Thursday 8 February 2018

Kesi ya Sugu yahairishwa kwa muda

Ubishani wa kisheria umeibuka katika kesi inayowakabili Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema),  Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu wa  Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya hoja ya wakili wa washtakiwa, Peter Kibatala kutaka kuanza na shahidi wa kwanza ambaye ni Mkuu Upelelezi Mkoa wa  Mbeya, kupingwa na Jamhuri.

Mabishano kati ya pande hizo mbili yametokea leo Februari 8, 2018 na kusababisha Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite kuahirisha kesi kwa muda na kuwaita mawakili wa pande zote na kwenda nao ofisini kwake ili wakajadiliane.

Awali, Kibatala aliieleza Mahakama hiyo kwamba wapo tayari kuendelea na utoaji ushahidi na ataanza na Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO).

“Mmh! Naona kama kuna ukakasi,  eti hakimu upande wa Serikali?” amehoji hakimu Mteite.

Wakili wa Jamhuri,  Joseph Pande alisimama na kupinga kwa shahidi huyo kuwa wa kwanza huku akisisitiza  kwamba katika utetezi huo, watuhumiwa ndiyo wanaopaswa kuanza.

"Kimsingi anayetakiwa kuanza ni mtuhumiwa kujitetea na kama atakuwa na  mashahidi ndipo wataitwa hao mashahidi wake. Sasa hii itakuwa ni jambo la ajabu kutokea kama ataanza shahidi tofauti na mhusika mkuu (mshtakiwa),” amesema Pande.

Kibatala alisimama na kumpinga Pande akidai hakuna kifungu cha sheria kinachozuia kufanya hivyo na wala hakuna athari yoyote.

“Hapa tutakuwa tunapoteza muda bure. Hakuna katazo  lolote kisheria,” amesema Kibatala.

Kutokana na mabishano hayo Mteute amewaita mawakili hao kwa ajili ya kujadiliana, hivyo kuahirisha kesi hiyo kwa muda.

Sugu na Masonga wanakabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambayo wanadaiwa kuitoa Desemba 30, 2017


Wanaume Arusha wagoma kwenda kliniki na wake zao

Kampeni  ya kuwataka wanaume waongozane na wenza wao wajawazito kiliniki kwa ajili ya kupata ushauri wa kitaalamu  kuhusu afya ya uzazi sambamba na uzazi wa mpango, inaelekea kukwama katika jiji la Arusha na hivyo kutishia kinamama kukosa matibabu.

Katika kampeni hiyo  ambayo mama anayeshindwa kufika na mumewe kiliniki hunyimwa  cheti ili  kuweka mkazo suala hilo.

Kutokana na hali hiyo, suala hilo limesababisha wajawazito  jijini Arusha  kubuni mbinu mpya ya kukodi vijana kuwasindikiza hospitali.

Naibu Meya wa Jiji la Arusha ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya  madiwani wa kupambana  na Ukimwi, Viola Likindikoki alitoa taarifa hiyo juzi wakati akiwasilisha taarifa yake ya robo tatu ya mwaka uliomalizika Januari mwaka huu.

Amesema mgomo wa wanaume wengi katika jiji la Arusha, unawapa  wakati mgumu  wanawake wanaotakiwa kuambatana na waume zao kliniki kutokana na kuwakatalia hivyo kuwalazimu kukodi vijana ili mradi tu waonekane na waume zao ili wapatiwe huduma.

Amewataka viongozi wote wa ngazi ya kata na vijiji kuungana kusisitiza umuhimu wa watu wote kuhudhuria kliniki au kupima maambukizo  kwa lengo la kutambua hali halisi na kupata msaada wa haraka.

“Unajua wafadhili waliokuwa wanafadhili hizi kampeni za kutokomeza Ukimwi wengi wamejitoa, hivyo sisi viongozi tunaowawakilisha wananchi tusibweteke bali iwe chachu ya sisi kupambania maisha ya wananchi wetu.”

Akizungumza na waandishi wa habari, Diwani wa Ngarenaro, Issaya Doita amesema wanaume wengi wanakimbia kuongozana na wanawake hao kutokana na wengi siyo waume zao au wanabanwa na shughuli nyingi za kikazi

“Huu mji ni wa utalii, una pilikapilika nyingi za kusaka uchumi wa nyumbani hivyo wanaume wengi wanakwambia wana kazi nyingi hawawezi kwenda kukaa kliniki halafu jioni walale njaa, lakini sababu nyingine wanayotuambia baadhi yao si wake zao bali ni ‘mchepuko’ hivyo wanaogopa taarifa zao kuwekwa,” amesema Doita.

