Saturday 20 January 2018

VIDEO: Mtulia Uso Kwa Uso Na Meneja

Aliyekuwa meneja wa kampeni wa Maulid Mtulia kwenye uchaguzi wa 2015 Kinondoni,  Rajabu Salim Jumaa amerejesha fomu ya kuombea kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwania nafasi hiyo.

Jumaa ambaye amerejesha fomu hizo leo Januari 20, 2018 katika ofisi ya uchaguzi  wa jimbo la Kinondoni iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam, amesema hatua ya Chadema kusimamisha mgombea katika uchaguzi huo ni kudhoofisha upinzani.

Mwaka 2015 mgombea wa CUF Mtulia alishinda ubunge wa jimbo hilo lakini alijivua uanachama wa CUF na kuhamia CCM na hivyo kupoteza sifa ya ubunge. Hata hivyo Mtulia amepitishwa na chama hicho tawala kugombea ubunge katika jimbo hilo, leo anatarajia kurejesha fomu za NEC.

Jumaa ambaye yupo CUF upande unaomuunga mkono mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, amesema hatua ya Chadema kusimamisha mgombea katika uchaguzi huo ni kudhoofisha upinzani.

"Chadema wanakuja kupoteza nguvu na kuja kugawa kura za wapinzani. CUF ililipata jimbo la Kinondoni kukiwa na ushirikiano wa Ukawa na siyo mtu mmoja.

Chama kilichoshirikiana katika mchakato huo bado kipo na kimemsimamisha mgombea iweje leo Chadema wamesimamisha mgombea," amehoji.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......... USISAHAU KUSUBSCRIBE

Mawaziri Wakutana Dar Kuanza Kutekeleza Ujenzi wa Reli

Mawaziri wa Miundombinu na Uchukuzi kutoka Tanzania na Rwanda wamekutana leo jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa maelekezo ya Marais wa nchi hizo mbili yaliyotolewa hivi karibuni kuhusu na makubaliano ya Ujenzi wa Reli ya kisasa ya yenye urefu wa kilomita 572 itakayoanzia Isaka mpaka Kigali Rwanda.Katika mazungumzo yao, mawaziri hao wameridhia kwa pamoja rasimu ya kujenga reli ya kisasa kwa lengo la kuendeleza uhusiano wa nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na kurahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji, kuunganisha miundombinu, kukuza za uchumi na kutoa huduma bora kwa wakazi ws ukanda huu.

Kata hatua nyingine, Mawaziri Dk Augustine Mahiga na Waziri wa Fedha Philip Mpango ambao ni miongoni wa Viongozi waliohudhuria mazungumzo hayo wamesema ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa baina ya Tanznaia na Rwanda itakuwa ni kiungo muhimu cha kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wa nchi hizo.

Nitashinda Ubunge Asubuhi Mapema - Mgombea CHADEMA

Mgombea ubunge wa Jimbo la Siha, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Elvis Mosi, amesema atashinda ubunge wa jimbo hilo mapema asubuhi kutokana na mgombea aliyepitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Godwin Mollel, kutokuwa na nguvu ya kushinda kwani amekosa sifa za kuwa kiongozi kwa madai kuwa ni mtu mwenye tamaa na asiyekuwa na msimamo.

Mgombea huyo amesema chama chake kimemuamini na kumpitisha baada ya kumpima na kuona anao uwezo wa kukabiliana na Dk. Mollel na kwamba ushindi wake utapatikana asubuhi.

“Mgombea wa CCM hawezi kamwe kushindana na mimi yaani ni ardhi na mbingu na sifa ya kumshinda tunayo, kwanza ni mtu aliye na tamaa na asiyekuwa na msimamo wananchi hawawezi kumchagua mtu wa namna hiyo kwani walimuamini lakini amewasaliti,” amesema.

Naibu Waziri Aagiza Kutoa Vikwazo Vyuo Vya Ufundi

Naibu waziri wa elimu sayansi na Teknolojia William Ole Nasha ameviagiza vyuo vya ufundi kote nchini kuondoa vikwazo na kutoa upendeleo maalum kwa wanafunzi wa kike wenye sifa wanaojiunga na elimu ya ufundi kwakuwa  idadi kubwa wanafunzi wa kike wanaichukia elimu ya ufundi kutokana na vikwazo vilivyopo kwenye vyuo hivyo dhidi yao.

Naibu waziri Ole Nasha ametoa kauli hiyo alipokuwa anazungumza na wahitimu wa fani mbalimbali za ufundi kwenye chuo cha ufundi Arusha ATC.

Kaimu mkuu wa chuo cha ufundi Arusha Dkt. Masud Senzia amesema chuo hicho kimetekeleza kwa vitendo adhima ya serikali ya viwanda kwani kimeanza kufanya majaribio ya kuzalisha umeme kwa njia ya maji.

Mkurugenzi wa elimu ya ufundi Thomas Katebalirwe akaelza mikakati ya serikali katika kuboresha elimu ya ufundi.

Man Fongo Amvaa Sholo Mwamba

Msanii wa miondoko ya singeli Man Fongo amesema hawezi kukaa na kumzungumzia Sholo Mwamba kwa madai yeye ni mfa maji ndiyo maana haishi kutapa tapa kila uchao kumtaja.

 Man Fongo ameeleza hayo baada ya masaa machache kupita tokea kuonekana kwa 'video' ya Sholo iliyorushwa na EATV katika kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) usiku wa kuamkia leo, ikiwa imemuonyesha akimlaumu msanii mwenzake kuwa hana kipaji cha kuendelea kufanya muziki mzuri ndani ya mwaka 2018 huku akimtaka arejee katika fani yake ya awali ya 'DJ'.

"Mimi kwa sasa siwezi kumzungumzia mtu yeyote kwa maana naangalia muziki wangu kwa sababu ndiyo unaonifanya nieleweke kwa wadau wangu, pia unasababisha familia yangu ipate kula. Kwa hiyo mtu akitaka kutoka kwa kutumia kiki na kupitia mgongo wangu nakuwa bado simuelewi. Hivyo siwezi kumtumikia Sholo Mwamba 'eti aniambie mimi nirudi katika fani yangu ya 'DJ' wakati yeye hayupo katika 'manegement' yangu na yeye ni msanii kama mimi", alisema Man Fongo wakati alipofanyiwa mahojiano maalum.

Pamoja na hayo, Man Fongo ameendelea kwa kusema "ninachopenda kumshauri Sholo Mwamba ni kwamba atoe ngoma mpya ili aweze kusikilizwa na raia anachokifanya, apambanie muziki wake aweze kufika mbali na asiangalie muziki wangu mimi", alisisitiza Man Fongo.

Kwa upande mwingine Man Fongo amesema mwaka 2018 amejiandaa vizuri katika ufanyaji kazi wake na wala haiwezi kuwa kama alivyosema mpinzani wake huyo ambae kwa muda mrefu wamekuwa wakitoleana mapovu katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

"Kazi mpya nimeangusha juzi tu na mpaka sasa ninapo kwambia inafanya vizuri hivyo Sholo Mwamba ni mfa maji tu kama mtu ambae anatapa tapa yaani mfa maji haishi kutapa tapa. Kwa hiyo ameona bora apate kiki kwa mgongo wangu ili aweze kutoka", alisema Man Fongo.

Viongozi CCM Moshi Waaswa Kubadilika

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amewataka viongozi wa chama hicho Manispaa ya Moshi, kuacha kutembea na watu mifukoni na kutengeneza kofia za ubaguzi ndani ya chama kwa kuwa hali hiyo imekuwa ikikigharimu chama wakati wa uchaguzi.

Polepole amesema chama hicho kimekuwa kikijikuta katika wakati mgumu wakati wa uchaguzi kutokana na baadhi ya viongozi ndani ya chama kupenda ubinafsi na kuweka mbele uheshimiwa badala ya utumishi.

Ametoa rai hiyo leo Jumamosi wakati akizungumza  kwenye kikao cha ndani cha Halmashauri Kuu ya CCM Manispaa ya Moshi kilichofanyika mjini Moshi katika ukumbi ulioko kwenye ofisi za chama hicho mkoa ambapo amesema sasa ni wakati wa kujiimarisha ili kuweza kushika hatamu kila ngazi.

Amesema kumekuwepo na baadhi ya viongozi ndani ya chama ambao wamekuwa wakitengeneza makundi ya walionacho na wasio nacho wakati wa uchaguzi hali ambayo imekuwa ikikifanya  chama kushindwa kila mwaka wa uchaguzi katika majimbo mbalimbali likiwemo jimbo la Moshi Mjini.

"Kushindwa kwa CCM  katika majimbo mengi Kilimanjaro hasa hili la Moshi Mjini, kulisababishwa na viongozi, kutembea na majina yao mifukoni na kuweka uheshimiwa mbele badala ya utumishi,  hali hii ilijenga makundi, sasa ni lazima  tubadilike," amesema Polepole

VIDEO: CHADEMA Watoa Kauli Nzito Uchaguzi Kinondoni


Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum Mwalimu amefanikiwa kurudisha fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Kinondoni huku akiwataka wanachama wa chama hicho kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha muda mfupi.

TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE

Mkurugenzi wa Maji Musoma atumbuliwa

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isaack Kamwelwe , ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said (pichani kushoto) ambaye anachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha kwenye Mradi wa Maji Bunda na akizivunja Bodi za Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira za Mikoa ya Arusha na Mara (Musoma) baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wao siyo mzuri.

Kamwele amefikia uamuzi huo leo baada kubaini kuwa kumekuwepo na uzembe wa utekelezaji wa miradi ya serikali ya maji kwa baadhi ya watendaji katika idara hizo.

“Kufuatia ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majliwa mkoani Mara, imebainika kuwa kumekuwepo na matatizo ya huyo Mkurugenzi Gantala ambaye Waziri Mkuu ameagiza Mkurugenzi huyu watendaji wengine wachunguzwe na TAKUKURU.

“Hivyo kuanzia leo Januari 20, 2017 ninatengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said na nafasi yake itakaimiwa na Eng. Robert Petro Mponya wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUASA), ninamuagiza aisaidie Musoma ili waweze kufanya kazi inayotakiwa,” alisema Kamwele.

Wolper awafunda mabinti

Msanii wa filamu bongo ambaye sasa amegeukia ujasiriamli, Jackline Wolper, amewapa somo mabinti na kuwafunda juu ya kujishughulisha ili kujipatia kipato chao, na hatimaye waweze kuheshimika.

Akizungumza kwenye Friday Night Live ya East Africa Television, Jackline Wolper amesema ni wakati sasa mabinti kuacha kutegemea pesa wanazopewa na wanaume, na badala yake wajishughulishe ili kutengeneza pesa yako mwenyewe.

“Wadogo zangu wa kike 2018 mi ntaendelea kuwatia hasira, na kuendelea kuwaambia kwamba hela ya mwanaume sio ya kwako, ukishachukua hela ya mwanaume fanya kitu chako, iwe hela yako, usikubali kunyanyasika, kwa hela ya mtu, kwa hiyo wadogo zangu nitaendelea kuwaisipire ili mfanye kazi ili utambe na hela yako, usitambe kwa hela ya kuhongwa”, amesema Wolper.

Hivi sasa Wolper anamiliki biashara yake ya mavazi ambayo ana buni na kushona mwenyewe, ambayo aliwahi kusikika akisema inamuingizia pesa nyingi ingawa watu wengi wakimdharau kwa kumuita 'fundi cherehani'.


Waziri Mkuu ataka Watumishi Na Madiwani kushirikiana

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa Halmashauri na Mji wa Bunda pamoja na Madiwani washirikiane katika utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maendeleo.

Pia amewaagiza watumishi wa umma katika halmashauri ya wilaya na mji wa Bunda wafanye kazi kwa bidii na wawahudumie wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 19, 2018) wakati akizungumza na watumishi na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya na wa Halmashauri Mji wa Bunda, katika ukumbi wa Halmashauri ya Bunda.

