Saturday 9 December 2017

BREAKING: ''Kuanzia leo Babu Seya aachiwe huru'' - Rais Magufuli

BREAKING: ''Kuanzia leo Babu Seya aachiwe huru'' - Rais Magufuli

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diamond Platnumz Ft Morgan _ Hallelujah Remix |

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

Diddy, Drake & Beyonce Are Three Of The Highest Paid Musicians Of 2017

It’s been quite the year for hip hop. It was finally identified as the most consumed genre in America and made helped break a few records along the way. So it should come as no surprise that hip hop has dominated the top earning spots on Forbes’ highest paid musicians list of 2017. They publication recently released their annual list and some of hip hop & R&B’s most revered artists of this year landed on the top spots.

According to Forbes, Diddy, Beyonce and Drake claim the top three spots while The Weeknd came in at number four. Diddy had his best year so far, income wise, with $130 million before taxes. Much of that credited to his Bad Boy Family Reunion Tour, Ciroc and the estimated $70 million he earned by selling a third of Sean John clothing. As the only other artist to make nine figures this year, Queen Bey came in with $105 million, which they say is due to the Formation World Tour. Although it wrapped up in 2016, it still ended up on her calendar and she made $250 million off it alone. Drake comes in at third with $94 million, largely due to his highly successful “Boy Meets World” Tour.

The Weeknd came $2 million short of Drake in earnings, making $92 million which they say is predominantly due to his Live Nation advance from touring.

Along them, Jay-Z hit number 19 on the list, making $42 million which ties him with Celine Dion.

Overall, it’s been a good year for hip hop and clearly, it’s been getting people paid out here.

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

New AUDIO: Burna Boy – Koni Baje

DOWNLOAD

New VIDEO: Jason Derulo ft French Montana – Tip Toe

New VIDEO: Jason Derulo ft French Montana – Tip Toe

New VIDEO: Jason Derulo ft French Montana – Tip Toe



Audio | Jay Moe – Bata | Mp3 Download

Audio | Jay Moe – Bata | Mp3 Download

Audio | Jay Moe – Bata | Mp3 Download

New VIDEO: Coyo – NyakaNyaka

New VIDEO: Coyo – NyakaNyaka

New VIDEO: Coyo – NyakaNyaka


DOWNLOAD

Audio | Mo Fedha – Baki Na Uzuri Wako | Mp3 Download

Audio | Mo Fedha – Baki Na Uzuri Wako | Mp3 Download

Audio | Mo Fedha – Baki Na Uzuri Wako | Mp3 Download

DOWNLOAD

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day

New VIDEO: Julio Batalia ft. Mucky Comando – One Day



DOWNLOAD

MTL Waanika Sababu za Kupotea kwa Mwandishi Azory Gwanda!

MTL Waanika Sababu za Kupotea kwa Mwandishi Azory Gwanda!


FULL VIDEO:Makomandoo Wakishuka kwenye Helkopta katika Maonesho ya Miaka 56 ya Uhuru

FULL VIDEO:Makomandoo Wakishuka kwenye Helkopta katika Maonesho ya Miaka 56 ya Uhuru

BREAKING NEWS: Babu Seya, Papii Kocha Waachiwa Huru kwa Msamaha wa JPM

BREAKING NEWS: Babu Seya, Papii Kocha Waachiwa Huru kwa Msamaha wa JPM



BABU SEYA AACHIWA HURU NA RAIS MAGUFULI LEO!

BABU SEYA AACHIWA HURU NA RAIS MAGUFULI LEO!


BREAKING: JPM ameagiza kuachiwa huru kwa Babu Seya na Familia yake


Maadhimisho ya Miaka 56 ya Uhuru - DODOMA


RC aagiza kusakwa kwa mwanaume aliyepanga njama za kumuua mkewe



Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanry ameliagiza Jeshi la polisi mkoani humo kumsaka na kumtia nguvuni mwanaume mmoja mkazi wa wilaya ya Urambo anaedaiwa kupanga njama za kumuua mke wake kwa kutumia jambazi ambae hakuweza kutimiza jukumu hilo.

RC Mwanry ametoa agizo hilo katika kilele cha kampeni ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia zilizofanyika katika uwanja wa Chipukizi mkoani humo zilizoandaliwa na kituo kimoja cha redio mkoani humo.

Kituo hicho baada ya kuandaa kampeni hiyo kilirekodi mkasa wa huyo mama aliofanyiwa na mumewe na kukiweka kipande hicho cha sauti kwenye redio. Huku mama huyo hakutakiwa kuonekana kwasababu za usalama wake.

Kufuatia kusikika kwa mama huyo redioni ndipo RC huyo akatoa maagizo kwa jeshi la polisi kumsaka popote alipo.

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kufuatia kuuawa kwa askari 14 DRC


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha askari 14 wa Jeshi la JWTZ kuuawa walipokuwa katika operesheni ya kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).



Waziri Kigwangalla ateua kamati ya Kitaifa ya Utambulisho wa Tanzania



Waziri wa Maliasili na Utalii Dk.Hamisi Kigwangalla  jana Desemba 8,2017 Mjini Dodoma, ameunda kamati ya kuongoza maandalizi ya namna watanzania na wageni wa Tanzania watakavyosherehekea Utanzania wao  kwenye mwezi maalum utakaojulikana kama ‘TANZANIA HERITAGE MONTH’.

Akielezea wakati wa kutangaza kamati hiyo iliyojumlisha wadau mbalimbali wakiwemo wanahabari, wanamichezo na wadau wengine mbalimbali na wafanyabishara, alisema:

“Kwenye mwezi huu kila kitu kitakuwa cha kitanzania na tutataka kwenye kila ofisi ya umma, ofisi binafsi, shule, chuo, hotel, balozi zetu n.k mtu akifika tu, ‘utanzania’ wetu uonekane!” alieleza Dk.Kigwangalla.

