Friday 1 December 2017

Rostam wakanusha kuimba matusi

Msanii wa muziki Bongo, Stamina amesema ngoma ya ‘Kiba_100’ haina matusi kama baadhi ya watu wanavyodai.                                                                                               

Kiba_100 ni ngoma ya Roma na Stamina (Rostam) ambayo kwa sasa inafanya vizuri. Akizungumza na XXL ya Clouds Fm Stamina amesema hata wale wanasema ngoma hiyo inastahili kufungiwa wanakosea.

“Ukisema hiki kitu kifungiwe, je kifungiwe kwa sababu gani ukiangalia hatuja tukana, hakuna tusi ambalo lipo cleared ambalo mtu anaweza kusema hili ni tusi, hakuna tusi tulilotukana” amesema Stm

“Sisi wenyewe katika uandishi tulifuata maadili ya kutofikisha vitu vingine kwa sababu ya ukali wa maneno, ukisema wimbo ufungiwe ni sawa na kusema niache kazi yangu ya muziki, halafu kuna kuwa hakuna uhuru wa msanii kwa sababu kuna vitu unashindwa kuvifikisha, kama umeongea kitu ambacho kina ukweli acha kifike” amesisitiza.

Kiba_100 ni ngoma ya pili kwa Rostam kutoa baada ya kufanya vizuri na ngoma ‘Hivi Ama Vile’.

No comments:

Post a Comment