“Watumishi wa umma  acheni kukaa sana maofisini tengeni muda wa kuwatembelea wananchi katika maeneo yao na shirikianneni nao katika kutatua kero zinazowakabili. Madiwani na watumishi lazima mshirikiane ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Alisema watumishi na madiwani wakishirikiana katika usimamizi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali  ya maendeleo, wilaya itafanikiwa katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Pia Waziri Mkuu aliwasisitiza watumishi hao kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu za utumishi  na wajiepushe na vitendo vya rushwa, wizi , ufisadi na uzembe kwa sababu vinarudisha nyuma maendeleo ya wananchi.

Awali, Waziri Mkuu alikagua mradi wa maji wa Bunda na baadae alizindua kikundi cha Ushirika cha Igembe Sabo na kukagua skimu ya umwagiliaji wa zao la mpunga ya Nyatwali wilayani Bunda.

Waziri Mkuu alihitimisha ziara yake wilayani Bunda kwa kuhutubia mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Stendi Mpya katika mji mdogo wa Bunda.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Sheria kali yaandaliwa kulinda misitu nchini

SERIKALI kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi wa misitu na bayoanui, inakamilisha taratibu za kutungwa sheria mpya pamoja na kanuni zake ili kudhibiti uharibifu wa misitu nchini.

Hatua hiyo inakuja kutokana na sheria zilizokuwepo kupitwa na wakati na kuchangia kuharibika kwa misitu kila mwaka.

Maamuzi ya kuanzisha sheria hiyo mpya yamekuja kutoka na sekta ya misitu na nyuki hapa nchini kuwa katika hatari ya kutoweka hali inayochangiwa kwa asilimia kubwa na vitendo vya uchomaji wa mkaa pamoja na ukataji kuni.

Akizindua mchakato wa kuhakiki rasimu ya taifa ya misitu, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga, alisema maamuzi ya kutunga sheria mpya yanatokana na ile iliyopo ya mwaka 1998 kutokuendana na mabadiliko ya jamii ya sasa ambayo yanatishia kwa kasi uhai wa sekta hiyo ya misitu.

Naibu Waziri alisema sekta ya misitu na nyuki ni mtambuka kwani inashirikisha wizara mbalimbali kama Nishati, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),Afya, Viwanda na Biashara hivyo kulingana na sheria mpya kazi ya kulinda misitu itakuwa ikifanywa kwa pamoja.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS),Profesa Dos Santos Silayo, alisema kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya itakuwa mkombozi wa misitu nchini kwa kuwa iliyopo ilitoa mwanya kwa baadhi ya watu kufanya uharibifu.

Alisema kuwa rasilimali za misitu zipo za kutosha kulingana na ikolojia mbalimbali za kila eneo kama kuweka sheria kali za kuhifadhi kuna hatari ya vizazi vijavyo vikashindwa kuzitumia rasilimali hizo.

Mtalaam wa misitu, Dk. Felician Kilahama,alisema kuwa sekta ya misitu inakabiliwa na changamoto kubwa ya usimamizi,ukataji wa miti ambapo katika kipindi cha miaka mitatu iliopita hekta 582 zilifanyiwa uharibifu kwa ajili ya shughuli za uchomaji wa mikaa na ukataji wa kuni.

Alisema kuwa kuanzishwa kwa sheria hiyo mpya ya misitu na kusimamiwa kwa pamoja , serikali pamoja na wadau kutawezesha kurudisha misitu ya asili kwa haraka ambayo imeanza kutoweka kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira.

Agizo la Waziri Mwigulu kwa Polisi kuhusu kukamata wazururaji

January 20, 2018 Waziri wa Mambo ya Ndani, Dr. Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi nchini kutafuta namna ya kupunguza wahalifu wanaokamatwa kwa makosa kama uzururaji ili kupunguza mrundikano kwenye mahabusu.

Ameeleza kuwa suala hili pia litaepusha watuhumiwa wanaopelekwa mahabusu kwa makosa ya uzururaji kupata nafasi ya kuzungumzia masuala ya uhalifu na watuhumiwa waliozoea.

Kwa upande mwingine Dr. Mwigulu ameagiza wananchi kushirikiana na serikali katika ujenzi wa vituo vya polisi kwa kuwa suala la ulinzi ni ajenda ya kila Mtanzania na linapaswa kupewa kipaumbele.

Akizungumza na wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Dr. Mwigulu amesema kuwa mkakati wa Halmashauri hiyo kujenga kituo cha kisasa cha polisi ni kitendo cha kupongezwa kwani wanalenga kukomesha uhalifu wa aina zote.

VIDEO: Le Mutuz, Awataka watumia mitandao waitumie kwa manufaa

Mtoto wa aliekuwa waziri mkuu mstaafu, William malecela 'Le Mutuz' amewataka watumia mitandao ya kijamii kuitumia vizuri kwa manufaa ili kujitengenezea kipato, ameyasema hayo leo akiwa katika chuo cha T I A kilichopo uhasibu ambapo alialikwa kama mgeni na kikundi cha Victorious Women Empowerment Ili kuelezana machache juu ya namna ya kumkomboa mwanamke.

vile vile amesisitiza na kuwataka kusoma kwa bidii wanafunzi ambao bado wako mashuleni wanasoma na kusema kuwa elimu ndio mafanikio yao na itawafanya kufikia leo, vile vile akawaeleza baadhi ya changamoto alizopitia hadi alipofikia hapo alipo kuwa alianza kulala stendi ya magari na kuchoma kuku KFC na hakujali kama baba yake alikuwa waziri mkuu.

TAZAMA FULL VIDEO HAPA...... USISAHAU KUSUBSCRIBE.....

Waziri arudi CCM atwae jimbo 2020

Mwanasiasa  wa upinzani na aliyekuwa Naibu Waziri katika serikali ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete, Goodluck Ole Medeye, ametangaza kurejea Chama Cha Mapinduzi huku akidai kuwa ameamua kufanya hivyo kwa kuwa vitendo vya rushwa,-Hususan nyakati za uchaguzi, vimemalizwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. John Magufuli.

 Ole Medeye juzi alisema kilichomkimbiza CCM mwaka 2015 na kujiunga na Chadema ni vitendo vya rushwa katika mchakato wa kupata wagombea wa chama hicho tawala.

Alisema anafurahi kuona sasa vitendo hivyo havipo ndani ya CCM baada ya kudhibitiwa na Rais Magufuli.Ole Medeye alikuwa mmoja wa wabunge watano wa CCM waliojiunga na Chadema Agosti 12, 2015 wakiongozwa na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (Monduli).

Ole Medeye aliteuliwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuwania nafasi ya Uspika wa Bunge baada ya Uchaguzi Mkuu.

Wengine waliohama pamoja na Lowassa ni Makongoro Mahanga (Segerea), James Lembeli (Kahama) na mbunge wa viti maalum, Esther Bulaya ambaye sasa ni mwakilishi wa wananchi wa Bunda Mjini (Chadema).

Hata hivyo, Ole Medeye alihama Chadema kabla ya mwaka kumalizika na kujiunga na UDP kinachoongozwa na John Cheyo Juni 12, 2016.

Medeye alisema alihamia UDP kwa kuwa inasimamia haki na demokrasia na kwamba yeye alikuwa akitaka demokrasia ya kweli na jukwaa la haki katika kuleta haki na maendeleo kwa Watanzania.

Alisema  kuwa alikaa chama hicho cha 'Bwana Mapesa' kwa miezi mitatu tu hata hivyo, kwa kuwa "nilikwenda kufanya kazi maalum."

Na sasa, Ole Medeye amesema ameamua kurejea CCM kwa kuwa kila mwanachama anayo fursa kushiriki uchaguzi, ikiwamo kugombea nafasi yoyote bila kutoa rushwa na akashinda.

"Mimi sijawahi kuwahonga watu ili wanichague," alisema Ole Mideye na "wakati huo CCM kulikuwa na rushwa sana; ndiyo maana nikaamua kukimbia.

"Lakini kwa sasa hakuna tena kitu kama hicho, hivyo nimeamua kurejea CCM."

Ole Medeye alisema katika Uchaguzi Mkuu ujao, mwaka 2020, anataka kurudi na kuwatumikia wananchi kupitia nafasi ya ubunge.

Maseneta wakwamisha serikali ya Trump

Bunge la Seneti nchini Marekani limeshindwa kuidhinisha mswada ambao ungeongeza ufadhili wa serikali ya kitaifa kwa mwezi mmoja.

Kufuatia hatua hiyo huduma nyingi za serikali zitakwama, hata hivyo athari kamili itaanza kuonekana siku ya Jumatatu, wakati wafanyakazi wa serikali watarejea kazini.

Mara ya mwisho shughuli za serikali zilikwama nchini Marekani ni mwaka wa elfu mbili na kumi na tatu, na ilidumu kwa muda wa siku kumi na sita wakati ambapo wafanyakazi wengi wa serikali walishurutishwa kwenda likizo ya lazima.

Ni mara ya kwanza kwa huduma za serikali kukwama huku chama cha Republican kudhibiti mabunge yote na ikulu ya White house.

Ikulu ya whitehouse imewalaumu wabunge wa Democrats kwa kuweka siasa juu ya maswala ya kiusalama , familia za wanajeshi, watoto walio katika mazingira magumu, na uwezo wa taifa hilo kuwahudumia raia wa Marekani.

Lakini kiongozi wa wabunge wa Democrats Chuch Schumer, alisema kuwa rais Trump alikataa makubaliano yasiopendelea upande wowote na hakukishinikza chama chake katika bunge la Congress.

Mkwamo wa huduma za serikali nchini Marekani ulifanyika mara ya mwisho 2013 na ukachukua muda wa siku 16.

Republicans waliutaja muswada huo kwa jina la ''Schumer Shutdown' na hawakukosea.

Chuck Schumer na wabunge wenzake wa Democrats kupitia usaidizi wa wabunge wachache wa Republican walizuia muswada ambao ungesaidia serikali kuendelea na shughuli zake, hata ijapokuwa kwa muda.

Hatahivyo kuchukua jukumu na kutoa lawama ni vitu viwili tofauti.

Democrats watasema kuwa walikuwa wamekubaliana na rais kupitisha muswada usiopendelea upande wowote kuhusu mabadiliko ya sheria ya uhamiaji, kabla ya kukiuka makubaliano hayo wakati wa mkutano katika afisi ya Oval wiki iliopita.

Swala la kurushiana lawama lilianza saa sita usiku na mshindi bado hajatangazwa.

Hatahivyo atakayeshindwa katika mkwamo huu ni chama kitakachoingia katika vita na idadi ndogo ya wabunge ikiwa ni habari mbaya kwa rais Trump na chama cha Republicans.

Habari njema ni kwamba , pande zote mbili na ngome zao za kisiasa zitafurahishwa kwa kufanya mambo kuwa magumu.

Kwa nini pande hizo mbili zisikubaliane?

Swala linalogombaniwa ni lile la Democrats kutaka zaidi ya wahamiaji wasio na vibali walioingia nchini Marekani kutofurushwa.

Wahamiaji hao walipatiwa vibali vya kuwa nchini humo kwa muda chini ya mradi ulioanzishwa na rais wa zamani Barrack Obama.

Mnamo mwezi Septemba, bwana Trump alitangaza alikuwa anasitisha mpango huo huku akilipatia bunge la Congress hadi mwezi Machi kuwa na mpango mbadala.

Waziri Ndalichako awapa wiki moja TBA

Waziri wa elimu,sayansi,na teknolojia na ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewapa wiki moja Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kuonyesha maendeleo ya mradi wa ujenzi wa madarasa, hostel na ofisi kwa ajili ya chuo kikuu cha Muhimbili Kampasi ya Mloganzil

Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo leo alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea mradi huo na kutoridhishwa nao, baada ya kukuta hauna maendeleo yoyote huku serikali ikiwa imeshalipa gharama za ujenzi.

