Saturday 25 November 2017

RC Aggrey Mwanri aamua kuwapa fursa hii vijana




Vijana Mkoani Tabora wametakiwa kuacha tabia ya kukaa vijiweni na kusikiliza maneno ambayo hayawasaidii wala kuwafundisha namna ya kupata maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri katika maeneo mbalimbali ya Kata za Wilaya ya Kaliua kwenye zoezi la uhamasishaji wa kilimo cha kisasa cha zao la Pamba na mazao mengine.

Aidha mkuu huyo wa mkoa amewataka vijana kutumia muda wao kujiajiri katika sekata ya kilimo na uzalishaji wa pamba pamoja na mazao mengine yatakayowasaidia kujipatia kipato na kuinua maisha yao.

“Kijana uliyekuja hapa leo ninakuambia kuwa kama unarafiki yako unashinda nae kijiweni na kucheza karata, Pool kuanzia leo achana naye, kwani hana nia njema nawewe, mwambie kuwa mkuu wa mkoa amenifundisha juu ya kulima pamba kisasa kuanzia sasa urafiki wangu mimi na wewe bye bye”, amesema RC Mwanri.

Mkuu wa Tabora yuko katika ziara mkoani mwake kuhamasisha kilimo cha kisasa cha zao la pamba na mazao mengine ambayo yatawasaidia wakulima kupata pesa zitakazoboresha maisha yao.

No comments:

Post a Comment