Saturday 25 November 2017

Filamu mpya ya bollywood yazua mzozo nchini India



Filamu mpya ya Bollywood  ambayo bado haijazinduliwa imeleta kizaazaa baina ya viongozi wa juu nchini India.

Filamu hiyo kwa jina la Padmavati imepingwa vikali na wanasiasa wa chama tawala serikalini pamoja na makundi ya mrengo wa kulia hata kabla ya uzinduzi wake.

Maisha ya mtayarishaji wa filamu hiyo pamoja na waigizaji yapo hatarini kutokana na kuigizizwa kwa filamu hiyo.

Filamu inaelezea historia ya Malkia Padmavati wa dini ya kihindu wakati wa karne ya 14.

Malikia Padmavati alijichoma moto akiwa hai baada ya Mfalme Khalji ambae alikuwa ni muislamu kuwavamia na kumuua mumewe.

Waigizaji maarufu Deepika Padukone na  Ranveer Singh wamecheza kama Padmavati na Sultan Khalji.

Makundi yanayoipinga filamu hiyo yanadai kuwa filamu hiyo imebadilisha baadhi ya matukio ya kihistoria.

Hata hivyo mtayarishaji wa filamu hiyo amekana tuhuma hizo.

Baadhi ya watu kutoka katika Kabila la warajput pamoja na waumini wa kihindu wamepinga filamu hiyo kutokana na mahusiano ya kimapenzi yaliyoonyeshwa kati ya mfalme wa kiislamu na malkia wa kihindu.

Wamedai ni aibu kubwa na uvunjaji heshima kwa kabila lao.

No comments:

Post a Comment