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athumani Kihamia amesema  watahakikisha wanawake kliniki wanakuwa na waume zao la sivyo watafuatilia taarifa zao na watakaobainika kukodi vijana wataumbuliwa.


Jaji Mkuu aionya serikali

Jaji Mkuu nchini Kenya David Maraga, ameilaumu serikali ya nchi hiyo kwa kufanya maamuzi kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi hiyo katika kukabiliana na upinzani.

Jaji Maraga ametoa kauli hiyo ikiwa imepita masaa kadhaa tokea kufukuzwa kwa mwanasheria maarufu ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshuhudia kuapishwa Raila Odinga katika viunga vya 'Uhuru Park' kufukuzwa nchini humo na kupelekwa Canada huku akiwa chini ya uangalizi wa serikali.

Katika maelezo yake Jaji Maraga, amesema malalamiko yaliyopelekwa Mahakamani yalikuwa wazi na majukumu ya kufanyia maamuzi yalikuwa ya Mahakama kutokana na kwamba ndio chombo pekee cha kutetea haki kwa kila mmoja pamoja na serikali yenyewe.

Jaji huyo ametoa tamko hilo la kuionya serikali kwa kushindwa kutii sheria kutokana na kitendo cha serikali ya Kenya kuonekana kudharau maamuzi ya mahakama


Mbosso aanza kuchekelea mafanikio WCB

Usiku wa kuamkia January 29 mwaka huu label ya WCB walimtambulisha msanii mpya ambaye ni Mbosso aliyekuwa Yamoto Band.

Licha ya Mbosso kutambulishwa usiku huu pia siku hii hiyo ndipo wimbo wake wa kwanza ‘Watakubali’ ulitoka official baada ya hapo awali kushirikishwa na WCB katika ngoma yao ya pamoja ‘Zilipendwa’.

Ikiwa ni zaidi ya wiki moja tangu wimbo huo utoke, leo February 8 umeweza kufikisha views milioni moja katika mtandao wa YouTube kitu ambacho Mbosso anasema hakuwahi kukifikiria.

“Sikuwahi kufikiria hata siku moja kama na Mimi kuna siku nitatoa wimbo wangu na ukapokelewa kwa mikono miwili kiasi hichi, ni Baraka tu za Mwenyezi Mungu na support kubwa mnayonipa wadau na mashabiki wa mziki,” amesema .

Diamond, Mobeto wamaliza fofauti zoa

Msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul maarufu Diamond amesema mazungumzo katika kesi yake Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upande wa watoto kati yake na mwanamitindo Hamisa Mobeto,  imekwenda vizuri.

“Niseme tu mambo yameenda vizuri na kama mnavyojua mambo ya mahakamani ikitokea ninahitajika nitakuja,” amesema.

Diamond alifika mahakamani hapo leo Februari 8, 2018  kusikiliza kesi inayomkabili ya matunzo ya mtoto Prince Abdul iliyofunguliwa na Mobeto.

Amesema yeye na Mobeto hawana shida yoyote, ila kuna watu waliokuwa wakizungumza maneno na kumchochea Mobeto.

"Tunahitaji kuweka mambo sawa. Tunahitaji kuwa katika mstari kwa sababu vitu vidogo vinaharibu upande wa mama na upande wa baba kwa hiyo tulikuwa tunaweka mambo sawa ili kesho na keshokutwa yasilete sintofahamu baina yetu,” amesema na Diamonda na kuongeza:

“Ikitokea kuna mtafaruku baina ya mtoto, kila mtu anakuwa na mawazo yake, kwa hiyo ni lazima kumjenga mtoto na kuhakikisha kuwa mtoto anajengwa na kulelewa  katika malezi bora.”

Alipoulizwa ni kiasi gani cha fedha anachoweza kumudu kutoa kwa ajili ya matunzo ya mtoto huyo, amesema kiasi cha fedha kinazungumzwa zaidi lakini mtoto anahitaji matunzo mengi.

"Kiasi cha pesa tunachoandika sehemu kama hizi tunazungumza tu. Mtoto ana mahitaji mengi wakati mwingine mtoto wako unaweza kumpa hata Sh100 milioni. Huwezi kusema siwezi kumpa kwa sababu niliandikisha nitampa Sh100,000. Tumeweka mazingira mazuri ya kiasi kitakachomfanya akue katika malezi bora,” amesema.

Msanii huyo amesema kupitia kesi hiyo amejifunza vitu vingi na kwamba,  mazungumzo yao ndani ya mahakama hiyo ni siri yao: “mambo yamekwisha.”

Amesema atahakikisha mtoto huyo anakuwa katika mazingira mazuri, kumsomesha kadri ya uwezo wake utakavyoruhusu kwa maelezo kuwa maisha ni kupanda na kushuka.

