Thursday 1 February 2018

Mwana FA: sijawahi kuvaa suruali za kubana

MKONGWE kwenye Muziki wa Bongo Fleva, Hamisi Mwinjuma, ‘MwanaFA’ amesema, katika maisha yake ya kisanii, hajawahi kuvaa suruali za kubana kama ilivyo kwa vijana wenzake wa kileo kwa kile alichodai nguo hizo zinamfanya ashindwe kupumua.

Akipiga stori na Showbiz Xtra, MwanaFA alisema, tamaduni za Muziki wa Hip Hop ndizo zilizomfanya ashindwe kabisa kuvaa suruali za kubana kwa kuwa kila anapojaribu kuvaa hujikuta anashindwa kupumua.

“Unajua nguo zetu sisi watu wa Hip Hop ni ile suruali pana na tisheti kubwa, nimekulia katika mavazi hayo, licha ya kwamba dunia inabadilika lakini mimi nashindwa kabisa kuvaa suruali za kubana kwa kuwa nguo hizo hunifanya nishindwe kuhema,” alisema MwanaFA.

No comments:

Post a Comment