Saturday 23 December 2017

Viongozi Wa Dini, Wanaharakati wakemea Vitendo vya Ubakaji



Dar es Salaam. Kuongezeka kwa matukio ya ubakaji na kunajisi mwaka 2017, yamewaibua viongozi wa dini na wanaharakati, wakisema jamii inachangia kwa sehemu kubwa huku wakitaka sheria na adhabu kali zitolewe kwa wahusika watakaobainika kutenda makosa hayo.
Taarifa ya usalama wa nchi ya Jeshi la Polisi iliyotolewa Desemba 20 na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Boaz inaonyesha kuwa matukio hayo yameongezeka kutoka 6,985 mwaka jana hadi 7,460 mwaka huu.
Alisema makosa dhidi ya binadamu, yanayojumuisha mauaji, kubaka, kulawati, wizi wa watoto, kutupa watoto, kunajisi pamoja na usafirishaji wa binadamu, yameongezeka kutoka 11,513 mwaka jana hadi 11,620 mwaka huu, ikiwa ni ongezeko la makosa 107.
Hata hivyo, DCI Boaz alibainisha kuwa makosa makubwa ya jinai yamepungua kutoka 68,204 mwaka jana hadi 61,794 yaliyoripotiwa katika kipindi kama hicho mwaka huu.
Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu takwimu za matukio, Askofu Msaidizi Jimbo Katoliki Bukoba mkoani Kagera, Methodius Kilaini alisema inasikitisha kuona bado kuna watu wanaendelea na vitendo vya ubakaji na kunajisi licha ya kuwepo adhabu kali.
“Sisi viongozi wa dini, kisiasa na jamii tunapaswa kukemea vitendo hivi ambavyo mara nyingi vinafanywa na watu wa karibu. Lakini kunaporipotiwa watu kutenda makosa haya adhabu kali zichukuliwe kwa haraka ili iwe funzo,” alisema Askofu Kilaini na kuongeza, “Mtoto ni malaika, unapoona mtu kamnajisi halafu unamfumbia macho kisa ni ndugu yako na mnakaa ndani ili kumaliza suala hili pembeni ni hatari, mtu anapomnajisi mtoto huyo ni shetani, hivyo jamii tukemee matendo haya kwa nguvu zote.”
Askofu Kilaini aliungwa mkono na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum akisema, “Ni jambo la kusikitisha. Elimu kwa jamii juu ya madhara haya ni ndogo, adhabu ni ndogo ila kubwa ni mmomonyoko wa maadili.”
“Mavazi ya baadhi ya watoto wa kike nayo yanachangia, uhuru wa watoto kuachwa wanacheza na wavulana hadi kufikia kumbaka, hivyo sheria iwe kali kwa atakayebainika lakini somo la maadili liongezwe nguvu kwani hadi mtu anafanya hayo anakuwa hana hofu ya Mungu.”
Katika taarifa yake, DCI Boaz anasema makosa dhidi ya maadili ya jamii nayo yalipungua kutoka 20,000 mwaka jana hadi kufikia 18,971 mwaka huu ikiwa ni sawa na pungufu ya makosa 1,029.
Akichambua taarifa hiyo ya Jeshi la Polisi, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Eda Sanga alisema ongezeko hilo limechangiwa na elimu inayotolewa ambayo imesaidia waathirika kutoa taarifa huku akiomba ushirikiano wa pamoja kumaliza tatizo hilo.
“Zamani watu walikuwa hawatoi taarifa, wakikutwa na tatizo wanakaa kimya lakini unapomuelimisha mtu anaelewa na anatoa taarifa lakini pia ukiielimisha jamii kuhusu madhara haya, inasaidia kupunguza tatizo,” alisema Sanga.
Sanga alisema kama kasi hiyo ya matukio ikiendelea hivyo mwaka 2018, siku za usoni kutakuwa na Taifa lisilokuwa na maadili hivyo viongozi wa dini, Serikali na jamii wanapaswa kukemea hili kwa nguvu zote na vitendo vyao vionekane kupinga hili.
Katibu mkuu mstaafu wa Jumuiya ya Makanisa ya Kikristo Tanzania (CCT), Leonard Mtaita alisema “Na mimi nimesikia lakini nanichoweza kusema ni siku za mwisho zimekaribia. Watu watatenda maovu na tutayaona mengi, kikubwa wamrudie Mungu na kuacha maovu.”

Viongozi 19 Wanusurika kwenda Rumande



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewanusuru viongozi 19 wa vyama vikuu vya ushirika vya mikoa ya Shinyanga (Shirecu) na Mwanza (NCU) kwenda rumande badala yake amewapa siku 23 wampe maelezo yatakayomridhisha kuhusu mahali zilipo mali za vyama hivyo viwili.
Majaliwa alifikia uamuzi huo jana wakati akifunga kikao cha wadau wa pamba alichokiitisha mkoani Shinyanga.
Viongozi hao wanatuhumiwa kwa upotevu wa mali zilizokuwa zikimilikiwa na vyama hivyo vya ushirika.
“Nataka kila mtu akaandae taarifa kuhusu mali za ushirika zilipo, au zimeenda wapi na kama mlizikopea, mseme ni wapi, lini na kwa ridhaa ya nani. Nataka maelezo ya kutosha kuniridhisha mali za ushirika zimeenda wapi,” alisema Waziri Mkuu katika taarifa iliyotolewa na ofisi yake jana.
Alisema, “Hawa nitakaowataja walipaswa kuchukuliwa na RPC, wakatoe maelezo yao na hatua dhidi yao zichukuliwe. Sasa nataka nikutane nao Dodoma Januari 15, 2018 saa 3:30 asubuhi ofisini kwangu,” alisema.
Kuhusu tuhuma za viongozi wa NCU, Waziri Mkuu alisema chama hicho kati ya mwaka 2001 na 2017, kiliuza mali kinyemela katika mazingira yenye utata na kwa bei ndogo ikilinganishwa na thamani halisi.
Aliwataja viongozi waliohusika na upotevu huo ambao wanatakiwa kutoa maelezo kuwa ni Murtazar Alloo ambaye ni mnunuzi wa maghala matatu mali ya NCU; Samson Ng’halida (mnunuzi wa New Era Oil Mills); Amos Njite Lili (mnunuzi wa ghala la Igogo); Antonia Zacharia (mnunuzi wa jengo la Kauma); Timothy Kilumile (mnunuzi wa jengo la Kauma); Robert Kisena (mnunuzi wa pili wa New Era Oil Mills); Peter Ng’hingi (aliyekuwa mjumbe wa bodi); Daniel Lugwisha (aliyekuwa mhasibu mkuu - NCU); George Makungwi (aliyekuwa ofisa miliki - NCU) na Sospeter Ndoli (aliyekuwa ofisa utumishi -NCU).
Kuhusu mali za Nyanza zinazoshikiliwa na Benki ya CRDB, Waziri Mkuu alisema benki hiyo inaidai NCU mikopo yenye thamani ya Sh2.123 bilioni na kwamba inashikilia mali 16 zenye thamani ya Sh18.132 bilioni.
Alitaka vyombo vya dola vifanye uchunguzi ili kubaini uwiano wa mikopo na mali zinazoshikiliwa na benki.
Kwa upande wa viongozi wa Shirecu, alisema wanatuhumiwa kwa upotevu wa zaidi ya Sh11 bilioni ambazo wanadaiwa na Benki ya TIB yakiwamo madeni ya mishahara ya watumishi ambayo yanafikia Sh1.2 bilioni.
“Shirecu kwa sasa haina mali zozote kwa sababu zinashikiliwa na TIB kutokana na mikopo,” alisema.
Aliwataja viongozi wa Shirecu ambao wanatakiwa kutoa maelezo kuwa ni Joseph Mihangwa (meneja mkuu); Sillu Mbogo (kaimu mhasibu mkuu); Maduhu Nkamakazi (kaimu mkaguzi wa ndani); James Kusekwa (kaimu meneja uendeshaji).
Wengine ni wajumbe wa bodi ya Shirecu Robert Mayongela (mwenyekiti); Mary Mabuga (makamu mwenyekiti); Sigu Maganda (mjumbe); Clement Bujiku (mjumbe) na Charles Lujiga.

Achomwa Moto paka Kufa baada ya kukataa kuchumbiwa



Picha ya mtu aliyevalishwa pete ya uchumba
Maafisa wa polisi katika mji wa kusini mwa India wa Hyderabad wanasema kuwa wamemkamata mwanamume mmoja baada ya mwanamke mmoja kuchomwa hadi kufa wakati wa mgogoro.
Sandhya Rani, mwenye umri wa miaka 25 alikuwa anaelekea nyumbani wakati aliposhambuliwa siku ya Alhamisi , polisi iliambia BBC.
Watu walikimbia kumsaidia bi Rani lakini alifariki akielekea hospitalini.
Mshukiwa huyo , Karthika Vanga , 28, ni mfanyikazi mwenzake wa zamani.
Alikuwa akifanya kazi katika kampuni moja na bi Rani hadi miezi michache iliopita, polisi liliambia ripota wa BBC Deepthi Bathini.
Wakati alipomkaribia siku ya Alhamisi wawili hao walionekana wakijibizana kabla ya mwanamume huyo kuchukua mafiua ya taa, na kumwagia mwilini na kumchoma moto , polisi walidai.
Walisema kuwa kulikuwa na madai kwamba bwana Vanga amekuwa akitaka kumchumbia bi Rani kwa kipindi cha miaka miwili.
Alikuwa amekataa mara kadhaa kuchumbiwa na bwana huyo ijapokuwa polisi wanasema haijulikani iwapo kulikuwa na malalamishi dhidi ya mtu huyo.
Mashambulizi dhidi ya wanawake nchini India yameongezeka tangu ubakaji wa gengi la mwaka 2012 na mauaji ya mwanafunzi katika basi moja mjini Delhi, na yamesababisha kuwekwa kwa sheria kali zinazolenga kukabiliana na mashambulio kama hayo.

Mwalimu atiwa Mbaroni Kwa kubaka wanafunzi wake



Mwalimu mbaroni akidaiwa kubaka wanafunzi wake tisa
MWALIMU wa Shule ya Msingi Itiryo, Samweli Bisendo (29), amekamatwa na jeshi la polisi akituhumiwa kubaka wanafunzi tisa wa shule yake iliyopo wilayani Tarime.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe, alisema kuwa mwalimu huyo anadaiwa kutenda unyama huo kwa nyakati tofauti hadi alipobainika.
"Jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mwalimu wa shule ya msingi Itiryo, Samweli Mariba Bisendo (29) kwa tuhuma ya kubaka watoto wapatao tisa ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi Itiryo,” alisema Kamanda Mwaibambe na kuongeza kuwa matukio hayo yalifanyika kati ya Novemba 30 na Desemba 6,mwaka huu.
“Alikamatwa wakati akiwa anajiandaa kutorokea nchi jirani ya Kenya," alisema Mwaibambe.
Aidha, Mwaibambe alipongeza ushirikiano kutoka kwa wananchi ambao ndiyo waliowezesha jitihada za polisi kuzaa matunda katika kumkamata mwalimu huyo.
"Pia mwalimu huyo, bila aibu, aliwafanyia matukio ya unyanyasaji wa kijinsia wanafunzi wengine watatu wa shule ya msingi Itiryo," alisema Mwaibambe.
Kamanda huyo alitoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa kwa vyombo vya dola pale wanapobaini kuwapo kwa uvunjaji wa hseria za nchi ili watuhumiwa wakamatwe na sheria kutwaa mkondo wake.

