Wednesday 31 January 2018

Shule iliyoongoza kidato cha nne yataja siri ya ufaulu


Baada ya shule ya Sekondari ya wasichana ya St. Francis Mjini Mbeya kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa jana wameeleza kuwa bidii ya walimu na wanafunzi ndio siri ya mafanikio hayo.

Wakizungumza na EATV  baadhi ya walimu akiwemo Mwalimu wa Somo la Kemia ambaye pia ni Mwalimu wa Nidhamu katika Shule hiyo, Neema Kimani, Mwalimu Msaidizi wa Taaluma Reginald Chiwangu bidii na kumtanguliza Mungu ndio siri ya mafanikio hayo.

''Kumtanguliza Mungu kwa kila jambo, bidii ya walimu na wanafunzi, utawala bora na kusikiliza ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali wa elimu ndio vimechangia shule yetu kuongoza kitaifa'', wamesema.

Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne shuleni hapo akiwemo Joyce Msigala, Lorette Leone na Bibiana Karumuna wamesema kuwa matokeo hayo yametoa mwanga wa jinsi gani  walijiandaa ili kufanya vizuri kwenye mtihani wao.

Wahitimu wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya St. Francis waliomaliza kidato cha nne mwaka jana ambao ndio wameongoza kitaifa kwa kushika nafasi ya kwanza walikuwa 92.

EATV.

No comments:

Post a Comment