Saturday 25 November 2017

CAF yataka Yanga, Simba Kupeleka Majina




Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezitaka Simba na Yanga haraka kupeleka majina ya wachezaji wake kwa Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kwa ajili ya ushiriki wa michuano yake mwakani, pia watakaguliwa mahesabu yao.

Yanga itashiriki Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuwa bingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, huku Simba wakishiriki Kombe la Shirikisho kutokana na kuwa mabingwa wa Kombe la FA.

Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas, alisema klabu hizo zinatakiwa kuwasilisha majina yao Caf mapema kabla ya mwisho wa mwezi huu.

“Simba na Yanga wanatakiwa kutuma majina ya usajili wa wachezaji wao mapema kabla ya Novemba 30, mwaka huu kwa sababu wakichelewa inaweza
kuwa tatizo kwao,” alisema Lucas.

 “Na kwa sasa kamati ya leseni za klabu inakwenda kufanya ukaguzi katika klabu hizo ili kufahamu kama zimetimiza matakwa ya kupata leseni ya kushiriki michuano ya Caf.

“Timu zitakaguliwa ofisini na watendaji wake, umiliki wa nyaraka mbalimbali, ukaguzi wa mahesabu na ripoti ya fedha ya mwaka mzima kama Kanuni ya 11 ya ligi kuu na kanuni ya saba ya Caf zinavyojieleza kuhusiana na leseni za klabu,” alisema Lucas.

No comments:

Post a Comment