Thursday 30 November 2017

Katika kutimiza miaka 20 ya ndoa yao, Lissu ampa ujumbe mzito mkewe



Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu leo ametimiza miaka 20 ya ndoa akiwa bado hospitalini Nairobi akijiuguza  ambapo pia amemshukuru mke wake Alicia na kusema kwamba ni mke ambaye anaishi katika kiapo cha siku walichofunga ndoa.

Kwa mujibu wa Diwani wa Sombetini-Arusha, Ally Bananga amesema kwamba Mh Lissu amemtaja Alicia kama kipande chake sahihi kwa upande wake.

"Leo Tundu Lissu na mkewe Alicia wametimiza miaka 20 ya ndoa yao. Mume yuko kitandani na mke amebaki pembeni yake kumuhudumia. Ndoa yenye baraka hii,  na Mh Lissu amemtaja Alicia kama kipande chake sahihi"  Bananga.

Aidha Diwani Bananga ameongeza kwamba "Lissu amesema mkewe anakiishi kiapo chao siku walipofunga ndoa kuwa watayakabili maumivu na vikwazo pamoja mpaka mwisho".

No comments:

Post a Comment