Utanzania huo ambapo kila mwezi huo utakapofika ambapo moja ya mambo hayo ni pamoja na aina ya mavazi maalum, vyakula,  na mambo mengine yanayobeba na kujumuisha Utanzania.


Zitto Kabwe azungumzia hatima ya ACT- Wazalenddo



Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Zuberi Kabwe amefunguka kuwa  ndani ya chama chake (ACT) kuna watu wengi wakiwemo wanachama wa kutosha  akimaanisha hajabaki mwenyewe.

Zitto amefunguka hayo akimjibu mfuasi wake wa kwenye mtandao wa kijamii ambaye alitoa maoni yake kwa kumuuliza Mh. Kabwe haoni kama amebaki peke yake, ikiwa ni muda mfupi baada ya aliyekuwa Mgombea urais wa chama chake Anna Mghwira kujiunga na CCM huko Dodoma.

Akimjibu mfuasi huyo Zitto amesema "Chama chetu ACT Wazalendo kina madiwani 42, kina wenyeviti wa mitaa, vitongoji na wajumbe wa Serikali za Vijiji/Mitaa 507, Viongozi kila mkoa na jimbo, wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu. Ni dhahiri tuna watu wengi na wanachama wengi wa kutosha"

Hivi karibuni CCM ilijivunia wanachama wapya ambao waliwahi kuwa na nafasi ya uongozi ACT Wazalendo ambapo baadhi yao ni Prof Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba, Alberto Msando na jana  Anna Mghwira.

Wabunge wa Chadema waachiwa kwa Dhamana



Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Morogoro imetupilia mbali hati ya kiapo cha kupinga dhamana ya wabunge Suzan Kiwanga(Mlimba), Peter Lijualikali (Kilombero) na washtakiwa wengine 37 waliofikishwa mahakamani hapo kwa makosa nane.

Mbele ya Hakimu, Ivan Msaki mahakama ilitupilia mbali kiapo hicho na kueleza kuwa washtakiwa wote dhamana yao iko wazi kwa masharti ya kuwa na wadhamini wawili kila mmoja watakaosaini dhamana ya Sh 5 milioni na pia barua za dhamana lazima zisainiwe na wenyeviti wa vijiji ama maofisa watendaji.

Katika kiapo kilichowasilishwa awali mahakamani hapo na upande wa mashtaka kupitia wanasheria wa Serikali, Sunday Hyera na Edga Bantulaki ulieleza sababu walizodai kuwa ni za msingi za kupinga dhamana na kwamba kuwepo nje kwa washtakiwa  kunaweza kuharibu upelelezi wa kesi hiyo.

Kufuatia hoja hiyo upande wa utetezi unaowakilishwa na mawakili wanne wakiongozwa na wakili Peter Kibatala uliamua kuwasilisha hati ya kupinga kiapo hicho kwa madai kuwa  kiliandikwa bila ya kuzingatia misingi na matakwa ya kisheria.

Wakili Kibatala alidai kuwa miongoni mwa mapungufu yaliyokuwemo kwenye kiapo hicho ni pamoja na kutokuonyesha majina ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Malinyi (OCD) ambaye alitajwa kwenye kiapo hicho kama chanzo kilichotoa taarifa zilizotengeneza mashtaka yanayowakabili wabunge hao na wenzao.

Alidai kuwa mapungufu mengine yaliyokuwepo kwenye kiapo hicho ni utofauti wa tarehe ya kuandika kiapo hicho na kusainiwa na hivyo waliiomba mahakama kuzingatia mapungufu hayo.

Kutokana na mvutano huo wa kisheria baina ya pande hizo mbili Hakimu Msaki aliamua kupitia hoja za msingi za kisheria na hivyo kubaini mapungufu yaliyopo kwenye kiapo hicho na kueleza kuwa mapungufu hayo hayawezi kurekebishwa na kwamba kazi ya mahakama ni kutafsiri sheria na si kufundisha namna ya kuandika kiapo.

Kwa msingi huo Hakimu Msaki alitupilia mbali hati hiyo ya kiapo cha kupinga dhamana na kueleza kuwa washtakiwa hao watakuwa nje kwa dhamana wakati kesi yao ikiendelea.

Kabla ya kupewa dhamana washtakiwa hao walikaa rumande kwa siku 12 hali iliyosababisha kesi hiyo kuvuta hisia za watu hususani viongozi na wanachama Chadema waliokuwa wakifulika mahakamani hapo.

CHUO CHA ST DAVID KIMARA DAR KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO




CHUO CHA ST DAVID COLLEGE OF HEALTH KILICHOPO KIMARA TEMBONI DSM NI CHUO CHA KIPEKEE KATIKA UKANDA HUU WA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KINACHOTOA KOZI ZA AFYA KWA NGAZI ZOTE ZA CHETI NA DIPLOMA.

SIFA KUU NI UFAULU MASOMO YA SAYANSI IKIWEO HESABU NA KIINGEREZA ANGALAU ALAMA D.

ADA ZETU NI NAFUU UTALIPA KIDOGO KIDOGO KUKIDHI UWEZO WAKO, KWA MAWASILIANO 0626 231 364 / 0783 785 747 /  0716 044 610 / 0718 229 977 AU INGIA MTANDAONI  www.stdavidcollege.ac.tc

WAHI SASA MUHULA MPYA TAYARI UMEANZA.
PIA KUNA KOZI MAALUMU KWA WOTE WASIO NA VIGEZO KAMILI KUMUWEZESHA KUPAMBANA MPAKA AFIKIE VIWANGO NA KUJIUNGA NA MEDICINE..CA/CO

JIUNGE NA KOZI INAYOTOLEWA ST DAVID COLLEGE PEKEE IITWAYO PRE-MEDICINE PROGRAME KWA KUSHIRIKIANA NA BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA NECTA TUMEKUANDALIA NJIA RAHISI KABISA.

