Saturday 2 December 2017

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download

Audio | Nay Wa Mitego Ft Billnas X Godzilla X Ay – Muda Wetu Remix.| Mp3 Download


                                       DOWNLOAD HERE

Ratiba kombe la Dunia yatoka, Misri yakabidhiwa wenyewji



Nigeria wamepangwa kwenye kundi moja na Argentina kwa mara nyingine, Misri nao wakapangwa na Urusi na Uruguay baada ya droo ya Kombe la Dunia 2018 kufanywa nchini Urusi.

Panama, ambao wanacheza Kombe la Dunia mara ya kwanza wamepangwa na Ubelgiji na England na Tunisia.

Iceland, walioshangaza wengi kwa kufuzu, wamepangwa kucheza na Nigeria, Croatia na Argentina katika Kundi D.

Mechi ya ufunguzi itakuwa kati ya Urusi na Saudi Arabia.

Droo kamili ya Kombe la Dunia:

Kundi A: Urusi, Saudi Arabia, Misri, Uruguay
Kundi B: Ureno, Uhispania, Morocco, Iran
Kundi C: Ufaransa, Australia, Peru, Denmark
Kundi D: Argentina, Croatia, Iceland, Nigeria
Kundi E: Brazil, Uswizi, Costa Rica, Serbia
Kundi F: Ujerumani , Mexico, Sweden, Korea Kusini
Kundi G: Ubelgiji , Panama, Tunisia, England
Kundi H: Poland, Senegal, Colombia, Japan.


Fifa wamepokea maombi 3.5 milioni ya tiketi, 300,000 yakiwa maombi ya tiketi za mechi ya fainali uwanjani Luzhniki.

Asilimia 57 ya maombi yametoka kwa wakazi wa nje ya Urusi. Tiketi ya bei nafuu zaidi ya fainali Kombe la Dunia ambayo raia asiye wa Urusi anaweza kununua ni ya £345.

Kombe la Shirikisho kuanza kutimua vumbi Desemba 22




Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa sasa itasimama kwa takribani majuma mawili sababu kubwa ni kupisha Kombe la Chalenji la CECAFA michuano inayoratibiwa na Baraza la Soka kwa nchi za Afrika Mashariki (CECAFA).

Kutokana na michuano hiyo kuingilia ratiba, kwa mujibu wa Shirikisho la soka nchini (TFF), Desemba 22, 23, 24 na 26, zitakuwa siku za mechi za kuwania Kombe la Shirikisho la Azam yaani Azam Sports Federation Cup (ASFC).

Mechi zitakazochezwa katika siku hizo zitafahamika Desemba 5, mwaka huu ambako imepangwa droo ya timu 64 zitakazocheza Raundi ya Tatu ya ASFC.

Timu 64 maana yake ni kuwa timu 16 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara; timu 24 za Ligi Daraja la Kwanza na timu 24 ambazo zimefuzu kutoka hatua awali; ya kwanza na pili.

Baada ya michezo hiyo, ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom itaendelea tena kwa michezo ya raundi ya 12 itakayofanyika Desemba 29, 30 na 31 kabla ya ligi tena kusimama kupisha michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Michuano ya CECAFA itafikia ukomo Desemba 17, mwaka huu na Shirikisho

Mbao FC waitwa mezani na Mshambuliaji wa Stand


Wakati Mbao FC ikiwa na tatizo katika safu ya ushambuliaji, mshambuliaji wa Stand United, Omary Kanyoro amesema yupo huru kuzungumza na timu yoyote inayotaka huduma yake.

Mbao imekuwa na tatizo katika safu ya ushambuliaji ambayo imekuwa ikikosa mabao ya wazi katika msimu huu wa Ligi Kuu.

Kanyoro alisema kwa sasa yuko huru kujiunga na klabu yoyote kwani msimu huu hakusajili Stand United katika dirisha kubwa la usajili.

Alisema anatamani kuchezea klabu ya Mbao ambayo katika msimu wa 2016/17 alitaka kusajiliwa, lakini Stand United wakapanda dau kuwazidi wachana Mbao hao wa jiji la Mwanza.