“Kuna wakati unakuwa hauna unasema leo mie sina basi mambo yanakuwa Bundasiliga leo mnakula mihogo maisha ndivyo yalivyo,” amesema.

Wabunge ANC wakutana kumjadili Zuma

Afrika Kusini.  Kamati ya Bunge ya Chama cha ANC (caucus) inakutana mchana huu katika kikao cha siri ambacho hata hivyo ajenda zake hazikuwekwa wazi kwa waandishi wa habari.

Kamati hiyo inakutana huku kukiwa na shinikizo linalomtaka Rais Jacob Zuma kuachia madaraka.

Duru za habari zinasema kiongozi mkuu wa ANC, Cyril Ramaphosa ndiye atayehutubia kikao cha kamati hiyo inayokutana mjini Cape Town.

Maofisa wa chama hicho hawakuwa tayari kueleza ajenda muhimu za mkutano huo wa dharura mbali ya kusisitiza kuwa ni mkutano wa ndani.

Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge hao huenda wakajadili suala la kuondoka madarakani kwa Rais Zuma na kipindi cha mpito kuelekea katika uchaguzi mkuu mwakani.

Awali, Ramaphosa amesema amekuwa akifanya  mazungumzo ya moja kwa moja na Rais Zuma kuhusiana na kipindi cha mabadiliko na masuala yanayohusu wadhifa wa rais wa nchi hiyo.

Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009 na ambaye anakabiliwa na madai ya ufisadi amekuwa na nafasi finyu ya ushawishi tangu Ramaphosa arithi nafasi ya kiongozi mkuu wa ANC.

Katika taarifa, Ramaphosa amesema yeye na Zuma wanatarajia kukamilisha mazungumzo na waifahamishe nchi kuhusiana na mazungumzo katika siku zijazo.

 Amesema mazungumzo hayo ni nafasi ya kutafuta suluhisho bila kuleta mgawanyiko nchini humo.

Wabunge ANC wakutana kumjadili Zuma

Afrika Kusini.  Kamati ya Bunge ya Chama cha ANC (caucus) inakutana mchana huu katika kikao cha siri ambacho hata hivyo ajenda zake hazikuwekwa wazi kwa waandishi wa habari.

Kamati hiyo inakutana huku kukiwa na shinikizo linalomtaka Rais Jacob Zuma kuachia madaraka.

Duru za habari zinasema kiongozi mkuu wa ANC, Cyril Ramaphosa ndiye atayehutubia kikao cha kamati hiyo inayokutana mjini Cape Town.

Maofisa wa chama hicho hawakuwa tayari kueleza ajenda muhimu za mkutano huo wa dharura mbali ya kusisitiza kuwa ni mkutano wa ndani.

Hata hivyo, taarifa zinasema wabunge hao huenda wakajadili suala la kuondoka madarakani kwa Rais Zuma na kipindi cha mpito kuelekea katika uchaguzi mkuu mwakani.

Awali, Ramaphosa amesema amekuwa akifanya  mazungumzo ya moja kwa moja na Rais Zuma kuhusiana na kipindi cha mabadiliko na masuala yanayohusu wadhifa wa rais wa nchi hiyo.

Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009 na ambaye anakabiliwa na madai ya ufisadi amekuwa na nafasi finyu ya ushawishi tangu Ramaphosa arithi nafasi ya kiongozi mkuu wa ANC.

Katika taarifa, Ramaphosa amesema yeye na Zuma wanatarajia kukamilisha mazungumzo na waifahamishe nchi kuhusiana na mazungumzo katika siku zijazo.

 Amesema mazungumzo hayo ni nafasi ya kutafuta suluhisho bila kuleta mgawanyiko nchini humo.

Tigo wapunguza gharama

Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo imepunguza gharama za kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kitaifa na kimataifa kwa asilimia 27.5.

Takwimu zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonyesha kuwapo kwa punguzo hilo katika robo ya nne ya mwaka iliyoishia Desemba 2017 ikilinganishwa na robo ya tatu ya mwaka ulioishia Septemba.

Ripoti ya robo ya tatu ilionyesha kuwa Tigo ndiyo mtandao wenye gharama kubwa Tanzania katika kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi kitaifa na kimataifa jambo ambalo limekuwa tofauti na robo ya nne ya mwaka.

Katika robo ya tatu ya mwaka wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh360 kwa dakika (kabla ya VAT) katika kupiga simu ndani ya mtandao ambayo imeshuka hadi kufikia Sh261 katika robo ya nne ya mwaka, ikiwa ni pungufu ya Sh99 sawa na asilimia 27.5.