“Ninawapa wiki moja, nataka hapa nione vifaa vyote vya ujenzi viwe vimemwagwa vywa kutosha, nataka nione mafundi wa kutosha, haiwezekani site kubwa kama hii mafundi hawafiki hata 40, kweli kazi itaenda!? Niliwaambia muongeze mafundi mwezi wa 11 lakini kwa sababu mlizozijua wenyewe hamjaongeza, sasa ndani ya wiki moja wasipoongeza mafundi, hatuwezi kuwa na mkandarasi ambaye haendani na matakwa ya mteja, nimekwisha wapatia bilioni 3 na milioni 900,  nikiangalia fedha nimezitoa tangu mwezi wa 8 sioni kazi ambayo inafanana na kiwango cha fedha ambayo nimewapatia, ndani ya wiki moja wasipotimiza angalieni namna ya kuvunja huo mkataba.”, amesema Waziri Ndalichako.

Waziri Ndalichako ameendelea kwa kulalamika kuwa wakandarasi hao wamekuwa wakiaminiwa na serikali na kuwapa miradi mingi, lakini wamekuwa wakisua kukamilisha miradi kwa muda.

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

New VIDEO: Mr. Blue – Mbwa Koko

DOWNLOAD VIDEO

Nafasi za kazi leo Jan 20

Kocha Mpya wa Simba apagawishwa na Okwi

KIKOSI cha Simba,  Alhamisi kilijitanua kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Singida United katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ambao Simba ilikuwa ikihitaji zaidi matokeo ya ushindi ili ijihakikishie nafasi yake ya kukaa kileleni, ilifanikiwa kupata bao la mapema dakika ya tatu lililofungwa na Shiza Kichuya. Beki wa kati wa timu hiyo,

Asante Kwasi, aliongeza bao la pili dakika ya 24 baada ya kukwepa mtego wa kuotea aliowekewa na mabeki wa Singida United.

Mara baada ya Kwasi kufunga bao hilo, kocha mpya wa Simba, Pierre Lechantre raia wa Ufaransa, alinyanyuka kwenye kiti chake akiwa jukwaani na kuanza kushangilia pamoja na ofisa habari wa timu hiyo, Haji Manara huku akiwapungia mkono mashabiki wa timu hiyo.

Dakika ya 65 wakati Emmanuel Okwi wa Simba anajiandaa kuingia kuchukua nafasi Mzamiru Yasin, mashabiki wa timu hiyo walikuwa wakimshangilia kwa nguvu jambo ambalo lilimhamasisha straika huyo na kuipatia Simba bao la tatu dakika ya 75.

Okwi aliongeza bao la nne dakika ya 82 ambapo kwa mara nyingine, Mfaransa, Lechantre aliinuka kwenye kiti na kushangilia kwa nguvu. Katika mchezo huo, Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji wawili ambapo ilianza kumtoa Mwinyi Kazimoto dakika ya 22 na nafasi yake kuchukuliwa na Said Ndemla kabla ya dakika ya 65 kutoka Mzamiru na kuingia Okwi.

Kwa upande wa Singida United, dakika ya 59 ilimtoa Kiggy Makasi na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Chuku. Kwa matokeo hayo, Simba inaendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 29 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 27. Mtibwa Sugar ni ya tatu ina pointi 24, Singida inakamata nafasi ya nne na pointi 23, huku Yanga ikiwa ya tano na pointi 22.

Wafanyabiashara waifungukia Serikali

Waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango

Wafanyabiashara nchini wameiomba Serikali kuacha kufanyakazi kwa kukurupuka ikiwamo kuwaadhibu kwa makosa ya wengine badala yake iwe kitu kimoja na sekta binafsi ambayo ina mchango mkubwa kwa Taifa.

Wito huo ulitolewa jana na makamu mwenyekiti wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Salum Shamte kwenye mkutano baina yao na Serikali ulifanyika katika ukumbi wa Hazina mjini hapa na kuhudhuriwa na wabunge na baadhi ya mawaziri.

Shamte alisema katika baadhi ya maeneo, Serikali imekuwa ikifanya mambo kwa kukurupuka na kujikuta ikiwaumiza wafanyabiashara ikiwamo masuala ya kodi.

Makamu mwenyekiti huyo alisema sekta binafsi inaumizwa kwa kiasi kikubwa na uamuzi wa kukurupuka hasa wa kuwaadhibu watu wasiohusika kwa kosa la mtu mmoja.

“Wakati mwingine watu wanaumizwa sana kwa ajili ya maamuzi haya, kodi na kufunga biashara za watu ilhali kosa linakuwa la mtu mmoja. Kwa nini hamuondoi kasoro hiyo?” alihoji Shamte wazo ambalo liliungwa mkono na mkurugenzi mtendaji wake, Godfrey Simbeye.

Akijibu hoja hiyo, waziri wa fedha na mipango, Dk Philip Mpango alikiri kuwapo kwa uamuzi wa kushtukiza serikalini na kusema wakati mwingine inalazimika kufanya hivyo.

Dk Mpango alisema wakati mwingine kuna madhara kwa watu kukurupuka na kufanya vitu visivyokuwepo na kusema ndani ya Serikali, kuna baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu ambao wanafanya vitu ama kwa kukurupuka au kutokujua.

“Nakiri kweli ndani ya Serikali kuna watu ambao wanafanya mambo ya ovyo na kuisababishia Serikali hasara kubwa, lakini kuna wakati tunafanya hivyo kwa sababu inabidi tufanye hivyo kwa masilahi ya nchi,” alisema Dk Mpango.

Hata hivyo, aliwatupia lawama baadhi ya wafanyabiashara akisema wamekuwa na tabia ya kukwepa kodi jambo ambalo ni kinyume na Serikali.

Sababu ya Engine kumchukua Wolper

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Engine ambaye hivi karibuni kulikuwa na tetesi za kumng'oa Jackline Wolper na kumuweka ndani, ameweka wazi sababu za kuamua kumtumia msanii huyo kwenye kazi yake.

Akizungumza kwenye Friday Night Live Engine amesema Wolper ni miongoni mwa wanawake wachache Tanzania wanaojitambua, na ndio sababu iliyomfanya asifikirie mara mbili kumfuata.

“Wolper ni mwanamke jasiri, mwanamke anayejitambua , anajituma yuko fit kila idara, na ndio maana nikamfuata”, amesema Engine.

Msanii huyo ambaye ameachia kazi yake mpya, amewaomba watanzania kufuatilia kazi zake kwani alishafanya kazi nyingi siku za nyuma lakini hazikuwahi kufanya vizuri.

Waziri Mkuu aagiza kiongozi huyu akamatwe

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameamuru Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara kumkamata na kumuhoji Mkurugenzi Mtendani wa Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) Mhandisi Gantala Said.

Agizo la Waziri Mkuu limekuja kufuatia tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji Wilayani Bunda mkoani Mara zinazomkabili Mkuregenzi huyo. Waziri Mkuu yupo Mkoani humo kwa ziara ya kikazi.

Mhandisi Gantala Said ameshindwa kueleza sababu zilizosababisha mradi wa maji mjini Bunda kutokamilika pamoja na Serikali kutoa fedha nyingi kwaajili ya kutekeleza Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani.

Majaliwa amesema Mkurugenzi huyo amekuwa akimlipa mkandarasi fedha kabla ya kufanya kazi ambapo hadi sasa tayari mkandarasi wa mradi huo ameshalipwa zaidi ya Sh. bilioni saba na mradi haujakamilika huku wananchi wakiendelea kutumia maji ambayo siyo salama.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw. Adam Malima ameagiza kufungwa kwa ofisi za MUWASA na kuwataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kutoruhusiwa kuingia ofisini hadi hapo uchungi utakapokamilika.

Wastara: "Sitozikwa na wasanii pekee"



Msanii Wastara Juma

Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amesema hatokuja kumladhimisha mtu yeyote katika tasnia ya 'bongo movie' kuwa yeye hana pesa ya kujitibia ugonjwa wake unaomsumbua kwa madai hata siku ikitokea akifa hawezi kuzikwa na hao pekee yao.

Wastara ametoa kauli hiyo kwenye kipindi cha 'FRIDAY NIGHT LIVE' (FNL) kinachorushwa na EATV tinga namba moja kwa vijana, baaada ya kuwepo kwa baadhi ya watu kutomuamini kwa kile kinachomsumbua huku wengine wakidiriki hata kujaribu kumwambia anatafuta kiki kupitia tatizo hilo linalomsumbua la mguu wake.

"Yani hapa mtu anaweza akaniumiza kwa maneno au vitendo kwa sababu yeye anaamini kwa mawazo yake na kichwa chake kwamba, mimi nimekaa kitandani siumwi au pengine nimejiona nimepotea katika ulimwengu hivyo natafuta kiki yaani nijifunue nguo niupige picha mguu wangu uliyochanika kisha niuweke kwenye gazeti ama kwenye runinga (Tv) ?", alihoji Wastara.

Hata hivyo Wastara amesema hawezi kubadilisha fikra za watu wanavyofikilia kwa kuwa hayo ndiyo maisha yao ya kutoamini jambo lolote lile.

"Na kama kuna wasanii ambao wanaamini mimi siumwi siwezi kumladhimisha hata siku moja na ambaye atasema hatokuja kumtembelea Wastara kwa sababu haumwi au hana shida pesa, mimi siwezi kumfanya aniamini kwamba sina pesa. Sitoweza kufanya hicho kitu kwa sababu maelezo ninayoyaeleza katika runinga ndiyo yaleyale hayotokuja kubadilika. Kwa hiyo ninachoongea hapa ni ukweli hautokuja kubadilika miaka yote hata nikifa", alisisitiza Wastara.

Pamoja na hayo Wastara aliendelea kwa kusema "wapo watu wa kweli wanaoamini na wengine wasioamini ambao huwezi kuwafanya waniamini. Watanzania wanaoniamini mimi wanatosha kwa sababu mwisho wa siku sitokuja kujizika mwenyewe au kuzikwa na wasanii pekee yake", alisema Wastara.


Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Yawaandikiia Barua Wabunge Kutaka Miamala Yao

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imewaandikia barua baadhi ya wabunge, ikiwataka kuwasilisha taarifa za miamala ya benki za kuanzia Januari hadi Desemba 2017.

Sekretarieti hiyo imetaka taarifa hizo ziwe zimeifikia ndani ya siku 30 kuanzia Januari 15, 2018.

Barua hiyo  inawataka wabunge hao  kutekeleza agizo hilo ili kuthibitisha taarifa zilizomo kwenye tamko lake  alilowasilisha.

Ofisa mmoja wa taasisi hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, alithibitisha kuwepo kwa barua hizo, akisema si wote walioandikiwa barua za kutakiwa kutoa taarifa hizo.

Hata hivyo, alisema wabunge walioandikiwa ni wale ambao fomu zao zinaonyesha haja ya uhakiki zaidi wa taarifa zao.

Rais wa John Pombe Magufuli ndiye alikuwa wa kwanza kuwasilisha fomu yake ya tamko kuhusu rasilimali na madeni katika ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma iliyopo Mtaa wa Ohio, Wilaya ya Ilala Jijini Dar es Salaam Desemba 28, 2017.

Baada ya kuwasilisha fomu hiyo, Rais aliipongeza sekretarieti hiyo kwa kazi inazofanya na kumtaka Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu, Harold Nsekela kutopokea fomu ya kiongozi yeyote ambaye angeshindwa kuwasilisha tamko la kabla ya Desemba31, 2017.

Kauli hiyo ya Rais iliwaamsha viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge na viongozi wengine wa Serikali kufurika kwenye ofisi hiyo kuwasilisha matamko yao ya mali walizonazo.

Chadema kugombea Kinondoni na Siha

 Wakati naibu katibu mkuu wa Chadema-Zanzibar, Salum Mwalimu akichukua fomu ya kuwania ubunge wa Kinondoni, mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ameeleza sababu zilizowafanya kurejea katika uchaguzi wa Februari 17.

Mwalimu na mwenzake wa Siha, Elvis Mosi walipitishwa na Kamati Kuu ya Chadema jana kugombea ubunge wa majimbo hayo huku Mbowe akisema, “hiki ni chama cha siasa si zege inayoendeshwa na matamanio na ushawishi wa wananchi.”

Chadema na vyama vinavyounda Ukawa- NLD, CUF, NCCR Mageuzi- pamoja na Chaumma na ACT Wazalendo vilisusia uchaguzi mdogo wa ubunge wa Longido, Songea Mjini na Singida Kaskazini uliofanyika Januari 13 kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutoridhishwa na mazingira ya uchaguzi wa udiwani katika kata 43 uliofanyika Novemba 26.

