Sunday 29 October 2017

Uturuki yalaani vikali shambulizi lililofanywa nchini Somalia

Uturuki yalaani vikali shambulizi lililofanywa nchini Somalia

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki amelaani vikali shambulizi lililosababisha vifo vya watu takriban kumi mjini Mogadishu.

Kwa mujibu wa habari,waziri huyo katika mtandao amewatakia amani wale wote waliopoteza maisha na kutuma salamu za rambirambi kwa familia zote zilizofikiwa na msiba huo.

Uturuki vilevile imeahidi kuwa na Somalia bega kwa bega katika kupambana na ugaidi.

Watu takriban kumi wamepoteza maisha huku wengine nane wakiwa wamejeruhiwa vibaya katika milipuko miwili ya gari katika moja ya hoteli mjini Mogadishu.

Ripoti zilizotolewa na kituo cha habari cha Somalia (SONNA) zimeonyesha kuwa kati ya waliopoteza maisha ni mbunge wa zamani Abdinasir Garane na Mkuu wa polisi wa zamani Mohamed Yusuf.

No comments:

Post a Comment