FIKA SASA KIMARA TEMBONI ZAMANI MOA AU OFISI ZETU ZILIZOPO MWANANYAMALA A CCM MINAZINI KWA DR DAVID B.MWANGANDA.

CHUO NI CHA KUTWA NA BWENI.





Breaking News: Papii Kocha na Babu Seya wapata msamaha wa Rais



Rais Dkt. John Magufuli ametoa msahama kwa wasanii Papii Kocha na baba yake Nguza Viking a.k.a Babu Seya waliokuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela.

Rais Magufuli amesema hayo leo mjini Dodoma wakati wa sherehe za miaka 66 ya Uhuru. Pia Rais Magufuli ametoa msamaha kwa watu 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa.

Nguza Viking na Papii Kocha walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa makosa ya kubaka na kulawiti watoto wadogo wa shule ya msingi.

Mzungu mwenye asili ya Israel afuata nyayo za AliKiba



Msanii wa muziki kutoka Kenya mwenye asili ya Israel Gilard Millo, amesema msanii wa bongo fleva Alikiba ndiye aliyemu-'insipire' kuimba Kiswahili, kitu ambacho kimempa mafanikio makubwa.

Akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live cha East Africa Television, Gilard ambaye hivi sasa ametua bongo, amesema wimbo wa 'Cinderela' wa Alikiba ndio ulimfanya azidi kupenda kuimba kwa lugha ya Kiswahili, baada ya kuona mashabiki wakimshangilia kwa nguvu alipoimba wimbo huo jukwaani.

"Cinderela ndio wimbo ulionifanya mimi nianze kuimba Kiswahili, nilikuwa nauimba na band live, na ndio wimbo wa kwanza wa Kiswahili nilioanza kuimba, sasa nikiimba watu wakawa wanashangilia huyu ni mzungu lakini anaimba Kiswahili, nikapenda nikaanza kuimba na zingine kwa Kiswahili, na mpaka leo naimba nyimbo zangu kwa Kiswahili", amesema Gilard.

Gilard ana kazi mbali mbali ambazo zimemfanya achukue tuzo za kimataifa, ambazo zimeimbwa kwa lugha ya Kiswahili, ikiwemo Unajua, Nairobi Yangu, Mapenzi, Sema milele na nyinginezo.

Spika Ndugai atuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya wanajeshi


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ametuma salamu za rambi rambi kwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, kufuatia vifo vya askari 14.

Spika Ndugai amesema amepokea kwa masikitiko taarifa za vifo vya askari hao ambao walikuwa wakilinda amani nchini Kongo, pamoja na wengine 44 waliojeruhiwa kufuatia mashambulizi yanayotekelezwa na askari waasi nchini humo.

Kufuatia tukio hilo, Spika Ndugai ametoa pole kwa familia za askari hao waliouawa, na kuwaombea wale waliojeruhiwa kupona haraka na kuendelea na shughuli za ujenzi wa Taifa.

Lwandamina agoma wachezaji vijana kutolewa kwa mkopo



ocha George Lwandamina ameonekana kuwa na imani kubwa na wachezaji vijana wa kikosi hicho.

Lwandamina âmezuia kuondoka kwa wachezaji wote vijana walio katika kikosi chake hasa wale waliokuwa wakiombwa kwa mkopo.

Kocha huyo raia wa Zambia, ameuisisitiza uongozi wa Yanga wachezaji wa Yanga walio katika kikosi hicho wanapaswa kuendelea kubaki.

“Kocha amekataa kabisa wachezaji vijana wasiondoke, amesisitiza waendelee kubaki hadi hapo baadaye kwa kuwa ana programu nao,” kilieleza chanzo.

Timu kadhaa, zilionekana kuanza kuwanyemelea wachezaji makinda wa Yanga katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo lakini Lwandamina ameonekana kuendelea kuwahitaji.

Lwandamina amekuwa ni muumini wa vijana na tokea ametua Yanga amekuwa akitoa nafasi kwa wachezaji vijana ambao wamekuwa wakionekana kufanya vema.

Bosi wa Ndemla ashindwa kutua Bongo kumalizana na Simba


BOSI wa Klabu ya AFC Eskelistuna ameshindwa kuwasili nchini wiki hii kumalizana na Simba kuhusu usajili wa timu hiyo, Said Ndemla baada ya mmoja kati anayehusika na ujio wake kupata msiba.

Kiongozi huyo alitarajiwa kuwasili nchini wiki hii kwa ajili ya suala la mchezaji huyo pamoja na masuala mengine ya kisoka lakini imeshindikana.

Ndemla alifanikiwa kufuzu majaribio mwezi uliopita katika klabu hiyo ya Sweden ambayo ilikuwa
 inashiriki ligi kuu na sasa imeshuka daraja.

Akizungumza na Championi Jumamosi, meneja wa Ndemla, Jamali Kisongo alisema kiongozi huyo ameshindwa kuwasili kutokana na matatizo hayo aliyoyapata mwenzao.

“Yule kiongozi alitakiwa kuwasili nchini wiki hii lakini imeshindikana kwa sababu mmoja kati ya watu anayehusika na ujio wake amepata msiba, hivyo sijafahamu baada ya hapo ratiba zake zitakuwaje.

“Lakini kama kutakuwa na lolote tutaweka wazi. Kwa upande wa mchezaji licha ya timu kushuka daraja lakini dili liko palepale, atajiunga nayo tu,” alisema Kisongo.

Rais Magufuli atoa msamaha kwa wafungwa 61 wa kunyongwa


Rais wa Tanzania John Magufuli kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa hilo amewasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa.