“Mbao ni timu nzuri na kwa sasa natamani kwenda kuchezea kwani ina kocha mzuri hivyo kama wakija basi nipo tayari kujiunga nao”alisema Kanyoro.

Hata hivyo Mshambuliaji huyo alisema pia anakaribisha ofa kwa klabu mbalimbali za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza ambapo yeye yuko tayari kukipiga iwapo watahafikiana kwenye maslahi.

“Sikuweza kusaini mkataba mpya na Stand United katika dirisha kubwa la usajili kutokana na sababu mbalimbali lakini kwa sasa niko huru hivyo klabu yoyote nakaribisha ofa zao,”alisema mshambuliaji huyo.

Chege afananisha ustaa na Jela



Msanii wa Bongo Flava, Chege amesema msanii kuwa staa ni sawa na jela.

Muimbaji huyo wa ngoma ‘Run Town’ ameiambia 5 Selekt ya EATV kuwa kwa wale wasiofahamu wanaweza kuchukulia hilo kawaida lakini ukishakuwa staa ndio utagundua hilo.

“Mtu unapokuwa unaangaika kutafuta ustaa lakini ustaa ni jela moja mbaya sana kwa mtu ambaye hajawahi kupitia hiyo kitu anaweza akaona huyu anaongea tu lakini ukishakua pale kwenye ustaa ndio unajua majukumu ya ustaa yakoje” amesema.

Chege amepongeza kuwa hilo halijamsumbua kwani toka awali alikuwa kwenye mafunzo ya kuupokea ustaa na alikaa na mastaa kwa muda mrefu kabla hajawa staa.

“Siyo kukaa nao tu na kukutana masikani, no! nilikua ndani ya kundi ambalo lina staa namba moja Tanzania nzima kwa hiyo hadi nakuja kuwa staa ule ushamba wa ustaa siwezi kuwa nao tena” amesema Chege.

Adhabu kutolewa kwa wanaosema uongo



Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa amewaonya baadhi ya watu wanaoendelea kutoa takwimu za uongo ambazo husababisha taifa kuingia kwenye mvutano na nchi wahisani wa maendeleo kwa kuogopa kusaidia wananchi.

Dkt. Chuwa amesema moja ya changamoto wanayokutana nayo katika ofisi yake na wadau wa maendeleo, ni baadhi ya takwimu kuonyesha ukubwa wa tatizo kwa kiwango ambacho hakijafikiwa, na kuleta hofu kwa wadau hao hali ambayo inasababisha taifa kukosa ushirikiano mzuri na nchi zingine, kwa kuogopa kusaidia taifa lenye nguvu kazi ya kusuasua.

Kutokana na hilo Mkurugenzi huyo anayesimamia masuala ya takwimu, ameagiza watendaji wake kuhakikisha wanawachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kutoa takwimu za uongo, na kuliingiza taifa katika hali ya sintofahamu.

Kwa upande mwengine baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameiomba jamii kuacha kusambaza takwimu za uongo, na kuziachia mamlaka husika za serikali kutekeleza jukumu hilo la utoaji wa takwimu zilizosahihi.

Guardiola hajutii kuongea na Redmond


Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amesema anajutia sana mazungumzo ambayo alifanya na mchezaji wa Southampton Nathan Redmond punde baada ya mechi yao kumalizika Jumatano.
City walishinda 2-1.

Guardiola, ambaye aliingia uwanjani na kuzungumza na winga huyo, ametakiwa kufafanua kuhusu kitendo hicho chake na Chama cha Soka cha England.

Redmond amesema Mhispania huyo alikuwa tu anamsifia.

Ijumaa, Guardiola alisema: "Siwezi kujidhibiti. Natumai nitaweza kufanya hivyo, natumai naweza kuimarika."

Meneja huyo wa zamani wa Barcelona na Bayern Munich amepewa hadi Jumatatu kutoa ufafanuzi.
"Kile Redmond alichosema ndicho hicho, navutiwa naye kama mchezaji na namshukuru kwa aliyoyasema," amesema.