Hata hivyo, kushuka kwa gharama za kupiga simu ndani ya mtandao katika robo ya nne, takwimu zinaonyesha kuwa  tozo za Tigo bado zipo juu ya wastani wa gharama za kupiga simu ambazo ni Sh249 kwa dakika.

Katika kupiga simu nje ya mtandao wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh480 kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imeshuka hadi kufikia Sh348 ambayo ni sawa na pungufu ya asilimia 27.5.

Licha ya kuwapo kwa punguzo hilo, tozo hiyo bado ipo juu ya wastani wa gharama za kupiga simu nje ya mtandao ambazo ni Sh329 kwa dakika.

Katika kupiga simu Afrika  mashariki wateja wa Tigo walikuwa wakilipia Sh1,022 kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imepungua hadi kufikia Sh739 katika robo ya nne ya mwaka ikiwa ni pungufu ya Sh283 sawa na asilimia 27.7.

"Kupungua kwa gharama hizo kumeifanya Kampuni ya Tigo kuwa miongoni mwa kampuni zinazotoza tozo iliyo chini ya kiwango cha wastani ya kupiga simu Afrika ya Mashariki ambayo ni Sh745 kwa dakika,"amesema.

Katika kupiga simu kimataifa, Tigo ilikuwa ikitoza Sh1,737 katika kupiga simu kwa dakika katika robo ya tatu ya mwaka ambayo imepungua hadi kufikia Sh1,258, ikiwa ni pungufu ya Sh479 sawa na asilimia 27.6.

Kupungua kwa gharama hizo kunaifanya Tigo kuwa chini ya wastani wa tozo za kupiga simu kimataifa ambayo ni Sh1,273.

Kutuma ujumbe mfupi
Katika kutuma ujumbe ndani ya mtandao, Kampuni ya Tigo imepunguza gharama hadi kufikia Sh51 katika robo ya nne ya mwaka kutoka Sh70 iliyokuwapo katika robo ya tatu ya mwaka, hiyo ni sawa na pungufu ya Sh19 sawa na asilimia 27.14.

Tozo hizo za kutuma ujumbe mfupi ziko sawa na wastani uliowekwa  wa Sh51 kwa kila ujumbe.

Katika kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kimataifa gharama imepungua hadi kufikia Sh156 katika robo ya nne ya mwaka kutoka Sh 215 ya robo ya tatu ya mwaka ikiwa ni pungufu ya Sh59 sawa na asilimia 27.4.

Gharama hizo ziko juu ya wastani wa tozo za kutuma ujumbe nje ya nchi ambayo ni Sh95.

Serikali yakiri uwepo wa mgogoro kati ya wananchi na JWTZ

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi amekiri kuwepo kwa mgogoro wa wananchi na Jeshi la Kujenga Taifa (JWTZ) eneo la Kisakasaka.

Akizungumza leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Jimbo la Dimani Juma Ally Juma aliehoji Kuna mgogoro wa  kati ya Jeshi la polisi na wananchi wa Kisakasaka hali iliyoleta  wasiwasi kwa wananchi,  Je? ni lini serikali itapatia ufumbuzi wa mgogoro huo?

“Ni kweli kwamba mgogoro huu ni wa muda mrefu nataka nimfahamishe Mh. Juma kwamba mimi binafsi nimefika eneo hilo nilifanya mazungumzo na uongozi wa kikosi pamoja na uongozi wa eneo pamoja na wananchi wa pale kulizungumza na kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi inachokwamisha kutatua sasa hivi ni suala la fedha za kupima kwasababu jeshi lilisharidhia kufanya mabadiliko ya mipaka yake ili wananchi wanaoonekana ndani ya kambi waweze kutolewa lakini   .Hata hivyo nitazungumza na Mh. Mbunge ili kumueleza zaidi ni hatua gani zinazostahili kuchukuliwa kwa mujibu wa ziara niliyoifanya pale na fedha zikipatikana,” amesema Waziri Mwinyi.

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

New AUDIO: Orezi ft. Tekno – Whine For Daddy

Orezi collaborates with Tekno on his first single of 2018 titled ‘Whine for Daddy.’ The song comes after his 2017 hit songs, ‘Hallelujah’ and ‘Cooking Pot’.

Orezi describes ‘Whine for Daddy’ as a “Sugar Daddy jam” aimed at making people dance. According to him, “I was just trying to make a record that people can dance to, just whine and Daddy will take care of you.”




Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download

Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download




Audio | Saida Karoli & Hanson Baliruno – Akatambala | Mp3 Download




Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Charly na Nina – Try me | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download

Audio | Mr Kesho – Nitakupa Love | Mp3 Download