,” alisema.

Alisema kampuni HID ambayo imepewa kazi hiyo wakati haijawahi kufanya kazi ya mradi wa hati za kusafiria mahali popote na imekuwa ikitengeneza kadi za ku-swap.

Silinde alisema kampuni hiyo imeingia ubia na watu ambao walikuwa Nida (Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa) wakati uliopita.

“Kwa hiyo mwenyekiti ufisadi bado upo na uchumi umeendelea kuyumba lakini watu wameendelea kufichaficha tu kwa namna fulani, kama tunapinga ufisadi lazima hatua ichukuliwe,” alisema.

Alisema taarifa walizonazo za ndani katika mradi wa hati za kusafiria, kuna ufisadi wa kutisha katika jambo hilo.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Mwigulu Nchemba alisema ufisadi hauna nafasi kwa Serikali ya Awamu ya Tano ambayo alisema iko macho.

“Taarifa alizosema si hizo, mwanzoni wakati hatua zilipokuwa zikichukuliwa kabla ya Serikali kuingilia kati ukubwa wa mradi ule na dola zilizokuwa zikihitajika kutumika ni 192 milioni,” alisema.

Alisema sehemu za mradi zilikuwa nne na gharama za dola 57.8 milioni za Marekani zitatumika kukamilisha mradi huo wa hati za kusafiria za kielektroniki.