Wednesday 31 January 2018

Kagame aanza kibarua chake cha AU kwa kasi


Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Paul Kagame ameanza kazi yake hiyo haraka baada ya kukutana na viongozi wa jukwaa la Biashara na Uwekezaji ambapo alisisitiza umuhimu wa sekta binafsi kushikishwa kikamilifu kwenye masuala ya utawala.

Kagame ambaye pia ni Rais wa Rwanda alisema Serikali nyingi za Kiafrika awali ziligundua kuwa ni ngumu kuwatumikia wananchi kwa haraka na ubora bila sekta binafsi hivyo akaomba ziungwe mkono ili ziweze kurahisisha maendeleo.

Alisema anaamini mazungumzo yake hayo na wataalamu hao yataenda sawa na vitendo hivyo kutaka sekta binafsi ziungwe mkono ambapo anaamini sasa ushirikiano mkubwa baina ya watawala na sekta binafsi utaendelezwa ili kuongeza chachu ya mafanikio.

" Mfano sisi Rwanda tumeongeza ushirikiano na makampuni ya nje katika kusaidia sekta ya afya hii haina maana kuwa tunabinafsisha hapana bali tunaongeza ubora wa huduma ili kuweza kuwasaidia wananchi wetu kwa haraka zaidi," Alisema Rais Kagame

No comments:

Post a Comment