Hata hivyo idadi ya wafungwa wengine walioachiwa huru kutokana na makossa mbali mbali ni 1,821 ambao amesema kuwa wanapaswa kuachiwa mara baada ya tangazo lake.

Wafungwa wengine 8157 wamepunguziwa adhabu zao. Idadi hiyo ya msamaha kwa wafungwa inatajwa kuwa ni kubwa katika awamu zote kuwahi kutokea na hasa zinazo wahusisha wafungwa wa kunyongwa na vifungo vya maisha.

Jeshi la Israel lashambulia maeneo matatu Ukanda wa Gaza



Jeshi la anga la Israel lashambulia mapema asubui maeneo matatu tofauti katika Ukanda wa Gaza.

Katika mashambulizi hayo yaliolenga Kusini mwa Gaza, mpalestina mmoja mwenye umri wa kati ya maika 20 na 30 ameripotiwa kufariki.

Majira ya jioni Ijumaa jeshi la Israel lilishambulia Kaskazini mwa Gaza na kuwajeruhi watu 15.

Wasanii washirikikatika sherehe za Uhuru Dodoma



 Baadhi ya Wasanii wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzania All Stars wakiwa katika sherehe za maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara,yanayoendelea kufanyika kwenye uwanja wa Jamhuri, mjini Dodoma.


tumia Asali Kwa Urembo Wa Nywele na Ngozi



Asali hutumika kulainisha Ngozi
Asali ina asili ya kuvuta unyevu kutoka kwenye hewa na kuipa ngozi uwezo wa kuhifadhi unyevu hivyo ni faida kwa mtu mwenye ngozi kavu.
Jinsi ya kuandaa
Chukua asali mbichi kijiko kimoja cha chai kisha paka usoni, kaa nayo kwa dakika 15 hadi 20 kisha safisha uso wako.
Asali katika kusafisha ngozi, kutibu na kuzuia chunusi
Kutokana na uwezo wa asali katika kuua bacteria na kuvuta uchafu katika matundu ya ngozi asali itakusaidia kutatua tatizo la chunusi.
Jinsi ya Kuandaa
Chukua asali mbichi Kijiko kimoja cha chakula changanya na mafuta ya nazi vijiko viwili changanya mchanganyiko uwe mlaini kisha paka usoni huku ukisugua taratibu kwa kufanya kama viduara huku ukiepuka kufikisha machoni. ukimaliza kusugua uso na mchanganyiko wako osha uso wako.
Jinsi ya kuandaa kama kisafisha ngozi, exfoliator
Changanya kijiko kimoja asali na kijiko kimoja baking soda. tumia mchanganyiko huu kusugua ngozi yako. Asali inaongeza lishe na chembe chembe kuzuia madhara yanayotokana na sumu za hewani zinazozeesha ngozi. Baking soda inasaidia kusafisha matundu ya ngozi.
Asali inasaidia ngozi iliyoungua na jua kujirudi na kung'aa.
Jinsi ya kutumia asali katika nywele
Asali inatibu nywele kavu zilizopauka, na kulainisha ngozi kavu ya kichwa na kutibu muwasho kichwani.
Jinsi ya kufanya
Changanya kijiko kikubwa cha asali na maji ya uvuguvugu kisha paka kichwani Acha kwa muda wa saa 1 iwe kama conditioner kisha safisha nywele zako.
Unaweza kuchanganya asali kiasi cha kijiko kimoja mpk viwili katika maji vikombe vitano kisha safishia nywele zako taratibu, yaani yapitishe tu hayo maji kwenye nywele zako ambazo ni safi.
Tahadhari: Asali kwa kiasi kikubwa hupausha weusi wa nywele kutokana na Hydrogen Peroxide inayopatikana ndani ya asali.
Ni vema ukatumia asali mbichi kujihakikishia faida za asali katika mwili wako.
Iwapo unavutiwa na matumizi ya kitu cha asili katika urembo wako unaweza kuongeza kitu hicho katika kitu kingine unachotumia mfano katika steaming yako au scrub unayotumia

Tambua Madhara ya Ulaji Wa chipsi



Chips ni aina ya chakula ambacho hupendwa na watu wengi na pia ni miongoni mwa vyakula vyenye mafuta mengi. chips pia inasemekana ni miongoini mwa vyakula ambavyo hupikwa katika joto la juu zaidi ya 300 degree.
Chips ni chakula chenye mafuta mengi na mafuta yanapoingia mwilini huenda kuzunguka sehemu ya mwili wa mwanadamu. kama ni mtu ambaye mazoezi pia hufanyi madhara yake ni kupata magonjwa ya moyo. hivi sasa idadi kubwa ya vijana wanaugua magonjwa mengi yanayo sababishwa na mkusanyiko wa mafuta katika miili yao amabayo huchangiwa na kuto kufanya mazoezi madhara yake mafuta kuziba mirija
Mafuta yakiliwa sana husababisha kuzidi mwilini.
Pia inasadikika mafuta yaliyopo katika chipsi katika sahani moja ya chisi ya moto endapo utaamua kuchuja kuna uwezekano wa kupata nusu glasi ya mafuta ya kupikia. Kwa hali hii ujue ni hatari.
Na mwili huwa hatupi kinachofaa, na badala yake kama hakitumiki wakati huo basi huhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye. Ndio maana tunapokula vyakula vyingi vyenye mafuta mengi hutupelekea kuongeza unene na uzito.
Unene huwa ni chanzo cha magonjwa mengi ,Kwani (High Blood pressure) hutokana na kuwa na mafuta mengi mwilini ambayo hupelekea mirija ya kusafirisha damu kuwa na mafuta. Hii husababisha njia ya kupitia damu kuwa nyembamba hivyo kusababisha nguvu ya ziada itumike kusukuma damu hiyo ili isambae mwilini kama inavyotakiwa. Nguvu hii ya ziada huongeza au kupunguza mapigo ya moyo.
Mapigo ya moyo yanapoongezeka sana ni hatari na yanapo pungua sana pia ni hatari.
Hivyo basi ni vizuri kwa watumiaji wa chipsi kujitahidi kutumia kwa kiasi kidogo au kuacha kabisa vile vile mazoezi pia ni muhimu ili kupunguza mrundikano wa mafuta katika mwili.
Pia inasemekana kuwa wanasayansi wamegundua kuwa chipsi husababisha kukuza hips hivyo kwa wanaume wengi hawatapenda kuwa katika hali hiyo, hivyo ni muhimu kujiepusha na pia isije ikawa kichocheo kwa wanawake kutumia sana ili kukuza sehemu hizo za maumbile bali wapunguze kutumia chipsi pamoja na kufanya mazoezi ili kuweka mwili katika hali ya kuepuka magonjwa yasiyo ya lazima.pia ulaji wa chips kupita kiasi husababisha wanaume na wanawake kuzeeka mapema.