Watu 22 wahofiwa kufa maji na 115 kuokolewa Ziwa Tanganyika



Watu 22 wanahofiwa kufa maji katika Ziwa Tanganyika katika ajali ya boti iliyotokea iliotokea leo alfajiri.
Imeelezwa miili ya watu wanne imeopolewa na imetambuliwa na ndugu zao huku watu wengine 115 wameokolewa wakiwa hai baada ya boti kugonga mtumbwi.
Ofisa wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) Mkoa wa Kigoma, Amaniel Sekulu amesema ajali hiyo imetokea katika kitongoji cha Lubengela kijijini Msihezi, Kata ya Sunuka wilayani Uvinza.
Amesema mtumbwi uitwao Mv Pasaka uligongwa ubavuni na boti ya Atakalo Mola na kupasuka, hivyo kuzama ziwani.
Sekulu amesema mtumbwi ulikuwa umebeba abiria 137 waliokuwa wanakwenda kwenye mkutano wa injili katika Kijiji cha Sunuka.
Amesema boti ilikuwa ikitokea Kigoma kwenda Kalya ikiwa imebeba abiria 65.
Sekulu amesema boti na mitumbwi inayobeba abiria hairuhusu kufanya safari usiku.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Sweetbert Njewike akizungumzia ajali hiyo amesema wanaendelea kuwatafuta watu ambao hawajaonekana waliokuwa wakisafiri na vyombo hivyo.
Amesema shughuli za uokoaji zinafanywa kwa pamoja na vikosi vya Polisi, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Mwanamvua Mrindoko amesema uchunguzi wa awali unaonyesha kulikuwa na dosari zilizosababisha ajali hiyo.
Amezitaja dosari hizo kuwa ni ukosefu wa vifaa vya uokoaji, vifaa vya kuzima moto na boti kufanya safari usiku.
Diwani wa Sunuka, Athumani Chuma amesema ajali hiyo imeacha simanzi kutokana na mazingira iliyotokea.
Amesema licha ya ajali kutokea saa tisa usiku, wanakijiji wameonyesha mshikamano katika kuokoa watu wakiwa hai na hatimaye kuopoa maiti nne.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Msihezi, George Gasper amesema ajali ilitokea umbali wa mita takriban 150 kutoka ufukweni, ikiwa ni muda mfupi baada ya boti la Atakalo Mola kushusha na kupakia abiria katika Kitongoji cha Lubengela.
Desemba 20, watu saba walikufa papohapo na wengine 12 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Saratoga kugongana uso kwa uso na gari ndogo la abiria.
Ajali hiyo imetokea saa 4:30 asubuhi katika Kijiji cha Kabeba katani Mwakizega wilayani Uvinza.

Hamisa Mobetto Na Zari Warushiana Vijembe



Usiku wa kuamkia leo kwenye jiji la Kampala Uganda kulifanyika Party mbili ambapo moja Hamisa Mobetto alihudhuria inaitwa Gal Power na nyingine ni ya Zari All White Party.
Sasa baada ya kumalizika kwa party hizo maneno ya Mashabiki yakaanza wengine wakiponda ya Zari na wengine wakiponda ya Hamisa kwamba ilikua na watu wachache.
Wao wenyewe wameandika vitu kwenye Snapchat zao na ikaonekana kama ni vijembe ambapo Zari ndio alianza kwa kuandika “Kuna tofauti kati ya Tembo na Mbu” ambapo Hamisa alijibu kwa kuandika “Tembo hana madhara sana kwa Binadamu ila mbu….. kila siku watu wanalazwa”

Haji Manara; kitendo cha Klabu yangu kufungwa kwa penanti ni aibu ya mwaka



Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Klabu ya Simba SC, Haji Manara amefunguka na kusema kitendo cha klabu yake ya Simba jana kufungwa kwa njia ya penati na kuondolewa kwenye michuano ya Azam Sports Federation Cup ni aibu ya mwaka.
Haji Manara alisema hayo jana baada ya waliokuwa mabingwa watetezi wa (Azam Sports Federation Cup) Simba kupigwa na Green Warriors na kuondolewa katika michuano hiyo kwa penati 4-3
"Shame!! Aibu!!!Fedheha!!! Haivumiliki!!!Tumewakera fans wetu zaidi ya twenty millions... nimeumia kuliko siku zote toka nimeanza kazi Simba..Aibu ya mwaka" aliandika Haji Manara

Mtoto aliyefanyiwa upasuaji mara 10 aomba msaada kunusuru maisha yake




Uzinduzi wa kampeni ya Tuko Pamoja, Okoa Maisha ya Mariam imezinduliwa leo jijini Dar es salam huku ikilenga kuarifu Umma wakiwemo wadau kupitia vyombo mbalimbali vya habari kuhusu msichana mdogo Mariam (16) anayesumbuliwa na ugonjwa ujulikanao kama ”Intestinal Obstruction”.
Akizungumza na waandishi wa habari mkurugenzi masoko wa DataVision International, ambaye pia ni Msemaji wa Dar24, Teddy Ntemi Qirtu katika ukumbi wa Serena amesema kuwa uzinduzi huo unalenga kuokoa maisha ya Mariamu na kuwaomba watanzania kwa ujumla kuhusika katika kampeni hiyo kwa kuchangia kwa namna moja au nyingine ili pamoja kuokoa maisha ya msichana huyo.
Aidha Qirtu amewaomba wananchi na wadau kwa ujumla kumchangia mtoto Mariam ili aweze kwenda nchini India kufanyiwa matibabu, mara baada ya jitihada za madaktari bingwa kutoka hospitali mbalimbali hapa nchini ikiwemo Muhimbili kushindwa kutatua tatizo hilo na kupelekea kumfanyia oparesheni kumi bila mafanikio.
''Gharama za kuratibu shughuli nzima ya matibabu hayo akiwa nchini India ni kiasi cha shilingi milioni 44 za kitanzania'' alisema
Hivyo amewaomba wananchi kuungana na Dar24 kupigania maisha ya Mariam kwa kuchangia fedha kupitia M-lipa, tigo pesa, Airtell Money na Mpesa kwa kuandika namba ya kampuni 400700 na kumbukumbu namba 400700 au kupitia akaunti ya benki ya CRDB kwa akaunti namba 0150021209500 jina la akaunti ni Data Vision International – Tuko Pamoja.
Kupitia vyomba mbalimbali vya habari amewashukuru wale ambao tayari wamekwisha wasilisha michango yao kupitia mfumo maalumu wa M-lipa kama ambavyo imeelekezwa na kuwaomba wadau kuendelea kuchangia kampeni hiyo inayolenga kuokoa maisha ya Mariam ambae kwa sasa anashindwa kuendelea na masomo.

Vigezo anavyotumia mwanamke kupenda



Watu wengu hujisikia vizuri wanapowavutia wenzao wa jinsia nyingine. Je, unafikiri ni kitu gani kinachomfanya mwanamke aonekane wa kuvutia?
Kuna vitu vingi vinavyojulikana vizuri zaidi kwa upande wa mwanamke kama vile; mwili mzuri, sauti yenye mvuto, nywele, mikono mizuri na mengineyo mengi. Lakini, kuna vingine ambavyo siyo vya kawaida vinavyohusu mwanaume kumvutia mwanamke.
Je, ni vitu au mambo gani ya kipekee ambayo, humfanya mwanamke aguswe na mwanaume fulani na huku mwanamke mwingine akishangaa ni kwa nini mwanamke mwenzake ameguswa sana na huyo jamaa?
Inawezekana yapo mengi ambayo, huyajui. Kwa mfano, mwanamke anaweza akavutiwa na jina la kwanza au la ukoo la mwananume fulani. Hapa mwanamke hufikiri kwamba, huyo mwenye hilo jina hawezi kuwa mtu wa kawaida, na kila kitu anachofanya ni lazima kiwe cha ajabu.
Labda ni kutokana na jina hilo kuwa ni la kigeni au anatoka kwenye ukoo ambao ni bora au wa kipekee au anafikiri labda huyo mwanaume atamwezesha kile ambacho, mara nyingi amekuwa hakipati.
Lakini, inawezekana kabisa kwamba, mwanamume huyo si mzuri sana wa kuvutia au ni mbaya sana kuliko wengine. Hakuna anayejua, labda anachotaka mwanamke huyo ni kujaribu bahati yake ili aone kitakachotokea kwa uhakika ziadi.
Inawezekana pia kuwa, mwanamke anaweza kuchanganyikiwa zaidi baada ya kuona umbo la mwanamume huyo au gari lake. Pengine mambo hayo ndiyo ambayo, amekuwa akiyapenda zaidi. Inawezekana ikawa ni dalili ya bahati kwake kwamba, ametokea katika maisha yake mtu ambae, kwa muda mrefu amekuwa akitamani kumpata.
Upo uwezekano pia kwamba, mwanamke akavutiwa na mwandiko au sahihi ya mwanamume fulani. Wakati mwingine mwanamke hutokea kuwa na uhakika zaidi na kuamini yale anayoambiwa kuhusu tabia ya mwanaume huyo, bila hata kufanya uchunguzi wa kina. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, upo uwezekano wa kuisoma tabia ya mwanaume huyo kwenye sahihi au mwandiko wake.
Mwanamke pia huvutiwa na lafudhi ya mwanamume, fani yake, hobi, na kitu kingine kisicho cha kawaida ambacho mwanamume huyo anakipenda na kukifanya. Hata hivyo, mwanamke anatakiwa awe mwangalifu mno na upande wa pili wa mtu huyo ambao, yeye haujui. Hapa ikiwa na maana kuwa , pamoja na sifa zote hizo alizozibaini kutoka kwake, anapaswa kujua kwamba, mwanamume huyo kama binadamu asiyekamilika pia ana mapungufu na udhaifu mwingi.
Kuufahamu ukweli huu, kutamsaidia katika kuimarisha zaidi na kumfanya awe makini anapotafuta mwanaume wa kuishi naye. Na akumbuke kuwa, wapo wanaume ambao huficha makucha yao au kasoro zao kwa wapenzi wao.
Kuna mwanamke mwingine hupenda mwanaume mwenye vituko, kilema au mwenye kasoro nyingine za kimwili. Yote hayo hutokana na asili ya mwanamke. Na ni mambo yanayoongea ndani mwake kwamba, anataka kumjali na kumhurumia mwanaume huyo.
Kwa kawaida, mwanamke huvutiwa zaidi na kwa urahisi, pale mwanaume anapoonyesha tabia ya usikivu na utulivu. Hata hivyo, mtazamo huu kwa upande wa mwanamke, huhesabika kuwa ni ushindi kwake.
Hali kadhalika, mwanamke huvutiwa na tabia fulani ya kipekee ambayo, mwanaume anayo. Kwa mfano, jinsi mwanaume huo anavyoutumia mkono wake wa kushoto, kwani watu wengi wanatumia mkono wa kulia. Ukweli ni kwamba, labda huyo ndiye mwanaume ambae mwanamke huyo anamtaka, kwani pia wanawake wengine hawawezi kujizuia kuwapenda wanaume wenye macho ya bluu. Hilo pia ni jambo la kawaida.
Mwanamke anaweza kumpenda mwanaume kutokana na jinsi anavyofanya kazi za nguvu au kutokana na mwili wake kuwa na misuli. Ni jambo la kawaida kwa wanawake kufurahia wanaume waliojazia, na inavyoonekana wanawake huwaona wanaume ambao ni lainilaini kuwa wana haiba ya kike au ni mashoga.
Hapo ndipo mwanamke anapolazimika kufikiria kwa makini, kuhusu mwanaume anayetumia muda mwingi kujipodoa na fedha nyingi kwa mambo ya urembo na vipodozi kuliko hata mwanamke, kama kweli anamvutia na anamfaa.
Na kitu kingine ni kwamba, mwanamke humpenda mwanaume anayesaidia kufanya kazi za nyumbani. Kwa kufanya hivyo, mwanamke huamini kwamba, mwanaume huo anamjali na kumthamni.
Kwa kumalizia ni kwamba, mambo mengi yanayomchanganya mwanamke kuhusiana na mwanaume anayemtaka, kwa kweli ni ya kipekee sana na wakati mwingine huonekana kuwa ni kituko, ingawa wakati mwingine yanaweza yakaeleweka vizuri. Mara nyingi vigezo hivyo huonekana kuwa sahihi, iwapo tu mwanamke huyo atajisikia vizuri na kupata ridhiko la nafsi yake.

