Thursday 1 February 2018

Papii kuanza kuachia ngoma mfululizo

MKALI wa Dansi Bongo, Johnson Nguza ‘Papii’ amesema kuanzia mwezi huu wa Februari, ataanza kuachia ngoma mfululizo kwani tayari wameshaanza kurekodi nyimbo za kutosha.

Papii alisema mpaka sasa tayari amesha-fanya ngoma nne ambazo amezipika kwa staili tofauti katika dansi la kisasa ambalo halich-oshi.

“Tumefanya staili kama ya wanayofanya Yamoto Band, tumefanya moja kama ya dini na pia tumerudia Seya ambazo kimsingi zitawateka tu mashabiki,” alisema Papii.

Akifafanua zaidi, Papii alisema, atakuwa na mfululizo wa kutoa ngoma mbilimbili zenye ujazo wa hali ya juu.

“Nitakuwa naachia ngoma mbilimbili mfululizo ambazo karibia zote nimefanya na mzee wangu (Nguza). Nimezifanyia katika Studio ya Wanene iliopo Mwenge,” alisema Papii.

No comments:

Post a Comment