Friday 8 December 2017






Mwanza. Sakata la mwanamke aliyemvisha pete ya uchumba mwanamke mwenzake limechukua sura mpya baada ya jeshi la polisi kufanikiwa kuwatia mbaroni watu wengine watatu akiwemo aliyevishwa pete.
Sura mpya ya kwanza ni mtuhumiwa Milembe Suleiman (36), anayedaiwa kumvalisha pete mwanamke mwenzake Janeth Shonza, aliyekuwa akishikiliwa na polisi mkoani Geita kuhamishiwa mkoani Mwanza.
Pili, jeshi la polisi pia limefanikiwa kumtia mbaroni mwanamke aliyevishwa pete, Janeth Shonza (25), mwanafunzi wa mwaka wa nne wa sheria katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Mwanza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa akiwa mafichoni eneo la Puma mkoani Singida.
Amewataja wengine wanaoshikiliwa na kutarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote uchunguzi utakapokamilika kuwa ni Richard Fabian (28), mkazi wa Buzuruga jijini Mwanza aliyepiga na kusambaza mitandaoni picha za wanawake hao wakivishana pete mitandaoni.
Kamanda Msangi amemtaja mwingine anayeshikiliwa kuwa ni Aneth Mkuki (24), mkazi wa Nyasaka jijini Mwanza, mpenzi mwingine wa Janeth aliyemsaidia kutoroka kukwepa kutiwa mbaroni na polisi baada ya video yao kusambazwa mitandaoni.

Kanisa la Mch Gwajima Labomolewa usiku

Kufuatia zoezi la serikali la kupanua na kuboresha miundo mbinu mbalimbali nchini hususan ya barabara katika jiji la Dar es Salaam ambapo imelazimu baadhi ya maeneo kubomolewa ili kupisha zoezi hilo la upanuzi, Kanisa la Ufufuo na Uzima la Askofu Josephat Gwajima nalo limekumbwa na kadhia ya kubomolewa.
Kanisa hilo lililoko jirani kabisa na Barabara ya Morogoro ambayo serikali imepanga kuipanua ili kurahisisha usafiri na kupunguza foleni, lilitakiwa kubomolewa kutokana na kuwa ndani ya eneo la hifadhi ya barabara hiyo.
Mchungaji Biyagaza wa Kanisa la Ufufuo na Uzima lililoko chini ya Askofu Gwajima, ameeleza kuwa serikali iliwapatia notisi ya siku 30 ili wabomoe kipande cha jengo la kanisa hilo kilichopo ndani ya eneo la hifadhi ya barabara.
“Ni kweli tunayo notice ya mwezi mmoja ya kuhakikisha kwamba eneo ambalo ni hifadhi ya barabara tunaliacha. Na hifadhi ya barabara ni mita 90 kuanzia katikati. Bahati nzuri wale waliokuja kuweka alama zao walipofika hapa na wahandisi , mafundi na baadhi ya watu wa kanisani walikuwepo. Basi tukawaambia wapime mita 90 zinapoishia. Kwa hiyo wakapima mita 90 zilipoishia wakaweka alama, wakasema basi nyie mnaweza mkabomoa upande huu na upande huu mkauacha kwa ajili ya hifadhi ya barabara,” alisema Mchungaji Biyagaza.
“Sisi baada ya hapo tukaona tujipange kwa ajili kuachia eneo la barabara ili shughuli nyingine ambazo ni mpango wa maendeleo ya serikali ziweze kuendelea na sisi tuweze kuendelea na eneo letu vizuri. Kwa hivyo kile kipande chote ambacho ni cha barabara na tukaongeza ndani kidogo chote tumekiondoa. Na hili eneo linalobaki tunapaimarisha ili nyumba ya Bwana iweze kufanya kazi yake ya kutoa huduma za kiroho,” aliongeza.
Mchungaji Biyagaza alieleza japokuwa eneo la jengo limepungua, eneo lililobakia linaimarishwa ili kanisa hilo liweze kuendelea kutoa huduma za kiroho kwa waumini wake.
Aidha kufuatia zoezi hilo la upanuzi wa barabara ya Morogoro ambalo linaenda sambamba na ujenzi wa barabara za juu (fly-over) katika makutano ya barabara eneo la Ubungo, umepelekea kubomolewa kwa majengo mbalimbali ikiwemo majengo ya wizara ya Maji na Umwagiliaji pamoja na jengo la Makao Makuu ya Shirika la Umeme Tanzania ambayo yamebomolewa kufuatia agizo la Rais Dkt. John pombe Magufuli.

