Monday 29 January 2018

Pep Guardiola azidisha sifa EPL, sasa kumnasa Laporte


Mlinzi wa Athletico Bilbao, Aymeric Laporte akikabiliana ba Staa wa Barcelona Lionel Messi

Hizi sasa sifa! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya klabu ya Manchester City kufikia makubaliano na klabu ya Athletic Bilbao kulipa kiasi cha £57m  takribani shilingi bilioni 158 kwaajili ya kukamilisha usajili wa mlinzi wa kati wa klabu hiyo Aymeric Laporte.

Kiasi hicho ambacho Man City inakilipa kwa Bilbao ni kwa ajili ya kuvunja mkataba wa mchezaji huyo (Buy Out Clause) na Pep Guardiola ameonekana kuhitaji huduma ya beki huyo ili kuimarisha safu yake ya ulinzi.

Ripoti nchini England zinasema kuwa Laporte raia wa Ufaransa mwenye miaka 23 huenda kesho akakamilisha vipimo na kusaini mkataba na vinara hao wa ligi kuu soka nchini humo.

Endapo Laporte atatua ndani ya Man City atakuwa ndiye mchezaji ghali zaidi akivunja rekodi ya usajili ya klabu hiyo inayoshikiliwa na kiungo Kevin de Bruyne ambaye alisajiliwa kwa dau la £55m mwaka 2015 akitokea VfL Wolfsburg ya Ujerumani.

Laporte huenda akaungana na walinzi wengine ghali duniani ambao ni John Stones na Kyle Walker waliosajiliwa ndani ya uongozi wa Pep Guardiola.


No comments:

Post a Comment