Vyama hivyo viliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kusitisha uchaguzi huo ili kutoka fursa ya kukutana na kufanya tathmini ya mazingira ya uchaguzi huo jambo ambalo tume hiyo ililipinga ikisema inasimamia sheria.

Jana, Mbowe alisema walipotangaza kutoshiriki uchaguzi wa Januari 13 walitoa sababu za kutoridhishwa na uchaguzi wa madiwani wa kata 43. “Hatukusema kwamba hatutashiriki kabisa uchaguzi hapana, tulitoa sababu kuwa hatukuridhishwa na uchaguzi wa zile kata 43. Bila shaka mmeona wenyewe hata uchaguzi ulivyokuwa, kama haukuwepo na hata vyama vingine vilivyoshiriki kama havikuwepo vile,” alisema mbunge huyo wa Hai.

“Kilio chetu kimesikika ndani na nje ya nchi, kimesikika kwa wananchi na kwa hatua hiyohiyo tumeona hatutawatendea haki wananchi wa Kinondoni na Siha ambao wamewekewa wagombea ambao hawawataki na hilo kila mtu analijua.”

Mgombea wa CCM aliyepitishwa kugombea Jimbo la Kinondoni ni Maulid Mtulia, ambaye alikuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CUF kabla ya kuhamia chama tawala kwa madai ya kuunga mkono utendaji kazi wa Rais John Magufuli. Katika Jimbo la Siha, chama tawala kimemuweka Dk Mollel aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia Chadema, lakini akakihama chama hicho na kujiunga CCM kwa madai ya kuunga mkono utendaji kazi wa Rais Magufuli.

Mbowe alisema, “Tunarudi katika uchaguzi, vyombo vinavyopaswa kusimamia haki vifanye hivyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vingine vyote, hatutaidai tena haki kwa kupiga magoti hivyo watekeleze majukumu yao ipasavyo.”

Alipoulizwa ilikuwaje wakampitisha Mwalimu ambaye hakushiriki kura za maoni, Mbowe alisema utaratibu wa kura ya maoni ndani ya Chadema haupo kikatiba, wanaamini maridhiano ndiyo njia sahihi ya kutokukigawa chama.

“...Unajua unapofanya kura za maoni unaweza kuwa na makundi mawili na adui yako akayatumia makundi hayo kufanikisha kumpata mtu ambaye ni dhaifu, kwa hiyo Kamati Kuu imeyaona hayo na ililiona hilo Kinondoni ndiyo maana ikamteua Mwalimu,” alisema Mbowe

Vuguvugu laisukuma

Wakati Mbowe akitoa sababu hizo, baadhi ya watu waliojitokeza kuomba kuteuliwa kugombea ubunge wa Kinondoni walisema vuguvugu la kuanzisha mchakato wa kuchukua fomu limesaidia chama hicho kushiriki uchaguzi huo mdogo.

Vuguvugu hilo lilitokana na Chadema Wilaya ya Kinondoni kutoa ruhusa kwa wanachama wao kutangaza nia ya kugombea jimbo hilo kisha mchakato wa kuchukua na kurudisha fomu kwa ajili ya kuomba kuteuliwa uliofanyika Januari 16.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki, mkurugenzi wa mambo ya nje na itifaki wa Chadema, John Mrema alinukuliwa akisema msimamo wa Ukawa wa kutoshiriki uchaguzi wa majimbo ya Siha na Kinondoni haujabadilika na kwamba wameunda kamati ndogo inayofanya utafiti kuhusu mchakato huo.

Alisema hata mchakato wa kuchukua fomu uliokuwa unafanywa na ngazi hiyo ya wilaya haukuwa na baraka za ngazi za juu.

Pamoja na hayo, mchakato wa kura za maoni Kinondoni uliendelea kwa wanachama saba ambao ni David Assey, Nicholus Agrey, Rose Moshi, Mustafa Muro, Ray Kimbitor, Juma Uloleulole na Mozah Ally kupigiwa kura.

Katika mchakato huo wa kura za maoni, Kimbitor aliibuka kidedea kwa kuwabwaga wenzake na baada ya kumalizika viongozi wa wilaya walisema wanayapeleka majina hayo yote saba katika kikao cha dharura cha Kamati Kuu kilichoketi jana ili kupata baraka na kusubiri uteuzi wa mgombea mmoja kutoka katika chombo hicho cha uamuzi.

Akizungumzia uamuzi huo wa Kamati Kuu, Kimbitor ambaye pia ni Diwani wa Hananasif alisema shida yao ni kuona Chadema inashiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na kuna dalili za chama hicho kuibuka mshindi kutokana na misingi bora iliyojiwekea.

“Kila mtu anajua kulikuwa na sintofahamu Chadema kushiriki au kutoshiriki. Ndiyo maana sisi tulianzisha lile vuguvugu la kuchukua fomu ndani ya chama na hatimaye limezaa matunda kwa chama kuingia katika uchaguzi huu,” alisema Kimbitor.

Katibu wa Chadema Mkoa Dar es Salaam, Henry Kilewo alisema Kamati Kuu ilipelekewa majina tisa na jina la Mwalimu lilirudi baada ya kupendekezwa na alisisitiza mchakato uliofanywa na ngazi ya wilaya haukuwa na baraka ya juu.

“Kesho (leo) tutatoa ratiba za kampeni baada ya mchakato huu kukamilika. Nawaomba wana-Chadema na Ukawa wawe watulivu kila kitu kitakwenda sawa na mgombea wao yupo makini,” alisema Kilewo.

Kwa upande wake, Mwalimu ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, 2015 aligombea Jimbo la Kikwajuni na kushindwa na mgombea wa CCM, Hamad Yussuf Masauni aliishukuru Chadema kwa imani naye na kumpa nafasi hiyo.

“Naingia katika kinyang’anyiro cha kuomba ridhaa ya wakazi wa Kinondoni kuwa mbunge wa Kinondoni. Siendi kuwa mbunge wa Chadema au Ukawa, nitakuwa mbunge wa watu wa Kinondoni,” alisema Mwalimu na kuongeza.

“...Naomba wakazi wa Kinondoni watupime, watuchuje na watutathmini wagombea na baadaye waamue nani anakidhi vigezo na anatosha kuwatumikia katika kipindi cha miaka mitatu iliyobakia.”

Alisema Kinondoni ni taswira na sura ya nchi na imebeba vitu vingi kuliko kawaida na ana imani ya wakazi wa jimbo hilo watawapima vizuri kabla ya kufanya uamuzi wa kuwachagua na atahakikisha anasimamia vyema masilahi ya Taifa.

Amber Lulu afunguka historia ya kusikitisha ya maisha yake

Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alipata umaarufu kwa kupiga picha za utupu na kuweka mitandaoni, Amber Lulu, amesimulia historia ya maisha yake ambayo imemfanya abadilike na kuwa alivyo sasa.

Akizungumza kwenye Backstage ya Bongo Fleva Top 20 ya East Africa Radio, Amber Lulu amesema maisha yake ya nyuma yalikuwa yenye mahangaiko ya maisha akiwa na umri mdogo, huku akilazimika kujitafutia hadi pesa ya shule.

Amber Lulu amesema wakati yupo mdogo akisoma mama yake alikuwa na tatizo na lililomfanya ashindwe kutimiza majukumu mengi ya kifamilia, hivyo akaamua kujiingiza kwenye masuala mbali mbali ya kujitafutia riziki ili aweze gharama za kumudu maisha.

FAHAMU KWA UNDANI UGONJWA WA PUMU (ASTHMA)


LEO tutaangalia ugonjwa wa pumu au kitaalamu huitwa asthma. Ugonjwa wa pumu huathiri njia za hewa ambazo huingiza na kutoa hewa katika mapafu. Mtu mwenye ugonjwa huu kuta zake za ndani za njia ya hewa hupata maumivu ambayo kitaalamu huitwa inflammation na kuvimba.

Maumivu katika njia za hewa huzifanya njia hizo za hewa kujihami kwa kusinyaa na hivyo kupunguza kiasi cha hewa kinachopita kwenda kwenye mapafu. Hali hii husababisha mgonjwa kutoa mlio kama wa filimbi au mluzi wakati wa kupumua. Ugonjwa wa pumu unaweza kudhibitiwa kama vile ugonjwa wa kisukari na moyo unavyoweza kudhibitiwa.

AINA ZA PUMU
Kuna aina kuu mbili za pumu. Aina ya kwanza ni ile inayoanza mapema kitaalamu huitwa early onset asthma na aina ya pili ni ile inayochelewa kuanza yaani late onset asthma. Tuchambue kwa kifupi aina hizo za pumu. Pumu inayoanza mapema (early onset asthma) Aina hii ya pumu huanza kumkumba mtu akiwa mtoto ambapo miili yao hutengeneza kingamwili (antibodies) za IgE. Wagonjwa wa aina hii ya pumu hutambuliwa kwa vipimo maalum vya ngozi ambapo huonyesha kuathirika kwa asilimia kubwa ya vipimo hivyo vinapofanywa. Pia wagonjwa hawa huwa na matatizo mengine ya mzio (allergic disorders) kama mafua na ukurutu (eczema).

Pumu inayochelewa kuanza (late onset asthma) Aina hii ya pumu,tofauti na iliyopita, humkumba mtu akiwa mkubwa. Hakuna ushahidi wowote unaohusisha maradhi haya na mizio (allergens) vinavyotokana na mazingira na uwezo wa kusababisha aina hii ya pumu. Haifahamiki hasa ni sababu zipi zinazofanya njia za hewa kupata maumivu na hivyo kusababisha mtu kupata ugonjwa huu wa pumu. Vyanzo mbalimbali vinaonyesha kuwa ni kutokana na mseto wa vitu kama tumbaku, maradhi na baadhi ya vitu vinavyosababisha mzio.

Kuna vitu katika mazingira ambavyo vinaweza kusababisha mtu kushambuliwa na pumu. Vitu vinavyosababisha mzio ni kama vumbi, mende, chavua (pollen) kutoka kwenye miti na majani, viwasho (irritants) kama moshi wa sigara, uchafuzi wa hewa, harufu kali kutoka kwenye rangi au kitu chochote kitoacho harufu, au msongo wa mawazo na maradhi yatokanayo na virusi au manyoya au magamba ya wanyama.
Mtu anaweza kupata pumu kutokana na kuwa na mzio na madawa kama aspirin, ugonjwa wa kucheua, viwasho au vizio vitokanavyo na kemikali au kuwa na magonjwa ya njia ya hewa n.k Mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu kama anaishi katika miji mikubwa na kukumbana na vitu ambavyo kwake
humsababishia mzio, au kuvuta hewa iliyo na moshi, kemikali zitokanazo na kilimo,dawa za kutengeneza nywele, rangi, vyuma, plastiki au vifaa vya elektroniki. Mtoto anaweza kuwa na pumu kwa kurithi kwa mmoja wa wazazi wake mwenye pumu au baada ya kuathirika na maradhi ya mfumo wa hewa kama kikohozi na mafua wakati wa utoto au kutokana na kuwa na unene wa kupita kiasi (obesity), kuwa na ugonjwa wa kucheua na kiungulia (Gastro esophageal reflux disease).

DALILI ZA PUMU Baadhi ya dalili za kawaida za ugonjwa wa pumu ni kama zifuatazo: Mgonjwa kushikwa na kikohozi: Mara nyingi kikohozi cha pumu huwa kikali nyakati za usiku au alfajiri na hivyo kumfanya mgonjwa kutolala vizuri usiku. Mgonjwa kutoa sauti ya mfano wa mtu anayepiga mluzi au filimbi wakati wa kupumua, kifua kubana ambapo mgonjwa husikia kama kitu kinakandamiza kifuani au wakati mwingine husikia kama mtu amemkalia kifuani. Dalili nyingine ni mgonjwa kukosa hewa na kujikuta kama hawawezi kupumua kwa hewa inayoingia na kutoka kwenye mapafu. Kutokana na hilo mgonjwa huyo atakuwa anapumua harakaharaka. Dalili hizo zinaweza kuwa mbaya kiasi cha kuhatarisha maisha. Wengine hupata dalili hizo mara moja tu kwa mwezi, wengine kila wiki na wengine hupata dalili kila siku.