Jerry Muro amesema uwezowake ajilinganisha na Wabunge 10 Chadema




Aliyekuwa Msemaji wa Yanga SC, Jerry Muro amesema kutokana na uwezo wake katika mambo mbali mbali anaweza kujilinganisha na wabunge 10 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katika mahojiano na kipindi cha Maisha Mseto cha Times Fm, Jerry amesema kutokana na uwezo wake suala la ubunge kwake ni jambo rahisi tu sawa na kubofya button.

“Mimi Jerry Muro mmoja ni sawa na wabunge 10 wa Chadema, nimewazidi kifikra, kinguvu, kipesa, maadili, kihoja na mambo mengine mengi sana” amese Jerry.

Katika hatua nyingine Jerry amesema mwaka 2020 si ajabu kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Edward Lowassa wakirejea katika Chama cha Mapinduzi (CCM).

Watu wawili waliokutwa na Mayai ya Mbuni wahukumiwa miaka 25 Jela



Serengeti. Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya  Serengeti imewahukumu kifungo cha miaka 25 washitakiwa wawili na gari lao kutaifishwa kwa kosa la kukutwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni.

Waliokumbwa na adhabu hiyo ni Marwa Matiko(32) na Julius Marwa (42) wakazi Tarime mjini.

Akitoa hukumu leo Ijumaa katika kesi ya uhujumu uchumi namba 128/2016 hakimu wa mahakama hiyo, Ismael  Ngaile amesema kila mshitakiwa atahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela na gari lao kutaifishwa liuzwe.

Mapema mwendesha mashitaka wa Jamhuri, Emmanuel Zumba ameiambia Mahakama kuwa, washitakiwa hao walikamatwa Desemba 7, 2016 wakiwa kwenye nyumba ya kulala wageni Serengeti wakiwa na mayai 16 ya mbuni yenye thamani ya zaidi ya Sh 42 milioni kinyume cha sheria.

Amesema mayai hayo walikuwa wameyaficha ndani ya gari lao.

Amesema washitakiwa wakidai kuwa walikuwa wanapeleka nchini Kenya kwa ajili ya kuuza kwa watu wanaotengeneza dawa ya ukimwi.

Akamatwa na Polisi baada ya kumuua nesi



Polisi siku ya Jumatano walimkamata mgonjwa aliyemuua nesi kwa kumpiga risasi ya kichwa kwenye kituo cha afya cha Chiromo huko Westlands, Nairobi

Mgonjwa huyo aliyetambuliwa kwa jina la Joseph Njoroge Mungai mwenye kibali cha kumiliki silaha alimpiga risasi ya kichwa daktari huyo aliyefahamika kwa jina la Faustine Mwandime Mwandilu

Kamanda wa polisi wa Nairobi Japheth Koome amesema mtuhumiwa atapelekwa mahakamani kwa kesi ya mauaji

Mtuhumiwa huyo mwenye matatizo ya akili alipelekwa na kulazwa hospitalini hapo akiwa na bunduki baada ya kukataa kuiwasilisha kwa walinzi wa hospitali

Askari Mgambo Kizuizini kwa kujifanya Maofisa Uhamiaji



Mwanza. Idara ya uhamiaji jijini Mwanza inawashikilia kwa mahojiano askari mgambo wawili wa jiji la Mwanza kwa tuhuma za kujifanya maofisa wa idara hiyo na kupita maeneo ya biashara ikiwemo mahoteli kukagua vibali vya ukaazi wa wageni.

Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Paul Eranga akitoa taarifa leo Ijumaa amesema mgambo hao walikamatwa walipofika kwenye moja ya hoteli za kitalii jijini Mwanza kwa lengo la kukagua wageni waliofikia hapo iwapo wana nyaraka na vibali halali vya kuingia nchini.

Amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni Chacha Kichele, mkazi wa Bugarika Wilaya ya Nyamagana na mwenzake Michael Julius, mkazi wa Kiloleli wilayani Ilemela.

“Walitumia mwanya wa sare zao kufanana na zile za idara ya Uhamiaji kupita kwenye mahoteli kukagua wageni wakijifanya ni maofisa Uhamiaji hadi uongozi wa hoteli moja ulipowashtukia na kutoa taarifa,” amesema Eranga

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download

Video | Bahati – Lala Amka | Mp4 Download


DOWNLOAD

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

Audio | Mwana FA Ft Maua Sama – Hata Sielewi | Mp3 Download

DOWNLOAD

Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download

Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download
Video | Diamond Platnumz ft Rick Ross – Waka | Download



Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download

Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download

Audio | Waje Ft Yemi Alade – I’m Available | Mp3 Download


Thursday 7 December 2017

Shilole afunga pingu za maisha na mchumba wake



Ashraf Uchebe akiwa na mkewe, Shilole.

Hatimaye msanii wa Bongo Fleva, Shilole amefungua ndoa na mpenzi wake Ashraf Uchebe huko Masaki usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam.

Staa huyo alikuwa akisisitiza kufunga ndoa mwaka huu lakini watu walikuwa wakichukulia poa kwa sababu si mara ya kwanza kutoa kauli kama hiyo lakini jana Desemba 6 akafanya kweli.

Baada ya picha kusambaa mtandaoni aliyekuwa mpenzi wa Shilole, Nuh Mziwanda ameandika ujumbe katika ukurasa wa Instagram ambao unaweza kutafsiriwa kama ametupa kijembe kwenye ndoa hiyo.  Nuh ameandika;

Alie LaLa na BiBi harusi’wiki Moja KabLa ya harusi’Na wala sio Bwana Harusi’Bado mnanishauri harusi 😏 (all girls are pretenders )

Alichokiandika Nuh Mziwanda ni mistari kutoka kwenye wimbo wa Mwana FA ‘Bado Nipo Nipo’ ambao ulitoka takribani miaka 10 iliyopita.