Friday 22 December 2017

Tanzania yapolomoka katika viwango vya FIFA



TANZANIA imezidi kuporomoka katika viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ambapo hivi sasa inashika nafasi ya 147 kutoka 142 ya mwezi Oktoba.
Jana Alhamisi, Fifa ilitoa viwango hivyo ambapo inaonyesha ndani ya miezi mitano kuanzia Julai, mwaka huu, Tanzania imeshuka kwa jumla ya nafasi 33.
Ikumbukwe kuwa, kwa siku za hivi karibuni, Tanzania ilifanya vizuri kwenye viwango vya Juni baada ya kushika nafasi ya 114 kutoka nafasi ya 139 ya mwezi Mei. Baada ya hapo, Julai ikashika nafasi ya 120, Agosti 125, Septemba 136, Oktoba 142 na sasa Novemba ni 147.
Kushuka huko kwa Tanzania kunatokana na Novemba, mwaka huu, Taifa Stars kutoka sare ya bao 1-1 na Benin katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye Uwanja wa l’Amitie, Benin.
Katika 10 Bora ya duniani, Ujerumani inaongoza ikifuatiwa na Brazil, Ureno, Argentina, Ubelgiji, Hispania, Poland, Uswisi, Ufaransa na Chile.

Waziri Kigwangalla kuwakutanisha Joketi Na Wema Sepetu





Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk.Hamisi Kigwangalla jana Desemba 21, 2017 aliteua majina mengine ya Kamati ya Kitaifa ya kuandaa mwezi maalum wa maadhimisho ya Urithi wa Tanzania. Miongoni mwa wajumbe walioteuliwa ni makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jokate Mwegelo na Wema Sepetu ambao wataungana na wajumbe 23 aliowateua awali kuunda Kamati ya Kitaifa ya Kuandaa Mwezi Maalumu wa Maadhimisho ya Urithi wa Tanzania.

Mashindano Ya Miss Tanzania kutokuwepo 2017



WAANDAAJI wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, Kampuni ya Lino International Agency Limited, wamesema kwamba hakutakuwa na Fainali za Taifa za shindano la Miss Tanzania kwa mwaka 2017.
Katika taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo imeeleza kuwa sababu kubwa ya kuahirishwa kwa shindano hilo ni ukosefu wa Wadhamini ambao kwa njia moja au nyingine huwezesha kufanyika kwa mashindano hayo kwa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo zawadi za washiriki.
Aidha waandaaji hao pia wamesema kuwa kuchelewa kupata kibali cha kuanza mchakato wa Miss Tanzania 2017, ambacho kilitolewa na BASATA mwezi Septemba mwaka huu pia kimechangia kukosa kwasababu muda ulikuwa umeshaenda.
Mashindano ya kutafuta warembo wa Miss Tanzania yamekuwa yakifanyika kila mwaka na baadae kuibua mastaa mbalimbali kama Wema Sepetu, Lulu Diva, Jokate Mwegelo na wengine 

Thursday 21 December 2017

Orodha ya mastaa BONGO waliopata watoto mwaka huu 2017




Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto
MWAKA 2017 ndiyo huo unayoyoma na zimebaki siku kumi tu kuingia mwaka 2018. Mwaka 2007, mengi yametokea kwa kila mtu katika maisha yake ya kawaida.
Wapo waliofanikiwa, waliofeli na wapendwa wetu wengine walitutoka kabisa. Kama ilivyo kwenye maisha ya kawaida kuwa na mengi yaliyotokea, vivyo hivyo kwenye ulimwengu wa burudani. Ukiachana na kiki zilizotikisa, matukio ya kuvutia na mengine mengi mazuri na mabaya tumeyashuhudia kwa staa mmojammoja.Miongoni mwa hayo mazuri ni kwa baadhi ya mastaa wa kike ambao walihabatika kuitwa mama kama ifuatavyo;
Muigizaji Faiza Ally akiwa na mtoto wake Lil Junior
MAMA KAIRO (HAPPINESS MILLEN MAGESE):
Mwishoni mwa Julai, mwaka huu, baada ya kutafuta mtoto kwa muda mrefu, mwanamitindo maarufu wa kimataifa, Happiness Millen Magese ‘Ladiva Millen’ alijibiwa kilio chake na Mungu wake.
Millen alijaliwa mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Kairo Michael Magese. Kupitia ukurasa wake wa Mtandao wa Instagram, Millen alionesha furaha yake kwa kuandika ujumbe matata ambapo pia alifafanua jina la mtoto wake huyo la Kairo kwamba, linamaanisha ‘utukufu kwa Mungu.’
MAMA JADEN (CHUCHU HANS):
Uhusiano wake na muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ ulianza kama siri. Ghafla, muigizaji Chuchu Hans ni mjamzito. Baadaye mambo yalikuwa wazi hasa Mwezi Januari, Chuchu alipojifungua mtoto wa kiume ambaye yeye na mpenzi wake, Ray walimpa jina la Jaden.
MAMA GOLD (AIKA):
Baada ya kudumu kwenye uhusiano kwa zaidi ya miaka nane, Aika na mpenzi wake, Nahreel, mwanzoni mwa Mwezi Desemba walibahatika kupata mtoto wa kiume ambaye
walimpa jina la Gold.
MAMA PRINCE ABDUL (HAMISA MOBETO);
Mwanamitindo wa kimataifa, Hamisa Mobeto naye anaingia kwenye orodha hii baada ya Mwezi Agosti, mwaka huu kupata mtoto wa kiume aliyempa jina la Prince Abdul. Kwa Hamisa, huyu ni mtoto wa pili kufuatia awali kupata mtoto wa kike aitwaye Fantas.
MAMA CLARIBELL (ESHA BUHETI);
Wakati ikiwa imepita siku moja tu baada ya mwanamitindo Hamisa Mobeto kupata mtoto wa kiume, muigizaji Esha Buheti naye alibahatika kupata mtoto
wa kike ambaye alimpa jina la Claribell. Kama ilivyo kwa Hamisa, kwa Esha pia huyo naye ni mtoto wake wa pili. Mtoto wa kwanza anaitwa Clarisa.
MAMA LIL JUNIOR (FAIZA ALLY);
Muigizaji Faiza Ally naye yumo kwenye orodha hii. Mwaka 2017, kwake umekuwa na mafanikio mengi ikiwemo kupata mtoto wa kiume ambaye amemuita Lil Junior. Naye ni mtoto wake wa pili baada ya Sasha aliyezaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’. Wengine waliopata watoto kwa mwaka 2017 ni pamoja na staa wa Bongo Fleva, Estarlina Sanga ‘Linah’ Khadija Nito na muigizaji Welu Sengo.

Shilole afunguka kuhusu ndoa yake



STAA wa miondoko ya mduara, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ amefunguka kuwa, watu wasimfikirie ameamua kuingia kwenye ndoa kama maonyesho bali amedhamiria kwenda kuwa mke anayestahili kuwa mfano wa kuigwa.
Mrembo huyo anayesumbua na wimbo wa Hatutoi Kiki, alisema kuwa anajua wazi watu wengi wanamuhesabia siku za uhusiano wao kuvunjika kama ilivyo kwa mastaa wengine, lakini kwa jinsi alivyodhamiria kutulia kwenye ndoa atawashangaza walimwengu.
“Najua wazi watu watakuwa wananihesabia siku ndani ya ndoa yangu lakini ukweli ni kwamba nitawashangaza watu wengi na sina sababu ya kuacha kuwa mke bora na mwenye heshima kwa
mume,” alisema

Ben Pol awataka wasanii Wa bongo kuacha uvivu



Msanii wa kiume wa bongo fleva Ben Pol, amewataka wasanii wenzake kuacha uvivu na kufanya kazi kwa bidii, kwani licha ya sanaa kuwahitaji, pia wana majukumu ya kutimiza.
Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Ben Pol amesema wao kama wasanii wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii, kwani kuna watu wanawategemea, ikiwemo familia zao na mashabiki wao.
“Niwaambie wasanii wenzangu tuache uvivu hii ni kazi yetu, familia zinatutegemea, tuna-teams ambazo zinaishi kupitia sisi, tuna mashabiki wanatuangalia, turudi studio turudi studio tutoe albam, kama kuna changamoto tutakabiliana nazo mbele kwa mbele”, amesema Ben Pol.
Ben Pol hakuishia hapo aliendelea kwa kuitaka serikali kuhakikisha wanasimamia ipasavyo kazi zao za sanaa, kwani na wao tayari wameshaanza kuchangia pato la serikali kwa kukatwa kodi.
“Tushaanza kulipwa kodi, kwenye shows tunakatwa, mtu anakuja pale mlangoni na mashine, kwa hiyo na wao serikali watusaidie kwenye biashara yetu”, amesema Ben Pol.
Ifahamike kwamba Ben Pol ni miongoni mwa wasanii wachache ambao mwaka huu wameachia albam, kitendo ambacho wasanii wengi wanakiogopa.