UCHUNGUZI Mgonjwa ni lazima afanyiwe kipimo kwa kuangalia jinsi mapafu yanavyofanya kazi. Kipimo hicho hujulikana kitaalamu spirometry na hutumika kwa watu kuanzia miaka
mitano na kuendelea na hutathmini kiasi cha hewa mtu awezacho kukitoa baada ya kuvuta hewa kwa nguvu na kwa haraka. Kipimo hiki cah spirometry pia hutumika kutathmini jinsi mgonjwa wa pumu anavyoendelea, kupata nafuu au tatizo kuongezeka. Mgonjwa pia anaweza kufanyiwa kipimo cha mzio (Allergy Test). Kipimo cha ugonjwa wa kucheua na kiungulia pia hufanyiwa mgonjwa.

Mgonjwa pia ni lazima apimwe mapafu kwa X-ray ili kuona iwapo kuna kitu chochote kilichoziba njia ya hewa au kama kuna maradhi yoyote katika mapafu au moyo. TIBA Kuna aina mbili za matibabu ya pumu, moja ni ile ya dharura ili kutoa msaada au nafuu ya haraka. Dawa hizi ni zile zinazosaidia kutanua njia za hewa ambazo zimesinyaa yaani bronchopdilators ambazo pia husaidia kuilainisha misuli ya njia za hewa iliyosinyaa ili iweze kutanuka na kuruhusu hewa ya kutosha kuingia kwenye mapafu. Aina nyingine ya dawa ni zile za muda mrefu. Aina hizi za dawa hutumiwa mara kwa mara kwa kipindi kirefu kuzuia dalili za pumu na mashambulizi. Watu wenye pumu isiyoisha wanahitaji matumizi ya dawa ya muda mrefu.Kotikosteroidi za kuvuta (inhaled corticosteroids) ni nzuri kwa aina hii ya pumu.

TIBA KWA WATOTO Watoto wenye pumu kama ilivyo kwa watu wazima wanapaswa kumwona daktari wale walio na umri mdogo wanahitaji uangalizi wa wazazi/ walezi ili kudhibiti pumu. Watu wazima wanaweza kutakiwa kupunguza au kuongeza matumizi ya dawa za pumu kutokana na maradhi mengine waliyonayo. Madawa kama ya kutibu shinikizo la juu la damu, ugonjwa unaotanua mboni ya jicho na kutatiza kuona (glaucoma),aspirini na dawa za maumivu (non steroidal anti inflammatory drugs) huingiliana na utendaji wa dawa za pumu au zenyewe kusababisha pumu, hivyo matumizi yake yanahitaji ushauri wa daktari.

Wajawazito wenye pumu wanahitaji ushauri wa karibu wa daktari kwa kuwa ikiwa pumu itasababisha kusinyaa kwa njia ya hewa basi wanaweza kusababisha upungufu wa hewa ya oksijeni kwa mtoto hali ambayo ni hatari kwa mtoto tumboni. Dawa nyingi za pumu hazina madhara kwa mtoto aliye tumboni, hivyo ni muhimu kuendelea na matibabu wakati wa mimba kwa ushauri wa daktari kuliko kuacha.

KINGA Njia pekee ya kujikinga na pumu ni kuepuka mzio au vitu vinavyoweza kusababisha ugonjwa huo kwa kusafisha nyumba kila wiki kupunguza vumbi, kuwaepusha watoto na baridi au kukumbatia paka au wanyama, kuepuka kufanya mazoezi kwenye baridi, kuepuka moshi wa sigara, kudhibiti ugonjwa wa kucheua na kiungulia na kadhalika.

DALILI ZA MIMBA KUTUNGA NJE YA MJI WA UZAZI


HILI ni tatizo ambalo linawaathiri wanawake wengi. Kwa kawaida, mimba zinazotungwa nje ya mfuko wa uzazi hazina uwezo wa kukua kuwa mtoto kamili. Mimba hizi ni hatari kwa afya ya mjamzito kwa vile humfanya kupoteza damu nyingi na hatimaye kusababisha kifo asipowahi kutibiwa. Katika mfumo wa uzazi wa mwanamke, kuna sehemu nyingi ambazo kila moja ina umuhimu wake.

Ikiwa sehemu mojawapo itapata hitilafu, husababisha athari katika mfumo wa uzazi. Miongoni mwa sehemu muhimu ni ovari ambayo ndiyo sehemu mayai ya uzazi yanapotengenezwa. Mayai haya husafiri kupitia mirija ya fallopian.

Kazi za mirija ya fallopian ni kusafirisha mayai kutoka katika kiwanda chake cha uzalishaji (ovari) mpaka kwenye mfuko wa uzazi (uterus). Utungisho wa yai la kike (ovum) na mbegu ya kiume (sperm) hufanyika kwenye mirija hii.

Mara baada ya utungisho, misuli inayozunguka mirija ya fallopian ikishirikiana na vinyweleo vilivyopo ndani ya mirija hii husukuma kiinitete au yai lililorutubishwa na kulipeleka kwenye uterus. Yai lililorutubishwa au
kiinitete, lifikapo kwenye uterus hujipachika katika mojawapo ya kuta zake kwa ajili ya kuendelea kurutubishwa, kukua taratibu na hatimaye kufanya mtoto.

RIPOTI MAALUM: NI KWELI KUNA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU KIUME -3


MSOMAJI,bado naendelea kukufungua ufahamu kuhusu suala la tatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Wiki iliyopita tuliona jinsi wataalamu walivyoelezea mishipa ya damu inavyosababisha ukosefu wa nguvu za kiume kama ina hitilafu. Tuliona pia jinsi moyo ukiwa na hitilafu unavyosababisha mwanaume kukosa nguvu hizo za kufanya tendo la ndoa, endelea sehemu hii ya tatu ambayo inajikita zaidi na virutubisho katika mwili vinavyosaidia kumpa nguvu yule ambaye hana nguvu za kiume.
Endelea: Toleo lililopita tuliona kuwa upungufu wa nguvu za kiume unasababishwa na mambo mengi kama vile mishipa ya damu kuwa na kasoro lakini leo tutafafanua kuhusu ukosefu wa virutubisho muhimu mwilini na jinsi ya kuongeza nguvu za kiume bila kutumia dawa za viwandani.

Ni jambo muhimu kama mtu atazingatia kula vizuri na kufanya mazoezi ili kuthibiti nguvu za kiume. Mazoezi yapo ya aina nyingi, kwa wale wenye umri mkubwa wanaweza kufanya mazoezi ya kutembea kwa mwendo wa kasi kwa dakika 35 au saa nzima kila siku. Wakati mwingine pia wanaweza kufanya mazoezi ya kukimbia kwa zaidi ya dakika 30, kuogelea au mazoezi ya kufanyia kwenye vyumba maalum vya mazoezi(gym), kufanya jogging mkiwa katika makundi au mmoja mmoja.

Mazoezi ni tiba ya vitu vingi mwilini ikiwa ni pamoja kuondoa presha na kwa wale wenye matatizo ya nguvu za kiume. Ili kuongeza nguvu za kiume si lazima kutumia dawa kali kama viagra au vilevi vikali. Dawa na pombe hukupa nguvu zinazodumu na kuisha kwa muda mfupi, lakini hukuletea madhara makubwa yatakayoathiri mwili kwa muda mrefu zaidi.

Ili kupata suluhisho la uhakika la nguvu za kiume Mtaalamu wa Lishe, Abdallah Mandai anasema ni vizuri kuzingatia vyakula vinavyoweza kukuongezea stamina na kujenga mwili wako vizuri na kukupa uwezo wa kufanya mapenzi vizuri zaidi bila kutumia dawa; vyakula ni suluhisho maridhawa kwa kila kitu maishani mwako. Anasema mwili wako una maarifa ya kujirekebisha pasipo kuhitaji dawa au vilevi, unachotakiwa kuzingatia ni chakula bora tu.

Sehemu za viungo vya uzazi kwa mwanaume kutokuwa na kiwango cha kutosha cha homoni ya Testosterone, kupungukiwa protini na hivyo kukosa amino asidi mwilini na kusababisha ukosefu wa nguvu za kiume. Leo napenda tuangalie vyakula ambavyo vinasaidia kuongeza na kuboresha nguvu za kiume na kusaidia kwa kiasi kikubwa kudumisha mapenzi na kulinda uhusiano na ndoa, hivyo hii ni dawa nzuri ya asili ya kurejesha nguvu za kiume.

Matunda ambayo husaidia kuondoa tatizo hilo ni haya yafuatayo:
BLUEBERRY Blueberry ni matunda yanayosaidia sana kuongeza nguvu za kiume, wengi hupendelea kuyaita ‘viagra’ asilia kutokana na kazi nzuri inayoifanya mwilini ya kuongeza nguvu za kiume. Kama tulivyoona wiki iliyopita kuwa mishipa ya damu ni muhimu, Mtaalamu wa Lishe, Abdallah Mandai anasema, blueberries ina virutubishi vinavyoimarisha mishipa ya damu na kusaidia mzunguko mzuri wa damu mwilini, niwakumbushe tu kuwa damu ndiyo kila kitu katika nguvu za kiume.

Anasema blueberries zina nyuzinyuzi (fiber) ambazo husaidia kuondoa kolesteroli (Cholestrol) mwilini kabla hazijanganda kwenye mishipa ya damu. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu husaidia mwanaume kuwa na nguvu za kiume hivyo kuhimili kufanya mpenzi wa muda mrefu zaidi. “Kuna matunda yanayoitwa mtini (figs); ni matunda yenye kiwango kikubwa cha amino asidi, ambayo ni kiungo kikubwa katika kuzalisha homoni mwilini. Homoni ndiyo kishawishi cha nguvu za kiume mwilini. Kukosa amino asidi huweza kusababisha kukosa hamu ya mapenzi au kupungukiwa na nguvu za kiume,” anasema Mandai.

CHAZA/KOMBE (RAW OYSTERS)
Anaongeza kusema chaza wana kiwango kikubwa
cha madini ya zinc. Madini za zinc hutumika katika utengenezaji wa homoni ya testosterone, na mbegu za kiume. Uwingi wa uzalishwaji wa testosterone mwilini huathiri pia hamu ya mapenzi na nguvu za kiume ikiwa kidogo huondoa hamu, ikiwa nyingi humfanya mtu kuwa na hamu na nguvu zaidi. Kupungukiwa kwa madini ya zinc husababisha kupungua kwa nguvu za kiume, udhaifu na kushuka kwa kiwango cha uwezo wa kufanya ngono.
KARANGA
Mtaalamu huyo anasema, karanga ni chanzo kikubwa cha kujenga protini mwilini kwani huwa na kiwango kikubwa cha amino asidi ambayo husaidia kuweka vizuri mfumo wa damu, hivyo kusababisha kuongezeka kwa kiwango cha nguvu za kiume.

VITUNGUU SAUMU Anaongeza kuwa kitunguu saumu kina allicin, kiambato kinachosaidia mzunguko mzuri wa
damu kwenye viungo vya uzazi. Kuwa na mzunguko mzuri wa damu kwenye uume ni sababu kubwa ya kuongeza stamina ya kufanya mapenzi.

NDIZI Anasisitiza kuwa ndizi ni chanzo kikubwa cha vitamin B ambayo husaidia sana katika kuongeza stamina na nguvu mwilini hasa wakati wa kufanya kazi nzito. Ndizi ina kimeng’enyo cha Bromelain ambacho huongeza nguvu za kiume na ashki ya mapenzi (libido).
CHOCOLATE
Kuhusu chocolate mtaalamu huyo anasema inasaidia kuongeza stamina kwenye kufanya kwa sababu ina viambato vya phenylethylamine na alkaloid. Anasema Phenylethylamine ni kiambato kinachofanya mtu kujisikia vizuri, hasa wakati wa kufanya mapenzi na alkaloid huongeza stamina na nguvu za kiume.