Baada ya Mwandishi wa Mwananchi kupotea, OJADACT yataka uchunguzi ufanyike


Mwandishi wa kujitegemea wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Azory Gwanda.

Chama cha Waandishi wa Habari wa Kupinga Vita Matumizi Dawa za Kulevya na Uhalifu (Ojadact), kimevitaka vyombo vya dola na mamlaka nyingine serikalini kumtafuta na kumpata mwandishi wa kujitegemea wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Azory Gwanda.

Gwanda ambaye kituo chake cha kazi ni Pwani ametoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 21 na mpaka sasa hajulikani alipo.

Mbali ya Ojadact, vyombo vya habari vya kimataifa na wadau mbalimbali wa habari wamezungumzia kutoweka kwa Gwanda wakitaka juhudi za makusudi za kutafutwa na kupatikana kwa mwandishi huyo.

Akizungumza na mwaandishi wa habari jijini hapa jana, Mwenyekiti wa Ojadact, Edwine Soko aliwaomba wadau wa habari nchini kuunganisha nguvu katika kumtafuta na kuvishinikiza vyombo na mamlaka husika kumtafuta mwandishi huyo.

“Hatuwezi kuendelea kuvumilia tabia inayoanza kuzoeleka nchini ya watu kupotea bila kujulikana walipo huku vyombo vya dola vyenye dhamana ya ulinzi na usalama wa raia vikichukulia kawaida, kama jamii lazima tusema hapana kwa sababu huo siyo aina ya Utanzania tuliouzoea,” alisema Soko.

Soko alisema jamii haipaswi kuendelea kufumbia macho vitendo vya watu kupotea na wengine miili yao kuokotwa katika fukwe za bahari na mito nchini kwa sababu vinakiuka Ibara ya 14 ya Katiba inayolinda haki ya kuishi kwa kila mtu.

Alisema tukio la Gwanda lina dalili zote za uovu kwa sababu muda ambao hajaonekana unazidi hata ule unaoruhusiwa mtuhumiwa kushikiliwa kisheria hata na vyombo vya dola kabla ya kumfikisha mahakamani.

Kwa mujibu wa mkewe, Anna Pinon (35), Novemba 21, Agwanda aliaga nyumbani kwake Kibiti kuwa kuwa anaenda kazini lakini hakufika wala kurejea nyumbani.

Mmoja wa waandishi wa habari jijini Mwanza, Halima Juma alisema kitendo cha Gwanda kupotea kimeibua hofu miongoni mwa waandishi wa habari nchini, hasa wanaofuatilia na kuibua habari zinazopiga vita uovu, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka kwa watu wenye uwezo na mamlaka.

Kupitia kurasa zake za kujamii, mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliandika ‘’Maswali kwa @MwananchiNews 1) alikuwa ana ‘assignment’ yeyote kutoka kwenu alipotekwa huko Kibiti? 2) kama ndio kwanini hamsemi hilo? 3) Mna Habari yake yeyote hamjaichapisha gazetini?

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kilisema ‘’tunaungana na uongozi wa @MwananchiNews kutoa wito kwa Jeshi la Polisi Tanzania…kuchukua hatua ili ndugu Azory Gwanda aweze kupatikana. #MrudisheniAzoryGwanda.”

Vituo vya habari za kimataifa vya Fox News, New York Times, Daily Nation walizungumzia kupotea kwa mwandishi Gwanda.


Kitendo cha Trump kuutambua Jerusalem kuwa mji mku wa Israel,Saudi Arabia walaani hatua hiyo


Donald Trump

Saudi Arabia imelaani hatua ya Marekani ya kuutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel huku pia shutuma zikizidi kuongezeka kufuatia hatua hiyo.

Katika taarifa, taifa hilo la ghuba lilisema kuwa tangazo hilo la Trump sio la haki.

Lakini waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu alilitaja tangazo hilo kuwa la kihistoria.

Hatma ya mji wa Jerusalem ni moja masuala makuu kwenye mzozo katika ya Israel na Palestina.

Mataifa 8 kati ya 15 ambayo kwa sasa ni wanachama wa baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa yametaka shirika hilo kufanya mkutano wa dharura kufuatia uamuzi huo wa Marekani.

Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel ni jambo ambalo halijatambuliwa kimataifa na hadi sasa nchi zote zimeweka balozi zao kweny mji wa Tel Aviv.

Jerusalem una semue takatifu kwa dini tatu za kiyahudi, kiislamu na kikristo.

Wapalestina walichoma picha za Trump



Wananchi wakubaliana na Vita dhidi ya rushwa inayoendeshwa na Rais



 Dar es Salaam. Wananchi wanaonekana kukubaliana na vita dhidi ya rushwa inayoendeshwa na Rais John Magufuli, matokeo ya utafiti yamebainisha.

Utafiti huo kuhusu hali ya rushwa nchini uliofanywa na taasisi ya Repoa kwa kuwezeshwa na taasisi ya Afro Barometer, ulihusisha wananchi 2,400 katika mikoa yote.

Utafiti huo unaoitwa “Mtazamo wa Wananchi Katika Rushwa wa 2017”, unaonyesha kuwa ushiriki wa Serikali katika kupambana na vita dhidi ya rushwa umeongezeka.

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti huo yaliyotangazwa jana, wananchi saba kati ya 10 (asilimia 71) ya waliohojiwa walisema ushiriki wa Serikali katika kupambana na vita dhidi ya rushwa ni mzuri, imani hiyo ikiongezeka kutoka asilimia 37 kulingana na matokeo ya mwaka 2014/15.

Akiwasilisha matokeo hayo, Profesa Pellizzio Riccard kutoka Repoa alisema utafiti huo unaonyesha imani ya wananchi kuongezeka katika vita dhidi ya rushwa ndani ya taasisi za Serikali.

