Thursday 30 November 2017

Punda wanane watupwa jela kwa kuharibu mimea yenye thamani nchini India



Punda wanane wametupwa gerezani kwa muda wa siku nne nchini India kwa kosa la kuharibu mimea yenye thamani katika bustani .

Kituo cha runinga cha New Delhi kimefahamisha kuwa  uongozi wa jimbo la Uttar Pradesh uliwatupa jela punda hao kwa lengo la kuwaadhibu.

Mlinzi wa gereza la Jalaun  RK Mishra amesema kuwa wanayama hao waliharibu mimea yenye thamani katika bustani hiyo.

Mlinzi huyo aliendelea kusema kuwa mmiliki wa wanyama hao alipewa tahadhari kuhusu wanyama wake.

Wananyama hao waliachwa huru baada ya mwanasiasa mmoja kujitolea kulipa gharama zote zilizosababishwa na wanyama hao.

No comments:

Post a Comment