Haishauriwi kutumia dawa kama Viagra kuongeza nguvu za kiume badala yake watu wanatakiwa kutumia njia asilia katika kutatua matatizo hayo ya kiafya. Mwili una njia zake za kurekebisha kila kitu. Ukiona kuna tatizo mwilini, inaashiria kuna upungufu ambao unatakiwa kurekebishwa.

Kutumia madawa makali hudhoofisha mwili na hivyo kuupunguzia uwezo wa kufanya kazi kama inavyotakiwa. Ni vizuri kama utamuona daktari kama ukiona hakuna kinachowezekana kabla hujaanza kutumia dawa za viwandani.

Mara nyingi njia asilia ya kutumia vyakula hutumia muda mrefu sana kuleta mabadiliko, lakini matokeo yake hudumu zaidi kuliko kutumia madawa makali ambayo hutibua mfumo wa kawaida wa ufanyaji kazi wa mwili wako.

Ni vizuri kula kwa kiasi kabla ya kufanya mapenzi, hasa wakati wa usiku kabla ya kwenda kulala. Ni vizuri ukajaribu kubadilisha chakula unachokula, fanya mazoezi mara kwa mara ili kupata mwili wenye nguvu. Itaendelea wiki ijayo.
Na Elvan Stambuli

VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUONDOA MAUMIVU WAKATI WA HEDHI


WIKI iliyopita tuliona jinsi matunda yanavyosaidia kutibu maradhi mbalimbali mwilini, leo tutaangalia aina mbalimbali za matunda yanayoweza kutibu matatizo mbalimbali yanayowahusu wanawake wakati wa siku zao (menstruation period). Miongoni mwa matunda hayo ni papai bichi lakini lililokomaa ambalo lina uwezo wa kulainisha misuli ya njia ya uzazi hivyo kufanya kipindi cha hedhi kutokuwa na maumivu.

Katika suala hili, ili wanawake kujiepusha na kupatwa na matatizo ya maumivu, kutokwa damu kwa wingi kusiko kawaida, kuchelewa kuona siku zao, wanashauriwa kuzingatia suala la lishe. Wanapaswa kujua vyakula gani wale na vipi wasile ili kujiwekea kinga ya kudumu dhidi ya tatizo hili.

LISHE YA KUDHIBITI MATATIZO YA HEDHI
Matatizo mbalimbali yanayohusiana na hedhi, yanaweza kudhibitiwa na hatimaye kutokomezwa kabisa kwa kutibu mfumo mzima wa mwili, ili kuondoa sumu iliyojilimbikiza katika mwili wa mgonjwa kwa kipindi cha muda mrefu, sumu ambayo imegeuka na kuwa chanzo cha matatizo yanayojitokeza wakati wa hedhi.

Mfumo mzima wa mwili unapokuwa umezingirwa na sumu (toxins), ndiyo huwa chanzo cha matatizo mbalimbali, yakiwemo hayo yanayojitokeza kwa wanawake wakati wa hedhi na dawa pekee katika hili ni kwanza, kuondoa sumu hizo mwilini kwa njia ya lishe.

Ili kuondoa sumu hizo mwilini, mgonjwa anatakiwa kuanza mpango maalum wa kula matunda na mbogamboga pekee, kutwa mara tatu kwa muda wa siku tano mfululizo. Katika siku hizo, anachokuwa anakula ni matunda, juisi za matunda kama machungwa, mananasi, zabibu, tufaa, papai bichi, karoti, parachichi, nyanya, mboga mbalimbali pamoja na maji, kila wakati wa kula unapowadia, maji hayo mtu anywe nusu saa baada ya mlo.

Hii ina maana kwamba mlo wa mtu huyu, katika kipindi cha siku hizo tano, utakuwa vyakula vilivyotajwa hapo juu, kuanzia asubuhi, mchana na jioni, katika kipindi hicho, matunda, juisi na mbogamboga atakazokuwa anakula zitakuwa zinafanya kitu kinachoitwa kitaalamu ‘detoxification’, yaani uondoshaji wa sumu mwilini kwa njia ya asili
aliyotuumba nayo Mungu. Hata hivyo, kwa wale wanawake ambao ni wembamba sana, ambao pengine katika kipindi cha funga hiyo ya matunda wanaweza kupoteza uzito sana, wanaweza kunywa glasi ya maziwa freshi sambamba na mlo wao wa matunda. Hii ni kwa sababu ya kuepuka kupoteza uzito kuliko kawaida.

UFUATE MLO KAMILI Baada ya kumaliza siku tano za kula na kunywa juisi na matunda, mtu mwenye kufanya zoezi hili atatakiwa kuzingatia ulaji wa mlo kamili utakaotilia maanani matunda, mboga za majani, vyakula vya nafaka kama ugali wa mahindi, mtama, ulezi n.k. Nafaka zinazoshauriwa ni zile ambazo hazijakobolewa na kuondolewa viini lishe (wholegrain).

Waepuke kula vyakula vitokanavyo na unga mweupe, ikiwemo mikate myeupe, sukari, vitu vitamu (confectioneries), vyakula vya kwenye makopo. Aidha, mtu huyu anashauriwa kuepuka kunywa chai iliyowekwa majani mengi au kahawa iliyowekwa kahawa nyingi

. UVUTAJI SIGARA UKOME Kwa wale akina mama wenye matatizo wakati wa siku zao na ambao wameamua kuingia katika mpango huu wa kusafisha mwili, hawana budi kuachana kabisa na uvutaji sigara kama ni wavutaji ili kufanikisha zoezi hilo. Kwa ujumla uvutaji sigara ni mbaya kwa afya ya binadamu.

Makala hii imeandaliwa na Mtaalamu wa Lishe, Abdallah Mandai, kwa ushauri wasiliana naye kwa namba 0754391743 au 0717 961 795. Usikose pia kusoma makala zangu za Afya Yako kwenye Gazeti la Ijumaa Wikienda kila Jumatatu uelimike.

VYAKULA HATARI KWA AFYA YAKO


CHAKULA bora ni muhimu kwa afya na furaha yako, bila chakula bora, hakuna raha katika maisha yako hapa duniani. Katika mada yetu ya leo tunaangalia vitu ambavyo kwa namna moja au nyingine hupunguza uhai kwa binadamu, hivi ni vyakula ambavyo vinaweza kukufanya ukapata magonjwa usiyotarajia, mfano saratani (cancer), kisukari na magonjwa ya shinikizo la damu au moyo.

Upo usemi unasema ‘tunakula ili tuishi, si tunaishi ili tule’. Hapa maana yake ni kwamba wale wanaopenda kuishi ili kula hufakamia chochote ili mradi kiwe chakula, tofauti na wale wanaoishi ili kula maana hujali zaidi afya zao kwanza kuliko njaa, utamu au mvuto wa chakula. Kuwa na uwezo wa kupata vyakula mbalimbali vitamu huwa haiwezi kumfanya mtu makini asahau vitu muhimu kwa afya yake.

VYAKULA VYA KUSINDIKA
Vyakula vingi vya kusindika ambavyo hutumiwa na watu wenye uwezo kifedha huweza kukaa muda mrefu kwa kutumia dawa, sukari, mafuta na chumvi kwa kiwango kikubwa sana, hivyo kuwa hatari kwa mtumiaji.
Vyakula vilivyohifadhiwa kwenye makopo au chupa hakuna hata kimoja kinachokusaidia mwilini bali hukuletea madhara zaidi. Hivyo, ili kuwa na afya bora, unashauriwa kupunguza kula vyakula vya kusindika na pendelea kula vyakula asilia, hasa mboga za majani na matunda.

SODA
Mara nyingi vinywaji visivyo na vilevi vimekuwa havimo kwenye orodha ya vitu visivyo vya afya. Lakini ukweli ni kwamba, vinywaji vingi sana vinavyouzwa viwandani si vizuri kwa afya yako. Mfano mzuri ni soda. Soda ina kiwango kikubwa sana cha sukari. Madaktari wengi wameonyesha kuwa madhara ya soda hayatofautiani na madhara ya
kuvuta sigara. Kiwango cha sukari na dawa zilizomo kwenye soda humfanya mtu kuzeeka na kumletea madhara ya magonjwa kama kisukari kwa muda mfupi.

NYAMA NYEKUNDU

Kwa muda mrefu sana nyama nyekundu imegundulika kuwa chanzo cha magonjwa sugu kama magonjwa ya moyo kutokana na mafuta yake kuganda na kuziba mishipa ya damu na husababisha saratani. Nyama siyo nzuri kwa afya sababu husababisha kuongezeka kwa uzito kupita kiasi kama ikiliwa kwa kiwango kikubwa sana.

POMBE
Pombe haihitaji maelezo mengi. Kila mtu anafahamu madhara yake ya muda mfupi, ambayo huleta matokeo mabaya zaidi kwa wale watumiaji wa muda mrefu. Pombe, inayonywewa kwa kiwango kikubwa kila mara,

CHAKULA
hupunguza sana urefu wa maisha sababu huharibu chembechembe muhimu mwilini hivyo kuufanya mwili kukosa kinga, na kudhoofika. Ikifikia kiwango hiki inakuwa rahisi kupata magonjwa, na kutoweza kuwa na kinga ya kutosha mwilini.
ZINGATIA HAYA
Ni vizuri kujali afya, hivyo basi, ni vizuri ukizingatia haya machache: Pendelea vyakula asilia hasa mboga za majani na nafaka bora, tumia matunda zaidi, ni bora kuliko juisi inayoongezwa sukari au soda za kununua, pendelea kula chakula nyumbani kilichoandaliwa vizuri kwa afya.

Usitumie kilevi, kama huwezi, basi kunywa kiasi, ili usiharibu afya yako. Pendelea kuangalia kiwango cha virutubisho kwenye kila chakula unachokula na hakikisha unakunywa maji kwa kiwango kinachotakiwa, acha kula vyakula vyenye mafuta mengi, hasa ya wanyama, kwani husababisha matatizo ya kuziba mirija ya damu..

TWITTER @Winokemedia

INSTAGRAM @Winokemedia

FAHAMU MAKUNDI YA VYAKULA MUHIMU MWILINI



CHAKULA ni muhimu kwa maisha ya binadamu kwani humwezesha kupata nguvu na virutubisho ambavyo husaidia kuujenga mwili na kuupa kinga dhidi ya maradhi mbalimbali.

Kuna aina za vyakula ambavyo pia vina kazi tofauti mwilini na vina virutubisho tofautitofauti, hivyo mtu anatakiwa kula vyakula vya aina mbalimbali kwani aina moja haiwezi kuwa na virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini.
Virutubisho vina kazi maalumu mwilini na hii huwezesha mfumo wa mwili kufanya kazi vizuri. Vyakula vimegawanyika katika makundi mbalimbali kulingana na kazi za vyakula hivyo mwilini.

Hata hivyo, vyakula vilivyo katika kundi moja huweza kuwa na aina ya viwango tofauti vya virutubisho na wakati mwingine hata aina ya virutubisho vilivyomo.
Kwa hali hiyo basi, mtu anatakiwa kula mchanganyiko wa vyakula mbalimbali ili kupata virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini.
Mlo wenye mchanganyiko wa vyakula vyenye virutubishi vya aina zote, huitwa mlo kamili ambao ni muhimu sana hasa kwa watoto, ambao huwasaidia kukua vizuri na kuwa na afya njema.

Mlo kamili humwezesha mtu kujikinga na maradhi mbalimbali kama vile malaria, surua, kuharisha, shinikizo la damu, kisukari, magonjwa ya moyo na hata ukimwi.
Mlo kamili na wa kutosha hutoa virutubishi kama vile protini, vitamini, madini na nishati. Vile vile mlo kamili ni muhimu kwa wazee na wagonjwa katika kujenga mwili na kusaidia uponaji wa majeraha, na kupata nguvu baada ya kukabiliana na maradhi.
VYAKULA VYENYE WANGA
Vyakula vya wanga ni muhimu katika kuupa nguvu mwili za kufanya kazi mbali mbali.
Vyakula vyenye wanga ni nafaka, kama mahindi, mchele, ngano, mtama, ulezi, uwele na kadhalika.
Wanga pia hupatikana katika mihogo, viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, magimbi, ndizi, miwa na asali.
 
