Wednesday 29 November 2017

Kilimanjaro Stars yaanza kujifua




Timu ya Taifa ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars imeendelea na kambi ya maandalizi kuelekea kwenye michuano ya kombe la CECAFA Challenge.

Kilimanjaro Stars chini ya kocha Ammy Ninje imefanya mazoezi mbalimbali katika Uwanja wa Gymkhana, Dar es Salaam leo Novemba 28, 2017.

Timu hiyo inajiandaa kucheza Kombe la CECAFA Challange 2017 huko Kenya kuanzia Desemba 3 hadi 17 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa na kocha Ninje kutoka vilabu mbalimbali vya ligi kuu soka nchini wamesharipoti kambini baada ya ligi kusimama kwa muda kupisha michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment