Friday 1 December 2017

Jifunze jambo hili ili kuyadumisha mahusiano yako ya mapenzi



Unapokuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu sahihi, kila wakati jitahidi kuwa na mawasiliano ya karibu na mtu huyo mara kwa mara. Haijarishi upo busy kiasi gani, kwani ukweli ambao upo wazi unasema ya kwamba mapenzi ya kweli hujengwa na mawasiliano thabiti.

Nasema hivi nikiwa na maana ya kwamba hivi ukimpigia simu mpenzi wako zaidi ya mara tatu bila kupokea huwa unajisikiaje? Bila shaka huwa huwa unajisikia vibaya sana, achilia mbali kutokupokea  simu, vipi tena ukitumia mpenzi wako ujumbe mfupi wa maandishi (sms) na asijibu kwa wakati, bila shaka suala hilo nalo litakufanya unisikie vibaya.

Kwa dalili hizo utaona ni kwa kiasi gani mawasiliano yalivyo na nguvu katika suala la kuhakikisha mahusiano yako yanasonga mbele. Hivyo haijalishi upo mbali au karibu na mpenzi wako kiasi gani,  hivyo unachotakiwa ili kulifanya penzi lenu liwe imara ni lazima uhakikishe ya kwamba unajibu sms za mpenzi wako kwa wakati, na hata simu zake ni lazima uzipokee kwa wakati pia.

Hii ni kwa sababu ipo  kauli isemayo mapenzi ni hisia. Inawezekana fika wakati mpenzi wako anakautumia sms hiyo, anakuwa na hisia kali na wewe na hivyo endapo utachelewa kujibu utafanya ajisikiye vibaya, kwani dawa ya njaa ni chakula, hivyo jifunze kuwa karibu na mpenzi wako kwa kumjibu na kupokea simu yako kwa wakati hii itasaidia kuamsha hisia mpya za kimapenzi.

Lakini pia epukana na kumjibu mpenzi wako kauli ambazo zitamfanya mpenzi wako huyo kukushusha hadhi ya kuendelea kukupenda wewe na kumfanya aweze mawazo hasi juu yako.

Mwisho nimalize kwa kusema mawasiliano ya kweli ni chachu dhidi ya kuongeza hamasa na mvuto wa kimapenzi.

No comments:

Post a Comment