Saturday 3 February 2018

Nchemba awataka wanaotoa vitambulisho wawe makini

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amewataka watendaji wanaosimamia usajili wa wananchi kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho wa Taifa kuwa makini.

Akizungumza leo Februari 3, 2018 katika uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho hivyo kwa wakazi wa Tabora,  Mwigulu amesema umakini huo utasaidia vitambulisho hivyo kutotolewa kwa watu wasiostahili.

Amesema miaka ya nyuma wakati utaratibu wa kutoa vitambulisho hivyo haujaanza, baadhi ya raia wa kigeni walikuwa wakitumia mwanya huo kunufaika na huduma za jamii kama elimu.

“Watu hao walipomaliza masomo walirejea katika nchi zao na kuzinufaisha kwa namna moja au nyingine wakati wametumia pesa za watanzania. Mnapaswa kuwa makini ili kubaini wageni,” amesema Mwigulu.

Amesema kila mwananchi anatakiwa kuwa mlinzi wa mwenzake ili kuhakikisha hakuna mgeni anayepenya na kupata kitambulisho hicho.

“Uandikishaji na utoaji wa vitambulisho hivi ni bure. Wananchi hawapaswi kutozwa fedha yoyote,” amesema.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Andrew Massawe amesema lengo ni kuhakikisha mpaka Desemba, 2018 utoaji wa vitambulisho hivyo uwe umefanyika nchi nzima.

Ametaja faida za vitambulisho hivyo kuwa ni kusaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa nchi na wananchi kutambulika haraka wanapokwenda kupata huduma mbalimbali, zikiwemo afya na elimu

Wanaofanya udanganyifu kwenye asasi za kiraia waonywa

Asasi za kiraia zimetakiwa kufuata taratibu kabla ya kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi ili kukwepa udanganyifu, ikiwa ni pamoja na kuwachangisha fedha na kutokomea kusikujulikana.

Kauli hiyo imetolewa leo Februari 3, 2018  na ofisa maendeleo ya jamii Manispaa ya Temeke, John Bwana wakati akizindua  mradi wa kuwajengea wanawake uwezo kuhusu ujasiriamali ili  kujiinua kiuchumi ulioandaliwa na asasi ya Iwapoa.

Amesema kuna lundo la asasi za kiraia zinazotoa mafunzo kiholela na kuwatapeli wanawake kwa kuwachangisha michango na kutokomea na fedha zao.

“Iwapoa mmefanya jambo la maana kufuata taratibu za kuonana na mamlaka husika na kupata wataalamu kutoka katika kata mtakazofanya kampeni hii ya kupunguza umasikini kwa kuwajengea wanawake uwezo,|” amesema na kuongeza,

“Nawaunga mkono na ninatoa rai kwa asasi nyingine zisizofuata utaratibu zifanye hivyo mara moja kwa sababu tunazifuatilia na tukizibaini tutazizuia kufanya kazi zake katika maeneo yetu.”

Mratibu wa  mradi huo kutoka Iwapoa,  Yusuph Kutegwa amesema mradi huo utatekelezwa katika kata sita za Manispaa ya Temeke.

Amezitaja kata hizo kuwa ni Buza, Keko, Chamazi, Vituka, Azimio na Charambe.

Amesema utawafikia wanawake 150 kutoka katika maeneo hayo waliyoyachagua kutokana na kuwa na wingi wa watu, wakiwamo wanawake wasiokuwa na shughuli za kudumu.

“Ili kuwapatia masoko na mitaji tutawaunganisha katika vikundi vya watu watano watano, ili iwe rahisi kuwapa ujuzi kwa pamoja, ”amesema Kutegwa.

Nduda, Mbonde njiani kurejea dimbani

Mlinda mlango namba mbili wa Simba, Said Mohammed 'Nduda' wiki ijayo anatarajia kujiunga na wenzake tayari kuanza mazoezi baada ya kuwa nje kwa miezi mitano, kufuatia kufanyiwa upasuaji wa goti Oktoba mwaka jana nchini India.

Nduda aliyesajiliwa na klabu ya  Simba Julai mwaka jana akitokea Mtibwa Sugar ya Morogoro, hajacheza mechi yoyote msimu huu kutokana na maumivu ya goti aliyoyapata Agosti mwaka jana mazoezini akiwa visiwani Zanzibar wakati Simba inajiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu wa jadi, Yanga Agosti 23, mwaka jana Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.

Kwa sasa mlinda mlango huyo ameanza programu za mazoezi yake binafsi tangu mwanzoni mwa mwaka huu, akijifua ufukweni kwa mazoezi.

Wakati huo huo, beki wa kati wa Simba, Salim Mbonde anaendelea na mazoezi ya gym baada ya kuwa nje kwa zaidi ya miezi mitatu kufuatia kuumia Oktoba 15, mwaka jana katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara dhidi ya timu yake ya zamani, Mtibwa Sugar uliomalizika kwa sare ya 1-1 mjini Dar es Salaam.

Kiongozi mwengine wa Upinzani akamatwa Kenya

Mbunge mwingine nchini Kenya, amekamatwa kuhusiana na mzozo unaozunguka kujiapisha kwa aliyekuwa waziri mkuu Raia Odinga kwa kile anachokitaja kama rais wa watu wa Kenya.

Mbunge wa Makadara jijini Nairobi George Aladwa alikamatwa asubuhi ya Jumamosi nyumbani kwake na maafisa wa idara ya upelelezi na kupelekwa hadi makao makuu ya idara hiyo kwa mahojiano zaidi.

Aladwa ambaye amewahi kuwa meya wa jiji la Nairobi, alikuwa katika mstari wa mbele katika mipango ya sherehe hizo ambayo haikuwa na idhini ya serikali.

Aladwa sasa ni mbunge wa pili kukamatwa kuhusiana na hafla hiyo ambayo pia imeshutumiwa na jamii ya kimataifa.

Mbunge mwingine wa Nairobi Tom Kajwang alikamatwa na kufikishwa mahakamani na hatimaye kuachiliwa kwa dhamana.

Mwanaharakati mwingine wa upinzani wakili Miguna miguna pia alikamatwa siku ya Ijumaa na angali anazuliwa na polisi licha ya mahakama kuruhusu kuachiliwa kwake kwa dhamana.

Bwana Aladwa alikamatwa siku ya Ijumaa usiku katika nyumba yake iliopo Buruburu kulingana na kiranja wa walio wachache bungeni Junet Mohamed.

Bwana Mohammed ambaye pia mbunge wa Suna Mashariki alisema kuwa bwana Aladwa kwa sasa anazuiliwa katika makao makuu ya ujasusi.

Polisi hawajatoa tamko lolote kuhusiana na kukamatwa kwa Aladwa

Msanii Radio azikwa kwao Uganda

Msanii Radio wa nchini Uganda ambaye alifariki Februari 1, amezikwa leo kijijini kwao Nakawuka nchini Uganda, na kuhdhuriwa na maelfu ya watu kutoka sehemu mbali mbali za nchi hiyo na wasanii wa nchi jirani.

Hapo jana Ijumaa ya Februari 2, wananchi wa Uganda na mashabiki wa muziki walipata fursa ya kufanya ibada ya mwisho ya kumuombea marehemu kanisani, na kisha baadaye mwili wake kupelekwa kwenye uwanja wa michezo wa Airstip, ambapo walikesha nao huku kukipigwa show ya nguvu kutoka kwa wasanii mbali mbali wa nchini Uganda.

