Friday 2 February 2018

Helikopta mbili zagongana nchini Ufaransa


Ndege mbili za jeshi la Ufaransa zimegongana na kusababisha vifo vya watu watano,katika mji wa Marseille kusini mwa Ufaransa.

Gazeti la Var Metin limeripoti kuwa ajali hiyo imetokea majira ya asubuhi karibu na ziwa la Carces.

Ripoti zinaonyesha kuwa helikopta zilikuwa na jumla ya abiria sita na hivyo mmoja bado hajulikani alipo.

Timu za uokoaji zinaendelea kumtafuta abiria wa sita.

Gavana wa mkoa huo amesema kuwa helikopta hizo zilikuwa za shule ya kujifunza Urubani ya jeshi la Ufaransa na ajali hiyo imetokea mile 50 kutokea mji wa kitalii wa Saint Tropez.

No comments:

Post a Comment