VYAKULA VYENYE PROTINI
Protini ni muhimu sana katika kujenga mwili na kuwezesha ukuaji wa mwili hasa kwa watoto na pia husaidia kutengeneza kinga ya mwili.
Vyakula vyenye protini ni pamoja na nyama ya ng’ombe, mbuzi, kondoo, nguruwe, kuku, bata, samaki nk.
Protini pia hupatikana kwa kula mayai, maziwa na kunde, maharage, soya, dengu, choroko, njegere, mbaazi, na njugu mawe.
 
VYAKULA VYENYE MAFUTA
Vyakula vyenye mafuta huleta joto mwilini, na vile vile huleta nguvu mwilini na kulinda. Hulainisha ngozi na pia utando (membrane).
Mafuta hutokana na mimea na huwa yanauzwa madukani kama vile, mafuta ya karanga, alizeti, nazi, ufuta, korosho, mawese, mbegu za maboga, mbegu za pamba.
 
MATUNDA NA MBOGA
Matunda na mboga ni muhimu sana katika mwili, kwa vile vyakula hivi vina vitamini na madini mbalimbali ambayo ni muhimu mwilini.
 
Vitamini na madini huhitajika kwa kiwango kidogo sana, lakini ni muhimu kwa mwili kuweza kufanya kazi zake vizuri.
Upungufu wa vitamini na madini mwilini unaweza kusababisha hitilafu mbalimbali katika mwili na hata kusababisha kasoro zinazoambatana na maradhi mwilini.
 
VITAMINI
Kuna vitamini mbalimbali ambazo ni Vitamini A, Vitamini B, Vitamini C, Vitamini, D na nyinginezo.
Vitamini A ni muhimu katika ukuaji hasa kwa watoto na utengenezaji wa chembechembe za mwili.
 
Husaidia kuongeza kinga mwilini na kuwezesha macho kufanya kazi vizuri. Vitamini A ni muhimu katika kutunza ngozi.
Vitamini A, hupatikana katika matunda na mboga zenye rangi ya machungwa na manjano, kama vile karoti, viazi vitamu vya manjano, maembe, na nyanya. Pia hupatikana katika mboga za majani, maini na maziwa.
 
Vitamini A husaidia kuzuia magonjwa mbalimbali hasa yanayosababisha ngozi kubabuka hasa katika zile sehemu zinazopigwa na jua au kama chakula kinashindwa kusagika vizuri na kusababisha kuharisha.
Ukosefu wa vitamin B unasababisha beriberi, ugonjwa unaofanya mtu kupungua uzito, moyo unaweza kuwa mkubwa, miguu kuvimba na kujaa maji.
 
Ukosefu wa vitamini B pia unaweza kusababisha midomo kupasuka, na dalili nyinginezo. Hupatikana katika mboga za majani kama vile spinachi, mchicha, matembele na kadhalika.
Vitamini C ni muhimu mwilini, husaidia ukuaji, kuongeza kinga mwilini na kusaidia mwili kutumia madini ya chuma.
 
Hupatikana katika machungwa, limao, machenza, mananasi na mboga za majani ambazo hazikupikwa mpaka kuiva sana.

TU FOLLOW KWENYE MITANDAO YA KIJAMII 



MATATIZO YA MOYO YANAVYOSABABISHA VIFO-5


MAKALA haya maalumu lengo lake ni kujadili masuala mbalimbali yanayohusu afya na tiba ili kupata ufahamu zaidi kuhusu kuimarisha afya zetu na jamii nzima kwa ujumla. Leo tunaendelea kujadili magonjwa ya moyo na tutaelezea tatizo la tundu katika kuta za chini za moyo.
Endelea: Tundu katika kuta za chini za moyo Katika muendelezo wa magonjwa ya moyo, leo tutazungumzia ugonjwa unaojulikana kama tundu katika kuta za ventrikali za moyo au kwa kitaalamu Ventricular Septal Defect (VSD), tatizo ambalo hutokea mara nyingi ambapo watoto wawili hadi sita kati ya 1,000 huzaliwa na tatizo hilo.

Dk. Marise Richard anasema tundu katika kuta za chini za moyo au VSD ni pale panapokuwepo na uwazi katika sehemu ya kuta ya septum inayotenganisha chemba za ventrikali ambazo ni chemba za chini za moyo.

“Pale moyo unapoanza kuumbika huanza kama bomba lililo wazi na kuendelea kujigawa katika sehemu
mbalimbali na kuunda kuta. “Iwapo kitendo hicho hakitatekelezeka ipasavyo, hutokea uwazi katika kuta ya septum kwenye chemba za chini,” anasema Dk. Richard.

Kuwepo tundu hilo huruhusu damu yenye oksijeni kupita
kutoka chemba ya kushoto ya chini ya moyo na kuingia katika chemba ya kulia ya chini ya moyo, badala ya kuingia kwenye mshipa wa aorta na kuelekea nje ya moyo kama inavyotakiwa.

Tundu la VSD linaweza kuwa dogo, la kati au kubwa. Tundu dogo katika kuta za chini za moyo huruhusu damu ndogo kutoka upande mmoja wa moyo kwenda wa pili, hivyo haliathiri utendaji wa kawaida wa moyo na kwa kawaida huwa halihitaji matibabu maalumu.

Anasema matundu ya aina hiyo huziba yenyewe wakati moyo unapoendelea kukua kipindi cha utotoni. Matundu yenye ukubwa wa kati na kubwa katika kuta za chini za moyo huruhusu kiwango kikubwa zaidi cha damu kupenya kutoka upande mmoja wa moyo kwenda mwingine, na mara nyingi huhitajia matibabu maalumu.

Dk Richard anafafanua kuwa watoto wenye tundu dogo katika moyo, huweza kukua bila matatizo yoyote, wakati wale wenye tundu kubwa huanza kuonesha dalili mapema. Vifuatavyo ni vihatarishi ambavyo vinaweza kusababisha mtoto kuzaliwa na tundu katika kuta za chini za moyo.

1) Maambukizi ya rubella katika kipindi cha ujauzito.

2) Ugonjwa wa kisukari cha wakati wa ujauzito ambao haujadhibitiwa

3) Matumizi ya pombe, dawa za kulevya na baadhi ya dawa za hospitali katika kipindi cha ujauzito pia huweza kusababisha mtoto azaliwe na tundu katika kuta za chini za moyo.

Mpenzi msomaji, ninajua unajiuliza je, mtoto anayezaliwa na tundu katika kuta za chini za moyo huwa na dalili gani? Kama nilivyosema iwapo tundu ni dogo huwa halina dalili yoyote na pale mtoto anapoendelea kukua tundu hilo hujifunga lenyewe. Lakini tundu likiwa kubwa, ijapokuwa mtoto anayezaliwa huwa haonyeshi dalili yoyote katika kipindi hicho, lakini baadaye huwa na dalili zifuatazo.

1) Rangi ya ngozi, midomo na kucha hubadilika na kuwa ya bluu.

2) Kunyonya au kula kwa shida sana, na pia ukuaji wa shida.

3) Kupumua kwa shida.

4) Kuchoka haraka.

5) Kujaa miguu na kuvimba tumbo.

6) Kuwa na mapigo ya moyo ya haraka

7) Anapopimwa mtaalamu huweza kusikia ishara ya ongezeko la sauti ya ziada ya mapigo ya moyo wa mtoto hali ambayo wataalamu huiita holosystolic murmur kwa kutumia kifaa cha hupima mapigo ya moyo. Dk Richard anasema madhara ambayo yanaweza kusababishwa na tundu katika kuta za chini za moyo ni Eisenmenger syndrome.

Hali ambayo hutokea pia pale mtu anapokuwa na tundu katika kuta za juu za moyo. Tatizo hili hutokea wakati mtiririko wa damu unapoongezeka kutoka kushoto kwenda kulia kupitia tundu katika kuta za moyo, suala ambalo huongeza mtiririko wa damu katika mishipa ya mapafu na kusababisha shinikizo la damu katika mapafu. Itaendelea wiki ijayo.

MATATIZO YA MOYO YANAVYOSABABISHA VIFO-6



TUNAENDELEA kuchambua matatizo ya moyo na namna yanavyoweza kusababisha vifo.
Wiki iliyopita tulizungumzia ugonjwa wa mshtuko wa moyo, na tulieleza dalili za ugonjwa huo na makundi ya watu yaliyo kwenye hatari ya kupatwa na mshtuko wa moyo au heart attack.
Leo tutaendelea kuzungumzia ugonjwa huo na tutaelezea namna ya kutibu mshtuko wa moyo na namna ya kujikinga na ugonjwa huo; endelea.

FAHAMU NAMNA YA KUTIBU MSHTUKO WA MOYO
Mshtuko wa moyo unahitaji kushughulikiwa haraka. Kama unamshuhudia mtu akipatwa na mshtuko wa moyo unapaswa kuomba msaada haraka au kumfikisha kituo cha afya haraka iwezekanavyo.
Kama mtu aliyepatwa na mshtuko wa moyo amepoteza fahamu, baada ya kuomba msaada kituo cha afya cha karibu, unapaswa kumfanyia CPR mara moja kama unajua kufanya hivyo.

CPR ni kitendo ambacho husaidia kufikisha hewa ya oksijeni katika ubongo.
Kwanza hakikisha njia za hewa za mgonjwa ziko wazi, yaani hakikisha mdomoni na puani kwake hakuna kitu kinachozuia hewa kupita na msaidie kwa hewa kila baada ya kumkandamiza kifuani au (chest compress) mara 30.

Kama hujuia CPR pia unapaswa kuanza kumkandamiza kifuani mgonjwa aliyepoteza fahamu kutokana na mshtuko wa moyo, kwani kufanya hivyo huenda kukaokoa maisha yake.
Tutaelekeza hapa namna ya kumkandamiza kifuani mgonjwa aliyepatwa na mshtuko wa moyo na aliyepoteza fahamu.

Weka kiganya cha mkono wako mmoja katika mfupa wa kifua (chestbone) katikati ya matiti na kiganya cha pili juu ya cha kwanza, na kandamiza kwa kiasi cha inchi mbili au sentimeta 5 kuelekea chini. Eendelea kukandamiza na kuachia mara 30.

Kama unajua namna ya kufanya CPR mfanyie mgonjwa na kama hujui endele kumkandamiza sehemu hiyo ya kifua hadi msaada utakapowasili au hadi mgonjwa atakapopata fahamu au kuonyesha dalili za kupumua.
Matibabu ya ugonjwa wa mshituko wa moyo hufanyika hospitali kwa njia tofauti kulingana na hali ya mgonjwa.
Kila dakika inavyopita baada ya kutokea mshituko wa moyo, ndivyo tishu ya moyo inavyopoteza oksijeni na kuharibika au kufa.

Njia kuu ya kuzuia moyo usiharibike ni kurejesha tena haraka mzunguko wa damu.
Mgonjwa wa mshtuko wa moyo huweza kutibiwa kwa dawa au njia nyinginezo za tiba kwa kutegemea namna gani tishu ya moyo ilivyoharibika.

Dawa tofauti zinazotumika kutibu mshituko wa moyo ni kama aspirin, dawa zinazoyeyusha damu ili kuondoa damu iliyoganda ambazo huitwa kitaalamu kama clot buster, dawa aina ya heparin na nyinginezo ambazo hutofautiana kutokana na utendaji wake mwilini.

Baadhi ya wakati athari za mshituko wa moyo huwa kubwa ambapo mgonjwa hutibiwa kwa njia inayoitwa Angioplasty.
Hiyo siyo operesheni bali ni matibabu ya kufungua mishipa ya damu iliyoziba au kudhoofika na kusabisha mshituko wa moyo. Mara nyingine wagonjwa wa heart attack hutibiwa kwa upasuaji unaoitwa bypass surgery.
Baada ya kujua namna ya kutibu mshituko wa moyo, sasa tuangalie ni jinsi gani tunaweza kujiepusha na ugonjwa huo wenye madhara makubwa kwa miili yetu.