Kabla ya mazishi hayo kuliibuka mvutano mkubwa wa nguo ya kuvalishwa marehemu, huku Lilian Mbabazi ambaye ni mama wa watoto wake wawili ambaye mwenyewe alimtambulisha kama mke wake akitaka marehemu azikwe na suti aliyovaa kwenye tamasha la 'Nakudata' ambayo ndio ngoma iliyompa umaarufu na kumfanya atoboe kwenye game, na mwanamke wake mzungu ambaye amezaa naye mtoto mmoja akisema marehemu alitaka akifa azikwe na nguo za jeshi kwani alipenda kuitwa mwanajeshi, na hatimaye akavalishwa gwanda za jeshi.

Asubuhi ya leo mwili huo ulipelekwa kijijni kwao Nakawuka na kuwekwa kwenye makazi yake ya milele, ambapo kwenye tukio hilo watu walionekana kuwa wengi na baadhi wakizimia.

Miongoni mwa wasanii waliohudhuria mazishi hayo ni msanii na mbunge Jaguar wa Kenya, wasanii mbali mbali wa Uganda na viongozi wa serikali.

Diwani Dar Aja Na Mpango Kunusuru Wananchi Wake



Diwani wa kata ya Salanga jijini Dar es salaam Harun Mdoe amekuwa na mpango mkakati wa mda mfupi na mrefu kuhusiana na barabara ambayo kwa sasa imekua kero kwa wananchi wa eneo hilo.

Mdoe amesema hayo leo alipotembelea barabara hiyo ambayo inaunganisha Matangini, Michungwani, King'ongo, Matosa, Kata ya Goba pia kuelekea Bagamoyo ambapo kwa mkakapi wa mda mfupi wamekuwa wakiweka vifusi ambavyo vinasaidia angalau kupitika kwa urahisi.

Kutokana na kero hiyo pia amewataka wananchi wanaoishi maeneo hayo kuacha mara moja tabia ya kumwaga maji barabarani ambayo yanasababisha uharibifu na wataoendelea kufanya hivyo watachukuliwa hatua za sheria.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Michungwani Ismaili Kipungula amesema kuwa kuna shida kubwa katika barabara hiyo ambayo inaunganisha mitaa mitatu.

"hii barabara imekuwa ni tatizo kwamba imeoza na sio kuharibika tumejaribu kuhangaika kama mtaa tukishirikiana na wananchi pamoja  Diwani wetu kama mnavyoona hizi ni jitihada za wananchi wenyewe lakini barabara bado sio nzuri hivyo tunaiomba Serikali waiangalie hii barabara pia wenzetu wa Tarura ambao wamekubali kutengeza wafanya haraka kwani ilifika hatua tulika mawasiliano" amesema Kipungula

Aidha kwa upanda wake mkazi na mtumiaji wa barabara hiyo Upendo Mbise amesema kuwa kina mama wamekuwa wakijifungulia njiani kutokana na adha na ubovu ulipo mimi mwenyewe nikiwa kama shahidi juzi mama mmoja alijifungulia njiani hali ambayo ni hatari pia inaweza kupelekea hata kifo


Mkuu wa shule aingia matatani kwa kuchangisha michango



Sumbawanga. Mkuu wa mkoa wa Rukwa, Joachim Wangabo ameagiza mkuu wa shule ya sekondari Muhama manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa kuchukuliwa hatua kwa tuhuma za kuwatoza wanafunzi michango ya Sh5,000 kama gharama ya kuwapatiwa fomu za maelezo ya kujiunga na shule hiyo.

Wangabo ametoa agizo hilo jana Februari 2, 2018 wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara kata ya Malangali baada ya baadhi ya wananchi kufichua jambo hilo.

Mmoja wa wananchi hao, Sadock Kalinga amesema wazazi wamekuwa wakichangishwa kiasi hicho cha fedha ili wapatiwe fomu hizo.

“Tulilazimika kutoa fedha hizi na kupewa stakabadhi kwa kuwa tuliambiwa mwanachi ambaye hatotoa fedha  hawezi kupewa fomu hizo na hivyo kukosa sifa ya kujiunga katika shule hii,” amesema Kalinga.

Baada ya kupokea malalamiko hayo na kuonyeshwa risiti iliyotolewa kama ushahidi, Wangabo amemhoji Mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga, Hamidu Njovu kuhusu uhalali wa mchango huo ambapo naye alikana kufahamu jambo hilo.

Alimuagiza mkurugenzi huyo kumchukulia hatua mkuu huyo wa shule kwa kuwa kitendo alichokifanya si sahihi kwa sababu Serikali imepiga marufuku michango shuleni.

“Ni marufuku kwa mwalimu yeyote kujihusisha na michango katika mkoa huu. Walimu kazi yao ni kufundisha na sio kuchangisha. Nakuagiza mkurugenzi kuchukua hatua katika hili na ninataka nipate taarifa’,” amesema.

Mwananchi:

Tume yaundwa kufuatilia korosho zenye kokoto

Serikali mkoani Lindi imeunda timu ya kuchunguza matukio ya baadhi ya wakulima kuchanganya mchanga na korosho kwa nia ya kuongeza uzito wakati wa kupima kwenye mizani, ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika kufanya hhujuma hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bw. Godfrey Zambi amewaambia waandishi wa habari mjini Lindi kuwa, korosho iliyochanganywa na mchanga kugundulika kwenye ghala la Buko mjini humo na korosho nyingine iliyochanganywa na kokoto za lami iligundulika nchini Vietnam baada ya kusafirishwa kutoka Tanzania, ambapo mwenye korosho hizo alidai alizinunua wilayani Liwale mkoani humo.

Amesema baada ya kupata taarifa hizo zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kuchafua taswira ya Tanzania kibiashara, imemlazimu kukutana na viongozi wa mkoa kujadili suala hilo na hatimaye kuunda timu ya uchunguzi wa matukio hayo ili hatua zichukuliwe haraka.

Pamoja na uchunguzi unaoendelea, Mkuu huyo wa Mkoa ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wa Chama cha Ushirika cha Pangatena wilayani Lindi wanashikiliwa kwa uchunguzi na kusimamishwa kwa bodi ya chama hicho baada ya kubainika korosho walizofikisha kwenye ghala kuu la BUCCO zina viroba vya mchanganyiko wa korosho na mchangaTume

Rais Trump awasiliana na viongozi wa Japan na Korea Kusini

Rais wa Marekani Donald Trump amewapigia simu viongozi wa Japan na Korea Kusini siku chache kabla ya michezo ya Olimpiki kuanza nchini Korea Kusini.

Kwa mujibu wa habari,Trump amefanya mazungumzo na waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe.

Viongozi hao wawili wamezungumzia mfumo wa ulinzi wa makombora wa Japan na vilevile uhamisho wa ngome ya Marekani katika kisiwa cha Okinawa.

Japan na Korea Kusini zimekuwa zikijitahidi kuidhibiti Korea Kaskazini kutofanya majaribio ya makombora ya nyuklia.

Korea Kaskazini ilirusha kombora la nyuklia mnamo mwezi Novemba mwaka jana.

Watatu wafariki kutokana na baridi kali

Watu watatu waripotiwa kufariki  nchini Uswidi kutokana na baridi kali Kaskazini mwa Uswidi.

Baridi kali katika eneo hilo la Kaskzini mwa Uswidi ilifuatiwa na theluji kali ambapo nyuzi joto ilikuwa 20 chini ya sifuri.