Wednesday 20 December 2017

Diwani CHADEMA Ajiuzulu na Kujiunga CCM



KILIMANJARO: Diwani wa Donyomurwak kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Siha mkoani Kilimanjaro, Lwite Ndossi amejiuzulu nafasi yake na kujivua uanachama wake katika chama hicho na kijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole amethibitisha hilo na kusema kuwa wamempokea diwani huyo ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kupoteza baadhi ya viongozi wake katika ngazi mbalimbali ambao wamekuwa wakijiuzulu nafasi zao na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kile wanachosema wanaunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuli na Serikali yake.

Kamati Ya Ushauri Wa Mazingira Yazindiliwa



Serikali imezindua kamati ya Taifa ya ushauri wa mazingira ambayo itakuwa ikijihusisha na uchunguzi wa masuala yanayohusu kulinda mazingira na kupendekeza hatua za kuchukua.
Akizungumza jana katika uzinduzi huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba alisema kamati hiyo inayoundwa na wataalamu kutoka sekta mbalimbali ina mchango wa kutatua changamoto za mazingira bila kuwa na misigano. “Yote hayo ni kumjengea uwezo waziri mwenye dhamana ya mazingira ili katika kutekeleza majukumu yake awe na imput za kitaalamu,” alisema.
Katibu mkuu wa wizara hiyo, Joseph Malongo alisema kamati hiyo imeanzishwa kwa mujibu wa sheria na kwamba wananchi wanapaswa kujua na kuzingatia umuhimu wa mazingira katika kila jambo.

Vyama Vya Upinzani Vyamkosoa Mzee Makamba



Baadhi ya vyama vya upinzani vimekosoa kauli iliyotolewa juzi na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba vikisema imelenga kudhoofisha upinzani nchini.
Juzi, akihutubia Mkutano wa Mkuu wa CCM, Makamba alisema Rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa ‘anabatiza’ kwa maji, lakini Rais John Magufuli anafanya hivyo kwa moto na mfano mzuri ni uchaguzi wa marudio wa kata 43 ambao CCM ilizoa viti 42.
“Huu si ubatizo wa moto? Kazi tunayoifanya leo ni kuchagua kocha ambaye ni wewe (Rais Magufuli), kocha msaidizi Mangula (Philip) na Dk Shein (Ali Mohamed). Kama haitoshi unatakiwa uchague dawati la ufundi Kamati Kuu, sasa wenzangu wajue nimlisikia rafiki mmoja alikwenda kwa jimbo la Mnyika (John) na kusema 2020 njia nyeupe,” alisema mwanasiasa huyo.
“Njia nyeupe kwa utaratibu huu, kwa matokeo haya na ubatizo huu wa moto 2020 mshindi ni CCM we’ lala. Naomba mniruhusu niwaambie kina Mrema (Lyatonga), ubatizo ni uleule na leo sitaki kutabiri.Natabiri 2020 mheshimiwa Lowassa (Edward), Mbowe (Freeman) na Mapesa (John Cheyo ), John Shibuda wajue njia si nyepesi.”
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema hakutarajia kama Makamba angetoa kauli hiyo kutokana na alichodai kuwa ni kuminywa kwa demokrasia nchini.
Alisema kinachofanyika sasa dhidi ya wapinzani ni sawa na refa anayechezesha mpira wa miguu kuwapa kadi nyekundu wachezaji wote wa timu husika, halafu timu nyingine inaendelea kucheza.
Naibu Katibu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema kauli hiyo haileti picha nzuri kwa siasa.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alisema Makamba yupo sahihi na upinzani unabidi kufanya kazi ya ziada kama wanataka kushinda 2020.
“Tulikosea na tulichelewa kuunda upinzani, mwaka 1995 tulikuwa na nafasi nzuri sana ya kuungana kwa sababu hakukuwa na rais kama Magufuli, lakini sasa hivi yupo na sisi wapinzani tusipobadilika na siasa zetu za kususa watatuchapa kweli 2020,” alisema Mrema.
Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen-Kijo Bisimba alisema Makamba alisema ukweli kutokana na hali na mazingira ya siasa nchini.

Wanaochakachua Pesa Za Tasaf waonywa



KAIMU Katibu Tawala Mkoa wa Tabora, Natalis Linuma, ameiomba serikali kusaidia vijiji ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika mkoa na vijiji.
Aliyasema hayo wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tasaf III kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika.
Linuma alisema vijiji vingi ambavyo havijaingizwa kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini, watu wake wana hali duni na baadhi wameachwa na watoto yatima.
Aidha, alisema kutokana na kaya hizo kutoingizwa katika mpango huo, kumesababisha malalamiko.Linuma alimwambia Waziri Mkuchika kuwa kaya 953ziliondolewa wakati wa uhakiki wa kubaini kaya zisizokuwa nasifa.
Alisema, Mkoa wa Tabora una jumla ya wilaya saba na tarafa 19, kata 174 na vijiji 696, mitaa148 ambayo mpango huo unatekeleza uhawilishaji katika kaya zenye sifa.
Lengo lilikuwa ni utambuzi na uandikishwaji wa kaya 52,558 na kaya 47,805 ziliandikishwa, kuanzia mwezi Agosti 2017.
Aidha, jumla ya Sh. 20,038,121.000 zilihawilishwa kwa walengwa 39,293.
Katika halmashauri zote za mkoa wa Tabora, mpango wa kunusuru kaya maskini umesaidia kuwapatia elimu watoto wenye wazazi wasio na uwezo.
Waziri Mkuchika alisema amepokea taarifa hiyo, lakini alipata fununu kuwa kuna baadhi ya viongozi wasio waaminifu.
Mkuchika alisema kuwa taarifa alizozipata ni baadhi ya viongozi kuomba rushwa na kuwaonya wakiendelea na tabia hiyo watakiona cha mtemakuni.

Hamisa Mobeto Anasa kwenye mtego Wa Zari



Mwanamitindo Hamisa Mobeto.
Mwanamitindo Hamisa Mobeto anadaiwa kunasa mtegoni baada ya ‘kuuvaa mkenge’ ulioratibiwa na hasimu wake wa siku za hivi karibuni, Zarinah Hassan ‘Zari’.
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na Zari, inadaiwa kuwa mjasiriamali huyo alimtumia mtu aitwaye William Bugeme ambaye pia ana ukaribu naye wa damu, ili aweze kumchukua mwanamitindo huyo, ambaye amezaa na baba wa watoto wake wawili.
Inadaiwa lengo la Zari ni kuona wawili hao wakiwa karibu, basi ni dhahiri kuwa ukaribu kati ya Hamisa na baba watoto wake utaisha, kwani uhusiano wa kimapenzi na William hauwezi kukubalika.
“Mnajua kuwa huyo Hamisa amenasa kwa Bugeme lakini hajui kuwa huo ni mpango wa Zari ili amtoe kwa baba mtoto wake, asipoangalia atatumika tu kisha atabwagwa kwani jamaa yupo kimaslahi zaidi kwa ajili ya kuokoa penzi la dada yake,” alisema Sosi huyo.
Kwa mujibu wa sosi huyo, picha za wawili hao wakiwa katika pozi tofauti zilinaswa hivi karibuni zikiwa zimerushwa mtandaoni.
Zarinah Hassan ‘Zari’
Sosi huyo alikwenda mbali zaidi na kuvujisha siri ya Zari kuwa ndiye anayemtuma ndugu yake huyo ili akifanikisha kuwa naye kimapenzi itakuwa rahisi kuachana na baba wa watoto wake.
Hata hivyo sosi huyo alidai fungu kubwa na zuri limeandaliwa kuhakikisha Hamisa hakwepi mtego huo.
“Mwanamke ni mjanja sana sana haongei ni pesa ndio inaongea, Bugeme toka zamani anafahamiana na Hamisa sasa ameamua kumtumia huyo huyo ili kuumaliza mchezo wake kabisa, unadhani mzazi mwenzake akiona ameingia kwenye penzi na Bugeme ataendelea naye, amecheza kwelikweli,” kilitiririka chanzo.
Risasi Jumatano lilimtafuta hewani Hamisa ili azungumzie sakata hilo kama ameshalifahamu au anajipanga vipi, lakini pia kuzungumzia picha zake zinazomuonesha akiwa na kaka huyo, lakini alipopokea simu yake alisikiliza madai yote kisha akakata simu.

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download

Video | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp4 Download



DOWNLOAD

Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download


Audio | Rayvanny ft Maphorisa x Dj Buckz – Makulusa | Mp3 Download






Dalili Tano za Tezi Dume



Ugonjwa wa tezi tume imeelezwa ya kwamba ni miongoni mwa magonjwa ambayo yanasumbua jamii yetu kwa kiwango kikubwa sana na hata kupelekea kusababisha vifo.
Hata hivyo tafiti mbalimbali zinazidi kuonesha ya kwamba wanaume ambao wanatumia pombe kali kwa kiwango kikubwa wapo hatarini kupata ugonjwa huo. Licha ya wanywaji wa pombe kali lakini inasadikika ya kwamba wanaume ambao wanafanya kazi za viwandani, husasani viwanda vya rangi au wanaofanya kazi ya kupaka rangi wapo hatarini kupata ugonjwa huo.
Lakini pia wanaume ambao wapo hatarini kupata ugonjwa huo ni pamoja na wanaume wenye historia ya tatizo hili wenye familia zao, yaani wale ambao mmoja wa ndugu zake (kaka au mdogo wa kiume) au baba kama amewahi ugua ugonjwa huu.
Lakini pia watalamu mbalimbali wa masuala ya afya, wanazidi kueleza ya kwamba wanaume wenye umri wa kati ya miaka 40-70 wapo hatarini kupata ugonjwa huu wa tezi dumi.
Lakini licha ya kuendelea kusambaa kwa kasi kwa ugonjwa huu watalamu wa afya wanaeleza ya kwamba endapo ugonjwa huu wa tezi tume utaweza kutambulika mapema unaweza kutibika.
Dalili za ugonjwa wa saratani dume.
Katika hatua zake za awali, dalili za saratani ya tezi dum hazitofautiani na zile za kuvimba kwa tezi dume (BPH). Dalili hizo ni pamoja na
1. Kukojoa mkojo uliochnanganyika na damu.
2. Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za usiku.
3. Kukojoa mkojo wenye mtiririko mchafu.
4. Kutirirka kwa mkojo baada ya kumaliza kukojoa.
5. Kupata maamuvu wakati unapoanza kukojoa.

Faida zingine za Maji Mwilini



Moja kati ya kauli mbiu ambayo ipo katika matumizi ya maji wanasema ya kwamba, maji ni uhai. Huo ni ukweli usiopingika juu ya kauli hiyo ijapokua watu wengi huwa hawatumii maji hayo.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwa watu hao Makala haya yatakufaa kwani utakwenda kujua ukweli kuhusu faida za maji mwilini.
Faida za maji mwilini ni kama ifuatavyo;
1. Unywaji wa maji husaidia kuifanya ngozi yako kuwa nyororo na nadhifu.
2. Maji husaidia kwa kiwango kikubwa katika mfumo wa kuchanganya chakula katika mwili wa mwanadamu. Lakini pia maji husaidia kupunguza uwezekano wa kuapata saratani ya colonikwa asilimia 45.
3. Maji husaidia kupunguza calories mwilini, yaani badala ya kunywa vimininika vingine kama vile soda, juisi na bia ambavyo vina calories, hivyo unashauriwa utumie maji kwani yenyewe hayana calories. Lakini pia unashauriwa ya kwamba kila wakati uendelee kutumia maji kwani yenyewe hayana mafuta, sukari ambavyo husababisha athari mbaya katika mwili wa binadamu.
4. Kwa wale ambao hushambuliwa na maumivu ya kichwa, tunaambiwa ya kwamba maji husaidia kutibu maamivu ya kichwa, kwani inasdikia ya kwamba upungufu wa maji mwilini husababisha kichwa kuuma, hivyo kila wakati ni vyema ukatumia maji ili ujitibu.
5. Utumiaji wa maji kwa kiwango kikubwa kila wakati humsaidia mtu kuweza kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya moyo, hivyo unashauriwa kwa siku tunywe zaidi walau bilau nane kwa siku

Tuesday 19 December 2017

Mwenyekiti Sau Kuzikwa Disember 22



Mwenyekiti wa Chama cha Sauti ya Umma (SAU), Dk Paul Kyara aliyefariki dunia jana anatarajiwa kuzikwa Desemba 22,2017 kijijini Legho, Kilema mkoani Kilimanjaro.
Dk Kyara alifariki dunia jana asubuhi Jumatatu Desemba 18,2017 akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam.
Katibu wa chama hicho, Johnson Mwangosi amesema Desemba 21,2017 saa tano asubuhi wanatarajia kuwa na ibada na kuaga mwili wa marehemu nyumbani kwake Madale.
Mwangosi amesema baada ya shughuli hiyo mwili wa Kyara utasafirishwa kwenda kijijini Legho.
Majaliwa, mtoto wa marehemu Kyara amesema baba yake alikuwa akisumbuliwa na figo tangu mwaka 2012.
Amesema Ijumaa Desemba 15,2017 alipata tatizo la shinikizo la damu na sukari ilipanda.
Majaliwa amesema alipelekwa hospitali alikopatiwa matibabu na aliruhusiwa kurejea nyumbani.
Amesema Jumamosi Desemba 16,2017 alizidiwa na saa tatu usiku walimpeleka katika Hospitali ya Regency kwa matibabu.
Amesema madaktari walijitahidi kuokoa maisha yake lakini shinikizo la damu na kisukari hakikushuka hivyo kusababisha kifo chake.
“Nitamkumbuka baba, wakati amelazwa neno alilokuwa akisisitiza ni upendo na umoja," amesema Majaliwa.

Airtel yaja na ofa kabambe msimu huu Wa sikukuu



Kampuni ya Simu za Mkononi nchini Airtel imezidi kuonesha ukomavu wake katika kuwaletea wateja wake huduma bomba baada ya sasa kuja na kifurushi cha Smatika ambacho kinaanzia Sh 2,00 hadi Laki moja.
Vifurushi hivyo vimekuja mahususi kwa lengo la kukata kiu ya bando la intaneti kwa watumiaji wa Airtel huku wakiboresha vifurushi hivyo katika msimu huu wa Sikukuu ambapo kifurushi cha MB 50 kwa Sh 250 sasa kitakujia kwa Sh 2,00 ili kwenda sawa na vocha za 2,00 zilizopo lakini kikikupatia bando la MB 40 kwa siku.
Airtel pia imekuja na bando jipya kabisa la Sh 2,000 ambalo litakua na kifurushi chenye ujazo wa GB 3 kwa siku tatu kulinganisha na awali ambapo Sh 2,000 mteja alikuwa akipata kifurushi cha GB 1.3 kwa siku.
Akizungumzia lawama ambazo zimekuwa zikitolewa na wateja wa mtandao huo kuhusu kupunguzwa kwa vifurushi vya mtandao huo, Meneja Masoko Airtel, Aneth Muga alisema wateja wengi wamekuwa wakilalamika kuhusu kuondolewa kwa vifurushi vya UNI lakini wamesahau kuwa vifurushi hivyo vilikuwa maalumu kwa ajili ya wanafunzi wa vyuo.
“ Ndugu zangu wanahabari Airtel imeendelea kukata kiu ya watumiaji wa mtandao wetu, watu wengi wanalalamika kuwa tumepunguza vifurushi vyetu bila kuangalia kwa undani, mathalani kifurushi cha 250 kilikuwa kikimpatia mteja MB 50 lakini sasa tunatoa MB 40 kwa Sh 200.
“ Ukiangalia hapo huoni utofauti wowote lakini pia kuwa na kifurushi cha Sh 200 kunampa unafuu mteja ambaye ananunua vocha za Sh 200,” alisema Aneth.

Rais Magufuli amwaga Neema Ruvuma



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia wizara ya Nishati, ametoa kiasi cha shilingi bilioni 210 kwaajili ya ujenzi wa mradi mkubwa wa Umeme unaojengwa mkoani Ruvuma.
Akiongea katika ziara yake ya siku tatu mkoani Ruvuma Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amesema Rais Magufuli ametoa fedha hizo kwa kushirikiana na wahisani wengine.
“Mheshimiwa Rais ndio ametoa fedha hizi bilioni 210 kwa kushirikiana na wahisani ambapo bilioni 104 ni kwaajili ya kusambaza umeme katika wilaya zote za mikoa ya Ruvuma na Songea”, amesema Waziri Kalemani.
Mradi huo wa umeme unatarajiwa kuwafikia wananchi zaidi ya 32,000 katika vijiji 120 vya mikoa hiyo. Waziri ameongeza kuwa mradi huo utawawezesha wananchi kuingiza fedha nyingi kutokana na fursa zitakazojitokeza baada ya kukamilika.
Kalemani amewataka Wakandarasi kumaliza kwa wakati mradi huo kwani tayari wameshapewa fedha zao bila kucheleweshewa. Mradi unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti 2018.

Mtulia Kurudi tena Kinondoni



Aliyekuwa Mbunge Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia ambaye amehamia CCM ametangaza nia ya kugombea tena ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya chama hicho tawala.
Desemba 2 Mtulia amejiuzulu nafasi ya ubunge, huku akisema amefikia uamuzi huo bila kushawishiwa mtu yeyote na amebaini Serikali ya CCM inafanya kazi kubwa ya kutekeleza Ilani na imefanya vizuri katika mambo mengi ambayo upinzani iliahidi kuyatekeleza.
Baada ya hatua hiyo, chama cha CUF upande wa Profesa Ibrahim Lipumba ametangaza kuwaomba radhi wapiga kura wa Kinondoni kwa Mtulia kujiuzulu uanachama kisha ubunge.
Lakini leo Jumanne Desemba 19, 2017 kupitia andiko lake alilolituma kwa vyombo vya habari, Mtulia amesema atachukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa ndani ya CCM ili agombee tena nafasi hiyo.
“Chama changu kikiridhia nitakwenda mbele ya Wanakinondoni kuomba ridhaa ya kuwatumikia katika nafasi ya ubunge kupitia CCM. Pia nawapa pole sana kwa maumivu mliyoyapata kutokana na uamuzi wangu wa kujiuzulu ubunge wa Kinondoni,” amesema Mtulia.
Hata hivyo, Mtulia amewahakikishia wakazi wa Kinondoni kuwa bado anawapenda na yupo tayari kutumikia tena kwa lengo la kuleta maendeleo ya jimbo hilo ambalo awali lilikuwa likishirikiliwa na CCM kwa kipindi cha muda mrefu.

