Saturday 25 November 2017

Mali: Maafisa 4 wa UN wauawa



Umoja wa Mataifa umesema maafisa wake wanne walinda amani pamoja na mwanajeshi mmoja wameuawa na wengine kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa eneo la mpakani baina ya Mali na Niger.

Afisa mkuu anayekiongoza kikosi hicho cha walinda amani walioko Mali bw. Mahamat Saleh Annadif, bila kutaja washambulizi ni akina nani, amelaani vikali tukio hilo akisema ametamaushwa na kisa hicho dhidi ya maafisa wake ambao walikuwa wakiendeleza kazi ya udumishwaji wa amani na vilevile kutoa misaada hasa ya kimatibabu kwa wakaazi wa maeneo ambayo yamekumbwa na hali mbaya ya kuzorota kwa usalama.

Kuna makundi kadhaa ya wapiganaji yanayopatikana eneo hilo la Mali, yaliyo na uhusiano na kundi la Al Qaeda.

Umoja wa mataifa umekuwa na kikosi cha walinda amani huko Mali tangu 2013 wakisaidiwa pia na kikosi cha kijeshi cha Ufaransa.

No comments:

Post a Comment