Monday 29 January 2018

Mourinho aweka rekodi nyingine Man Utd


Kocha wa Manchester United Jose Mourinho ametimiza mechi 100 tangu ajiunge na timu huku akiwa na wastani mzuri wa ushindi akiwazidi makocha waliomtangulia akiwemo Sir Alex Ferguson.

Mourinho ambaye alijiunga na United majira ya kiangazi mwaka 2016 amedumu na klabu hiyo kwa msimu mmoja na nusu sasa, na hivi karibuni ameongeza mwaka mmoja kwenye mkataba wake uliokuwa unamalizika 2019.

Katika mechi zake 100 Mourinho amefanikiwa kuiongoza United katika mechi za EPL 62 ambapo ameshinda 34, sare 20 na kufungwa 8. Katika mechi 6 za UEFA Mourinho ameshinda 5 na kupoteza moja.

Kwa upande wa EUROPA Mreno huyo ameshinda mechi 10 akitoka sare mara tatu na kupoteza mbili. Kwa upande wa Kombe la FA amecheza mechi 6 akishinda 5 na kupoteza moja. Kombe la Ligi EFL kocha huyo ameshinda mechi saba na kupoteza mbili.

Kwa upande wa makocha waliomtangulia Ferguson alishinda mechi 48, Moyes ambaye alikomea mechi 51 alishinda 27 pekee huku Louis Van Gaal akishinda mechi 52. Mourinho yupo juu yao akiwa ameshinda jumla ya mechi 62.


No comments:

Post a Comment