Thursday 30 November 2017

Baba wa Neymar aponda taarifa za mwanaye kuamia Real Madrid



Baba mzazi na wakala wa Neymar Jr, Neymar Santos Sr amesema yeye na mwanae hawana wazo la kuhamia Real Madrid kwa wakati huu.

Neymar Sr amesema hawafikirii kuhamia Real Madrid kama inavyodaiwa, akisisitiza kuwa mkataba wa Neymar Jr ndani ya PSG bado ni mrefu sana hivyo kwasasa wanaangalia kufanya vizuri ndani ya PSG.
Hatuna wazo hilo kwasasa, Neymar ana mkataba wa miaka mitano na PSG unaanzaje kuzungumzia mambo ya kuhama kwasasa, sio rahisi hivi vitu vinazungumzwa tu lakini havina uhalisia”, amesema Neymar Sr.

Paris Saint-Germain ilimsajili Neymar Jr kwa dau la kuvunja rekodi ya dunia ya €222 takribani bilioni moja za Tanzania ukijumulisha na gharama zote zilizohusika kukamilisha usajili huo.

Neymar Jr mwenye miaka 25 amekuwa akihusishwa kujiunga na Real Madrid ya Hispania kwa dau la €250 mwishoni mwa msimu wa 2017/18.

No comments:

Post a Comment