Friday 3 November 2017

Maduka yanaodurufu CD za wasanii yafungiwa na TRA

Maduka yanaodurufu CD za wasanii yafungiwa na TRA

       

              



MAMLAKA ya mapato nchini (TRA) ikishirikiana na kampuni ya Msama Auction Mart ambao ni wasimamizi na wasambazaji wa kazi za muziki wa Injili, chini ya Mkurugenzi wake, Alex Mwita Msama, imefanya oparesheni ya kuwafungia maduka na kuwahoji watu wanaodurufu CD feki yaani zisizofuata utaratibu uliopo.


Akizungumza wakati wa oparesheni hiyo iliyofanyika jana jioni Kariakoo jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Kodi za Ndani (TRA), Elijah Mwandubya, alisema wamekuwa wakiwatahadharisha watu hao kuachana na kazi hiyo ya kudurufu CD feki hivyo lakini wamekuwa hawaitikii tahadhari hiyo na sasa mamlaka hiyo.

Aliongeza kwamba, kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali, wamejidhatiti vilivyo kuhakikisha kazi za wasanii nchini zinalindwa na serikali inapata mapato yake kutokana na wengi wao kukwepa kulipa kodi na kuuza CD feki.

Alisema serikali inatengeneza mazingira safi na wafanyabiashara waaminifu wanaofuata utaratibu sahihi, ukiwemo ulipaji wa kodi kwa wakati na hivyo wataendelea
kuhakikisha kazi za wasanii zinalindwa na kuheshimika ipasavyo, kwani zoezi litaendelea maeneo mbalimbali nchin

No comments:

Post a Comment