Monday 27 November 2017

Mrembo wa Afrika Kusini atwaa taji la Miss Universe 2017

Ni furaha kubwa kusikia nchi yenu imefanikiwa kuzibwaga nchi nyingine katika mashindano ya dunia. Shangwe limetawala nchini Afrika Kusini baada ya mrembo wao Demi-Leigh Nel-Peters kufanikiwa kushinda taji la Miss Universe kwa mwaka huu.


Demi ambaye ana umri wa miaka 22, amefanikiwa kutwaa taji hilo Jumapili hii mjini Las Vegas nchini Marekani ambapo shindano hilo lilipokuwa linafanyika.

Mrembo huyo alifanikiwa kuwabwaga washiriki wengine ambao waliingia katika hatua ya tano bora akiwemo mrembo kutoka Colombia, Jamaica, Thailand na Venezuela.



Picha ya washiriki wa Miss Universe ambao walifanikiwa kuingia kwenye tano bora



No comments:

Post a Comment