Uongozi wa eneo la Vesternorrland nchini Uswidi umefahamisha kuwa bariki kali katika eneo hilo imesababisha vifo vya watu watatu.

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini Uswidi imetoa tahadhari kwa raia  kutokana na kiwango kÅŸkubwa cha theluji ambacho kinatarajiwa katika za usoni.

Singida United yaipiga Mwadui FC 3-2

Singida United wameshinda kwa mabao 3-2 dhidi ya Mwadui FC katika mechi kali ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Namfua mjini Singida.

Wageni Mwadui walitangulia kwa mabao mawili kabla ya Singida kusawazisha na kufunga la ushindi.

Mechi hiyo ilikuwa ni ya kushambuliana kwa zamu ingawa Singida United walifanya mashambulizi mengi zaidi mwishoni.

Shuja wa Singida United alikuwa Kenny Ally Mwambungu ambaye alifunga bao kwa shuti kali ndani ya dakika 3 za nyongeza baada ya mwamuzi kuongeza dakika 5.


Shuti kali alilopiga na kumshinda kipa Massawe wa Mwadui ni baada ya kupokea pasi nzuri ya Mudathiri Yahya.

Mabao mawili ya Singida United ikisawazisha, yalifungwa na Salum Chuku na Deus Kaseke aliyeng'ara katika mchezo huo.

Vituo 46 vya kupigia kura kinondoni kuhamishwa

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeridhia kuhamishwa kwa vituo 46 vya kupigia Kura katika kata tatu za jimbo la Kinondoni zitakazofanya Uchaguzi mdogo wa Ubunge Februari 17 mwaka huu.

Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Ramadhani Kailima ameeleza kuwa uamuzi wa NEC kuridhia kuhamishwa kwa vituo hivyo, umetokana na makubaliano yaliyofikiwa katika Mkutano wa Msimamizi  wa Uchaguzi wa  jimbo la Kinondoni na Vyama vya siasa juu ya kuhamishwa kwa vituo hivyo vilivyokuwa kwenye nyumba za Ibada, Zahanati na maeneo ya majengo ya watu binafsi.

Amesema Tume imeridhika na uamuzi huo kwasababu hatua zilizochukuliwa ni sahihi kwa mujibu sheria na kanuni namba 21 ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambayo inaeleza kuwa ;  Vituo vya Kupigia Kura havitakiwi kuwekwa katika majengo ya nyumba za Ibada, kambi za jeshi, nyumba za watu binafsi na  ofisi za vyama vya siasa.

“ Tumejiridhisha kuwa baadhi ya vituo katika Kata ya  Kigogo vilikuwa katika nyumba za Ibada na vingine kuwa katika maeneo yenye ufinyu wa nafasi hivyo tumeridhia vituo hivyo vihamishwe na kupelekwa katika majengo ya umma” Amesema.

Amesema kuwa baadhi ya vituo vya kupigia Kura vilivyokuwa katika majengo ya umma ikiwemo Zahanati vimehamishwa katika shule za msingi za umma zilizo katika kata hizo  ili kuondoa usumbufu kwa wagonjwa.

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Mwananyamala Bi. Barima Omari ameeleza kuwa kata ya Mwananyamala ina vituo vya kupigia kura 65 na wapiga kura 27,589 na kuongeza kuwa vituo nane (8) vilivyokuwa katika shule ya Sekondari Kambangwa mtaa wa msisiri A vimehamishwa. Kati ya hivyo 6 vimehamishiwa katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa ya Msolomi na 2 kuhamishiwa uwanja wa kwakopa.

Naye Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi  Kata ya Kijitonyama Elizabeth Minga ameeleza kuwa Kata hiyo ina jumla ya vituo vya kupigia Kura 101, kati ya hivyo vituo 22 vimehamishwa.

Akifafanua kuhusu vituo hivyo amesema vituo 6 vilivyokuwa katika shule ya Sekondari Kenton vimehamia shule ya Msingi Mapambano na vituo 5 vilivyokuwa nje ya Ofisi ya serikali ya Mtaa wa Bwawani vimehamishiwa mbele ya ofisi hiyo.

Aidha, vituo 6  vilivyokuwa nje ya soko la Makumbusho vimehamia ndani ya Ofisi ya Meneja wa Soko hilo na vituo 5 vilivyokuwa  katika Ofisi ya Serikali za mitaa kijitonyama vimehamishiwa katika shule ya msingi kijitonyama.

Kwa upande wake Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Kigogo Bw. Singoro Mdegela ameeleza kuwa kata yake ina idadi ya Wapiga kura 27,000 na Vituo vya Kupigia Kura  59.

Amesema katika Kata hiyo vituo 16 vimehamishwa ambapo vituo 5 vilivyokuwa eneo la Kiwenge kwenye Msikiti wa Shiha vimehamia Uwanja wa People na Vituo 6 vilivyokuwa kwenye Zahanati ya Kigogo vimehamishiwa katika Shule ya Msingi Kigogo ili kuruhusu shughuli za matibabu kwa wagonjwa kuendelea.

Aidha, vituo 5 katika ofisi ya serikali ya mtaa wa Mkwajuni vimehamishiwa katika  shule ya secondari Kigogo.

Masoko ya mazao kuimarishwa

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali inataka kuimarisha masoko ya mazao yanayolimwa nchini ili kuwawezesha wakulima kupata tija.

Taarifa iliyotolewa leo Februari 3, 2018  na ofisi ya Waziri Mkuu inaeleza kuwa ametoa kauli hiyo jana Januari 2, 2018 wakati akikagua Kampuni ya Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), iliyoanzishwa kwa lengo la kuimarisha masoko.

Amesema kupitia Wizara ya Kilimo, Serikali imedhamiria kuimarisha masoko ya mazao yanayolimwa nchini ili kuwawezesha wakulima kujikwamua kiuchumi.

“Kupitia Wizara ya Kilimo tunataka kuimarisha masoko ya mazao yanayolimwa nchini. Wakati umefika kwa wakulima nchini kuona tija ya mazao wanayolima,” amesema.

Ametoa mfano zao la pamba ambalo wakulima walikuwa wanaingia mikataba na wanunuzi, mfumo ambao ulikuwa unawanyonya badala ya kuwanufaisha.

Awali, ofisa mtendaji mkuu wa TMX, Godfrey Malekano amemhakikishia Waziri Mkuu kuwa wamejipanga vyema kuanza minada ya mazao.

“Tutaanzia na zao la ufuta mwezi Mei, 2018 na kuendelea na mazao mengine kwa kadiri ya misimu ya mazao hayo ilivyo,” amesema.

Amesema kufanikiwa kwa soko la bidhaa na mfumo wa stakabadhi ghalani kunategemea msaada wa Serikali, “Soko la bidhaa la Ethiopia linalotajwa sana kwa mafanikio limefikia malengo yake kutokana na mkono wa Serikali.”

Tshishimbi apiga bao, Yanga ikiiua Lipuli 2-0


YANGA SC imejivuta kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Lipuli Uwanja wa Samora mjini Iringa.

Ushindi huo unaifanya Yanga SC ifikishe pointi 31 baada ya kucheza mechi 16, ikipanda hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu, sasa ikiwazidi kwa pointi Azam FC ambao wanacheza mechi yao ya 16 usiku dhidi ya Ndanda FC Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Yanga pia imepunguza pengo la pointi inazozidiwa na vinara, Simba SC hadi kubaki tano – lakini Wekundu wa Msimbazi nao watacheza mechi yao ya 16 kesho dhidi ya Ruvu Shooting Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Erick Onoka aliyesaidiwa na Geoffrey Kihwilio na Janeth Balama, Yanga ilipata bao moja kila kipindi.

