Monday 27 November 2017

Guardiola akiri maajabu

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola, amesema timu yake imeonesha ushindani wa ajabu wakati ikihangaika kusawazisha na kuongeza bao la ushindi kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka nchini England jana dhidi ya Huddersfield.


Guardiola amekiri kuwa kama timu inataka kushinda ubingwa lazima iwe tayari kuonesha maajabu kama ilivyokuwa jana huku akisisitiza kuwa wachezaji wake wanatakiwa kuzoea hali hiyo.

Manchester City ilitoka nyumba kwa bao 1-0 kabla ya kusawazisha kupitia kwa Sergio Aguero kisha kuongeza bao la ushindi kupitia kwa Raheem Sterling. Baada ya ushindi huo matajiri hao wa jiji la Manchester wamefanikiwa kuendelea kukaa kileleni wakifikisha alama 37 dhidi ya 29 za wapinzani wao Manchester United wanaoshika nafasi ya pili.




Pia vinara hao wa ligi wamefikia rekodi yao ya mwaka 2015 ya kushinda mechi 11 za ligi mfululizo. Man City jana ilipata ushindi kwa mara ya kwanza tangu Aprili 1995 ikitokea nyuma kipindi cha kwanza kisha kushinda kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment