Friday 24 November 2017

Kumbe mpango wa Kane ni kuvunja rekodi ya Shearer



Mshambuliaji nyota wa Tottenham Hotspurs, Harry Kane amesema anataka kufunga mabao katika kila mchezo.

Kane amefunga mabao 29 katika Ligi Kuu England na mkakati wake ni kufikia rekodi ya nguli wa zamani wa England Alan Shearer.

Nahodha huyo wa zamani wa England ana rekodi ya kufunga mabao 36 alipokuwa mchezaji wa Blackburn Rovers mwaka 1995.

Kane ametoa kauli hiyo wakati Spurs leo itakuwa ugenini kumenyana na West Brom katika mchezo wa Ligi Kuu England kwenye Uwanja wa Wembley.

 “Nilikosa baadhi ya mechi kutokana majeraha. Nilicheza michezo miwili au mitatu,” alisema nahodha huyo wa England.

Mshambuliaji huyo alidokeza anataka kufunga kila mchezo katika mechi tisa zilizobaki kabla ya mwezi ujao. Kane alifunga bao katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund, Jumanne iliyopita.

No comments:

Post a Comment