Na mabao hayo yalikuja baada ya Yanga kupata pigo dakika ya 17 kufuatia kipa wake wa kwanza Mcameroon, Youthe Rostand kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo nafasi yake ikichukuliwa na chipukizi, Ramadhan Awam Kabwili.

Kiungo kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Papy Kabamba Tshishimbi alifunga bao la kwanza dakika ya 19 kwa kichwa akimalizia mpira uliotemwa na kipa Agathon Anthony Mkwando baada ya kichwa cha kuparaza cha winga Emmanuel Martin kufuatia kona ya kiungo Pius Charles Buswita

Kipindi cha pili, Yanga ya kocha Mzambia, George Lwandamina ilirudi na mchezo mzuri na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa na Buswita dakika ya 55, aliyempiga chenga kipa Mkwando baada ya pasi nzuri mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa kutokea pembeni kulia na kufunga bao zuri.

Yanga ilijitahidi kuendelea kusaka mabao zaidi, lakini Lipuli walikuwa imara na kumaliza mchezo kwa kipigo cha mabao 2-0.

Lipuli FC; Agathon Mkwando, Stephen Mganga, Ally Mtoni, Martin Kazila, Joseph Owino, Novaty Lufunga, Seif Karihe/Tola Mangonela dk69, Mussa Nampaka/Zawadi Mawiya dk71, Adam Salamba, Malimi Busungu na Jamal Mnyate/Jerome Lembele dk78.

Yanga SC; Youthe Rostand/Ramadhani Kabwili dk17, Hassan Kessy, Gardiel Michael, Kelvin Yondan, Said Juma ‘Makapu’, Papy Kabamba Tshishimbi, Emmanuel Martin, Raphael Daudi/Raphael Daudi dk86, Obrey Chirwa, Pius Buswita na Geoffrey Mwashiuya/Maka Edward dk81.

Man City yaambulia sare mikononi mwa Burnley

Mshambuliaji wa Manchester City, Raheem Sterling akikosa bao la wazi kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya wenyeji, Burnley leo Uwanja wa Turf Moor timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Man City ilitangulia kwa bao la Danilo dakika ya 22 kabla ya Johann Berg Gudmundsson kuisawazishia Burnley dakika ya 82.

New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods

New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods

New VIDEO: Justin Timberlake – Man Of The Woods

Justin Timberlake just delivered his fifth studio album Man Of The Woods and now he doubles down with an official music video for the project’s title-track featuring a cameo by his wife Jessica Biel, directed by Paul Hunter.


Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download

Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download
Audio | Chidinma X Young D X Toby Grey X Daphne – Egwu | Mp3 Download

Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

Audio | Marisa – UKARONDA | Mp3 Download

DOWNLOAD MP3

Yanga yajihakikishia ushindi dhidi ya Lipuli leo



KOCHA wa Yanga, George Lwandamina, amesema kama watashindwa kupata ushindi kwenye mchezo wa leo dhidi ya Lipuli ya Iringa watajiweka pabaya katika kuutetea ubingwa wao msimu huu.

Lwandamina, alisema kuwa kwenye mchezo wa leo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, wana kila sababu za kuhakikisha wanapata ushindi ili kuendelea kuifukuzia Simba inayoongoza ligi.

Yanga itaingia kwenye uwanja huo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 18 tangu Lipuli ilishuka daraja mwaka 1999 na kuwafanya mashabiki wa mkoa wa Iringa kushindwa kuziona timu kubwa na kongwe zenye mashabiki wengi, ikiwemo Yanga.

“Ni mchezo mgumu kama ilivyo michezo mingine, tupo ugenini lakini kwa namna mambo yalivyo ni lazima tupambane ili kutoongeza pengo la pointi na wanaoongoza ligi,” alisema Lwandamina.

Yanga imeachwa kwa pointi saba na Simba wenye pointi 35 huku Azam wanaoshika nafasi ya pili wakiachwa kwa pointi tano na vinara hao, kikosi cha Lwandamina kinashika nafasi ya tatu kwa kuwa na pointi 28.

Mchezo wa leo utamshuhudia mshambuliaji Ibrahim Ajibu akirejea uwajani baada ya kuukosa mchezo wa kombe la FA dhidi ya Ihefu, muunganiko wake na Obrey Chirwa unatazamiwa kuwa chachu ya ushindi kwa mabingwa hao watetezi.

Canavaro anena

Kuelekea kwenye mchezo wa leo, nahodha wa timu hiyo, Nadir Haroub ‘Canavaro’, amesema watahakikisha wanapambana mpaka dakika ya mwisho kuhakikisha wanapata ushindi.

“Tulitoka sare kwenye mchezo wetu wa kwanza Dar es Salaam, hiyo inaonyesha Lipuli si timu ya kuibeza, kama wachezaji tutahakikisha tunakuwa makini na kupambana muda wote,” alisema Canavaro.

Naye kocha wa Lipuli, Selemani Matola, aliiambia Nipashe kuwa wamejiandaa vyema kuwakabili mabingwa hao watetezi.

Askari Magereza watiwa mbaroni wakidaiwa kuua

KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA, EDWARD BUKOMBE.

ASKARI 12 wa Jeshi la Magereza wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wanahojiwa na polisi kwa tuhuma za mauaji yaliyochochewa na ugomvi wa mapenzi.

Askari hao wanadaiwa kumshambulia mkazi wa kijiji cha Kerenge wilayani hapa, Aloys Makalla na kusababisha kifo chake mwishoni mwa mwezi uliopita huku wakiwa wamevaa kininja.

Katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, imedaiwa kuwa saa chache kabla ya kifo chake, marehemu alikuwa amepigana na mmoja wa askari.

Kamanda Bukombe alisema tukio hilo lilitokea Januari 28 na kwamba askari 12 wa Magereza wanahojiwa na polisi katika upepelezi wake.

“Ni kweli tumepata taarifa za tukio hilo la mauaji ya mwanakijiji huyo na askari 12 tunawachunguza kupata ukweli wake, ili kuona kama kuna wanaohusika hatua ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Kamanda Bukombe.

Akihadithia mkasa wa mauaji hayo, mkazi wa kijiji cha Kerenge, Juma Salim, alisema marehemu alikuwa na mzozo wa muda mrefu na askari Magereza mmoja (jina tunalihifadhi) wakituhumiana kuingiliana katika penzi la mmoja wa wanawake kijijini hapo.

"Na siku hiyo (mzozo huo) ulizusha vurugu kubwa," alisema Salim.

Salim alisema katika ugomvi huo kati ya askari na Makalla, Magereza huyo alijeruhiwa na kurudi kwenye makazi yao lakini baada ya muda alirejea kijijini hapo na wenzake wakiwa wamevalia kininja na kuwapiga wenyeji.

Baadaye walimkamata Makalla waliyemtuhumu kumpiga mwenzao na kuondoka naye, alisema Salim.

Naye Jeniffer Leonard, mkazi mwingine wa Kerenge alisema askari hao waliondoka na Makalla kwa madai ya kumpeleka kituo cha polisi lakini walishangaa kupata taarifa za kifo chake baadaye.

HAKUMTAJA JINAAkielezea tukio hilo, Kamanda Bukombe alisema taarifa zinaonyesha kutokea ugomvi baina ya askari ambaye hata hivyo hakumtaja jina wala cheo chake na marehemu huyo, hali iliyosababisha Magereza kujeruhiwa.