"Iwapo FA wanataka taarifa yangu tena, ninaweza kufafanua chochote wanachotaka nifafanue. Ikiwa hawaniamini, sijui nafanya nini hapa."

Guardiola alimwendea Redmond muda baada ya Raheem Sterling kufunga bao la ushindi la City dakika ya 96 uwanjani Etihad.

Alianza kusema kwa sauti na kuashiria kwa mikono yake, huku Redmond akionekana kufunika mdomo wake na kumjibu.

Redmond baadaye amesema: "Nilimwambia kwamba nilikuwa ninafanya kile nilichoambiwa na meneja wangu kufanya kwenye mechi hiyo. Hivyo tu."

City watakuwa wenyeji wa West Ham saa 16:00 Jumapili nao Southampton watakuwa ugenini dhidi ya Bournemouth saa 13:30 siku hiyo.



Diamond adaiwa kumkacha Ali Kiba


Muimbaji Diamond Platnumz wiki hii baada ya kuachia nyimbo mbili, Sikomi na Niache, aliahidi Ijumaa hii kuachia rasmi wimbo wake mpya uitwao ‘Waka’.

Meneja wa nyota huyo, Sallam SK amewaomba radhi mashabiki wa muimbaji huyo mwenye tuzo nyingi za kimataifa kwa madai kuna dharura imetokea hivyo atashindwa kuachia project hiyo inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa muziki.

“Tunaomba msamaha wimbo wa ‘Waka’ ulitakuwa kutoka siku ya leo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu kwahiyo hautaweza kutoka leo lakini muda sio mrefu tutawajuza!! Sorry for any inconvenience,” aliandika meneja huyo.

Wadau wa mambo wamedai muimbaji huyo ameshindwa kuachia kazi hiyo mpya ili kuepusha kazi hiyo kushindanishwa na wimbo mpya wa msanii wa RockStar4000, Alikiba, ‘Maumivu Per Day’.

Hata hivyo mashabiki wa Diamond wameonyesha kuchukizwa vikali na uamuzi huo huku wengine wakiwa na maoni tofauti.

Mark Hughes aponda kiwango cha Atkinson



Meneja wa klabu ya Stoke City Mark Hughes amesema Martin Atkinson hafai kutumiwa kama mwamuzi mechi za Ligi ya Premia msimu huu baada ya kufanya "kosa kubwa" mechi za katikati ya wiki.

Atkinson alimpa mlindalango wa Liverpool Simon Mignolet kandi ya manjano pekee kwa kumwangusha mshambuliaji wa Stoke Mame Diouf, akiwa ndiye mchezaji wa mwisho Jumatano.
Stoke walikuwa 1-0 chini wakati huo.

Walishindwa 3-0 mwishowe na Hughes alisema "kila mtu alijua" hiyo ilifaa kuwa kadi nyekundu.
"Sioni ni kwa nini anafaa kusimamia mechi wikendi hii," aliongeza.

"Hisia zangu ni sawa na za kila mtu: waamuzi ambao walitazama tena kisa hicho na kila mtu uwanjani, kando na mmoja pekee.

"Kuna maamuzi yanayoniuma sana mimi kama meneja - na mameneja wengine.

"Sababu ya hiyo kutokuwa (kadi nyekundu) mimi sijui. Ulikuwa uamuzi rahisi sana kwangu lakini haukufanywa. Hilo lilitunyima fursa ya kujipatia nafuu. Nimekasirishwa sana na hilo."

Atkinson atasimamia mechi ya Watford nyumbani dhidi ya Tottenham Ligi ya Premia Jumamosi.

Aprili 2016, Bodi ya Kimataifa vya Soka (IFAB) iliidhinisha kubadilishwa kwa kanuni za soka na kuondoa hitaji la kadi nyekundu moja kwa moja kwa mchezaji anayefanya kosa linalomnyima mpinzani nafasi wazi ya kufunga bao.



