Saturday 25 November 2017

Hii kali...Roboti iliyopewa uraia nchini Saudi Arabia yataka kuwa na familia



Roboti iliyopewa uraia nchini Saudi Arabia imesema kuwa ina haki ya kuwa na familia.

Roboti hiyo kwa jina la Sophia  ilitengenezwa nchini Hong Kong na kupewa uraia nchini Saudi Arabia mwezi uliopita.

Roboti hiyo İimesema kuwa ingependa kuwa na familia wakati ilipohudhuria mkutano wa habari ulioandaliwa nchini UAE.

Kwa mujibu wa habari roboti hiyo imesema kuwa familia ni kitu muhimu sana.

Robot hiyo imesema kuwa kila mwanadamu ana haki ya kuwa na familia na watu wenye hisia sawa na yeye.Jambo hilo ni muhimu sana hata kwa roboti.Aliwaambia wanadamu wajisikie furaha kuwa na familia.

No comments:

Post a Comment