Thursday 30 November 2017

Gigy Money ampa makavu Rado.


Msanii Gigy Money amemtolea povu muigizaji wa filamu wa bongo Rado, ambaye wiki iliyopita alisikika akisema wasanii wa kike wa bongo fleva hawana vigezo vya kuolewa, na kusema kwamba ndoa siku hizi haina dili kwani wanwake wanajioa wenyewe.

Gigy ameyasema hayo alipokuwa akiongea na mwandishi wa East Africa Radio, na kusema kwamba suala la kuolewa halina dili sana kwani wanawake wanaoa wenyewe kwa kujilipia mahari, na kumtaka Rado apambane na hali yake kwa kutokuwa na hela ya kuweza kuwapata watoto wazuri.


No comments:

Post a Comment