Friday 24 November 2017

Serikali ya Rwanda yatangaza kuwa ipo tayari kupokea wahamiaji 30 000 waliokumbwa na madhila nchini Libya


Kufuatia matendo ya unyanyasaji na ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Libya ambapo  wahamiaji haramu waliokuwa wakitaraji kusafiri kupitia Libya kuelekea barani Ulaya kujipata katika mnada, Rwanda  imetangaza kuwa ipo tayari kuwapokea wahamiaji 30 000 katika ardhi yake.

Moussa Faki Mahamat, kamishna mkuu wa Umoja wa Afrika katika ukurasa wake  wa Twitter amefahamisha kuwa amefurahishwa na  serikali ya Rwanda  kujitolea kuwapokea wahamiaji kutoka Libya na kuahidi kuwa ipo tayari pia kuandaa  safari za wahamiaji hao katika mataifa yao iwapo watakuwa tayari kurejea kwa hiari.


No comments:

Post a Comment