Kwa mujibu wa utafiti huo, rushwa katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imepungua hadi asilimia 14 kutoka 37, Takukuru (asilimia 11 kutoka 29), Jeshi la Polisi (asilimia 36 kutoka 50), mahakimu na majaji imepungua hadi asilimia 21 kutoka 35.

Tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani mwaka 2015, imekuwa ikiwafikisha mahakamani watu wanaotuhumiwa kuhusika katika kashfa kubwa kama uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.

Pia imepambana na ufisadi katika mashirika ya umma, ukwepaji kodi, utoroshaji makontena bandarini na kutimua wafanyakazi wa umma wanaojihusisha na ufisadi.

Hata hivyo, mmoja wa wasomi waliohudhuria hafla ya kutangazwa kwa matokeo hayo jana, Dk Simeon Mesaki alisema mtazamo huo unaweza kuwa tofauti na hali halisi.

“Kama utafiti unahusu mtazamo, matokeo yanaweza kuwa tofauti na hali halisi. It is the all about perception against reality (ni suala la mtazamo dhidi ya uhalisia),” alisema.

“Lakini, pili inawezekana kwamba jinsi Serikali inavyofanya kazi na watu wakaona, basi imani ni wazi itaongezeka. Kwa mfano, wananchi wanaona vigogo wa Escrow wanapandishwa mahakamani basi imani inaongezeka.”

Dk Mesaki alihofia kama kasi hiyo inaweza kudumu. “Je, vita hii itaendelea na kasi yake au ni povu tu kwa sababu Serikali iliyopo imeamua kutengeneza legitimacy (uhalali) yake?” alihoji.

Mbali ya Profesa Riccard, uwasilishaji wa matokeo hayo uliohudhuriwa na wasomi, wadau kutoka balozi na taasisi mbalimbali ulifanywa pia na mtafiti Lulu Silas kutoka Repoa.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakaluka alisema kupungua kwa vitendo vya rushwa kumetokana na hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kuimarisha nidhamu na kurejesha imani ya polisi kwa wananchi.

Mwakaluka alisema wapo askari waliochukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo kufukuzwa kazi, kupewa onyo kali huku kiwango cha uelimishaji kikiongezeka kwa wananchi kupitia vyombo vya habari.

Jeshi la Polisi na mahakama zimekuwa zikitajwa mara kwa mara kuwa taasisi ambazo wananchi wanaziona kuwa zinaongoza kwa vitendo vya rushwa.

Mbali ya matokeo hayo, mkurugenzi mkuu wa Repoa, Dk Donald Mmari alisema pamoja na imani kuongeza, bado wananchi wanaogopa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa.

Dk Mmari alisema hiyo inatokana na woga wa kujulikana endapo watatoa taarifa hizo.


Hizi ndizo timu zilizofuzu hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa Ulaya


TIMU ZILIZOFUZU HATUA YA 16 BORA YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Wafanyabiashara wametoa kilio chao kwa wingi wa Kodi kwa Dk Mpango



Dodoma. Wafanyabiashara wametoa kilio chao cha wingi wa kodi zinazotozwa na Serikali na mazingira yasiyo ya ushindani sawa wa kibiashara nchini, jambo linalowafanya kushindwa kuchangia ipasavyo katika maendeleo.

Mambo mengine waliyolalamikia ni kutozwa kodi mara mbili, baadhi ya wafanyabiashara kuingiza nguo kutoka nje ya nchi kwa njia za panya, utaratibu wa utoaji wa vibali kwa mamlaka za Serikali na kodi na ushuru katika sekta ya kilimo.

Wakizungumza jana katika mkutano wao na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango wafanyabiashara hao walisema hawawezi kushindana kibiashara kama hakutakuwa na ushindani ulio sawa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania, Felician Kilahama alisema kuna wafanyabiashara wa mbao ambao wamekuwa wakitozwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) lakini wengine hawatozwi, jambo ambalo haliweki ushindani sawa wa kibiashara nchini. “Unakuta wale wanaotozwa VAT bidhaa zao zinakuwa juu ya wale ambao hawatozwi kodi jambo ambalo halileti ushindani sawa katika biashara,” alisema Kilahama.

Alisema pia kuna tatizo la wafanyabiashara kuidai Serikali fedha za VAT inazotakiwa kurejesha na kuitaka kuangalia jinsi ya kutatua tatizo hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Mahoteli, Nura Karamagi alilamikia tozo ya Serikali ya kuingia katika mageti ambayo wanatozwa watalii kwamba inapunguza ufanisi katika sekta hiyo.

Licha ya Kamishna Mkuu wa TRA, Charles Kichere kusema kuwa kodi hiyo ilishafutwa tangu Julai, Karamagi alisema bado wenye hoteli wamekuwa wakitozwa na inajionyesha katika karatasi za malipo.

Mwenyekiti wa Wasindikaji Mafuta (Tasupa), Ringo Ringo alilamikia kiwango kikubwa cha kodi kinachotozwa cha VAT ikilinganishwa na nchi nyingine kama za Kenya. “Kenya wao wanatoza asilimia 14 tu lakini sisi hapa tunatozwa asilimia 18,” alisema.

Akijibu hoja hizo, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James alisema changamoto iliyojitokeza katika urejeshaji wa VAT ni udanganyifu na kwamba ili kuwalipa malipo halali, Serikali inakagua madai hayo.

Alisema wameanza kuirejesha na kwamba Oktoba walirudisha Sh33 bilioni na Novemba Sh15 bilioni. “Na Desemba tunatarajia kulipa zaidi ya Sh10 bilioni, bado tunapitia hesabu.”

Dk Mpango alisema kukutana na wafanyabiashara hao kulilenga kuwasikiliza na kujumuisha hoja zao katika bajeti ijayo.