Kwa wale ambao tayari wameshapatwa na ugonjwa huu pia wanashauriwa kuendelea kutumia dawa walizopewa hospitalini lakini pia kubadilisha mienendo ya maisha yao ili kuzuia kupatwa tena na mshituko wa moyo katika siku zijazo.
Itaendelea wiki ijayo.

MAPISHI YA MAKANGE YA KUKU


LEO tutaona jinsi ya kupika makange ya nyama ya kuku ikiwa ni kutokana na mfululizo wa kujifunza kupika vyakula vya aina mbalimbali.

MATAYARISHO NA KUPIKA
Kuku 1
Mafuta ya kupikia lita 1
Tangawizi iliyotwangwa (kusagwa) vijiko vikubwa 3
Kitunguu saumu kilichotwangwa- kijiko kikubwa 1
Kitunguu maji kikubwa 1
Karoti kubwa 1
Pilipili Hoho kubwa 1
Ndimu 2
Chumvi vijiko vikubwa 3
Masala ya kuku (chicken masala) vijiko vikubwa 3
Nyanya ya pakti kijiko kikubwa 1
Nyanya kubwa 1
Pilipili 1

MATAYARISHO
Osha kuku wako vizuri kisha mkate vipande upendavyo.
Muwekee viungo vyako kama tangawizi, vitunguu saumu, ndimu 1 na kipande (kipande kimoja weka pembeni), chumvi vijiko 2, masala ya kuku vijiko 2 kisha mchanganye vizuri na muweke kwenye friji kwa saa mbili.
Kata karoti, pilipili hoho na kitunguu maji kwa urefu au umbo upendalo, ila viwe vipande vikubwa vinavyoonekana baada ya kuiva.
Saga nyanya iweke kwenye kibakuli.

JINSI YA KUPIKA
Chukua kikaango, mimina mafuta na yaache yapate moto wa wastani. Anza kumkaanga kuku taratibu mpaka aive. Tumia kikaango hichohicho, punguza mafuta yabakize kidogo kwa ajili ya kukaanga viungo vilivyobakia. Anza kukaanga kitunguu kisha weka pilipili hoho halafu malizia na karoti. Usikaange kwa muda mrefu kwani havitakiwi kuiva sana.
Weka nyanya ulizosaga, koroga na malizia kwa kuweka chumvi, masala, nyanya ya paketi, pilipili na ile ndimu kipande kilichobakia. Mimina kuku wako na mkoroge kidogo ili aenee vile viungo, kisha mtoe weka kwenye sahani. Hapo makange yako yatakuwa tayari kwa kula, unaweza kula kwa wali au ugali.



JINSI MWANAMKE ANAVYOWEZA KUPATA SARATANI YA MATITI-2


WIKI iliyopita nilianza kuzungumzia namna mwanamke anavyoweza kupata saratani ya matiti. Wiki hii nitaimalizia mada hii ili nianze mada nyingine. Iko hivi, saratani ya matiti pia inarithiwa. Endapo katika familia yenu au ndugu mwingine wa karibu sana alipatwa na saratani ya matiti, basi upo uwezekano wa wewe kupata saratani hii. Vinasaba vya saratani vinavyozunguka katika ukoo wenu ambavyo husababisha watu wa kwenu wapate saratani ya matiti, vinasaba vya saratani ya matiti vinaitwa BRCA 1 na BRCA 2.

Hali ya maisha pia huchangia mwanamke kupata saratani ya matiti. Wanawake walio katika hali bora ya maisha mfano wale wasomi wenye kipato kizuri au wafanyabiashara na wengine ambao wapo vizuri kiuchumi wapo hatarini kupatwa na tatizo hili. Wengine ni wanawake ambao wanazaa halafu hawanyonyeshi watoto au wanawanyonyesha kwa kipindi kifupi kutokana na sababu Jinsi

mbalimbali pia wapo hatarini kupata saratani hii. Mionzi iwe ya Xray au ya viwandani ikielekezwa mara kwa mara kwenye kifua cha mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka thelathini basi anaweza kuja kupata saratani ya matiti miaka ijayo. Ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi mfano nyama choma, kitimoto, unywaji wa pombe na hata uvutaji wa sigara kwa mwanamke vinaweza kuleta madhara baadaye na kujikuta unapata tatizo hili.

Wengine wanaoathirika na tatizo hili ni wanawake wanene sana. Unene uliopitiliza utaujua kwa kupima uzito kwa kiwango cha BMI au Body Mass Index. Mwanamke mnene ana kiwango kikubwa cha homoni ya Estrojen inayoweza kumletea saratani ya matiti. Mwanamke ambaye tayari alishawahi kutibiwa saratani ya titi moja naye yupo hatarini kuathirika titi la pili. Matumizi holela ya vidonge vya uzazi wa mpango bila ya ushauri wa kitaalamu unaweza kuchochea kutokea kwa tatizo hili la saratani ya matiti.

Tatizo hili huanza kuwatokea wanawake kuanzia umri wa miaka ishirini hadi arobaini, hawa ndiyo kundi kubwa na likitokea katika umri wa zaidi ya miaka arobaini hali huwa mbaya zaidi. Kuna baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba, makundi mengine ya wanawake walio hatarini kupatwa na saratani ya matiti ni wale wanaofanya kazi za usiku, endapo watakaa karibu na taa za umeme zenye mwanga mkali kwa kipimo cha 50-60Hz, kutokana na miale yake ya magnetic kuzuia hali ya kawaida ya utoaji wa vichocheo vya melatonin ambavyo hasa hutoka wakati wa usiku mwilini mwa kila mwanamke, vikiwa na kazi maalumu ya kudhibiti utolewaji holela wa vichocheo vya Estrojeni ambavyo vikizidi ndipo saratani hii inatokea.

Makundi mengine ni wanawake wasagaji kutokana na tabia yao ya kutozaa au kuja kuzaa katika umri mkubwa wapo hatarini kupatwa na tatizo hili la saratani ya matiti, wafanyakazi wa kwenye ndege, hawa hupata saratani ya matiti.

NINI CHA KUFANYA? Saratani ya matiti ni rahisi kuidhibiti. Kuwepo na utaratibu wa mwanamke mmoja mmoja au kwa vikundi kumwona daktari au wataalamu wa afya kwa uchunguzi. Uwepo utaratibu wa maeneo ya kazi kuwafanyia upimaji wakinamama. Saratani ya matiti ikichelewa unaweza kupoteza uhai.

Ni vema uwahi hospitali kwa uchunguzi wa kina na tiba. Endapo itathibitika kuna tatizo kwenye titi lako, basi vipimo vya awali ni ultrasound, mamography, X-ray ya kifua na majimaji au kinyama kwenye titi ni muhimu. Endapo utahisi titi linauma, linatoa majimaji wakati hunyonyeshi au ukikamua linatoa damu, basi muone haraka daktari wako. Dalili nyingine ni kuhisi titi gumu au kuna uvimbe kwapani au ndani ya titi, chuchu zimezama ndani au ngozi ya titi inakuwa na makunyanzi kama ganda la chungwa.
DK. CHALE SIMU: +255713350084

TAHADHARI KUHUSU HOMA YA CHIKUNGUNYA, HAKUNA TIBA MAHUSI WALA KINGA

Serikali kupitia Wizara ya Afya imeutahadharisha umma kuhusu ugonjwa wa Homa ya Chikungunya ambao huambukizwa na mbu aina ya aedes na hauna tiba mahsusi wala kinga. Isome taarifa hii kuelewa zaidi kuhusu ugonjwa huo.








MAJALIWA ‘AMTUPA’ KIGOGO MIKONONI MWA TAKUKURU


BREAKING NEWS: WAZIRI AMTUMBUA MKURUGENZI WA MAJI MUSOMA



Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Isaack Kamwelwe , ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said (pichani kushoto) ambaye anachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha kwenye Mradi wa Maji Bunda na akizivunja Bodi za Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira za Mikoa ya Arusha na Mara (Musoma) baada ya kujiridhisha kuwa utendaji wao siyo mzuri.

Kamwele amefikia uamuzi huo leo baada kubaini kuwa kumekuwepo na uzembe wa utekelezaji wa miradi ya serikali ya maji kwa baadhi ya watendaji katika idara hizo.

“Kufuatia ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majliwa mkoani Mara, imebainika kuwa kumekuwepo na matatizo ya huyo Mkurugenzi Gantala ambaye Waziri Mkuu ameagiza Mkurugenzi huyu watendaji wengine wachunguzwe na TAKUKURU.

“Hivyo kuanzia leo Januari 20, 2017 ninatengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Mji wa Musoma, Gantala Said na nafasi yake itakaimiwa na Eng. Robert Petro Mponya wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUASA), ninamuagiza aisaidie Musoma ili waweze kufanya kazi inayotakiwa,” alisema Kamwele.
VIDEO: FUATILIA TUKIO HILO HAPA

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

Audio | Isha Mashauzi – Nibembeleze | Mp3 Download

DOWNLOAD MP3

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya

New AUDIO & VIDEO: Chombaa – Baby Sumaya
DOWNLOAD VIDEO

DOWNLOAD MP3

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download
 
Audio | Mr Blue – Mbwa Koko | Mp3 Download

DOWNLOAD Mp3

Wadaiwa kubakwa baada ya kujifungua hospitalini Kenya



Waziri wa afya nchini Kenya Dkt Cleopha Mailu ameamrisha uchunguzi kufanywa katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta baada ya wanawake waliojifungua kudai kwamba wanadhalilishwa kingono.

Taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao zinadai kina mama waliojifungua wamekuwa wanashambuliwa na baadhi ya wafanyikazi wakati wakienda kwenye chumba cha watoto wachanga kuwanyonyesha watoto wao.

Chumba hicho cha watoto huwa ghorofa tofauti na wadi za wanawake waliojifungua.

Wasimamizi wa hospitali hiyo wamesema hawajapokea malalamiko yoyote.

Yote yalianza baada ya ujumbe kuandikwa aktika ukurasa wa Facebook kwa jina Buyer Beware ambao mara nyingi hutumiwa kuwatahadharisha wateja na wanunuzi wa bidhaa na huduma.

Ujumbe uliwatahadharisha kina mama wanaojifungulia katika hospitali hiyo kwamba wamo hatarini ya kudhalilishwa kingono na baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo.

Wanawake wengine walichangia na kudai wamewahi kudhalilishwa au jaribio kufanywa, au jamaa na marafiki zao wakadhalilishwa.

Wengi wanadai kina mama waliojifungua waliviziwa wakiwa njiani kuelekea chumba hicho cha kunyonyeshea watoto au wakirudi chumba chao baada ya kunyonyesha.

Baadhi ya wanaodaiwa kunyanyaswa kingono, ujumbe unasema, walitendewa kitendo hicho siku chache baada yao kujifungua kupitia upasuaji.

Waziri Mailu ameagiza uchunguzi wa dharura kufanyika na ripoti kamili kuwasilishwa kwake kufikia Jumatatu.

Afisa mkuu mtendaji wa hospitali hiyo Lily Koros amesema hakuna mwanamke hata mmoja aliyewahi kulalamika kwamba alidhalilishwa kingono hospitalini humo.

Amesema hospitali hiyo huwa chini ya uangalizi wa kamera za usalama (CCTV) wakati wowote na hakuna kisa hata kimoja kilichogunduliwa.

Amewataka walio na habari kupiga ripoti kwa maafisa wa hospitali au polisi.

Hospitali ya taifa ya Kenyatta, Nairobi huwahudumia kina mama takriban 100 wanaojifungua kila siku.

Watoto waliozaliwa huwekwa chumbani ghorofa ya kwanza nao wanawake kwenye wodi za kujifungulia kwenye ghorofa ya chini.

Maswali sasa yameanza kuulizwa kuhusu muundo na mpangilio wa vyumba katika hospitali hiyo ambao huwalazimu kina mama waliojifungua kupanda ngazi au lifti kwenda kuwanyonyesha watoto wao, ikizingatiwa kwamba baadhi hujifungua kupitia upasuaji.