Wednesday 31 January 2018

Karia kuongoza ujumbe wa TFF mkutano wa CAF


Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF limetoa taarifa leo kuwa viongozi wake watatu wa juu watakuwa ni miongoni mwa wajumbe watakaohudhuria mkutano mkuu wa CAF.

Viongozi hao ni Rais wa TFF Wallace Karia, Makamu wa Rais wa TFF Michael Wambura na Kaimu Katibu Mkuu wa TFF Kidao Wilfred.

Mkutano huo mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF utafanyika Februari 2, 2018 nchini Morocco.

Morocco ni mwenyeji wa michuano ya kuwania ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN zilizoanza Januari 13 na leo ni hatua ya nusu fainali ambapo wenyeji Morocoo wanacheza na Libya huku Sudan wakikipiga na Nigeria.

No comments:

Post a Comment