
Wastara kwa kipindi kirefu sasa amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya mguu na yupo kwenye maandalizi ya safari kwenda India kwa matibabu zaidi.
Waziri Mwakyembe akiambatana na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu na Katibu Mtendaji wa BASATA alimtakia kheri Wastara na kumkabidhi mchango wa Shs. 1,000,000/= (milioni moja).
Aidha, Mwakyembe aliwasihi wasanii na Watanzania kwa ujumla kumchangia Wastara kwa hali na mali ili aweze kupata fedha za kumwezesha kwenda India kwa matibabu zaidi.
No comments:
Post a Comment