Friday 1 December 2017

Wilshere hatihati kucheza Kombe la Dunia



Kocha wa timu ya Taifa ya England, Gareth Southgate amemuweka katika mazingira magumu kiungo mshambuliaji wa Arsenal, Jack Wilshere.

Mchezaji huyo anasubiri simu ya kocha huyo wa timu ya Taifa ya England kumjumuisha katika kikosi cha Kombe la Dunia mwakani nchini Russia.

Ingawa Wilshere anajipa matumaini ya kuwemo katika kikosi hicho, lakini Southgate amemtaka kupata namba katika kikosi cha kwanza cha Arsenal.

Mchezaji huyo anahaha kupata namba kikosi cha kwanza Arsenal, baada ya kurejea kutoka Bournemouth alikokuwa akicheza kwa mkopo.

“Simu yangu haikua wazi siku zote, Jack anatakiwa kupata nafasi Arsenal. Amesugua benchi katika mechi nyingi, hivyo napaswa kumchunguza, “alisema Southgate.


No comments:

Post a Comment