Friday 24 November 2017

Okwi bado hana nafasi ya kuivaa Lipuli



Simba imeendelea kujifua lakini kiungo mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi bado hajawa fiti na tayari kuichezea Simba katika mechi dhidi ya Lipuli.

Simba itaivaa Lipuli katika mechi yake ya 11 ya Ligi Kuu Bara katika msimu huu. Mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Okwi ambaye ni kinara w akufunga mabao aliumia enka na inaonekana bado hajawa fiti kwa kuwa hakushiriki mazoezi ya Simba leo.

No comments:

Post a Comment