Saturday 25 November 2017

Baada ya kimya kirefu, Jokate afunguka kuhusu Lulu



MWANAMITINDO Jokate Mwegelo hivi karibuni baada ya kukaa kimya bila kumposti msanii mwenzake Elizabeth Michael ‘Lulu’ wala kuongea lolote kuhusiana na hukumu yake ambapo mastaa kibao walionesha kumuhurumia na k
umposti kwa kuweka maneno tofauti tofauti, yeye ameibuka na kusema kuwa anamuombea dua huko alikoenda kwani ndio jambo pekee ambalo anaweza kulifanya.

Akilonga na Risasi Jumamosi, Jokate alisema kuwa yeye anamuombea dua Lulu Mungu amfanyie wepesi huko alikokwenda kwani ndio njia pekee ya kumfariji.

Mwanamitindo huyo aliongea hayo baada ya kuulizwa sababu ya yeye kutomposti na maoni yake juu ya hukumu hiyo. “Kikubwa ni kumuombea na mimi namuombea ndicho ninachoweza kusema,” alisema Jokate.




No comments:

Post a Comment