Wednesday 31 January 2018

Meya Sitta Apokea Msaada Wa Vifaa Tiba Vyenye Thamani Ya Milioni 30



Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sitta amepokea vifaa tiba vitakavyotumika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es salaam vyenye thamani ya Shilingi milioni 30 kutoka kwa taasisi ya Binti Filamu Foundation ambayo inaundwa na wasanii kumi wa filamu nchini Tanzania.

Meya Sitta ameishukuru taasisi hiyo kwa kutoa vifaa hivyo ikiwa ni lengo la kusaidia jamii kukabiliana na changamoto zinazoikumba sekta ya afya  hususani mama na mtoto ambao ni wahitaji wakubwa wa misaada hiyo.
"Ninafurahi na naawapongeza Binti Filamu Foundation kwa kutoa msaada huu na iwe chachu kwa wasanii wengine kuiga mfano kama wenu kwa kusaidia jamii yenye mahitaji kuliko kila siku kuigwa na kuandikwa mabaya, lazima mtumie akili zenu ili watu waige yaliyo  mazuri, amesema Meya sitta.

Kwa upande wake mlezi na mshauri wa Taasisi hiyo Bi, Asha Baraka amesema kuwa lengo ni kusaidia watoto, kinamama na baadae wazee ili kuunga jitithada za Mama Janeth Magufulli ambae anasaidia wazee na kina mama ambao hawana uwezo.


Nae Kaimu Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala Dr. Isdory Kiwale ameishukuru taasisi hiyo kwani siyo mara ya kwanza kufika hospitalini hapo na kutoa msaada walishanya hivyo kipindi ilipohitajika damu ili kuokoa maisha ya watu, walijitolea kutoa damu.

Akisoma risala mbele ya mgeni Halima Yahaya amesema kuwa Binti Filamu Foundation imefikia kina mama zaidi  ya elfu 7 Tanzania bara na visiwani  huku wakitoa elimu kupinga unyanyasaji wa kijinsia ambao upo kwenye jamii ya Kitanzania.

 Aidha kupitia mpango huu tunashirikiana na taasisi mbalimbali za wanawake  kama vile jukwaa la wanawake  ambapo huendesha kampeni ijulikanayo kama ''ELIMIKA NA BINTI FILAMU'' mwaka 2016/2017 na mwaka huu kauli mbiu ni ''Silaha ya mwanamke ni malengo'' ikiwa lengo na la kuwafikia wanawake zaidi ili kuwaelimisha kuhusiana na unyanyasaji na pia kusaidia sekta ya afya  kwani malengo hayawezi kufikiwa bila kuwa na afya bora.



No comments:

Post a Comment