Mambo Ambayo Unatakiwa Kuyakumbuka Kila Wakati



Naomba pia nitumie wasaha huu kuweza kukaribisha katika makala yetu ya leo ili tuweze kujifunza juu ya mafanikio. Naamini unajua kujifunza hakuna mwisho, hivyo unatakiwa kila siku kuweka maarifa ya kukusaidia, ukishindwa kufanya hivyo utakwama.

Katika makala yetu ya leo nitaomba tu nikukumbushe mambo ambayo unatakiwa uyakumbuke kila wakati kwenye  maisha yako . Ni mambo ya msingi kwani yatakusaidia kuweza kuwa na mtazamo chanya na kubadili mambo mengi sana kwako.

1. Mambo yaliyopita hayawezi kubadilishwa tena.
Unatakiwa kuelewa kama kuna mambo ambayo yameshapita huwezi kuyabadilisha tena hata kama yalikuumiza au ulifanya makosa kiasi gani. Kwa sasa unatakiwa kuganga yajayo, habari ya mambo yaliyopita yatumie kama fundisho tu kwako, lakini ndio yameshapita, usiumize kichwa na kujilaumu sana.

2. Maoni ya watu hayaamui hatima ya maisha yako.
Hata siku moja usije ukakaa ukafikiri kwamba maoni ya watu wengine wanayosema juu ya wewe ndiyo yanaamua maisha yako yawe vipi. Maisha yako yanabaki hivyo yalivyo kwa sababu wewe umeamua yawe hivyo. Lakini usikubali hata siku moja maoni ya watu yakurudishe nyuma na usiyatumie kama kisingizio.

3. Maisha yako yatakuwa mazuri tu ukijipa muda.
Ukiamua siku zote kubadilisha maisha yako unaweza. Kikubwa jipe muda wa kutosha kubadilisha maisha yako hatua kwa hatua na kila kitu kitabadalika. Haijalishi unaona maisha yako ni magumu kiasi gani, lakini muda ndio kila kitu. Muda unaweza kusawazisha mambo mabaya na yakawa mazuri kabisa. Tumia muda wako vizuri.

4. Utashindwa tu, kama utakata tamaa.
Ndoto yoyote ile uliyonayo au ambayo unatamani kuifikia una uwezo mkubwa wa kuifikia. Ila hautaweza kuifikia ndoto yako hiyo ikiwa utafika mahali wewe mwenyewe utaamua kukata tamaa. Moja ya sumu kubwa ya kimafanikio ni kukata tamaa, ukikata tamaa ujue kila kitu kwako kimeishia hapo na hutaweza kusogea tena.

5. Furaha ya kweli inapatikana ndani mwako.
Ukweli huu hautakaa ubadilike kamwe kwamba furaha ya kweli inapatikana ndani mwako na wala si nje yako. Unaweza ukakazana sana kutafuta furaha nje kwa kufanya vitu ambavyo unaamini vitakupa furaha, lakini ukivipata vitu hivyo unashangaa ile furaha tena bado huna. Hivyo jifunze kutafuta furaha ya kweli ndani mwako.

6. Mawazo chanya, ni njia ya mabadiliko chanya pia.
Mbinu mojawapo ya kuwa na maisha bora. Ni kwa wewe kuwa na mawazo chanya. Unapokuwa na mawazo chanya ni rahisi sana kwa wewe kuweza kuleta mabadiliko chanya pia. Watu wengi wanashindwa kwa sababu ya kuwa na mlundikano wa mawazo mengi ambayo kwao ni hasi. Kuwa na mawazo chanya ubadili maisha yako.

Yapo mambo mengi ya kukumbuka kila unapoelekea kwenye mafanikio yako. Kwa leo hii nimekukumbusha mambo haya machache. Kwa kuyafanyia kazi itakuwa sehemu kubwa ya mabadiliko kwenye maisha yako.

Nufaika Na Kilimo Bora Cha Matango



Habari rafiki na karibu sana katika safu hii ya makala za kilimo. Katika somo liliopita tuliangalia juu ya umuhimu wa kutumia mbegu bora na faida zake. Sasa leo tutaangalia kilimo cha matango kwa kutumia mbegu bora inayoitwa Hybrid Cucumber YETU F1 ambayo utaanza kuvuna baada ya siku 45-50 kutoka kupandwa kwake.

