Friday 3 November 2017

Anaswa na wananchi akimbaka mtoto wa miaka miwili

Anaswa na wananchi akimbaka mtoto wa miaka miwili



Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba 

Polisi wanamshikilia mkazi wa Kijiji cha Magamba wilayani hapa kutokana na tuhuma za kumbaka mtoto mwenye miaka miwili.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba, tukio hilo lilitokea juzi Kitongoji cha Komkola Chang’ombe.

Wakazi wa kitongoji hicho waliozungumza na gazeti hili, walisema walisikia mtoto akilia nyumbani kwa mtuhumiwa na walipokwenda walikuta akimbaka mtoto huyo.

“Huu ni unyama umevuka kiwango kijana anathubutu kumbaka mtoto mdogo kama yule, sijui tunaelekea wapi vijana wa namna hii hawastahili kuishi na jamii,” alisema Hussen Juma.

Kamanda Wakulyamba alisema mtoto aliyebakwa amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni akiendelea na matibabu na kwamba, mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Alitoa wito kwa wazazi kutowaacha watoto wao kuzurura mitaani, ili kuwalinda wasitendewe vitendo vya kikatili kama hivyo

No comments:

Post a Comment