Tuesday 30 January 2018

Mashabiki wa Arsenal wamuona Aubameyang kama Henry mpya


Mashabiki wa Arsenal tayari wamenunua jezi ya Pierre-Emerick Aubameyang yenye namba 14, wakati nyota huyo wa Dortmund akiwa njiani kwenda Emirates.

Baadhi ya mashabiki wa Arsenal wameonekana wakiwa wamevaa jezi ya mshambuliaji huyo wa Dortmund ikiwa na jina lake namba 14, namba hiyo ilikuwa kivaliwa na mshambuliaji Thierry Henry na Theo Walcott.

Gunners sasa inakimbizana na muda katika kukamilisha utakaovunja rekodi wa pauni 55.4milioni kwa nyota huyo wa Gabon (28).

Hiyo itampa nafasi Aubameyang kuungana na nyota mwenzake wa zamani wa Dortmund Henrikh Mkhitaryan alijiunga na Arsenal akitokea na Manchester United kwa kubadilishana na Alexis Sanchez wiki iliyopita.

Ujio wa Aubameyang unamweka katika wakati mgumu mshambuliaji Alexandre Lacazette aliyesajiliwa mwanzo wa msimu huu kwa pauni 46.5milioni akitokea Lyon.

Hata hivyo uamuzi wa shabiki kupiga picha akiwa na jezi ya Aubameyang umepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wengine wa Emirates.

Taarifa zinasema kuwa Arsenal wamekubali kununua nyota huyo ambaye anatagemewa kuaga Borussia Dortmund ndani ya saa 24 zijazo.

Shabiki mmoja alitweeted: Love you Aubameyang." Lakini wenzake wakamjibu "Acha kwanza asaini."

No comments:

Post a Comment