Tuesday 31 October 2017

Mvua kubwa zatarajiwa kuanza kunyesha usiku wa leo

Mvua kubwa zatarajiwa kuanza kunyesha usiku wa leo




Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa(TMA) imetangaza vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya masaa 24 vinatarajiwa kuanza usiku wa kuanzia leo Jumanne.

Taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo Jumanne imeeleza kuwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam na Pwani pamoja visiwa vya Unguja na Pemba yataaririka.

“Mvua hiyo inatarajiwa kusambaa katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Lindi kuelekea siku ya Ijumaa ya tarehe 3 Novemba 2017.”

“Hali hii inatokana na kuwepo na kuimarika kwa ukanda wa mvua (Inter Tropical Convergency Zone –ITCZ) katika maeneo hayo.”

Mamlaka hiyo imewataka wakazi wa maeneo yaliyotajwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zinazotolewa

“Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo kila itakapobidi

No comments:

Post a Comment