Bukombe alisema baada ya kujeruhiwa, askari huyo alikwenda kambini kuchukua wenzake ambapo walirudi kwa mara ya pili na kumkamata marehemu, kumpakia kwenye gari na kuondoka naye kwa madai ya kumpeleka kituo cha polisi.

Kamanda Bukombe alisema taarifa kutoka kwa askari Magereza zinadai wakati wakiwa njiani, marehemu aliruka kutoka kwenye gari hiyo na kuanguka barabarani ambako alifikwa na mauti.

“Tunachunguza upi (ndiyo) ukweli wa marehemu," alisema Kamanda Bukombe. "Kauawa kwa kipigo cha askari hao ama (ni) kifo kinachotokana na kuanguka kwa kuruka kwenye gari."Mambo hayo ndiyo tunayoyachunguza tupate ukweli.”

Alisema matokeo ya uchunguzi huo ndiyo yatakayoamua kama kuna hoja na ukweli kwamba askari wamehusika na kifo cha marehemu na hatua zitachukuliwa, ikiwemo kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote.

Makamu wa Rais aguswa na Cover ya wimbo wa Nandy na Aslay



Makamu wa Rais, Bi Samia Suluhu Hassan (katikati) akiwa na wasanii Nandy na Aslay.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana jioni aliwakaribisha nyumbani kwake wasanii wa Bongo Fleva, Aslay Isihaka ‘Dogo Aslay’ na Faustina Charles maarufu kama Nandy kwa ajili ya mazungumzo mafupi na chakula cha jioni.

Katika mazungumzo yake na wasanii hao, Bi Samia alieleza kuvutiwa sana na marudio ya kibao cha SUBALKHERI kilichorudiwa na wakali hao wa Bongo Fleva hivi karibuni na kuwapa wosia wa kuendelea kufanya kazi nzuri zaidi na kujiepusha na makundi mabaya.

Esma aweka wazi mahaba yake kwa Wema Sepetu


Esma Abdul ‘Esma Platnumz’

MWANADADA Esma Abdul ‘Esma Platnumz’ ameonesha mahaba yake kwa staa mkubwa wa filamu Bongo, Wema Sepetu akidai kuwa, amekuwa shosti wake kwa muda mrefu na hivyo hawezi kujitenga naye.

Akipiga stori na gazeti hili, Esma alisema Wema ametoka naye mbali kiasi kwamba leo hii hawezi kumuweka pembeni na kujiweka zaidi kwa wifi wake wa sasa,  Zarina Hassan ‘Zari’.

“Jamani Wema hata kidogo siwezi kumuweka pembeni, hata kama aliachana na kaka yangu lakini kwangu bado ana umuhimu. Kama kila anayeachana na kaka basi
niwe naye mbali, nikifa inabidi nikazikwe Uganda au Sauzi maana Bongo sitakuwa na rafiki,” alisema Esma

Kauli ya kocha wa Simba yamwacha mdomo wazi Tambwe


KAULI ya Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma, aliyedai kwamba atafurahi zaidi kama straika wake Emmanuel Okwi atafunga mabao 30 msimu huu, imemshitua mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe.

Tambwe ambaye anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi katika msimu wa 2015/16 akifunga mabao 21, baada ya kusikia kauli hiyo ya Djuma alisema; “Siyo kazi rahisi Okwi kufunga mabao 30.”

Akizungumza na Championi Jumamosi, Tambwe alisema ili Okwi ambaye hivi sasa anaongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 12, aweze kufikisha mabao 30, anatakiwa kufunga katika kila mechi atakayocheza.

“Siyo kazi rahisi kwa Okwi kufunga mabao 30, kwani mzunguko wa pili ligi huwa ni ngumu sana, kila timu hupambana kuhakikisha inafanya vizuri ili kuwania ubingwa, nyingine zinapambana zisishuke daraja.

“Inabidi Okwi apambane kwelikweli na ajitahidi pia kufunga katika viwanja vya mikoani lakini kama ataendelea kutegemea Uwanja wa Uhuru na ule wa Taifa pekee, itakuwa ni vigumu kufikisha mabao hayo,” alisema Tambwe.

Uchebe akana madai ya kuwa Sangoma



Mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ akiwa na mume wake Ashrafu Uchebe.

MUME wa mwanamuziki Zuwena Mohammed ‘Shilole’ Ashrafu Uchebe amekana kuwa mganga (Sangoma) wa kutumia vitabu na kuweka wazi kuwa kazi yake ni ufundi wa magari.

Maelezo hayo yamekuja kutokana na madai yaliyokuwa yumeenea kwamba, mbali na kufanya mambo mengine lakini pia anatibu kwa kutumia Quran na amekuwa akifanya hivyo tangu alipokuwa Zanzibar.

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Uchebe alifunguka hivi: “Kama unavyojua kumuombea mtu dua ni jambo la kawaida lakini anayesaidia ni Mungu, hata wewe nakuombea tu dua na Mungu ndiye anasaidia ila hilo la kuwa mganga sijawahi, kazi yangu ni fundi wa magari,” alisema Uchebe

Jokate afunguka kuanzisha familia mwaka huu



Jokate Mwegelo

MWANAMITINDO ambaye ni kada wa CCM, Jokate Mwegelo baada ya kuanika kuwa mwaka huu ni sahihi kuingia kwenye maisha ya ndoa, ameibuka tena na kuanika kuwa 2018 ni mwaka wa kuwa na familia pia.

Akiongea na Risasi Jumamosi Jokate alisisitiza kuwa mwaka huu ni wa neema kwake na kufafanua kuwa ana mpango wa kuanzisha familia yake.

“Watu wajue tu kuwa mwaka huu nitaanzisha familia, sio kama ninawafumba lakini kwa uwezo wake Mungu wataona tu, wakae wakisubiri kwani lisemwalo lipo kama halipo linakuja,” alisema Jokate ambaye hakuweka wazi mwanaume atakayemuoa na kuanzisha naye familia

Mrema awatolea uvivu UKAWA


Mwenyekiti wa chama cha TLP Lyatonga Augustino Mrema amefunguka na kusema kuwa UKAWA hawampendi wala hawamtaki ndiyo maaana walifanya kila namna kuhakikisha wanampokonya jimbo la Vunjo kwa kumsimamisha James Mbatia katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Mrema amesema hayo jana Januari 2, 2018 akiwa kwenye kampeni za kumnadi mgombea ubunge Jimbo la Kinondoni kupitia chama cha TLP, Dokta Godfrey Malisa na kusema kuwa wapinzani nchi hii wamekuwa wakimchukia.

"Ni kweli kwamba UKAWA hawanipendi, hawanitaki wakaninyang'anya lile jimbo wakampa James Mbatia angekuwa basi anafanya kazi za wananchi wa Vunjo wala nisingelalamika. Angelikuwa mwaminifu kwa Rais wetu wala nisingehangaika wala kulalamika, lakini walininyang'anya jimbo kwa ulaghai na utapeli kwa maneno ili kunimaliza kwa wananchi wa Vunjo wakasema Mrema ni mzee na kweli ni mzee ila kuwa mzee siyo kosa wala siyo dhambi kwamba wazee hawana manufaa" alisema Mrema

Mbali na hilo Mrema aliendelea kusema

"Hawa UKAWA wananiita marehemu mtarajiwa ndiyo wenzangu kwa hiyo wakaninyanyasa, wakanizodoa na ndiyo maana nawaambia UKAWA wakiendelea na tabia hii ya kuwakataa wazee kama Mrema kama hawana lolote, hamtakaa mpate kura za wazee wa nchi hii kwa sababu maneno yenu waliyasikia. Kwanini mnatukataa sisi wazee"


Aliyewabagua Waaafrika afutwa kazi


Klabu ya soka ya West Ham imemfuta kazi mkurugenzi wa uajiri wa wachezaji wa timu hiyo Tony Henry kutokana na kauli yake ya kuwabagua wachezaji kutoka Afrika.

