Wednesday 29 November 2017

Shirika hili la ndege kutobeba wanyama katika safari zake kuelekea Ujerumani



Ndege za Turkish Airlines zimetangaza kuwa hazitokubali mnyama wa aina yoyote katika safari zake za kuelekea Ujerumani.

Kwa mujibu wa habari,Turkish Airlines imetoa tangazo hilo baada ya uamuzi kutoka katika serikali ya Ujerumani.

Ripoti zinaonyesha kuwa ndege za mizigo na abiria hazitokubali wanyama kuelekea Ujerumani.

Abiria wote wanaoelekea Ujerumani wameombwa kufuata sheria hiyo mpaka hapo serikali ya Ujerumani itakapotoa tangazo jingine.

No comments:

Post a Comment