YETU F1 ni mbegu chotara ambayo ina umbo zuri na hupendwa sana na walaji. Kiasi cha mbegu 300g(Gramu 300) huweza kutosha ekari moja ambayo utainununua kwa shilingi laki tatu(300,000/=) za kitanzania.

 UANDAAJI WA SHAMBA.
Chagua sehemu iliyo nzuri,na ukipata sehumu ya tifutifu iliyo changanyikana na mchanga itakuwa vizuri zaidi.

Pia ukipata sehemu yenye udongo mzito lakini usiwe una tuamisha maji.
Lima shamba na hakikisha umelisawazisha vizuri(yaani hallowing),baada yapo panga matuta yako.

KIASI CHA MBEGU.
Gramu 300 zenye kiasi ya YETU F1 kinatosha kupanda eneo la ekari moja(100m×40m).
Na hii aina ya mbegu 1g ina mbegu 30-40.

KUPANDA.
Kabla ya kupanda hakikisha una mbolea ya kupandia kama DAP ikichanganywa na Agrigrow starter yenye madini mengi ya phosphorus.

Panda mbegu kwa nafasi 150cm×45cm mbegu mbili mbili kila shimo.
Na hii mbegu huota baada ya siku tatu hadi tano,hivyo huchukua muda mfupi kuota.
Mara baada ya kuota tumia mbolea ya majani Agrigrow starter ambayo itaimarisha mizizi hivyo kurahisisha mmea kupata chakula kutoka kwenye udongo.
Huu mmea huchukua muda mfupi kukua hivyo hivyo mara baada ya kuota baada ya siku chache tumia mbolea ya yara mila winner kukuzia.

Pia yatakavyo anza kutambaa tumia mbolea ya majani Agrigrow vegetative hii itafanya yawe na matawi mengi hivyo kuongeza uzalishaji.

Maua yakianza kuonekana tuu,tumia mbolea ya majani Agrigrow flowering and fruiting,hii itasaidia maua kuto pukutika,pia itaboresha muonekano wa tunda,itafanya maua yawe mengi hivyo na kupatikana kwa matunda mengi.

Epuka kumwagilia maji jioni sana kwa kuwa unaweza ukasababisha magonjwa kama ya fangasi kwa mmea.

Pia epuka kupulizia dawa pale wadudu wa muhimu wawapo shambani(kama nyuki)kwani kutafanya kupunguza kwa mazao shambani.

DAWA ZA WADUDU
Ukiwa ni mkulima unayelima kitaalamu na unayetaka mafanikio kupitia kilimo yakufaa kuwa na dawa za wadudu zifuatazo.

1. Prosper 720EC yenye mchanganyiko wa sumu mbili(Profenofos 600g/L +Cypermethrin 120g/L),hii ni dawa ambayo ina ua wadudu katika wigo mpana(yaani ni broad spectrum). Na mchanganyiko wake ni 2mls au 2cc kwa maji lita 1.
2. Avirmec 1.8EC (Yenye sumu ya Abamectin) hii itauwa utitili shambani wa aina yote,na mchanganyiko wake ni 7mls kwa lita 20 za maji.
3. Dawa ya ukungu Agrilax 72WP,hasa kwa nyakati za baridi,hii ni dawa ambayo ina mchanganyiko ya wa sumu mbili yaani Mancozeb na Metalaxyl,ambayo mancozeb kwa ajiri ya kukinga(Preventive)  na metalaxyl kwa kutibu(Curative).

Hivyo Agrilax hukinga na kutibu magonjwa yote yatokanayo na fangasi(yaani fungicide diseases).

