Tuesday 31 October 2017

CCM kupeleka vijana Ulaya

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimetoa fursa ya kuwapeleka barani Ulaya vijana watakaochaguliwa na shirikisho la soka nchini Tanzania TFF kwaajili ya kupata mafunzo ya kuchezesha soka.

Hilo limedhibitishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho ndugu Humphrey Polepole kwenye mahojiano na eatv.tv ambapo amebainisha kuwa fursa hiyo imetolewa na vyama rafiki vya chama hicho kwenye nchi za Ulaya.

Polepole amesema kupitia kikao kikubwa cha vyama vyote vya kijamaa barani Afrika na Ulaya kilichofanyika mapema mwaka huu ilitolewa fursa kwa CCM kuweza kupeleka vijana kwenye baadhi ya nchi barani Ulaya ili kupatiwa mafunzo hayo.

Aidha Polepole amebainisha kuwa zoezi hilo litasimamiwa na TFF kwasababu wao ndio wana dhamana ya kupitisha watu wanaohusiana na soka hivyo watashirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha vijana wanatumia fursa hiyo ambapo baada ya mafunzo hayo watarudi kuitumikia sekta ya michezo nchini.

No comments:

Post a Comment