Mambo ya kukumbukwa aliyoyafanya Rais Magufuli Mwaka 2017



RAIS Dk. John Magufuli amefanya mambo mengi ndani ya mwaka huu, lakini haya 10 yatazidi kukumbukwa na Watanzania.
BABU SEYA, PAPII KOCHA
Tukio la kuachiwa kwa wanamuziki Nguza Mbangu Viking (Babu Seya) na Johnson Nguza (Papii Kocha) lilitangazwa na Rais Magufuli wakati wa maadhimisho ya uhuru, Desemba 9, mwaka huu.
Rais alipotangaza msamaha kwa wanamuziki hao maarufu kuliamsha nderemo na vifijo kutoka kwa mashabiki wa muziki wa dansi nchini.
Familia hiyo ilianza kutumikia kifungo cha maisha jela tangu Juni mwaka 2004 kwa kosa la kuwalati wanafunzi wa Shule ya Msingi Mashujaa, jijini Dar es Salaam.
RELI YA KISASA
Tukio la ujenzi wa reli ya kisasa lilikuwa la kipekee kwa nchi yetu kwani Rais Magufuli alizindua rasmi ujenzi wake akasema itasafiri kwa mwendo wa kilomita 160 kwa saa.
Rais alisema Tanzania ndiyo nchi pekee barani Afrika ambayo imeweza kujenga mradi wa reli kama hiyo kwa fedha zake za ndani.
Ujenzi wake umeanzia Dar es Salaam kwenda Morogoro na utagharimu dola za Marekani bilioni 1.29 na shughuli za ujenzi wa reli hiyo zinaendelea.
TANESCO, WIZARA ZIVUNJWE
Mwaka huu pia, Rais Magufuli alitembelea mradi wa ujenzi wa barabara za juu eneo la Ubungo na kuagiza majengo ya makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Wizara ya Maji yavunjwe.
Alitoa maagizo hayo kutokana na majengo hayo kujengwa ndani ya hifadhi ya barabara ya Morogoro.
Majengo ya wizara tayari yamevunjwa na Tanesco inaendelea na mchakato wa ubomoaji.
MABWENI YA UDSM
Jambo jingine ambalo Rais Magufuli atakumbukwa nalo kwa mwaka huu, ni uzinduzi wa majengo mapya ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Mabweni hayo yana uwezo wa kuchukua wanafunzi 3,840 na yalijengwa chini ya mwaka mmoja na kugharimu sh. bilioni 10.
Hivi karibuni majengo hayo yaliripotiwa kuwa na nyufa, lakini Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) uliwatoa hofu wanafunzi kuwa hayana tatizo.
KUVUNJA BARAZA LA MAWAZIRI
Oktoba mwaka huu, Rais Magufuli alivunja Baraza la Mawaziri na kufanya mabadiliko kadhaa.
Katika mabadiliko hayo, aliongeza wizara na mawaziri kutoka 19 hadi 21. Nafasi za manaibu mawaziri ziliongezwa kutoka 16 hadi 21.
Lengo la mabadiliko hayo ilielezwa ni kuleta ufanisi wa kiutendaji serikalini.
DAWA ZA KULEVYA
Alipoingia madarakani alitangaza kiama cha wauzaji na watumiaji wa dawa za kulevya na vigogo kadhaa walikamatwa kujihusisha nazo.
Februari mwaka huu, rais alimteua Rogers Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA).
Baada ya uteuzi huo, Sianga alimhakikishia rais kuwa atapambana na dawa hizo hadi ushindi upatikane.
Agosti, mwaka huu, Rais Magufuli alimteua pia Luteni Kanali Frederick Felix Milanzi kuwa Kamishna wa Operesheni wa mamlaka hiyo ili kukoleza vizuri moto wa kukabiliana na dawa hizo nchini.
BANDARINI
Mwaka huu rais alifanya pia ziara ya kushtukiza bandarini na kukuta tena madudu mengine, ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake bandarini hapo.
Safari hii alikuta magari 50 yaliyoagizwa nchini na watu wasiojulikana kwa jina la Ofisi ya Rais.
Rais Magufuli alisema magari hayo siri yake ni kubwa kwani yamekaa bandarini tangu Juni mwaka 2015 na yaliletwa pamoja na magari ya serikali.
Akahoji,“inakuwaje rais nipate taarifa za magari kufichwa lakini waziri, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) msijue?”
MADENI YA WALIMU
Desemba mwaka huu, rais alirejesha matumani ya walimu ambao kwa muda mrefu wanasumbukia madai yao bila ufumbuzi.
Akizungumza na mamia ya wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Desemba 14, mwaka huu, mjini Dodoma, aliahidi kulipa takriban sh. bilioni 25 za madeni ya walimu.
“Ninawaahidi walimu wenzangu, mara baada ya uhakiki kuisha wale walimu ambao wanadai malipo halali watalipwa,”alisema.
Alisema kabla hajawa rais alikuwa mwalimu hivyo anazifahamu vizuri shida za walimu hivyo walimu wajisikie wana mwakilishi mzuri.
MADINI
Rais Magufuli aliunda tume mbili kuchunguza madai ya wizi na ufisadi unaodaiwa kufanywa na wawekezaji tangu walipoanza uzalishaji wa dhahabu nchini.
Ripoti ya kamati ya kwanza ilipotoka ikiongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma ilibaini kasoro za usimamiaji, hivyo rais alimfuta kazi Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na kuvunja Bodi ya Uwakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA).
Ripoti ya kamati ya pili iliongozwa na Profesa Nehemia Ossoro ilibaini usafirishaji wa mchanga umepotezea taifa fedha nyingi.
Profesa Ossoro alisema fedha zilizopotea tangu mwaka 1998 ni kati ya sh. trilioni 132 hadi trilioni 380.
BOMBA LA MAFUTA
Mwaka huu ulikuwa pia na tukio la aina yake. Ni uzinduzi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Bandari ya Tanga.
Bomba litapita mikoa nane, wilaya 24 na vijiji 124 na wakandarasi watatu kutoka nje wanasimamia mradi huo na kutoa fursa mbalimbali za ajira kwa wananchi wa pande hizo mbili.

Wananchi washerehekea kuuawa kwa Fisi 15



MAMIA ya wakazi wa Kijiji cha Buzanaki kata ya Nyamarimbe katika mkoa wa Geita, wamesherehekea kuuawa kwa fisi 15 hadi jana, katika matukio tofauti wiki moja baada ya mtoto wa miaka sita kuliwa na wanyama hao na wengine watatu kujeruhiwa.
Kwa mujibu wa wazazi wa mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Yusufu, Martha Musa na Simon Balele walidai marehemu alikamatwa na fisi saa moja jioni Desemba akiwa na watoto wengine wanne ambao baada ya tukio walikimbia na kutoa taarifa.
Desemba 2 mabaki ya mwili wa mtoto Yusufu yalipatikana kijijini hapo yakiwa yamebakia utumbo na mfupa mmoja wa paja ambavyo ndivyo vilivyozikwa kwa heshima ya familia.
Kutokana na tukio hilo, wanakijiji chini ya Mwenyekiti wa Kijiji Robert Maholosha, Ofisa Mtendaji, Rose Paul walitangaza msako wa fisi ulioongozwa na kuratibiwa na Musese Kabulizina ambaye ni ofisa wanyamapori wilaya ya Geita.
Hadi jana fisi 15 walikuwa wameuawa katika matukio tofauti katika kijiji cha Buzanaki fisi 6 na katika kijiji cha Idoselo fisi 9 wameuawa ambako nako wanakijiji watatu walijeruhiwa.
Kwa mujibu wa ofisi ya wanyamapori wilaya ya Geita mwaka 2010 hadi 2014 watu saba waliuawa na fisi huku mwaka 2017 ameuawa mtoto mmoja na wengine watatu kujeruhiwa.
Hata hivyo, tukio la Mei 7 mwaka 2012 lililotokea katika kijiji cha Luezera ndilo lililotisha zaidi kwani baada ya fisi kumkamata mtoto mwenye umri wa miaka 8 saa moja jioni wakati akitoka dukani kununua mafuta ya taa na kutoweka naye kuliibuka sintofahamu kubwa.
Katika tukio hilo, wanakijiji kadhaa walihamasishanana kuwaua watu watatu kwa marungu, mapanga na fimbo wakiwatuhumukuwafuga fisi hao kwa ajili ya ushirikina.
Katika tukio hilo pia wanakijiji hao waliteketeza nyumba 5 za familia tofauti kwa moto huku mzee mwenye umri wa zaidi ya miaka 70 akijinyonga kwa kuhofia naye kuuawa kwa kipigo na wananchi baada ya kutuhumiwa kuwa miongoni mwa watuhumiwa.
Hata hivyo, Musese Kabulizina, Ofisa Wanyamapori wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ameionya jamii kutoyahusisha matukio ya fisi na imani za kishirikina na badala yake anasema kuwapo kwa fisi wengi katika makazi ya watu ni matokeo ya uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi kwa wanyamapori wakiwamo fisi kuanza kuvamia makazi ya binadamu kusaka mahitaji kikiwamo chakula.

Watupwa Jela kwa kutumia vibaya madaraka


MAOFISA watano wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, wamehukumiwa kifungo kwenda jela mwaka mmoja na nusu kwa kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka.
Waliopata adhabu hiyo walikuwa wajumbe wa bodi ya zabuni ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.
Kabla ya kuhukumiwa kwenda jela, watumuhiwa hao walikuwa wamepewa adhabu hiyo au kulipa faini ya Sh. milioni 1. 5.
Watumishi hao ni Ramadhani Zongo aliyekuwa ofisa maendeleo ya jamii (amestaafu), Stephen Mayani (ofisa ugavi), Maduhu Magili (mhandisi wa maji), Joachim Leba (ofisa utumishi) na Leonard Batigashaga (ofisa biashara).
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mwandamizi wa Mahakama ya mkoa wa Simiyu, John Mkwabi.
Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo Mwendesha Mashtaka kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Simiyu, Polycarp Mtega, aliiambia mahakama kuwa washtakiwa wanakabiliwa na kesi ya jinai namba 30 ya 2016 chini ya kifungu cha 31 cha sheria ya makosa ya rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Mtega alidai kuwa washtakiwa wote wanatuhumiwa kwa kosa la kubadilisha maamuzi ya timu ya tathmini ya kumpata mkandarasi wa ujenzi wa bwawa katika halmashauri hiyo kinyume cha kifungu cha 75 cha sheria ya manunuzi namba 07 ya mwaka 2011.
Alidai kuwa maofisa hao kwa kujua kuwa wanatenda kinyume cha sheria, walitumia madaraka yao vibaya, kubadilisha mkandarasi aliyepitishwa na timu hiyo katika ujenzi wa bwawa la umwagiliaji lililoko katika Kijiji cha Ikungulyambeshi kwa Sh. bilioni 1.8.
Alisema Mei 7, 2012 maofisa hao wakiwa chini ya Mwenyekiti wa bodi ya zabuni ya halmashauri ambaye ni makamu mwenyekiti pamoja na wajumbe walimbadilisha mkandarasi GAT Engineering Co.Ltd aliyepitishwa na timu ya tathmini, badala yake kumpatia Jossam & Company Ltd kinyume cha utaratibu.
Aliongeza mkandarasi aliyepitishwa na maofisa hao kampuni yake ilikuwa na uwezo wa daraja la tano (v), wakati tangazo la zabuni lilihitaji mkandarasi mwenye darasa la nne hadi moja (1V-1) ambaye alikuwa GAT Engineering Co.Ltd.
Baada ya maelezo hayo, mwendesha mashtaka aliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa washtakiwa ili liwe fundisho kwa watumishi wengine wa umma kuacha kutumia madaraka yao vibaya.
Kwa upande wao washtakiwa hao waliiomba mahakama hiyo kuwapunguzia kifungo kutokana na kosa hilo kuwa la kwanza, huku wengine wakidai wana umri mkubwa na wanategemewa na familia zao.
Baada ya utetezi huo, kila mshtakiwa alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na nusu au kulipa faini Sh. milioni 1.7. Hata hivyo, wote walipelekwa gerezani baada ya kushindwa kulipa.