MAVUNO.
Matango(YETU F1) huwa tayari baada ya siku 45-50 kutoka siku ya kupandwa.
Je utakuwa na miche mingapi kwa ekari moja? Kwa kawaida miche hufikia 11850.
Tuliangalia katika somo la matikiti kanuni ya kutafuta idadi ya miche yaani Plant population(I.e PP)
Plant population(PP) =(Area/Spacing) ×no of seeds per hole.
 Kwa mfano:-Area(A)=1acre=4000m square.
-Spacing (SP)=150cm×45cm or 1.5m×0.45m.
-No of seeds to be sown per hole=2seeds.
-Required: Plant population (PP)

Then,from the formula;-
 PP=((A/SP))×no of seeds per hole.
 PP=((4000)÷(1.5×0.45))×2.
 PP=(4000÷0.675)×2
 PP=5925×2
 PP=11,850Plants/acre
Therefore, there will be 11,850plants per acre.

Na haya matango kwa matunzo mazuri, huwa na matunda mengi sana ambayo yataweza kufikisha viroba 150 kwa makadilio ya chini kabisa  ambayo utauza kwa sh 70,000/= kwa kiroba kimoja kwa bei ya chini kabisa.

Viroba 150@sh 70,000 ni sh 10,500,000/= kwa makadilio ya chini na hyo pesa ni kwa ekari moja tu.
Na hayo mapato ni kwa wale ambao wamepanda bila kuwekea nguzo(Non trellised)
Kwa wale watakao wekea nguzo(Trellised) wataweza kutumia eneo dogo na kupata mavuno mengi zaidi.

Na hivi ndivyo kilimo biashara kinavyotakiwa kuendeshwa(lima eneo dogo vuna mazao mengi)
Hebu tuangalie kwa wale watakao wekea nguzo(Trellised Cucumber)
Shamba la ekari moja(4000m square), Spacing =80cm×40cm(0,8m×0.4m),number of seeds per hole =1seed,Plant population (PP)=?

Therefore:-
PP=(Area/spacing) × no of seeds per hole.
PP=((4000)÷(0.8×0.4))×1.
PP=4000÷0.32
PP=12,500Plants/acre

  • -Na kwa kuiwekekea nguzo(Trellised cucumber) huweza kuzaa matunda mengi zaidi kuliko bila kuyawekea nguzo.
  • -Kwa kuyawekea nguzo mche mmoja huweza kuzaa matunda 15-30 kwa mche mmoja.
  • -Tuchukulie kwa makadilio madogo kabisa mche mmoja umezaa matunda 15
Kwa hiyo basi;-
1plant=15fruits
12500plants=x?

By crossing:
x=12500×15
x=187,500fruits/plants

  • -Kwa hiyo utakuwa na jumla ya matunda 187,500 kwa ekari moja
  • -Kwa kuuza kwa bei ndogo kabisa ya sh 50 kwa tunda moja,utakuwa na jumla ya fedha =187,500×50= Tzs 9,375,000/=
  • -Kwa watakao uza kwa sh 100 kwa tunda moja,basi utakuwa na jumla ya pesa 187,500×100=18,750,000/=.


Kazi kwako kwa wewe mkulima unaye taka mafanikio,tumia mbegu bora (Hybrid seeds) zikuletee mafanikio.

Funguo Tano Za Mafanikio Ya Mjasiriamali Wakati Wote



Kitu kizuri kwa mjasiaramali yoyote yule uwe unaanza au tayari safari hiyo  ulishaanza ni kujiandaa kuwa mshindi. Ni muhimu sana kujua wewe ni mshindi kwa kile unachokifanya bila kujali ni changamoto zipi unakutana nazo.

Lakini hata hivyo huwezi kuwa mshindi kama hutaweza kujua siri ya ushindi huo utaupata vipi. Kutokana na hilo sasa hapo ndipo unalazimika kuzijua funguo tano za  mafanikio ukiwa kama mjasiriamali.

Hizi ni funguo tano kweli kwa mjasiriamali ambazo ukizitumia, zitakupa mafanikio na kukufikisha kule unakotaka kufika . Funguo hizo ni zipi, fuatana nasi katika makala yetu ya leo kujifunza.

1. Weka kushindwa nyuma kabisa.
Kwa kawaida huwa yapo makosa  na kushindwa kwingi hasa pale unapoanza biashara au hata pia unapokuwa unaendelea na biashara yako. Yote hayo yanapotokea ikiwa kweli wewe ni mjasiriamali uliyenuia hebu yasahau.

