Tuesday 31 October 2017

Meya wa jiji la Mwanza afunguka

Meya wa jiji la Mwanza afunguka



Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, James Bwire amefunguka juu ya sababu zilizomfanya akamatwe na polisi wakati wa msafara wa Rais Magufuli alipokuwa Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari Meya huyo amesema sababu ya kukamatwa kwake alielezwa ni amri kutoka kwa viongozi wa juu ili asiwepo kwenye msafara wa Rais, na kupata fursa ya kuzungumza yale ambayo anayajua.

Meya Bwire ameendelea kwa kusema kwamba katika jiji hilo kuna vitendo vya matumizi mabaya ya fedha pamoja na kudhulumu haki za wananchi, na kamwe hatoacha kuzungumza hata kama anahatarisha kibarua chake

No comments:

Post a Comment