Saturday 25 November 2017

Serikali yatoa muongoza wa upigaji chapa



Serikali kupitia wizara ya mifugo na uvuvi imetoa muongozo wa upigaji chapa mifugo kufuatia kuibuka kwa changamoto ya upigaji holela unaoharibu ngozi hali inayoweza kuifanya bidhaa hiyo kukataliwa kwenye soko la ndani na nje ya nchi

Akizungumza mjini Dodoma wakati wa utoaji elimu wa zoezi hilo, kaimu mkurugenzi wa utafiti mafunzo na ugani katika wizara ya  mifugo na uvuvi, Dk. Erastus Mosha, amesema sehemu ambayo ni salama na isiyo na madhara ya upigaji chapa katika zao la ngozi ni mguu wa nyuma kulia mwa mnyama juu kidogo ya goti wakati.

Naye afisa mifugo manispaa ya Dodoma, Kiboma John, amesema zoezi hilo linatarajiwa kufikiwa na kata 40 lakini linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo la uhaba wa fedha, vitendea kazi na rasilimali watu, na kusababisha kwenda kwa kusuasua hivyo wameiomba serikali kuisaidia manispaa katika zoezi hilo.

No comments:

Post a Comment