CHADEMA yaikosoa CCM



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimekosoa kitendo cha CCM kuweka mgombea wake kwenye nafasi ya Spika wa Bunge la Afrika Mashariki wakati haikutakiwa kufanywa hivyo, na kusema kwamba kitendo hicho kitasababisha mgogoro wa kidiplomasia.
Kwenye taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari kutoka kwa chama hiko, imesema CCM imekiuka utaratibu wa Bunge hilo la kumtafuta Spika la kuliongoza kwa kumuweka mtu wao kwenye kinyang'anyiro, wakati kiutaratibu ilitakiwa Spika wa awamu hii atoke nchi ya Rwanda kulingana na mzunguko ambao ulikuwa unafuatwa, na kwamba kitendo hicho kinaweza kuleta migogoro itakayoathiri Jumuiya hiyo kama kipindi cha Idi Amin.
"Awamu hii Spika alipaswa kutoka Rwanda, lakini Tanzania kwa kuwa CCM imezoea kutokuheshimu sheria na kanuni zilizopo imemteua mbunge wake Adam Kimbisa kugombea nafasi ya Spika kinyume kabisa na kanuni za Bunge hilo, na huu ukiwa ni mwendelezo wa utamaduni wao wa kutokuheshimu sheria na kanuni, kitendo ambacho kinatishia ustawi na uwepo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki", imeandika Taarifa hiyo.
Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa .."CHADEMA tunalaani kitendo hiki, CCM wajue kuwa watabeba lawama zote kama kutakuwa na mgogoro ndani ya Bunge la Afrika Mashariki ambayo unaweza kupelekea mgogoro wa kidiplomasia katika Jumuiya nzima kutokana na tabia yao ya kutoheshimu taratibu zilizowekwa. Ttunataka kanuni za EAC ziheshimiwe, kwani tunakumbuka matendo ya Idd Amin mwaka 1977 yalivyovunja Jumuiya hii, hatutaki

yajirudie kamwe".

BREAKING : Sadifa Apata dhamana



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Dodoma iemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Sadifa Juma Khamis (Mbunge) anayekabiliwa na mashtaka ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi mkuu wa viongozi wa UVCCM Taifa.
Sadifa ameachiwa leo Desemba 19, 2017 baada ya mahakama kutupilia mbali pingamizi la upande wa mashtaka ambao waliliwasilisha mahakamani hapo kuweka zuio la kupewa dhamana.
Mtuhumiwa huyo ametakiwa kudhaminiwa na watu watatu pamoja na kusaini bondi ya Tsh. Milioni 1, huku akipewa masharti ya kutosafiri nje ya nchi.

JPM Atoa Onyo Kwa Viongozi Wa Serikali


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais John Magufuli ametoa onyo kwa viongozi wa Serikali na hasa anaowateua kuwaheshimu na kuzingatia maagizo yanayotolewa na viongozi wa chama hicho, vinginevyo atawachukulia hatua.
Dk Magufuli aliitoa kauli hiyo jana mara mbili alipokuwa anafungua mkutano mkuu wa chama hicho asubuhi na akairudia tena alipokuwa anaufunga usiku.
Katika mkutano huo uliofanyika siku nzima na kuonyeshwa muda wote moja kwa moja na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Magufuli alichaguliwa na wajumbe wa mkutano huo kuwa mwenyekiti wa CCM kwa kipindi cha miaka mitano baada ya kupigiwa kura zote 1,828 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete.
“Viongozi wa Serikali wanapaswa kutambua kwamba viongozi wa CCM ndio hasa wanaostahili. Kiongozi wa Serikali wa cheo chochote anawajibika kwa viongozi wa CCM,” alisema Rais Magufuli na kuamsha shangwe kutoka kwa wajumbe wa mkutano huo.
“Viongozi wa Serikali katika ngazi yoyote watambue kuwa waajiri wetu wakuu ni CCM, mimi bila CCM nisingekuwa Rais, CCM ndiyo kimejadili jina langu. Tupo hapa kwa ajili ya kutekeleza ilani ya CCM na wenye ilani hiyo ni hawa hapa (wajumbe) nendeni mkawasikilize,” alisema.
Dk Magufuli alionya asijitokeze kiongozi yeyote wa Serikali wa kusema hayajui (mambo) ya CCM.
“Kama mimi Rais niliyewateua ninayajua ya CCM asitokee mtu yoyote akasema hayajui mambo ya chama changu,” alisema.
Hata hivyo, alisema kauli hiyo isiwavimbishe kichwa viongozi wa CCM na kufanya mambo kinyume wakitegemea uongozi wao ndani ya chama hicho tawala.
“Nataka viongozi wa CCM kuheshimu viongozi wa Serikali na viongozi wa Serikali kuheshimu sana sana sana viongozi wa chama,” alisisitiza.
Achaguliwa kwa kura zote
Katika mkutano huo, Magufuli alichaguliwa kwa kupata kura zote 1,828, huku makamu mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula akichaguliwa kwa kura 1,827. Makamu mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein akichaguliwa kwa kura 1,819.
Viongozi hao watatu walichaguliwa kwa kupata asilimia 100 ya kura zilizopigwa.
Mkutano huo pia uliwachagua wajumbe 30 wa Halmashauri Kuu (NEC) kati yao 15 kutoka Tanzania Bara na 15 wa Zanzibar.
Miongoni mwa waliochaguliwa ni Stephen Wasira, Jerry Silaa, Dk Fenela Mukangara, Angel Akilimali, Jackson Msome, Dk Ibrahim Msengi, Theresia Mtewele, Mwantumu Zodo, Ernest Sungura, Deougratius Ruta, Burton Kihaka, William Sarakikya, Richard Charles, Anna Msuya na Charles Shanda.
Baadhi ya wajumbe wa Zanzibar ni, Nasri Omary Juma, Pereira Ame Silima, Faidha Juma, Sophia Mziray na Amina Omary.
Mbunge wa upinzani atathminiwa
Akifungua mkutano huo jana asubuhi, Magufuli alisema kuna watu wengi wanataka kurejea katika chama hicho ila wanawafanyia tathmini wasije kupokea mamluki.
Akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa CCM jana, Rais Magufuli alisema hicho ni kimbunga na wataisoma namba.
Alisema katika hamahama hiyo kuna mbunge wa upinzani ambaye amemuomba sana kuhamia CCM akiwa na madiwani wanane.
Kauli ya Rais Magufuli imekuja kukiwa na presha upande wa upinzani baada ya wabunge wawili kuhamia CCM wakiachia majimbo yao.
Wabunge hao walioachia nafasi zao ni aliyekuwa wa Kinondoni (CUF), Maulid Mtulia na Dk Godwin Mollel wa Siha (Chadema).
Licha ya Tume ya Uchaguzi (NEC) kutangaza uchaguzi mdogo wa majimbo matatu, kuna majimbo matano ambayo yapo wazi yakiwemo mawili ya Kinondoni na Siha ambayo wabunge wao walijiuzulu hivi karibuni. Uchaguzi wa Januari 13 mwakani utahusisha majimbo ya Singida Kaskazini, Songea Mjini na Longido.
Akizungumzia uchaguzi mdogo uliofanyika katika kata 43 Novemba 26, Rais Magufuli alisema CCM ilishinda kata 42.
“Katika tathmini ya uchaguzi huu uliofanyika, CCM inakubalika kwa wananchi, uimara na ukomavu wa chama pia umechagia ushindi kwa kuwa ni kikongwe kimetimiza miaka 40 na kinaongoza dola tangu kuanzishwa kwake,” alisema Rais Magufuli.
Alisema wameshinda kwa sababu wanaCCM wanao umoja na mshikamano mkubwa.
Uchaguzi ndani ya chama
Rais Magufuli alisema wagombea wengi walijitokeza, hiyo inadhihirisha ukomavu wa demokrasia ndani ya chama hicho.
Aliwataka wajumbe katika mkutano huo kuchagua kwa umakini bila kuangalia udini, ukabila, ukanda au kutegemea kupata masilahi.
“Nawahakikishia katika uchaguzi huu wagombea watakaobainika wameshinda kwa rushwa hatutasita kutengua ushindi wao,” alisema.
“Rushwa ni adui wa haki niwasihi sana wanaCCM wenzangu msichague mtoa rushwa mchague watu waadilifu, wachapakazi na wenye mapenzi na chama, rushwa inatumaliza,” alisema akifungua mkutano asubuhi.
Amshukuru Kikwete
Katika mkutano huo ambao ulihudhuriwa na marais wastaafu Rais Magufuli alisema, “Ilifika wakati mtu kama hana fedha hawezi kugombea wala kuchukua fomu namshukuru sana mwenyekiti mstaafu Kikwete (Jakaya) ingekuwa mtu anashinda kwa rushwa nisingepita, namshukuru sana mzee Kikwete.”
Uvunjaji makundi
Rais Magufuli aliwataka wana CCM kuvunja makundi yote yaliyokuwapo akisema, “Uchaguzi wowote kuna kushinda na kushindwa, uchaguzi usiwe chanzo cha mifarakano na kuvunjika kwa umoja na mshikamano.”
“Kafanyeni kazi kwa bidii kwa kuwaunga mkono waliochaguliwa, tuvunje makundi yote yalikuwapo wakati wa uchaguzi.”
Alisema chama hicho kamwe hakitamvumilia yeyote atakayeendeleza makundi awe kiongozi aliyechaguliwa au mwanachama wa kawaida aliyeshindwa.
Mageuzi ndani ya CCM
Rais Magufuli alizungumzia mageuzi katika chama hicho akieleza, “Mkutano unafanyika katika mazingira ya kipekee na kufuatia majadiliano ya kina tumefanya mageuzi ya mfumo, muundo na utendaji ili kukirudisha chama kwa wananchi.”
“Mageuzi haya yameleta uadilifu, uwajibikaji wa viongozi na wanachama,” alisema.
Aliongeza kuwa mabadiliko huwa yana changamoto zake, mageuzi yaliyofanyika ni makubwa lazima wasimamie na hasa viongozi ambao wamechaguliwa.
“Viongozi waendelee kusimamia mageuzi kwa kuimarisha na kuongeza idadi ya wanachama,” alisema. “Tunataka ikifika wakati wa uchaguzi washindani wetu wasiambulie chochote.”
Akiba ya fedha
Rais Magufuli alisema Tanzania ina akiba ya fedha za kigeni Dola 5,820.4 milioni za Marekani ambazo zinaweza kulipia bidhaa kwa miezi mitano hata kama Watanzania watakaa bila kufanya kazi kwa muda huo.
Mangula na Kinana wapeta
Akiwazungumzia Philip Mangula na Abdulrahman Kinana, Rais Magufuli alisema wamemsaidia sana akieleza kuwa kuna watu walijua hatamchagua Mangula, wengine wakiwa wanamuita Mangula ni mzee Mugabe.
“Hakuna kazi ya kukitumikia chama bila kutegemea wazee, ni muhimu sana busara zao zinahitajika sana,” alisema.
“Mangula amenisaidia sana mimi ni kijana wakati mwingine nakuwa nachemka, hawa makamu wangu Shein (Dk Ali Mohammed) na Mangula wananisaidia sana. Hawa wazee ni muhimu sana katika kunifanya niwe kiongozi mzuri.”
“Kinana amenisaidia sana kufanya mambo ya mageuzi ndani ya chama na mategemeo yangu makubwa ataendelea kunisaidia sana.”
Akizungumza baada ya Rais Magufuli, Kinana alisema anakubali kuendelea na nafasi hiyo katika chama hicho na kuahidi kuwa atafanya kazi kwa bidii na uaminifu.
“Haiwezekani kumkatalia mwenyekiti wako na Rais wako. Imani huzaa imani na uhakika umenitaka niendelee kuchapa kazi ndani ya chama chetu,” alisema Kinana.
“Kwa kuwa una imani nina uwezo wa kufanya kazi vizuri kauli ni amri, nakuhakikishia nitakitumikia chama changu kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu.”
Akifunga mkutano huo, Mafuguli alisema sekretarieti itaendelea hiyohiyo iliyokuwepo.
amempa uhuru katika baadhi ya maeneo na wakati mwingine akimwambia mambo magumu hucheka, jambo ambalo linampa faraja.
Akizungumzia suala la Rais Magufuli kubadilisha Katiba, alisema kuna baadhi ya watu wamekuwa wakibadilisha mambo yaliyofanywa na chama hicho kwa lengo la kumchafua mwenyekiti wa chama hicho.
Alitoa mfano kuwa wapo wanaosema kuwa wamebadilisha Katiba na kwamba Rais Magufuli atakapomaliza kipindi cha miaka mitano hakuna wa kumpinga ataendelea.
“Mimi sijawahi kuona hiyo, wala kwenye mageuzi hayapo lakini hiyo yote ni kutaka kumchafua mwenyekiti, lazima tukatae, msiyakubali ,” alisema.
Kinana alisema katika awamu zote Serikali zilikuwa zikipambana na rushwa lakini tofauti yake ni kwamba kwa awamu hii hatua kali zinachukuliwa papo hapo.
Shibuda, Cheyo wamsifia JPM
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa UDP, John Cheyo aliiomba CCM kuongoza vyama vingine kuamini kuwa siasa si vita.
Cheyo alisema hayo akitoa salamu katika mkutano huo akisema anashangazwa na watu ambao wanaamini siasa ni uadui.
Mwanasiasa huyo alianza kwa kauli ya kuwaita CCM ndugu zake, “Najua kuwaita ndugu zangu kesho nitashambuliwa kwenye vyombo vya habari, lakini ukweli ni kwamba mimi ni muumini wa kuwa siasa si uadui.”
“CCM ituongoze kuvifanya vyama vyetu vya siasa visiwe viwanda vya matusi.”
“Niwaambie wenzangu wanaojaribu kushindana na CCM kuwa CCM inatisha. Tusitumie muda mwingi kujaribu kuiangusha. Naomba wenzangu watambue kuwa Tanzania kwanza tuache mchezo wa susiasusia kila wakati.”
Aliongeza kuwa: “Tunaona kazi unayoifanya, tunakuhitaji, endelea kutusukuma kwenye maendeleo.”
Katibu Mkuu wa Ada Tadea na Mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa, John Shibuda alipongeza utendaji kazi wa Magufuli.
Shibuda alitumia fursa hiyo kuomba Sh20 milioni alizosema zinahitajika kwa kampeni za uchaguzi mdogo wa Januari 13.
Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema alimpongeza Rais Magufuli kwa kuwasamehe wafungwa zaidi ya 1,800 katika sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara.
Mrema pia ni mwenyekiti wa bodi ya Parole.