Tony Henry hivi karibuni alinukuliwa akisema kuwa timu hiyo haiwezi kusaini wachezaji kutoka Afrika kutokana na wachezaji hao kutowajibika vizuri kwenye baadhi ya majukumu yao.

Taarifa ya klabu hiyo imeeleza kuwa maneno ya Tony Henry sio msimamo wa klabu kwasababu timu haiamini katika ubaguzi wa aina yoyote ndio mana imeamua kumfuta kazi Henry ili hatua zingine zichukuliwe.

West Ham ina wachezaji sita kwenye kikosi cha kwanza wenye asili ya Kiafrika ambao ni  Cheikhou Kouyate, Pedro Obiang, Joao Mario, Angelo Ogbonna, Arthur Masuaku na Edimilson Fernandes.

Wengine ni mshambuliaji wa Senegal Diafra Sakho ambaye ameondoka kwenye dirisha dogo la Januari akajiunga na Rennes ya Ufaransa huku Andre Ayew wa  wa Ghana akielekea Swansea.

Mose Iyobo awachezeshea kichapo Shilawadu


 Watangazaji wa Kipindi maarufu cha Shilawadu kinachorushwa na Clouds tv,Soudy Brown na Kwisa wamechezea kichapo kutoka kwa Dancer wa Diamond,Mose Iyobo,usiku wa kuamkia  ijumaa,baada ya kutaka kumuhoji kuhusu matukio yaliyotokea hivi karibuni kati ya familia yake na mwanadada Tunda.

Wakithibitisha kutokea kwa tukio hilo,Shilawadu wameandika katika ukurasa wao wa instagram:

Kazi yetu ina changamoto kubwa sana..asilimia kubwa ya ma star wanatuunga mkono.

Usiku wa Leo wakati tukiwa kazini tumenusurika kumwagwa damu na mtu tuliemfuata kumuomba kufanya naye mahojiano,kati yetu kuna walioumia viuno,mikono, etc.kuna uharibifu wa vifaa vyetu vya kazi umetokea pia,wenzetu wanaendelea na matibabu Mungu  ni mwema  Mungu ni wetu sote na hili litapita bado tuna wasiwasi tu kama mhusika ataendelea kututafuta kwa ajili ya kutudhuru zaidi,tunasikitishwa sana na matumizi ya nguvu dhidi yetu sisi Wanyonge #Shilawadu

Kuna watu watasema Shilawadu wamezidina kusahau kuwa sisi ni wana Habari kama wanahabari wengine na kupata habari ni haki ya kila mwananchi kama ilivyo haki nyingine yoyote ile.Kifungu cha 18 cha katiba  ya Jamhuri ya Muungano 1977 na hatimaye kufanyiwa marekebisho mwaka 2005 inampa haki mtu na uhuru wa kujieleza na kutoa mawazo,uhuru wa kutafuta habari,kupata habari,na kuneza habari bila kujali mipaka,pia sheria hiyo inampa haki mtu ya kuwasiliana bila kubughudhiwa na mawasiliano na kufahamishwa wakati wowote masuala yoyote muhimu yahusuyo maendeleo yake na yahusuyo jamii yake kwa ujumla.

Imeandikwa na Mtayarishaji wa Kipindi cha Shilawadu Benedict Noel

Mourinho atoa ujumbe huu kwenye birthday ya mtoto wake


 Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho amemtakia furaha ya kuzaliwa mwanawe wa kiume Zuca baada ya kutimiza miaka 18 huku akiposti picha ya utotoni inayomuonyesha wakiwa pamoja katika kiboti.

Meneja huyo wa Man United ameposti picha hiyo huku akiandika “Furaha ya kuzaliwa Zuca sasa unamiaka 18 huitaji uwepo wangu tena kwenda kuogelea pamoja katika kiboti,”ameandika Mourinho kupitia mtandao wake.

Picha hiyo inamuonyesha Mourinho akiendesha kiboti hicho huku akiwa na Zuca.

Mwaka jana Mourinho aliwahi kumtakia furaha ya kuzaliwa mwanawe kwa kuposti ujumbe unao fanana na huo.

Zuca anacheza nafasi ya goli kipa katika academy ya Fulham akiwa amesaini kandarasi ya miaka miwili  akiwa na umri wa miaka 16.

Hapo hawali Zuca alikuwa akiitumikia klabu ya Chelsea na Real Madrid wakati timu hizo zikitumikiwa na baba yake.

Baada ya kumdiss Donald Trump, Diego Maradona yamkuta makubwa


Gwiji wa zamani wa timu ya taifa ya Argentina Diego Maradona amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutoswa visa ya kwenda nchini Marekani kutokana na matamshi aliyoyatoa dhidi ya raisi Donald Trump.

Maradona ana kesi na aliyekuwa mke wake aitwaye Claudia Villafane na alipaswa kwenda hadi Miami kusikiliza kesi hiyo lakini maofisa wa uhamiaji walimuwekea ngumu kupata visa ya kwenda nchini humo.

Maradona siku zilizopita alisikika katika moja ya interview zake akimuita raisi Donald Trump “chirolita” jina ambalo kwa Waargentina linatumika kwa watu ambao ni vibaraka wa watu wengine.

Baada ya Maradona kushindwa kwenda nchini Marekani sasa itabidi wakili wake akwee pipa kuelekea Miami kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo huku ikiwa bado haijafahamika kwamba inawezekana ukawa mwisho wa Maradina kwenda Marekani ama laa.

Huu ni muendelezo wa matukio na visa vya Maradona nje ya uwanja, kwani miaka ya karibuni amekuwa akiyafanya na kwa sasa mchezaji huyo yuko falme za kiarabu kama kocha wa klabu ya Al Fujairah.

Manula, Bocco, Ndemla wapokea tuzo za mwezi


KIPA chaguo la kwanza wa Simba, Aishi Manula amekabidhiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi wa Wekundu wa Msimbazi katika sherehe fupi iliyofanyika juzi  nyumbani kwa Balozi wa Uturuki, Ali Davotuglu.

Manula, ambaye pia ni kipa chaguo la kwanza la timu ya Taifa (Taifa Stars) alishinda tuzo hiyo baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mechi nne zilizopita za ligi hiyo inayotarajiwa kuingia kwenye raundi ya pili kuanzia leo.

Mbali na Manula, wachezaji wengine waliopata tuzo katika sherehe hiyo pamoja na nahodha na mshambuliaji aliye kwenye kiwango cha juu, John Bocco na kiungo, Said Ndemla.

"Hizi ni tuzo ambazo zinatolewa na klabu yetu katika kuhamasisha wachezaji wafanye vizuri katika kila mechi wanayocheza na vile vile kusaidia kuipa timu ushindi," alisema Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Haji Manara.

Aliongeza kuwa katika hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na viongozi wa klabu hiyo pamoja na mwekezaji na bilionea, Mohamed Dewji "Mo", walifanya mazungumzo mbalimbali na kubadilishana mawazo ili kuifanya timu ifikie malengo yake msimu huu.

