Saturday 25 November 2017

Chelsea wawasili Liverpool tayari kwa kazi



Chelsea wametua salama jijini Liverpool kwa ajili ya mechi yao dhidi ya Liverpool ambayo inasubiriwa kwa hamu leo Anfield.

Lakini kiungo mkongwe wa timu hiyo, Cesc Fabregas amefanya kituko wakati wakiwasili, ameonekana akiwa amefunika uso wake gubi gubi.

Kwa kila timu, mechi hiyo ni muhimu, Liverpool ikataka kurejesha imani na kasi yake katika EPL lakini Chelsea ambao ni mabingwa watetezi wanataka kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kutetea taji.

No comments:

Post a Comment