Haya ndo Maajabu aliyoshudia Vanessa Mdee



Malkia wa Bongo Fleva anayefanya vizuri ndani na nje ya nchi, Vanessa Mdee amekiri kushuhudia maajabu ya Mungu baada ya kupitia changamoto miezi ya mwanzo wa mwaka na hatimaye kumaliza mwaka kwa kusaini mkataba mnene na Kampuni ya usambazaji wa muziki 'Univesal Music Group'.
Kupitia ukurasa wake wa Istagram Vanessa ameweka furaha yake na kushangilia na mashabiki wake ambapo amewaambia kwamba huo ni mwanzo tu na kwamba mambo mengine makubwa yapo njiani.
"Nimeona niitumie siku na fursa hii kuwajulisha wapendwa mashabiki zangu mwanzoni mwa mwaka huu. Nilipitia changamoto nyingi Sana. Lakini kwa neema za Mungu. Nilitoka mahali pale na sio kuona baraka tu bali na maajabu mengi yaliyotokea kwenye maisha yangu i kiwemo kuwa mmoja wa familia ya Universal Music Group in a unique joint signing between Universal Music Germany, Airforce1 na Universal Music Group. Vanessa Mdee.
Ameongeza "hii ni mara ya kwanza kwa msanii wa kiafrika kupata deal ya aina hii yenye mkwanja mrefuu sana...Hii ni habari njema kwa mashabiki wangu na ndiyo kwanza tumeanza. Mambo makubwa zaidi yanakuja. Kumbuka kila mwisho wa Jumapili ndiyo mwanzo wa Jumatatu, usiogope kuanza upya"
Vanessa amewashukuru mashabiki zake, ndugu jamaa na marafiki ambao walikuwa pamoja na yeye kuanzia mwaka kuanza japo ulikuwa na changamoto mpaka sasa anbapo mwaka unaelekea kuisha.

Polisi wamshikilia Daktari Feki



Jeshi la polisi mkoani Mwanza linamshikilia mtu mmoja kwa kosa la kujifanya daktari, katika hospitali ya mkoa Sekou Toure.
Joseph Mbagata 25,mkazi wa mtaa wa Mabatini jijini humo amekamatwa leo Desemba 18 na jeshi hilo baada ya kubainika kwamba sio mwanataaluma na alikuwa akiwatapeli wagonjwa kwa kuwaomba hongo, kitendo ambacho ni kosa kisheria.
Taarifa kutoka kwa jeshi hilo zimesema kwamba mtuhumiwa alikuwa akiwaomba hongo, huku akiahidi kuleta dawa muhimu na pia kufanya mipango ili mgonjwa apate huduma kwa haraka.
Awali zilipatikana taarifa kuwa siku chache zilizopita alionekana mtu aliyevalia mavazi ya udaktari na kujifanya daktari, kisha anapita wodini kuwaona wagonjwa. Pia ilisemekana kuwa mtu huyo tayari amechukua Sh30,000 kwa mgonjwa ili aweze kumpatia matibabu.
Aidha baada ya tuhuma hizo kufika katika uongozi wa hospitali waliweka mtego na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa, akiwa amevalia mavazi ya udaktari huku akiwa amesimama nje ya wodi ya upasuaji.
“Tumekuwa tukilalamikiwa kwamba kuna baadhi ya madaktari hapa hawana ujuzi wala hawajitambui, kumbe ni dhahiri kwamba hao watu wapo na kuanzia sasa lazima tufanye ukaguzi wa hali ya juu ili hali hiyo isije ikajitokeza tena maana ni sehemu ya kuhatarisha maisha,” amesema mmoja wa madakatri katika hospitali hiyo ambaye hakutaka kutajwa majina.
Baada ya daktari huyo feki kukamatwa, uongozi wa hospitali ulitoa taarifa polisi, ambapo askari walifika eneo la tukio na kumuweka mtuhumiwa chini ya ulinzi kisha kumfanyia upekuzi kwenye begi alilobeba na kukuta mavazi yanayotumiwa na madaktari katika vyumba vya upasuaji.
Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza naibu kamishina wa polisi Ahmed Msangi ametoa wito kwa wananchi hususani wagonjwa waliopo hospitalini akiwaomba kuwa makini na watu ambao ni matapeli wa aina kama hiyo wenye nia ovu dhidi yao.
Aidha pia aliwaomba viongozi wa hospitali zote kuendelea kutoa taarifa kwa polisi kuhusiana na watu wanao watilia shaka hospitalini, ili waweze kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Moyes asema anauwezo Wa kufundisha timu Yoyote duniani



Meneja wa wagonga nyundo wa London West Ham United David Moyes, amesema uwezo alionao kwa sasa anaweza kuifundisha timu yoyote duniani na anataka kuonesha kama ana uwezo huo akiwa na klabu yake ya West Ham United.
Tangu alipoteuliwa kuwa kocha wa West Ham United Moyes, ameisaidia timu hiyo kutoka katika mstari wa timu zinazotakiwa kushuka daraja kwa kutokufungwa michezo mitatu.
"Nina uwezo wa kufanya kazi hii katika klabu yoyote duniani na nina uhakika nitalifanya hili nikiwa na West Ham," alisema kocha huyo.
Kocha huyo raia wa Scotland mwenye umri wa miaka 54, anajaribu kurudisha heshima yake baada ya kufanya vibaya alipoviongoza vilabu vya Manchester United, Real Sociedad na Sunderland.
West Ham kwa sasa iko nafasi ya kumi na tano katika msimamo wa ligi kuu ya nchini England.

Diwani wa Chadema afunguka kuhama chama kwa masharti




Diwani wa (CHADEMA), Kata ya Sombetini, Ally Bananga amesema yupo tayari kurudi (CCM) ikiwa viongozi wa chama hicho ambao wanataka kumnunua ikiwa watamuonyesha watu waliowatuma kumuua Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo.
Mbunge wa jimbo la Kibamba, John Mnyika (kushoto) Diwani wa Sombetini Ally Banaga (Katikati) akiwa na Mstahiki Meya wa Ubungo Mhe. Boniface Jacob (Kulia).
Ally Banaga amedai kuwa yeye yupo tayari kurudi CCM kama viongozi hao watatimiza jambo hilo na kusema hiyo ndiyo itakuwa gharama yake kurudi CCM na siyo fedha au mali kama ambavyo wengine wanadaiwa kupewa.
"Ma CCM wanaotaka kuninunua, leo nataja gharama za kurudi CCM. Nionyesheni mliowatuma kumuuwa Mawazo, nitajiunga nanyi siku hiyo hiyo" alindika Ally Banaga
Aidha Banaga ameonyesha masikitiko yake makubwa kwa watu ambao wanakisaliti chama hicho na kusema kuwa wamesahau kuna watu kama kina Mawazo ambao wamekufa wakikipigania chama hicho.
"Nilishika jeneza lako nikikuangalia mwamba umelala. Ndipo nilipoamini kuwa sio stori, mwanaume wa kweli uliyefia vitani ukikitetea chama ambacho kuna Mambwa Koko yanakisaliti, yanakichezea yanakinajisi bila kuhisi maumivu yako ulipotoka roho kukipigania. Nilikuita kwangu Dar es Salaam tupumzike baada ya uchaguzi mkuu ambao CCM walikupora kwa nguvu ushindi wako, kaka ukakataa kwa neno moja " Nikiondoka Makanda watakufa moyo, ngoja niwape tafu, Tukutane Dodoma.....dah! Tukakutania Mwanza kwenye jeneza" alisema Banaga
Novemba 14, 2015 aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Busanda kupitia CHADEMA na Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Geita aliuawa kwa kupigwa mapanga na watu wasiojulikana na kupelekea kifo chake.