"Tunaamini hatua hii tuliyofika, itakuwa na matokeo chanya kwa sababu tutaimarisha mahusiano," Manara aliongeza.

Mume aliyeweka pilipili kwenye nguo ya mkewe aadhibiwa


Mahakama moja wilayani Lira nchini Uganda imemuhukumu mwanamume kifungo cha siku 40 kutumikia jamii baada ya kupatikana na hatia ya kupaka pilipili nguo ya ndani (chupi) ya mkewe.

Akisoma hukumu, hakimu Hilary Kiwanuka alisema ushahidi uliotolewa mahakamani umejitosheleza pasipo kuacha shaka kwamba mtuhumiwa Moses Okello alitenda kosa hilo.

Okello, mkazi wa Kijiji cha Barmola, Kaunti Ndogo ya Bala wilayani Kole atatakiwa kufanya kazi za kijamii katika kipindi cha siku 40 kutokana na kosa hilo.

Mahakama ilielezwa Januari 20,2018, Okello alipaka pilipili kwenye nguo hiyo na baadaye alimshauri mkewe aivae.

“Alinishauri kuivaa siku hiyo, nilipoivaa nilianza kuwashwa na mwasho huo haukuisha hata nilipooga,” mwanamke huyo aliieleza Mahakama.

Haikuelezwa ni kwa nini Okello aliamua kufanya kitendo hicho kwa mkewe ingawa baadaye alidai alikuwa akimtania.

Magufuli awatunuku 197


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatunuku kamisheni maofisa wanafunzi 197 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Sherehe hizo zimefanyika leo Februari 3, 2018 katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam, ambapo maofisa hao wapya ni wa Tanzania na kutoka nchi marafiki,  waliopata mafunzo katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli mkoani Arusha.

Katia tukio hilo ambalo lilipambwa na magwaride kutoka kwa Wanajeshi hao, lilihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Kitaifa.

Miongoni mwa waliotunukiwa kamisheni hizo wanawake ni 28, na waliobaki ni wanaume.

Majeruhi wailiza Azam FC


Kuelekea mchezo wa marudiano raundi ya pili ya ligi kuu soka Tanzania Bara dhidi ya Ndanda FC, klabu ya soka ya Azam FC imesema inakabiliwa na majeruhi wengi akiwemo nahodha wa kikosi hicho Himid Mao.

Akiongelea mchezo huo msemaji wa timu hiyo Jaffary Idd amesema pamoja na majeruhi hao lakini timu ina kikosi kipana hivyo mwalimu Aristica Cioaba amewaandaa wengine kupambana kwaajili ya kupata alama tatu.

Wachezaji wengine ambao ni majeruhi ndani ya kikosi hicho ni Waziri Junior, Joseph Kimwaga na Joseph Mahundi, wakati Abubakar Salum 'Sure Boy' anatumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyoipata kwenye mchezo dhidi ya Yanga.

Azam FC inaingia katika mchezo wa leo utakaopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex ikiwa katika nafasi ya pili na alama 30, nyuma ya Simba yenye alama 35 kileleni. Ndanda inashika nafasi ya 8 ikiwa na alama 16.

Mafuta ya Petroli kuanza kuchimbwa Septemba mwaka huu Morogoro


Serikali imesema mradi wa uchimbaji mafuta katika Kisima kilichoanishwa kuchimbwa kwenye eneo la kijiji cha Ipera Asilia, kwenye hifadhi tengefu ya bonde la Kilombero, mkoani Morogoro, unatarajiwa kuanza rasmi mwezi Septemba, 2018 ambapo kisima hicho kinakadiriwa kuwa na mafuta kuanzia lita milioni 180 hadi 200.

Akizungumza jana Februari 2, 2018 katika kipindi cha maswali na majibu kwenye kikao cha nne cha mkutano wa 10 wa Bunge mjini Dodoma, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kinachosubiriwa ni kibali kutoka Baraza la Mazingira nchini (NEMC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), ili uchimbaji huo uanze rasmi.

“Mkataba ulishasainiwa tangu mwaka 2012 kilihobaki ni utekelezaji wa uchimbaji na ugunduzi wa mafuta, mafuta yanayotarajiwa kuchimbwa kwenye eneo hilo yanafikia milionii 180 hadi 200, mtaji ni mkubwa na utakua na manufaa kwa wananchi wako na nchi kwa ujumla,” alisema na kuongeza.

“Kinachosubiriwa ni kibali cha mazingira kutoka NEMC na mamlaka ya TAWA, mwezi Julai mwaka huu tumehakikishiwa mkataba utapatikana na Septemba uchimbaji utaanza rasmi.”

Serikali kupitia shirika la Maendeleo ya Petroli (TPDC) liliingia mkataba wa utafiti na uchimbaji wa gesi na uvunaji mafuta na Kampuni ya Mafuta na gesi ya Swala (Swala Oil), ambapo katika utekelezaji wa mkataba huo iligundulika kuwepo kwa wingi mafuta ya petrol na gesi katika vijiji vya Mtimbira.

VIDEO: Ifahamu Dini Ya Kingunge Na Mengine Usioyajua



Enock Ngombale ambae ni mdogo wa Kingunge Ngambale Mwiru amefunguka kuhusu maisha ya kaka yake tangu alipozaliwa  na kusema kuwa kuna wakati unaweza ukawa huna dini lakini kuna wakati itakulazimu urudi kwenye imani yako, hivyo kaka yangu atazikwa Kikatoliki kama kanisa watakubali tunachosema sisi ndugu zake tunayemjua.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE

VIDEO: Aunty Ezekiel Aomba msamaha Shilawadu


Baada ya shilawadu, kunusurika kugongwa na gari ya mose iyobo na kuharibu mali ikiwemo, gari na kamera aunty ezekiel apiga simu na kuomba msamaha shilawadu pamoja na kutaka kuwa wavumilivu akirudi wayamalize


TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI..............USISAHA KUSUBSCRIBE.......................

Friday 2 February 2018

DC Matiro akabidhi hundi za mikopo mil 25 vikundi vya vijana na wanawake

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amekabidhi hundi za mikopo shilingi milioni 25 kwa vikundi vitatu vya vijana na kimoja cha wanawake zilizotolewa na halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Fedha hizo zinatokana na asilimia 10 ya makusanyo kutoka katika vyanzo vya mapato ndani ya halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa kipindi cha kuanzia Mwezi Julai 2o17 hadi Disemba 2017.

Vikundi vilivyokabidhiwa hundi ni kikundi cha Wanawake na Maendeleo kilichopo katika kijiji cha Ishololo kata ya Usule na vikundi vya vijana vya Umoja wa bodaboda, Jikwamue, Shukrani Group vilivyopo katika kijiji cha Didia kata ya Didia katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Akikabidhi hundi hizo kwa wawakilishi wa vikundi hivyo leo Ijumaa Februari katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri hiyo,Matiro aliwataka walionufaika na mikopo hiyo watumie pesa walizopata kwa malengo yaliyokusudiwa.

“Kila mtu aliyepata pesa akafanye kile alichokusudia kufanya, serikali inajitahidi kuwawezesha kwa kuwapatia mikopo ili mjikwamue kiuchumi,naomba mfanye kazi kwa bidii ili kubadilisha maisha yenu”,alieleza Matiro.DC

Utawala wa Jordani umekata mahusiano ya kidiplomasia na Korea Kaskazini.


