Friday 24 November 2017

Marekani yatoa tahadhari kwa raia wake kusafiri kuelekea nchini Saudi Arabia



Marekani imewatahadharisha raia wake kusafiri kuelekea nchini Saudi Arabia na kusema kuwa lna vitisho kutoka katika makundi ya kigaidi kushambulia kwa makombora kutoka nchini Yemen.

Saudi Arabia kwa upande wake haikutoa taarifa yeyote kuhusu tahadhari hiyo iliotolewa na Marekani.

Tangazo lililotolewa limefahamisha kuwa vitisho vya mashambulizi dhidi ya mji wa Riyadh, Jeddah na Dhahran vinaendelea .

Makundi ya kigaidi ikiwemo kundi la wanamgambo wa Daesh nchini Iraq na Syria yalilenga ofisi za serikali ya Saudi Arabia, miskiti na meneo mengine mengi ambayo raia wa kigeni wakiwemo wamarekani huwa wanapenda kutembelea.

Jeshi la Polisi la Saudi Arabia lilifaulu kuzuia mashambulizi ya kigaidi  yaliokuwa yakilenga mskiti wa  Macca na kupelekea kukatwa kwa baadhi ya viongozi wa Daesh.

No comments:

Post a Comment