Kitu kukubwa kwako angalia kule unakokwenda. Makosa ni sehemu pia ya kukusaidia kufanikiwa kule unakokwenda ikiwa utajifunza. Acha kuamini kwamba utashindwa kirahisi. Amini utashinda kwa hicho unachokifanya.

2. Weka juhudi nyingi kila siku.
Anza siku yako kila siku kwa kujua kwamba unakwenda kuweka juhudi nyingi sana ambazo kwa vyovyote vile zitakuletea matunda. Jione mshindi kila iitwapo leo. Acha kujiona mnyonge.

Unapokuwa mjasiriamali unayejitambua ni lazima uelewe hili kwamba mafanikio yako yanategemea sana pia kutokana na juhudi unazoziweka. Hakuna kubahatisha ni kuweka juhudi ndiko kutakapokupa matokeo chanya.

3. Jifunze na jirekebishe kila siku.
Usiruhusu kutokujifunza, kila siku jifunze unapokuwa kwenye safari yako ya ujasiriamali. Kuna njia nyingi za kujifunza kama semina, mitandao na hata kutumia vitabu, hapo chagua njia iliyo bora kwako na ujifunze kila siku.

Kujifunza kunakusaidia sana kuchukua taarifa kutoka kwa wajasiriamali waliobobea kutoka sehemu mbalimbali duniani na kunakufanya na wewe kuzidi kuwa bora. Tumia muda hapo japo kidogo kujifunza na usiache.

4. Fuatilia biashara yako kwa ukaribu sana.
Ni vyema kutambua upo umuhimu wa wewe kuifatilia biashara yako kwa ukaribu sana kuliko unavyofikiri. Acha kufanya sana biashara yako kwa simu, kuwa karibu nayo.

Hata pale inapotokea umeajiri watu wengine, hiyo isiwe eti ndio basi kila kitu kimeishia hapo. Upo ulazima pia wa wewe kufatilia hatua zingine nazo kwa ukaribu zaidi kila wakati.

5. Kataa kushindwa mapema.
Kukutana na magumu katika kitu chochote ni jambo la kawaida. Sasa najua wewe ni mjasiamali mkomavu jipe ahadi kwamba hata ikitokea magumu vipi, kukata tamaa mapema  lisiwe jambo rahisi kwako.

Kila wakati ukijifunza kutumia funguo hizi tano za mafanikio katika safari yako ya mafanikio utafanikiwa.

Hii Ndiyo Sababu Kwa Nini Utangaze Biashara Yako



Watu wengi wamekuwa wakijiuliza maswali mbalimbali ambayo yanahusiana na masuala ya kibiashara. Na miongoni mwa maswali ambayo wamekuwa wakiniuliza ni kuhusu ni nini faida ya kutangaza biashara kwa sehemu kubwa?

Swali hili ndilo limenifanya nishike kalamu yangu ili niweze kulijibu. Nakusihi twende sambamba ili niweze kueleza kwa kinagaubaga, kwa nini unapaswa kuitangaza biashara yako tena kwa nguvu zote.
Matangazo ni usambazaji wa taarifa  sahihi  kuhusu bidhaa au huduma kutoka kwa mfanyabiashara kwenda kwa mteja. Matangazo ndiyo roho ya biashara, kwani bila kufanya biashara yako bila matangazo ni sawa na bure.

Nafikiri pia utakubaliana nami ya kuwa ili uweze kufanya biashara  yenye tija ni lazima uitangaze biashara yako, kwani " biashara ni matangazo".  Matangazo ndiyo yatakuyokufanya uweze kuongeza mauzo ya kibiashara kila wakati.

Kwa kuzingatia hilo unaweza kuitangaza biashara yako kwa njia ambayo itakuwa ni rahisi kwako. Na sababu kubwa ya kuitangaza biashara yako ni kuongeza wateja wapya.

Leo na dhumuni kubwa la kutangaza biashara yako ni kukutana na na watu wapya,  ukiona umetangaza biashara yako na hakuna mteja mpya hata mmoja ujue fika kuna mahala ambapo umekosea.