Katika gazeti rasmi, imeandikwa kuwa "Baraza la Mawaziri lilipitisha Azimio No. 6056 la Januari 15, ambalo linasema kusimamishwe kwa mahusiano ya kidiplomasia na Korea ya Kaskazini".

Kwa mujibu wa habari,balozi wa Korea Kaskazini nchini Jordan atasimamishwa kazi.

Afisa Mkuu wa Jordan amesema  kwamba uamuzi wa kukata mahusiano na Korea Kaskazini ni kutokana na maslahi ya serikali.

Umoja wa Mataifa umeiwekea Korea Kaskazini vikwazo kutokana na majaribio yake ya makombora ya nyuklia.

Helikopta mbili zagongana nchini Ufaransa


Ndege mbili za jeshi la Ufaransa zimegongana na kusababisha vifo vya watu watano,katika mji wa Marseille kusini mwa Ufaransa.

Gazeti la Var Metin limeripoti kuwa ajali hiyo imetokea majira ya asubuhi karibu na ziwa la Carces.

Ripoti zinaonyesha kuwa helikopta zilikuwa na jumla ya abiria sita na hivyo mmoja bado hajulikani alipo.

Timu za uokoaji zinaendelea kumtafuta abiria wa sita.

Gavana wa mkoa huo amesema kuwa helikopta hizo zilikuwa za shule ya kujifunza Urubani ya jeshi la Ufaransa na ajali hiyo imetokea mile 50 kutokea mji wa kitalii wa Saint Tropez.

Meli ya mizigo yapinduka


Meli ya mizigo imetipotiwa kupinduka na kusababisha kifo cha mtu mmoja China.

Kwa mujibu wa habari,wafanyakazi sita wa meli hiyo walianguka katika maji baada ya ajali hiyo kutokea.

Shirika la Shingua limetangaza kuwa ajali hiyo imetokea katika mto wa Yangtze katika mji  wa Huanggang.

Meli hiyo ilikuwa ina wafanyakazi sita,mmoja wao akiwa amefariki huku watano wengine hawajulikani walipo mpaka sasa.

Timu ya uokoaji iliweza kumtoa mmoja wao katika maji lakini haikuwezekana kuyanusuru maisha yake.

Juhudi za kuwatafuta wafanyakazi watano waliobaki zinaendelea.

Tundu Lissu amlilia Mzee Kingunge


Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amezungumzia kifo cha Kingunge Ngombale Mwiru akisema historia itamkumbuka.

Akizungumza leo Februari 2, 2018 na Mwananchi akiwa nchini Ubelgiji anakoendelea na matibabu ya viungo, Lissu akizungumzia kifo hicho ameanza kwa kusema “namtakia mapumziko mema.”

Amesema Mzee Kingunge alikuwa miongoni mwa wazee wenye historia kubwa na alionyesha ujasiri mkubwa wa kuhama chama chake cha CCM bila kuhofia kuhudhuriwa kutokana na mazingira yalivyokuwa.

“Ni mmoja wa wazee walioonyesha ujasiri mkubwa katika mazingira ya siasa za Tanzania yalivyokuwa, akahama chama tena CCM bila hofu za kuhudhuriwa  akaeleza madhabi yake kuwa hiki chama (CCM) kinatupeleka kuzimu,” amesema Lissu na kuongeza “historia itamkumbuka.”

Kingunge aliyekuwa kada wa CCM mwenye kadi namba nane, Oktoba 4, 2015 alitangaza kukihama chama hicho na kusema hatojiunga na chama chochote lakini mara kadhaa alionekana akipanda majukwaa ya upinzani kumnadi aliyekuwa mgombea urais wa Chadema/Ukawa, Edward Lowassa kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, 2015..

Humud aipeleka KMC ligi kuu Bara


KMC imeongeza idadi ya timu zinazotokea Dar es Salaam katika Ligi Kuu Bara baada ya ushindi wake wa bao 1-0 dhidi ya JKT Mlale waliokuwa vinara wa Kundi B la Ligi Daraja la Kwanza.

Ushindi huo unaifanya KMC kupanda Ligi Kuu Bara kwa mara ya kwanza huku shujaa wake akiwa ni kiungo mkongwe Abdulhalim Humud aliyefunga bao hilo pekee.

Huenda furaha kuu itakuwa kwa kocha Fred Felix Minziro maarufu kama Majeshi ambaye aliipandisha Singida United na sasa amejiunga na KMC na kuipandisha pia.

JKT Mlale iliyokuwa nyumbani ilionekana ina nafasi kubwa zaidi ya kupanda kwa kuwa ndiyo ilikuwa kinara ikiwa na pointi 25 sawa na KMC.


Lakini ushindi huo wa KMC umeifanya ifikishe pointi 28 na kupaa kileleni ikifuatiwa na Coastal Union iliyoshinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Mawezi mjini Morogoro. Coastal imemaliza ikiwa na pointi 26 wakati Mlale wanabaki na 25.


KUNDI B
                                P   W   D   L   F   A  GD  Pts
1. KMC                     14   8   4   2   17  13  4    28
2. Coastal Union       14   7   5   2   18   9   9   26
3. JKT Mlale             14   7   4   3   13   7   6   25
4. Polisi Tanzania     14   6   6   2   18   12  6   24
5. Mbeya Kwanza      14   6   4   4   14   10  4   22
6. Mufindi            14   3   4   7   13   21 -8  13

Thursday 1 February 2018

Papii kuanza kuachia ngoma mfululizo

MKALI wa Dansi Bongo, Johnson Nguza ‘Papii’ amesema kuanzia mwezi huu wa Februari, ataanza kuachia ngoma mfululizo kwani tayari wameshaanza kurekodi nyimbo za kutosha.

Papii alisema mpaka sasa tayari amesha-fanya ngoma nne ambazo amezipika kwa staili tofauti katika dansi la kisasa ambalo halich-oshi.

“Tumefanya staili kama ya wanayofanya Yamoto Band, tumefanya moja kama ya dini na pia tumerudia Seya ambazo kimsingi zitawateka tu mashabiki,” alisema Papii.

Akifafanua zaidi, Papii alisema, atakuwa na mfululizo wa kutoa ngoma mbilimbili zenye ujazo wa hali ya juu.

“Nitakuwa naachia ngoma mbilimbili mfululizo ambazo karibia zote nimefanya na mzee wangu (Nguza). Nimezifanyia katika Studio ya Wanene iliopo Mwenge,” alisema Papii.

Mwana FA: sijawahi kuvaa suruali za kubana

MKONGWE kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Hamisi Mwinjuma, ‘MwanaFA’ amesema, katika maisha yake ya kisanii, hajawahi kuvaa suruali za kubana kama ilivyo kwa vijana wenzake wa kileo kwa kile alichodai nguo hizo zinamfanya ashindwe kupumua.

Akipiga stori na Showbiz Xtra, MwanaFA alisema, tamaduni za Muziki wa Hip Hop ndizo zilizomfanya ashindwe kabisa kuvaa suruali za kubana kwa kuwa kila anapojaribu kuvaa hujikuta anashindwa kupumua.

“Unajua nguo zetu sisi watu wa Hip Hop ni ile suruali pana na tisheti kubwa, nimekulia katika mavazi hayo, licha ya kwamba dunia inabadilika lakini mimi nashindwa kabisa kuvaa suruali za kubana kwa kuwa nguo hizo hunifanya nishindwe kuhema,” alisema MwanaFA.