Saturday 25 November 2017

Waziri wa zamani wa fedha Zimbabwe afikishwa mahakamani




Aliyekuwa waziri wa fedha wa Zimbabwe,Ignatius Chombo amefika mahakamani kujibu mashtaka ya  ulaji rushwa dhidi yake.

Kwa mujibu wa habari,Chombo huyo alikamatwa wiki mbili zilizopita wakati jeshi lilipochukua utawala nchini humo.

Bwana Chombo alifukuzwa katika chama cha ZANU-PF Jumapili iliyopita.

Hata hivyo Chombo ameonekana akiingia mahakamani akiwa hana wasiwasi.

Emmerosn Mnangagwa ameapishwa kuwa rais mpya wa Zimbabwe.Baada ya kuapishwa kwake rais huyo mpya ametakwa na baadhi ya wafuasi wake kulishughulikia kundi la G-40 linalosemekana kuwa lilikuwa likimuunga mkono Mugabe na mkewe.

Chombo alikuwa kati ya wanachama wa G40

No comments:

Post a Comment