Hivyo fanya tathimni upya na ujipange upya na kuona ni jinsi gani unaweza kuitangaza biashara hiyo. Vile vile katika upangaji wa malengo ya kibiashara hakikisha ya kwamba unapanga na mbinu za kukutana na watu wapya kila siku.

Nasisitiza juu ya kukutana na watu wapya, kwa sababu nimegundua ya biashara nyingi zimekuwa hazifanyi vizuri kwa sababu zimekuwa na watu ambao wanaizunguka biashara ile ni wale wale kila siku. Hivyo kila siku fanya tathimini juu wateja wapya ambao wamekuja katika biashara yako.

Asante kwa kutembelea mtandao huu wa dira ya mafanikio,  usisite kumshirikisha na mwingine ili aweze kujifunza

MAGAZETI YA LEO 2/11/2017

Friday 1 December 2017

Audio | Nyashinski – Hayawani | Mp3 Download

Audio | Nyashinski – Hayawani | Mp3 Download

Audio | Nyashinski – Hayawani | Mp3 Download


                                                 DOWNLOAD HERE

Audio | Sholo Mwamba – Kama Ronaldo | Mp3 Download

Audio | Sholo Mwamba – Kama Ronaldo | Mp3 Download

Audio | Sholo Mwamba – Kama Ronaldo | Mp3 Download


                                                              DOWNLOAD HERE

Audio | Diamond Platnumz Ft. Rick Ross – WAKA | Mp3 Download

Audio | Diamond Platnumz Ft. Rick Ross – WAKA | Mp3 Download

Diamond Platnumz Ft. Rick Ross - WAKA

Audio | Diamond Platnumz Ft. Rick Ross – WAKA | Mp3 Download


                                                     DOWNLOAD HERE

Umeme wakatika karibia nchi nzima kuanzia jana



Dar es Salaam. Wakati umeme ukiwa umekatika nchi nzima kuanzia jana Alhamis, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema huduma hiyo imeanza kurejea kwenye mikoa ya Iringa, Dodoma na Tanga.

Akizungumza leo Ijumaa, Desema 1, 2017, Kaimu Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Leila Mhaji amesema umeme umekatika katika mikoa yote iliyounganishwa katika gridi ya Taifa.

Amesema wataalam wa shirika hilo wanaendelea kurekebisha mifumo ya gridi ya Taifa ili kufanya matengenezo ya hitilafu iliyotokea.

“Marekebisho ya mafundi wetu yamesababisha umeme kurejea katika mikoa ya Iringa, Dodoma na Tanga,” amesema.

Amesema wataalam wamegundua mfumo wa gridi haujatengemaa vizuri na hivyo wanaendelea na kazi ya kurekebisha usiku na mchana ili kuhakikisha huduma hiyo inarejea katika hali yake ya kawaida.

“Tutaendelea kuwapa taarifa na tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza,” amesema.

Amewatahadharisha wananchi kutokushika wala kukanyaga nyaya zilizokatika au kuanguka kwa kuwa ni hatari.

Ameitaja mikoa ambayo umeme haujakatika kuwa ni Kagera na Ruvuma ambayo haijaunganishwa na gridi ya Taifa.

Barcelona kuimaliza Livepool


Barcelona imemgeukia kwa mara nyingine kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Philippe Coutinho, safari ikimtengea Pauni 130 milioni na mshahara mnono.

Barcelone imerejea Liverpool kwa maa ya tatu, baada ya dau lake la awali kukataliwa na klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu England.

Mbali na kutaka kumngoa kwa dau kubwa, Barcelona imepanga kumpa mshahara wa Pauni 137,000 kwa wiki ili kupata saini ya nyota huyo katika dirisha la usajili Januari, mwakani.

Barcelona imemuweka sokoni mchezaji Arda Turan ili kupata fedha za kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Brazil.

Endapo Barcelona itakosa saini ya kiungo huyo, imesema itamfuata katika usajili ujao wa majira ya kiangazi. Paris Saint Germain (PSG) nayo imejitosa kuwania saini ya Coutinho.